Kikwete ameteleza kushinikiza gas kupelekwa Dar es Salaam

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,898
President-Jakaya-Kikwete.jpg

Rais kikwete kutoguswa na shinikizo la maandamano ya wananchi wa Mtwara kuhusu usafirishaji wa bomba la Gas kwenda Dar es Slaam ni kutokuangalia kwa makini mambo ya msingi kwa mtazamo wa kiuchumi, usalama wa mradi na uwiano wa maendeleo kitaifa.

Usalama:

  • Ulimwengu wa leo wakati unakabiliwa na hatari ya maadui wenye kuharibu miundo mbinu sina hakika usalama wa bomba hilo la gas usalama wake toka Mtwara hadi Dar, kwani pamoja na umuhimu wake, kunaweza kutokea hujuma kubwa katika bomba hili kutokana na umbali huo, wakati vinu vya kufua umeme vingewezekana kujengwa eneo ambalo maliasili inapatikana.

  • Hatari kubwa Electric power plant kuwa sehemu moja, hujuma ikifanyika, au itokeapo vita shabaha moja italitia taifa zima gizani. Muhimu Electric power plants zikawa sehemu mbalimbali na grid network power iunganishwe. Ukikatwa umeme Dar es salaam basi nchi nzima gizani.
  • Ndege moja tu inatosha kudondosha bomu moja Ubungo na lingine Kinyerezi kisha taifa zima likawa gizani mara moja, no alternative, tutaonekana si watu wa kuona mbali. Ukaribu uliopo Ubungo na Kinyerezi vigumu kupata muda wa papo kwa papo emergency respond.

Kiuchumi:
Ujenzi wa vinu vya kufua umeme karibu na eneo inakopatikana rasilimali ni bora na inapunguza gharama nyingi. Litakapotokea tatizo la gas kutofika kwa kiwango kinachotakiwa toka Mtwara kuna ziada ya kuhangaika kutafuta uvujaji uliko kwa umbali mkubwa toka Dar hadi Mtwara, jambo ambalo linaweza kusababisha uhaba wa umeme kwa muda mrefu.

Ukuzaji wa bandari ya Mwara kwa uanzishwaji wa viwanda huko papo kuunganisha ukanda wa kusini na ukanda wa kusini nyanda za juu kunakopatikana makaa ya mawe na chuma kutaongeza msisimko wa maendeleo zaidi wakati Wachina wanampango wa kujenga reli toka Mkoa mpya wa Njombe hadi Mtwara. Uanzishwaji viwanda mikoa ya Ruvuma, Njombe, Lindi na Mtwara ni muhimu kutokana rasilimali nyingi kupatikana eneo hili.

Wanaosoma jiografia, mtakumbuka eneo la Essen nchini ujerumani lilivyo na viwanda vizito tokana na upatikanaji wa maliasili huko, Wajerumani hawakujenga miundo mbinu ya kuhamishia maliasili iende Berlin na kwengineko kwani kufanya hivyo kungekuwa na athari zaidi kiutendaji, kiuchumi na kiusalama pia, hali kadhalika kusahaulika wananchi wanaoishi maeneo inakopatikana maliasili.

Uwiano wa maendeleo
Uwiano wa maendeleo kitaifa ni jambo linalotakiwa kutiliwa maanani, kwani kushinikiza gasi ipelekwe Dar es Salaam kwa mahitaji ya nchini nzima si vema kwani ni kuongeza zaidi msongamano wa viwanda jijini Dar es Salaam hatari ya uchafuzi wa mazingira na hali ya hewa na papo kuzidi kuongeza mmiminiko wa watu kutafuta ajira huko badala ya kuanzishwa viwanda eneo la maliasili ili kuvutia watu wabaki huko kwa vile ajira ipo eneo lao.

Pamoja na kwamba uwiano wa maendeleo si rahisi kuwa sawa, lakini kuna sababu za msingi kutumia vyanzo vya rasilimali za mahali zinakopatikana kusaidia kuleta maendeleo kwa kuanzisha kwa makusudi miradi ya maendeleo kama uanzishwaji wa viwanda. Hatuhitaji machinga kuendelea kumiminika Dar es Salaam kwani wanachofuata ni hali njema ya maisha na ajira. Lakini ukishaweka mtego wa ajira na vivutio vingine kama hali nzuri ya umeme, viwanda nk hawatakuwa na sababu ya kuja Dar kwa vile wanachofuata dar kinapatikana kwao.

Tutakuwa tumekuwa na mtazamo finyu kama tutakubaliana na kauli ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwamba kwa sababu Dar es Salaam wanaota mapato makubwa ya kodi kwa kulisha nchini nzima basi iwe hoja ya kupeleka rasilimali pale. Nakumbuka Hayati Nyerere aliamua kiwanda cha SPM Mgolole, Mufindi karibu na Makambako kijengwe huko badala ya kusafirisha magogo kwa TAZARA kuja kutengeneza karatasi Dar es Salaam. Gharama nyingi ziliepukika na pia ajira ilipatikana sehemu hilo badala ya watu wa huko kulazimika kuja Dar kupata ajira.

Tungetazamia wabunge wangeanzisha mjadala wa jambo hili kuishinikiza serikali kusitisha mpango huu kwani hoja ya kuwauzia mitungi ya gas wananchi wa Mtwara si ufumbuzi wa ajira na mendeleo, bali ujenzi wa viwanda vitakavyoendeshwa au kuzalisha gas na pia ujenzi wa vinu vya kufua umeme huko kutawanufaisha zaidi wananchi, taifa, na pia kuondolea taifa msongo wa ukuaji jiji la Dar es Salaam.
 
Wakati mwingine nashawishika kwamba, washauri/hutuba zake zinaandaliwa na TOT chini ya Hadija Kopa! Maana hotuba zake zimejaa mipasho na vina vya mashairi kama ya Taarabu ati!!!!

Hivi kwanini huwa hachukui muda wa kutosha kufanyia utafiti jambo analo kashauriwa (kama ni kweli ana washauri)? Maana, mambo mengi anayo yatolea uamuzi hayaendani na hali halisi kama kiongozi mkuu!!!

Yale yale aliyosema waziri wa Nishati siku moja kabla ya hotuba ya Mkuu, ndio yalayale aliyo sema mkulu. Maana yake ni kwamba, hakuwa hata na muda wa kujiuliza yeye binafsi kuhusu nini misingi ya maandamano ya wananchi wa Mtwara/ Lindi!!!!

Hitimisho langu ni kwamba; watu walisha tia ndani pesa za watu, hivyo kuwageuka itakuwa ni kizaa zaa na ndiyo maana wanakazania gesi lazima iende Bagamoyo.

Mtwara/ Lindi komaeni. Haki/ Usawa haviji kwa kupigia watawala magoti. Lazima kuipigania kwa nguvu zote. Heri mkoloni mweupe maana alikuwa anajua siku moja lazima atarudi kwao, kuliko mkoloni mweusi ambaye anajuwa kwake ni hapahapa na akizembea mwisho wake ni kuishia gerezani.
 
Wakati mwingine nashawishika kwamba, washauri/hutuba zake zinaandaliwa na TOT chini ya Hadija Kopa! Maana hotuba zake zimejaa mipasho na vina vya mashairi kama ya Taarabu ati!!!!

Hivi kwanini huwa hachukui muda wa kutosha kufanyia utafiti jambo analo kashauriwa (kama ni kweli ana washauri)? Maana, mambo mengi anayo yatolea uamuzi hayaendani na hali halisi kama kiongozi mkuu!!!

Yale yale aliyosema waziri wa Nishati siku moja kabla ya hotuba ya Mkuu, ndio yalayale aliyo sema mkulu. Maana yake ni kwamba, hakuwa hata na muda wa kujiuliza yeye binafsi kuhusu nini misingi ya maandamano ya wananchi wa Mtwara/ Lindi!!!!

Hitimisho langu ni kwamba; watu walisha tia ndani pesa za watu, hivyo kuwageuka itakuwa ni kizaa zaa na ndiyo maana wanakazania gesi lazima iende Bagamoyo.

Mtwara/ Lindi komaeni. Haki/ Usawa haviji kwa kupigia watawala magoti. Lazima kuipigania kwa nguvu zote. Heri mkoloni mweupe maana alikuwa anajua siku moja lazima atarudi kwao, kuliko mkoloni mweusi ambaye anajuwa kwake ni hapahapa na akizembea mwisho wake ni kuishia gerezani.

CCM imejichimbia kaburi yenyewe mikoa ya Lindi na Mtwara, kwani vyama vikuu vya upinzania nchini Chadema na CUF vimeungana kutetea matakwa ya Wanamtwara na Wanalindi.

Sijaona sababu ya kung'ang'ania gas lazima iende Bagamoyo, kwani watu wa Mtwara hawahitaji viwanda na mwamko wa maendeleo? Hapa naona patachimbika.
 
CCM imejichimbia kaburi yenyewe mikoa ya Lindi na Mtwara, kwani vyama vikuu vya upinzania nchini Chadema na CUF vimeungana kutetea matakwa ya Wanamtwara na Wanalindi.

Sijaona sababu ya kung'ang'ania gas lazima iende Bagamoyo, kwani watu wa Mtwara hawahitaji viwanda na mwamko wa maendeleo? Hapa naona patachimbika.

KIla kitu Bagamoyo! Si mnakumbuka mshikemshike wa kuhamisha makao makuu ya Hifadhi ya Saadan ilivyo leta tibwilitibwili na wazee wa Pangani kipindi kile? Kwamba yahamie wilaya ya Bagamoyo!!!!??? Na wazee wa Pangani wakatia mpira kwapani.

Kusini komaeni. Msimuangalie shemeji usoni, bhaa!!!!!
 
KIla kitu Bagamoyo! Si mnakumbuka mshikemshike wa kuhamisha makao makuu ya Hifadhi ya Saadan ilivyo leta tibwilitibwili na wazee wa Pangani kipindi kile? Kwamba yahamie wilaya ya Bagamoyo!!!!??? Na wazee wa Pangani wakatia mpira kwapani.

Kusini komaeni. Msimuangalie shemeji usoni, bhaa!!!!!

Misitu ya kusini hatuijui zaidi ya wamakonde, wamakua na wamwera linakopia bomba hili. Wasiposikilizwa hao walishatamka siku ya maandamano kiakachoendelea kuhujumu mradi huo.
 
Wana Mtwara hakikisheni gas haisafiri kwenda Dar hata wakijenga hilo bomba, Yeye J.K si anajifanya anataka kushindana na nguvu ya umma? Muonesheni kuwa hakuna serikali duniani iliyowahi kushindana na wananchi wake halafu ikashinda.
 
Umeandika vizuri sana maana hata mtu akitaka kujenga kiwanda raw material availability is one of the deciding factor lakini hawa ccm sijui wanaongozwa na nini kufanya maamuzi
 
Wakati mwingine nashawishika kwamba, washauri/hutuba zake zinaandaliwa na TOT chini ya Hadija Kopa! Maana hotuba zake zimejaa mipasho na vina vya mashairi kama ya Taarabu ati!!!!

Hivi kwanini huwa hachukui muda wa kutosha kufanyia utafiti jambo analo kashauriwa (kama ni kweli ana washauri)? Maana, mambo mengi anayo yatolea uamuzi hayaendani na hali halisi kama kiongozi mkuu!!!

Yale yale aliyosema waziri wa Nishati siku moja kabla ya hotuba ya Mkuu, ndio yalayale aliyo sema mkulu. Maana yake ni kwamba, hakuwa hata na muda wa kujiuliza yeye binafsi kuhusu nini misingi ya maandamano ya wananchi wa Mtwara/ Lindi!!!!

Hitimisho langu ni kwamba; watu walisha tia ndani pesa za watu, hivyo kuwageuka itakuwa ni kizaa zaa na ndiyo maana wanakazania gesi lazima iende Bagamoyo.

Mtwara/ Lindi komaeni. Haki/ Usawa haviji kwa kupigia watawala magoti. Lazima kuipigania kwa nguvu zote. Heri mkoloni mweupe maana alikuwa anajua siku moja lazima atarudi kwao, kuliko mkoloni mweusi ambaye anajuwa kwake ni hapahapa na akizembea mwisho wake ni kuishia gerezani.

Waambie watu wa Mtwara. Mradi huo haubadilishwi ng'o!Ni mradi uliokoa kichwa cha mwana mfalme kukatwa huko uchina.
 
acha kutudanganya viwanda vingi Ujerumani vipo Baden Wurtemberg na si Essen! Na jaribu kutueleza ukweli hicho kiwanda cha Mgololo kipo wapi sasa? Hizi akili za kuharibu miundo mbinu ni za watu wenye utovu wa mawazo gesei itaenda Dar na manufaa yake yatakuwa makubwa zaidi hatuwezi kusema tuhamishe viwanda huko wakati gesi inaweza kufika viwanda vilipo.
 
Laiti kama Serikali yetu ingelikuwa sikivu, tungeokoa Gharama na pia kuinua wana-Mtwara kiuchumi. Kwa hili Kikwete atajitetea vipi kama akishutumiwa kwa Ubaguzi na Kujali alipotoka tu?
 
Waambie watu wa Mtwara. Mradi huo haubadilishwi ng'o!Ni mradi uliokoa kichwa cha mwana mfalme kukatwa huko uchina.

Alaaa...!!!!!!! Kumbeee!!!!!!!!!!!!! Ndiyo maana watu mishipa inawatokaaaaa kiasi hichoeeeee!!!!!!!!!!!!!
 
ni kweli gas inayopatikana Mtwara ni malia ya watanzania wote lakini busara na hekima kutoka kwa viongozi wa ngazi husika zinahitajika kuhusu suala hill.tuache politiki.Tumie akili /brain kuliko kutumia mdomo sana.
 
Laiti kama tungeelewa maana halisi ya mabadiliko ya muda, pengine tungelikuwa tofauti. Kuna ukweli fulani juu ya maandamano yale ingawa sio kamili kabisa.
We need pipelines to distribute gas from Mtwara to other places. Urusi inauza gas karibu ulaya yote through pipelines. Ingawa kwenye suala la kuzalisha umeme, pengine strategically Lindi ingelifaa zaidi maana ilivyo sasa Mtwara imeelemewa mno na shughuli nzima zinazoenda na utafutaji wa gas.
 
acha kutudanganya viwanda vingi Ujerumani vipo Baden Wurtemberg na si Essen! Na jaribu kutueleza ukweli hicho kiwanda cha Mgololo kipo wapi sasa? Hizi akili za kuharibu miundo mbinu ni za watu wenye utovu wa mawazo gesei itaenda Dar na manufaa yake yatakuwa makubwa zaidi hatuwezi kusema tuhamishe viwanda huko wakati gesi inaweza kufika viwanda vilipo.

Please elewa mada, viwanda vilivyoko Esseni ni vile vinavyotokana na machimbo ya madini yaliyokuwa yanapatikana huko, haina maana eneo jingine la Ujerumani halina viwanda. Madini kama chuma na makaa ya mawe yaliyokuwa yanapatikana hapo yalichochea uanzishwaji wa viwanda hivyo.

Kumbuka viwanda katika nchi za magharibi havifanyi kila kitu kwa sababu ya mfumo wa industrialization, process za awali hufanyika zinakopatikana raw material na kisha products husafirishwa kulisha viwanda vingine. Essen ilikuwa ni viwanda vya ku-process raw material na products zake zilipelekwa kwenye viwanda vingine. Hawakusafirisha mabongo ya madini ya chuma yaliyochimbuliwa ardhini kupelekwa huko unakosema ila processed products.

TAMKO LA MAKANISA YA P.C.T MKOA WA MTWARA KUHUSU GESI YA MNAZI BAY MTWARA
Baada ya kufuatilia kwa undani, na kwa upana kuhusu swala la gesi ambalo linaendelea kuwa ni mgongano au, ni mgogoro kati ya Serikali na wananchi wa Mkoa wa Mtwara/Lindi kuhusu ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwenda kinyerezi Dar- es –Salaam, tumebaini yafuatayo:-

1. Hakuna Sera ya gesi ambayo husababisha kupatikana Sheria baada ya kupelekwa Bungeni na kuidhinishwa bali kilichopo ni rasimu ya sera ambayo haina ushirikishwaji wa mawazo ya wananchi wa Mkoa wa Mtwara na Lindi, ambako vyanzo vya gesi hiyo ipo.

2. Elimu kuhusu gesi na manufaa yake kwa wananchi haikutolewa ili kujua haki zao kwa madhara yatokanayo na (Uvunaji) uzalishaji wa gesi hiyo, na jinsi watakavyonufaika.

Chama cha Mapinduzi katika Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2010 inatamka wazi katika Ibara ya 63 kifungu cha H na K juu ya gesi ya Mnazibay Mtwara na Songo songo Kilwa, Lindi kuhusu umeme wa (240 MW) Kinyerezi na (300MW) Umeme wa Mnazi bay Mtwara……

-Vifungu hivi vinafafanua:

• Gesi ya Mnazi bay itakuwa kwa ajili ya Mitambo ya kuzalisha umeme ambayo itajengwa Mtwara (300MW)

• Mitambo ya kuchakata gesi kujengwa Mtwara

• Ujenzi wa viwanda Mtwara ili malighafi itokanayo na gesi itumike kutengeneza mbolea, plastic vikiwemo na viwanda vya Cementi

2. Gesi ya Songo songo inafafanua wazi kuwa gesi hiyo itapelekwa Kinyerezi . Dar –es –Salaam kwa madhumuni hayo hayo.

• Kuendeleza viwanda mbali mbali

• Kuzalisha umeme (240 MW)

• Kuchakata gesi kwa kujenga mitambo

Katika ahadi ya Rais wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania alizotoa wakati wa Kampeni za uchaguzi katika hotuba yake ya tarehe 29/10/2010 alitamka wazi kuwa Mkoa wa Mtwara uwe tayari kwa maendeleo makubwa ambayo yanakuja kutokana na gesi iliyogunduliwa katika Mkoa wa Mtwara huko Mnazi bay

Alimainisha/aliainisha juu ya viwanda mbalimbali vitakavyojengwa hapa mkoani vya mbolea,cement, plastic n.k na kuwataka wananchi wajiandae kupokea maendeleo hayo kwa kujenga nyumba nzuri zenye sifa kwa ajili ya wageni. Pia wawasomeshe watoto wao ili wawe na elimu ya juu na kupata ajira katika Makampuni yanayokuja.

Hata baada ya uchaguzi Rais wetu alipokuja kuwashukuru wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kumchagua, alitamka tena katika hotuba yake akisisitiza ahadi yake ya kujenga viwanda ambavyo vitaleta maendeleo kwa Mikoa ya Kusini na kusababisha ajira kwa wana kusini, na kuagiza kwa Meya wa Manispaa Mtwara/Mikindani kuwapa maeneo ya kujenga viwanda hivyo, kwa kile kilichoonekana kukosa maeneo ya ujenzi huo kwa makampuni hayo. Ahadi hizi alizozitoa kwa wananchi kwa ujumla wao wamezipokea na kuendelea kuzifanyia kazi.

Chanzo cha Matatizo: Mara baada ya kuonekana kile walichokitarajia wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kutumia gesi ya Mnazi bay kuleta maendeleo yao kuwa imeamriwa kusafirishwa kwa bomba na kupelekwa Kinyerezi Dar –Es –Salaam ili kuzalisha umeme na kuchakata gesi na mitambo hiyo iwe huko.(Mgeuko wa Ilani ya Uchaguzi, na kutozingatia ahadi zake mwenyewe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa kinyume na kauli za usemi wake mwenyewe kwa kukitangaza kituo cha Kinyerezi kuwa ni sehemu ya mitambo ya gesi ya Mnazi bay-Mtwara na Songosongo-Lindi na kwamba bomba hilo litachukua miezi (18) mpaka kukamilika kwake, kwa matamshi haya ndiyo yaliyoleta hasira na chuki kwa wananchi wa Mtwara/Lindi kwa ujumla.

Hali hii imewafanya wananchi wa Kusini kutokuwa na Imani na Serikali na viongozi wake wahusika na sakata hili la gesi kwa semi mbalimbali za viongozi hawa-Mfano.

(1) Kwa hali yoyote gesi lazima itoke Mtwara (Kwa gharama yoyote ile) kwa kukubali ama kutokubali itakwenda Kinyerezi kwa bomba

(2) Kuitwa wahaini wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kuandamana

(3) Kuitwa wajinga, hawakusoma na kuwa watu wa vijiweni wasio na elimu ya gesi

(4) Nitafanya lolote hata kama nitalaumika na Mataifa mengine lakini wapo watakaochekea yatakayotokea na kauli zinazobadilika kila kunapokucha.

(5) Usemi wa kuigawa nchi vipande vipande

Viongozi hawa hawajui kuwa chanzo kipo kwao wenyewe, kwa kutozingatia kuwa wananchi hao ambao hawana elimu kama yao wanao upeo mkubwa wa kufikiri na kutoa maamuzi kama wanavyotoa wao….

Mfano.

(1) Gesi haitoki Mtwara

(2) Tupo tayari kufa wote kwa ajili ya gesi

(3) Haiwezekan mitambo ya aina zote

-Kufua umeme

-Kuchakata gesi

-Kunufaisha viwanda vya Dar-es-Salaam kwa gesi yetu

-Mikataba ya gesi ya Mnazibay kufutwa ili kuanzisha mikataba iliyo na manufaa kwa Mkoa wa Mtwara na wananchi wake.

(4) Kwa nini bomba la gesi kujengwa kwa muda wa miezi 18 na bara bara kwa miaka 51 ya uhuru haimalizwi kujengwa. Je kwenye gesi kuna nini nyuma yake.?

Hiki ni kiini cha matatizo yote kwa wananchi wa mkoa wa Mtwara kuandamana na mikutano mbalimbali ya kuhamasisha kutokubali gesi kuondoka Mtwara

Nukuu za Wananchi wa Mkoa wa Mtwara/Lindi

1-Kung'olewa kwa Reli

2-Kung'olewa kwa mashine za maji Newala na kupelekwa Dodoma.

3-Kung'olewa kwa taa za kuongoza ndege uwanja wa Mtwara na kupelekwa Uwanja wa KIA Moshi

4-Kuondolewa kwa Mtwara Korido

5-Kuwekezwa kwa bandari ya Mtwara kwa muda usiojulikana inaonyesha jinsi Serikali na viongozi wake wanavyohujumu Mikoa ya Kusini na wananchi wake kwa ujumla.

-Wananchi wa Mkoa wa Mtwara na Lindi wamefikia ukomo sasa wa kutengwa kimaendeleo, kimazingira na kutendewa uonevu wa makusudi na kilio chao cha mwisho ni hiyo gesi ambayo kauli mbiu yao ni GESI HAITOKI MTWARA KWA BOMBA KWENDA KINYEREZI DAR-ES-SALAAM.

-Wananchi wote wameungana juu ya kuitetea gesi kutoka Mtwara, badala yake Serikali ifuate mikataba ya kwanza inayohusu gesi ya Mtwara pamoja na Ilani ya uchaguzi ya CCM ifuatwe na Rais atekeleze ahadi zote alizotoa hapo kwanza na afute kauli yake ya kupeleka gesi Kinyerezi, na wala Serikali isitumie nguvu katika swala zima la gesi ya Mnazibay Mtwara.



TAMKO LA UMOJA WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE –P.C.T MKOA WA MTWARA

1. P.C.T kwa kuzingatia mwono uliopo wa hali tete yenye mwelekeo wa kumwagika damu na kuigawa nchi vipande vipande na kuondokewa amani, yafuatayo yafanyike

• Serikali isitishe mpango wake wa kuondoa gesi kutoka Mnazi bay Mtwara kwa kuisafirisha kwenda Kinyerezi Dar –es Salaam kwa bomba.

• Mitambo ya kuchakata gesi ijengwe Mtwara ili gesi isafirishwe kama mazao ya gesi na mabaki yake kutumiwa katika viwanda vya mbolea na plastic.

• Mitambo ya kuzalisha umeme ijengwe Mtwara na kusafirisha umeme na kuunganisha gridi ya Taifa.

• Viwanda vilivyoahidiwa vya mbolea,plastic,cemet n.k vianze kujengwa sasa na isiwe propaganda tu ya kisiasa toka kwa viongozi kwa kuondoa dhana iliyotokea huko nyuma ya kuonekana Kusini ni ukanda wa vita usiendelezwe.

Mfano kule Kilwa Lindi ambako ahadi ya kujenga kiwanda cha mbolea kwa gesi ya Songo songo mpaka leo hakijajengwa kwa kuwapatia nafasi ya ajira na kujiajiri kutokana na viwanda hivyo

• Serikali iwe sikivu kwa kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi ambako vyanzo vya uchumi wa gesi vipo kwa kutekeleza madai yao, kwa kuwa hawapingi kupelekwa umeme gridi ya Taifa na kuuza gesi iliyochakatwa tayari kwa kuliingizia Taifa mapato.

• Serikali ikamilishe sera za gesi na mafuta na kupatikana sheria ambayo italinda mikataba yote inayofanywa na serikali juu ya gesi na kulinda wananchi wa eneo husika mikoa ya Mtwara na Lindi kwa madhara yanayotokana na gesi kwa kuwashirikisha kutoa mawazo yao.

• Mazungumzo yafanyike kati ya Serikali na wananchi katika kupata ufumbuzi wa swala la gesi kwa njia ya Amani na wala isitumie nguvu zilizonazo kwani kufanya hivyo ni kuleta maafa yasiyo ya lazima kwa Taifa.

• -Serikali isisikilize wabunge wadanganyifu ambao hawana makubaliano na wananchi katika majimbo yao wanayotoka, ambao huchochea mgogoro huu kwa lengo lao binafsi.

• Viongozi ambao wametoa matusi kwa wananchi wafute usemi wao kwa wananchi wa Mkoa wa Mtwara ambao wamewaita wahaini kwa kuwaomba radhi bila masharti yeyote kwani semi hizo huleta chuki, uhasama, na matengano katika nchi, na kusababisha nchi isitawalike.

• Serikali ya Chama Cha Mapinduzi itekeleze Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2010 Ibara 63 Kifungu H na K ambavyo vipo wazi, hasa kwa kuzingatia kuwa sera zinazotekelezwa sasa na Serikali ni zile zote zilizoandikwa kwenye Ilani ya uchaguzi.

• Serikali irudishe tumaini kwa wananchi wa Mikoa ya Kusini na amani inayoonekana kutoweka kwa matamshi yanayoashiria kumwagika kwa damu bila kujali kuwa nchi ilipatikana bila kuwaga damu.

• Serikali iwatambue wananchi wa Mikoa ya Kusini kuwa wana haki ya kutimiziwa matakwa yao kama wananchi wa mikoa mingine kwa kupata maendeleo kutokana na vyanzo vya uchumi vilivyopo katika maeneo yao.

-Sisi viongozi wa dini tunamwomba Mungu awape hekima viongozi wetu wa Serikali kwa sababu wamepewa dhamana na Mungu kuliongoza Taifa.

-Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza, bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza Methali 11:3

-Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake, bali wenye haki watapona kwa maarifa. Methali 11:9

Imesainiwa na

BISHOP C. CHILUMBA

MWENYEKITI MKOA

PAMOJA NA:-

PASTOR SELEKWA

KATIBU PCT- MKOA WA MTWARA


Nakala:

• Mwenyekiti PCT Taifa-Dar –es –Salaam

• Maaskofu na Wachungaji wote wa PCT Mkoa wa Mtwara.

 
Kiufupi hatuwa na uwezo wa kujilinda dhidi ya wahujumu uchumi! Mfano: Ni mara ngapi watu wanashindwa kuzalisha sababu za kipuuzi na bado shirika husika la umeme linatembea kifua mbele bila kuwajibika? Lets wait for serious disaster when most of our people will suffer from long effects or poor services without any hope. This is Mtwara Oil and Gas Exploration Plant, Kazi inaendelea!!

168038_191421077553308_6924903_n.jpg
 
Laiti kama tungeelewa maana halisi ya mabadiliko ya muda, pengine tungelikuwa tofauti. Kuna ukweli fulani juu ya maandamano yale ingawa sio kamili kabisa.
We need pipelines to distribute gas from Mtwara to other places. Urusi inauza gas karibu ulaya yote through pipelines. Ingawa kwenye suala la kuzalisha umeme, pengine strategically Lindi ingelifaa zaidi maana ilivyo sasa Mtwara imeelemewa mno na shughuli nzima zinazoenda na utafutaji wa gas.

Sidhani kama shinikizo la Wanamtwara ni kugomea gas isiende Dar es Salaam, bali kwanza juhudi za wadi zionekane kuwanufaisha wananchi hawa ikiwemo miradi inayokusudia kujengwa Dar es salaam ijengwe Mtwara au Lindi.
  • Ahadi ya Kikwete kipindi cha kampeni ni kuijenga bandari ya Mtwara na kujenga kinu cha kufua umeme kutokana na gas Mtwara

KAULI HII YA VIONGOZI WA DINI KWA WENYE UELEWA SERIKALI IFIKIRIE UPYA

  1. Mtwara ina Bandari yenye kina kirefu katika Afrika ya mashariki yote lakini mpaka sasa mipango ya kuiendeleza imekuwa ni kizungurumkuti. Wananchi wana taarifa kuwa mipango ya kuiendeleza Bandari ya Mtwara imepindishwa na kupelekwa Bagamoyo.
  2. Wananchi wanakumbuka kwa uchungu zao lao la biashara la muhogo ambalo serikali ya Tanzania huru imeliacha linakufa kuwa zao la biashara.
  3. Wakulima wengi wanalima mihogo mingi na wanaishia kuitupa tu baada ya kuoza maana si tu kwamba haina soko bali hata teknolojia ya kulitunza kwa muda mrefu hawana. Mashamba wanayo na wanalima kwa bidii wanavuna mihogo mingi lakini wa kumuuzia tayari serikali ilishampoteza na haina mpango wa kulifufua zao hili kama zao la biashara.
  4. Wananchi wa Mtwara na kusini kwa ujumla wana kilio cha muda mrefu cha zao la korosho na mpaka sasa serikali inababaisha tu haina mpango wowote wa kuboresha soko la zao hili. Wananchi sasa wanapomaliza kuvuna korosho zao wanaambulia vikaratasi tu na kutakiwa wasubiri pesa zao kwa muda mrefu bila kuzipata. Ingawa ni jambo liliowazi kuwa zao la korosho linachangia kiasi kikubwa tu cha fedha katika serikali. Kwa mfano, kuna takwimu zinaonesha kuwa Katika Mwaka wa Uchumi unaoishia Novemba 2012, Korosho imeliingizia Taifa jumla ya dola za Kimarekani 151 milioni sawa na shingi billion mia mbili arobaini na moja na million mia sita (TZsh241,600,000,000). Katika mwaka 2011 zao hili liliingiza dola 130 milioni sawa na bilioni mia mbili na nane (208,000,000,000) wakati Pamba iliingiza dola 53 milioni tu sawa na shingi billion themanini na nne na milioni mia nane (84,800,000,000).


  • Wananchi wa Mtwara na kusini kwa ujumla wanazidi kulia tu na kusuasua kwa ujenzi wa Barabara ya Mtwara-Lindi-Dar es Salaam. Wanazidi kuumia wanapoona ile mikoa inoyoheshimiwa na serikali ikiwa na Barabara nzuri zinazopitika tena ujenzi wake umekamilika kwa muda mfupi sana.
  • Miaka minane ya Mh. Rais Kikwete zile kilomita 60 za barabara kutoka Ndundu mpaka Somanga hazijaisha lakini gesi anataka kuiwekea bomba na mradi ukamilike kwa miezi 18.
  • Wananchi wameshuudia reli ya kusini iking'olewa bila sababu za msingi na huku ikijulikana kuwa reli ni moja ya miundombinu muhimu katika kuchochea uchumi na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Reli haikung'olewa katika mikoa ambayo serikali inaiheshimu.
  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudi mashine ya maji kitangali Newala ikiondolewa na kupelekwa Dodoma ambayo ilikuwa msaada kutoka Finland.
  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudia kiwanda cha samaki Mtwara kikiondolewa na kupelekwa Dar es Salaam.

  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudia taa za mwanga mkali za uwanja wa ndege Mtwara ziking'olewa na kupelekwa Arusha.
  • Wananchi wa Mtwara wameshuhudia mkataba wa kutumika bandari ya Mtwara na Malawi kibiashara ukipindishwa na kupelekwa Bagamoyo.
  • Wananchi wa Mtwara wamekaa na giza kwa muda mrefu na giza hilo limechangia kutokuwepo kwa kichocheo cha uchumi kwa kukosekana umeme wenye uhakika.
  • Ni hivi karibuni tu baada ya kugunduliwa gesi na kumekuwepo na nishati ya umeme ambao hautoshi kwa maana ya kumfanya mjasriamali mwenye mtaji kuweza kuwekeza Mtwara katika sekta ya viwanda. Mwenyezi Mungu anasema:-
"Kwa hakika MwenyeziMungu anaamrisha uadilifu,na kufanya ihsani,na kuwapa jamaa(na wengineo),na anakataza uchafu na uovu,na dhuluma.Anakunasihini ili mpate kufahamu(mfuate)"(Qur'an 16:90)

"Na timizeni ahadi mnazozitoa kwa jina la MwenyeziMungu mnapoahidi;wala msivunje hizo ahadi baada ya kuzithubutisha,hali mmekwisha mfanya MwenyeziMungu kuwa shahidi wenu.Hakika MwenyeziMungu anayajua yote mnayoyayafanya"(Qur'an 16:91)

Sasa ghafla, wanakutana na mpango wa kustukiza wa serikali kutaka kusafirisha gesi hiyo kwenda Dar es Salaam bila kueleza kwa nini kituo cha kufulia umeme unaotokana na gesi asilia inakopatikana gesi hiyo kisijengwe Mtwara?. Wanapojaribu kuihoji serikali wanaambulia matusi, kejeli na kupuuzwa kutoka kwa viongozi wao waliowategemea kuwatetea. Kwao wanaona ni hujuma tu wanataka kufanyiwa kama walivyofanyiwa huko nyuma na ndio maana wameamua KUFA na GESI indepo na mara hii serikali itawapuuza. Serikali imefikia upeo wa juu wa kuwapuuza wana Mtwara na WanaMtwara nao wamefikia upeo wa juu wa uvumilivu na ndio maana wanasema GESI KWANZA UHAI BAADAYE. Haya ndio mazingira halisi ambayo ndiyo KIINI cha mgogoro wa gesi Mtwara. Sio wanasiasa bali ni historia ya kudharauliwa ndio yaliyoibua mgogoro huu wa gesi kama tulivyoeleza hapo juu. WanaMtwara wana mfano wa gesi ya Songosongo inayopelekwa Dar es Salaam. Zipo taarifa zinazoelezea kwamba kodi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa asilimi 0.3 (0.3%) ilikuwa inalipwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na kampuni ya Pan Africa Energy. Ni baada ya juhudi za mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu kuingilia kati ndio kodi ikaanza kulipwa Kilwa.

TAMKO
SHURA YA MAIMAM INAUNGANA NA WANANCHI WA MIKOA YA KUSINI KUITAKA SERIKALI ISITISHE MPANGO WA KUSAFIRISHA GESI ASILIAYA MTWARA KUPELEKWA DARES-SALAAM NA BADALA YAKE MTAMBO WA KUFUA UMEME WA MEGAWATT 300 UJENGWE MTWARA KAMA ULIVYOKUSUDIWA AWALI KABLA YA USHAURI MBAYA WA TPDC KWA SERIKALI. NA KWA KUWA TUNAAMINI KUWA SERIKALI YETU NI SIKIVU ITATUSIKILIZA WANANCHI WA MIKOA HII YA KUSINI kama ilivyowasikiliza wananchi wote wa Tanzania tulipoitaka serikali kuwa na mjadala kuhusu kuandikwa kwa KATIBA MPYA ingawa msimamo wa serikali mwanzo ulisema katiba iliyopo inakidhi haja za wakati huu.
Ee ALLAH shuhudia kuwa tumefikisha na tumetekeleza wajibu wetu
.
 
Mtwara Nadhani imelaaniwa toka kitambo!!! Nipo Mtwara kwa shughuli zangu kwa zaidi ya miaka mitatu sasa but yanayoendelea ni aibu kuyasema, Kabla ya Hili la GAS Nilitaka wananchi wa Mtwara waungane na Kumng'oa KANJI BAI ambae ndo mbunge wao, hana msaada zaidi ya kutumia fulsa ya yeye kuwa mbunge kuilinda Diplomatic Passport yake, pia Kama vila la Mbunge halitoshi wakachagua KANJI BAI mwingine kuwa Mwenyekiti wa Mkoa CCM, najua nitaibua hisia za watu wasioipenda CCM hapa lakini kama unafuatilia mambo mengi ya kisiasa hapa nchi basi maamuzi mengi ya Serikali yetu hufanywa na SISIEMU kwenye vikao vyao vya NEC na Kutekelezwa na SERIKALI yake, hivyo kuwa na watu wawili ambao nathubutu kusema kuwa sio watanzania potelea mbali nikiitwa MBAGUZI lakini sio watu amabao wanaweza kuwatetea WANAMTWARA kwenye shida zao. HIVYO UKOMBOZI WA MTWARA UANZIA HAPO KWANZA NA WAKIWA NA WAWAKILISHI MAKINI BASI NAFASI YA MADAI YA MSINGI HASA HILI LA GAS BASI LIOTAWEZEKANA. INATOSHA SASA KUTAWALIWA NA WAGENI
 
Mtwara Nadhani imelaaniwa toka kitambo!!! Nipo Mtwara kwa shughuli zangu kwa zaidi ya miaka mitatu sasa but yanayoendelea ni aibu kuyasema, Kabla ya Hili la GAS Nilitaka wananchi wa Mtwara waungane na Kumng'oa KANJI BAI ambae ndo mbunge wao, hana msaada zaidi ya kutumia fulsa ya yeye kuwa mbunge kuilinda Diplomatic Passport yake, pia Kama vila la Mbunge halitoshi wakachagua KANJI BAI mwingine kuwa Mwenyekiti wa Mkoa CCM, najua nitaibua hisia za watu wasioipenda CCM hapa lakini kama unafuatilia mambo mengi ya kisiasa hapa nchi basi maamuzi mengi ya Serikali yetu hufanywa na SISIEMU kwenye vikao vyao vya NEC na Kutekelezwa na SERIKALI yake, hivyo kuwa na watu wawili ambao nathubutu kusema kuwa sio watanzania potelea mbali nikiitwa MBAGUZI lakini sio watu amabao wanaweza kuwatetea WANAMTWARA kwenye shida zao. HIVYO UKOMBOZI WA MTWARA UANZIA HAPO KWANZA NA WAKIWA NA WAWAKILISHI MAKINI BASI NAFASI YA MADAI YA MSINGI HASA HILI LA GAS BASI LIOTAWEZEKANA. INATOSHA SASA KUTAWALIWA NA WAGENI
Hao ma-KHANJ BAI unaowasema mkuu ni watu wadogo sana, Mtwara na Lindi ina mawaziri katika serikali hii ambao kama wangekuwa na uwezo wa kujenga hoja kwa maana ya kuwa na uchungu wa kimaendeleo ya kusini, sidhani kama hata hilo wazo la kusafirisha gesi kwenda Dar kama lingekuwepo. Tatizo wabunge-mawazi wetu ni mazuzu. Nafikiri sasa hivi muda umefika kwa watu wa kusini kuangalia upande wa pili wa shilingi. CCM tumekuwa nayo kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote, hata kuanza kwa miradi ya gesi na mafuta ni juhudi binafsi za ex-president Ben. Mkapa. Otherwise nawashauri wenzangu wa Mtwara tujaribu kubadilisha, wabunge wa CCM hawana faida na sisi.
 
Back
Top Bottom