Kikwete ameteleza kushinikiza gas kupelekwa Dar es Salaam

Mtwara Nadhani imelaaniwa toka kitambo!!! Nipo Mtwara kwa shughuli zangu kwa zaidi ya miaka mitatu sasa but yanayoendelea ni aibu kuyasema, Kabla ya Hili la GAS Nilitaka wananchi wa Mtwara waungane na Kumng'oa KANJI BAI ambae ndo mbunge wao, hana msaada zaidi ya kutumia fulsa ya yeye kuwa mbunge kuilinda Diplomatic Passport yake, pia Kama vila la Mbunge halitoshi wakachagua KANJI BAI mwingine kuwa Mwenyekiti wa Mkoa CCM, najua nitaibua hisia za watu wasioipenda CCM hapa lakini kama unafuatilia mambo mengi ya kisiasa hapa nchi basi maamuzi mengi ya Serikali yetu hufanywa na SISIEMU kwenye vikao vyao vya NEC na Kutekelezwa na SERIKALI yake, hivyo kuwa na watu wawili ambao nathubutu kusema kuwa sio watanzania potelea mbali nikiitwa MBAGUZI lakini sio watu amabao wanaweza kuwatetea WANAMTWARA kwenye shida zao. HIVYO UKOMBOZI WA MTWARA UANZIA HAPO KWANZA NA WAKIWA NA WAWAKILISHI MAKINI BASI NAFASI YA MADAI YA MSINGI HASA HILI LA GAS BASI LIOTAWEZEKANA. INATOSHA SASA KUTAWALIWA NA WAGENI

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Mataifa Mheshimiwa Bernard Membe,
Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe, kuna wengine wengi mashuhuri kama akina Anna Abdalah, na mwingine mbunge wa siku nyingi alisimamia uchaguzi wa Speaker kule Dodoma.

Wapo akina Mkapa na wengineo lakini hakuna jitihada za kukumbuka kutetea ukanda wao si kwa upendeleo bali kutetea wananchi wanufaike na malighafi zipatikanazo huko.

Kinachoendelea ni sawa na wazungu wanavyokazania kukomba madini nchini na kutoroshea kwao sisi tumelala usingizi tu.

Wabunge wa huko kusini wajue Charity begins at home.

Filikunjombe amepigania Ludewa yake madini yachimbuliwe na viwanda vya kuyafinyanga vyuma vijengwe huko sambamba na plant ya umeme itakayoendeshwa na makaa ya mawe, kwa nini isiwe hivyo Mtwara?
 
Please elewa mada, viwanda vilivyoko Esseni ni vile vinavyotokana na machimbo ya madini yaliyokuwa yanapatikana huko, haina maana eneo jingine la Ujerumani halina viwanda. Madini kama chuma na makaa ya mawe yaliyokuwa yanapatikana hapo yalichochea uanzishwaji wa viwanda hivyo.

Kumbuka viwanda katika nchi za magharibi havifanyi kila kitu kwa sababu ya mfumo wa industrialization, process za awali hufanyika zinakopatikana raw material na kisha products husafirishwa kulisha viwanda vingine. Essen ilikuwa ni viwanda vya ku-process raw material na products zake zilipelekwa kwenye viwanda vingine. Hawakusafirisha mabongo ya madini ya chuma yaliyochimbuliwa ardhini kupelekwa huko unakosema ila processed products.
acha chokochoko za kuchochea watu wasusie juhudi za serikali kutumia rasilimali zile ulichoandika hapa hakina hata chembe ya uchumi zaidi ya ubinafsi mipango iliyoweka haimaanishi kwamba Mtwara hakutakuwa na viwanda vya bidhaa za gesi au zitokanazo na gesi, bali ukweli ni bomba lile litafungua milango ya uchumi kwa nchi nzima na litasafirisha kiasi tu cha gesi yoote iliyopo Mtwara, tuache majungu! Huko Essen unayoiongelea hakuna tofauti na Mtwara itakavyokuwa maana viwanda gesi vitakuwepo na bomba la gesi litajengwa kama vile Essen makaa ya mawe yapo na pia magari na bidhaa za chuma yanaundwa katika majimbo mengine ya Ujerumani. Huu ndio ukweli...
 
Mtazamo wa CCM ni kuwa Dar wanaishi wenye heri na malaika, 'mikoani' wanaishi mashetani, washenzi na wapuuzi
 
acha chokochoko za kuchochea watu wasusie juhudi za serikali kutumia rasilimali zile ulichoandika hapa hakina hata chembe ya uchumi zaidi ya ubinafsi mipango iliyoweka haimaanishi kwamba Mtwara hakutakuwa na viwanda vya bidhaa za gesi au zitokanazo na gesi, bali ukweli ni bomba lile litafungua milango ya uchumi kwa nchi nzima na litasafirisha kiasi tu cha gesi yoote iliyopo Mtwara, tuache majungu! Huko Essen unayoiongelea hakuna tofauti na Mtwara itakavyokuwa maana viwanda gesi vitakuwepo na bomba la gesi litajengwa kama vile Essen makaa ya mawe yapo na pia magari na bidhaa za chuma yanaundwa katika majimbo mengine ya Ujerumani. Huu ndio ukweli...


Kwa nini vinu vya kufua umeme visijengwe mwara ili umeme uanzie kunufaisha viwanda kule na nirahisi kuuvuta umeme toka Mtwara kuunganisha na grid ya taifa kuliko gasi iende Dar es Salaam halafu ufue umeme, lini umeme utafika Mtwara na Lindi. Acheni usanii, kizazi cha leo hatudanganyiki kamwe.
 
president-jakaya-kikwete.jpg

rais kikwete kutoguswa na shinikizo la maandamano ya wananchi wa mtwara kuhusu usafirishaji wa bomba la gas kwenda dar es slaam ni kutokuangalia kwa makini mambo ya msingi kwa mtazamo wa kiuchumi, usalama wa mradi na uwiano wa maendeleo kitaifa.

usalama:

  • ulimwengu wa leo wakati unakabiliwa na hatari ya maadui wenye kuharibu miundo mbinu sina hakika usalama wa bomba hilo la gas usalama wake toka mtwara hadi dar, kwani pamoja na umuhimu wake, kunaweza kutokea hujuma kubwa katika bomba hili kutokana na umbali huo, wakati vinu vya kufua umeme vingewezekana kujengwa eneo ambalo maliasili inapatikana.

  • hatari kubwa electric power plant kuwa sehemu moja, hujuma ikifanyika, au itokeapo vita shabaha moja italitia taifa zima gizani. Muhimu electric power plants zikawa sehemu mbalimbali na grid network power iunganishwe. Ukikatwa umeme dar es salaam basi nchi nzima gizani.
  • ndege moja tu inatosha kudondosha bomu moja ubungo na lingine kinyerezi kisha taifa zima likawa gizani mara moja, no alternative, tutaonekana si watu wa kuona mbali. Ukaribu uliopo ubungo na kinyerezi vigumu kupata muda wa papo kwa papo emergency respond.

kiuchumi:
ujenzi wa vinu vya kufua umeme karibu na eneo inakopatikana rasilimali ni bora na inapunguza gharama nyingi. Litakapotokea tatizo la gas kutofika kwa kiwango kinachotakiwa toka mtwara kuna ziada ya kuhangaika kutafuta uvujaji uliko kwa umbali mkubwa toka dar hadi mtwara, jambo ambalo linaweza kusababisha uhaba wa umeme kwa muda mrefu.

Ukuzaji wa bandari ya mwara kwa uanzishwaji wa viwanda huko papo kuunganisha ukanda wa kusini na ukanda wa kusini nyanda za juu kunakopatikana makaa ya mawe na chuma kutaongeza msisimko wa maendeleo zaidi wakati wachina wanampango wa kujenga reli toka mkoa mpya wa njombe hadi mtwara. Uanzishwaji viwanda mikoa ya ruvuma, njombe, lindi na mtwara ni muhimu kutokana rasilimali nyingi kupatikana eneo hili.

Wanaosoma jiografia, mtakumbuka eneo la essen nchini ujerumani lilivyo na viwanda vizito tokana na upatikanaji wa maliasili huko, wajerumani hawakujenga miundo mbinu ya kuhamishia maliasili iende berlin na kwengineko kwani kufanya hivyo kungekuwa na athari zaidi kiutendaji, kiuchumi na kiusalama pia, hali kadhalika kusahaulika wananchi wanaoishi maeneo inakopatikana maliasili.

uwiano wa maendeleo
uwiano wa maendeleo kitaifa ni jambo linalotakiwa kutiliwa maanani, kwani kushinikiza gasi ipelekwe dar es salaam kwa mahitaji ya nchini nzima si vema kwani ni kuongeza zaidi msongamano wa viwanda jijini dar es salaam hatari ya uchafuzi wa mazingira na hali ya hewa na papo kuzidi kuongeza mmiminiko wa watu kutafuta ajira huko badala ya kuanzishwa viwanda eneo la maliasili ili kuvutia watu wabaki huko kwa vile ajira ipo eneo lao.

Pamoja na kwamba uwiano wa maendeleo si rahisi kuwa sawa, lakini kuna sababu za msingi kutumia vyanzo vya rasilimali za mahali zinakopatikana kusaidia kuleta maendeleo kwa kuanzisha kwa makusudi miradi ya maendeleo kama uanzishwaji wa viwanda. Hatuhitaji machinga kuendelea kumiminika dar es salaam kwani wanachofuata ni hali njema ya maisha na ajira. Lakini ukishaweka mtego wa ajira na vivutio vingine kama hali nzuri ya umeme, viwanda nk hawatakuwa na sababu ya kuja dar kwa vile wanachofuata dar kinapatikana kwao.

Tutakuwa tumekuwa na mtazamo finyu kama tutakubaliana na kauli ya mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano kwamba kwa sababu dar es salaam wanaota mapato makubwa ya kodi kwa kulisha nchini nzima basi iwe hoja ya kupeleka rasilimali pale. Nakumbuka hayati nyerere aliamua kiwanda cha spm mgolole, mufindi karibu na makambako kijengwe huko badala ya kusafirisha magogo kwa tazara kuja kutengeneza karatasi dar es salaam. Gharama nyingi ziliepukika na pia ajira ilipatikana sehemu hilo badala ya watu wa huko kulazimika kuja dar kupata ajira.

Tungetazamia wabunge wangeanzisha mjadala wa jambo hili kuishinikiza serikali kusitisha mpango huu kwani hoja ya kuwauzia mitungi ya gas wananchi wa mtwara si ufumbuzi wa ajira na mendeleo, bali ujenzi wa viwanda vitakavyoendeshwa au kuzalisha gas na pia ujenzi wa vinu vya kufua umeme huko kutawanufaisha zaidi wananchi, taifa, na pia kuondolea taifa msongo wa ukuaji jiji la dar es salaam.




safi sana mkuuu

i second you
hata hivo gesi kutoka huku kazi itakua si ndogo hata kama watatumia jwtz kuilinda miundombinu hiyo
 
Kwani gas hikibaki mtwara alaf vikajengwa viwanda na mitambo ya kuzalisha nishati huko huko alaf nishati hiyo ikasafirishwa kutokea huko kutakuwa na tatizo gani?
 
Nadhani hawa jamaa they have genuine concern kuhusu hii gesi, wameangalia maeneo mengi tu nchini ambayo kuna natural resources kibao lakini wananchi maeneo hayo hakuna faida yeyote wanayopata, cha muhimu hapa ni government kukaa nao and address their concerns!
 
Kwani gas hikibaki mtwara alaf vikajengwa viwanda na mitambo ya kuzalisha nishati huko huko alaf nishati hiyo ikasafirishwa kutokea huko kutakuwa na tatizo gani?

Hilo ndilo wanalotaka wananchi wa Mtwara. Hata kama bomba la gas litajengwa kwenda Dar es Salaam, viwanda vikubwa kama vinu vya kufua umeme vijengwe Mtwara kuvutia viwanda vingine vya uzalishaji.

Miaka yote hii tangu uhuru umeme toka grid ya taifa haujavutwa kwenda Mtwara na Lindi. Kupatikana kwa gas yenye uwezo wa kuendeshea mitambo ya umeme ingekuwa faraja kwa mikoa ya kusini nao kuanza kuondokana na giza, lakini wapi wanavutia Mkoa wa Pwani na Dar, kupeleka umeme Mtwara itabaki tu mipango ya kwenye makaratasi.
 
acha kutudanganya viwanda vingi Ujerumani vipo Baden Wurtemberg na si Essen! Na jaribu kutueleza ukweli hicho kiwanda cha Mgololo kipo wapi sasa? Hizi akili za kuharibu miundo mbinu ni za watu wenye utovu wa mawazo gesei itaenda Dar na manufaa yake yatakuwa makubwa zaidi hatuwezi kusema tuhamishe viwanda huko wakati gesi inaweza kufika viwanda vilipo.

Jina lenyewe GEZA ULOLE!!! Si ndio wale wale wa Bagamoyo, eti?
 
Kwa nini vinu vya kufua umeme visijengwe mwara ili umeme uanzie kunufaisha viwanda kule na nirahisi kuuvuta umeme toka Mtwara kuunganisha na grid ya taifa kuliko gasi iende Dar es Salaam halafu ufue umeme, lini umeme utafika Mtwara na Lindi. Acheni usanii, kizazi cha leo hatudanganyiki kamwe.

gesi inaitaji gas heating electrical generators ambazo tayari zipo Dar na hata zinazojengwa zinawekwa karibu na Dar kurahisisha usafirishaji wa umeme mwingi karibu na viwanda kujenga grid ya kusafirisha umeme wa 700 MW ni gharama haswa kama kuna njia mbadala ya kuziepuka yaani kusafirisha gesi kwa generator za kuzalisha umeme pia kwa viwanda vya bidhaa za gesi kama plastic industries. Acha ubinafsi mzee, viwanda vingi vya nchi vilikufa kwa sababu ya mawazo kama yako! Kama ingekuwa hivi viwand vya mashine zote za kutumia mafuta vingekuwa middle east basi kwa vile wana mafuta, akili za matope hizi! :becky::becky:
 
gesi inaitaji gas heating electrical generators ambazo tayari zipo Dar na hata zinazojengwa zinawekwa karibu na Dar kurahisisha usafirishaji wa umeme mwingi karibu na viwanda kujenga grid ya kusafirisha umeme wa 700 MW ni gharama haswa kama kuna njia mbadala ya kuziepuka yaani kusafirisha gesi kwa generator za kuzalisha umeme pia kwa viwanda vya bidhaa za gesi kama plastic industries. Acha ubinafsi mzee, viwanda vingi vya nchi vilikufa kwa sababu ya mawazo kama yako! Kama ingekuwa hivi viwand vya mashine zote za kutumia mafuta vingekuwa middle east basi kwa vile wana mafuta, akili za matope hizi! :becky::becky:

Kama umeishiwa hoja tuachie wastaarabu majadiliano, matusi si sera ya great thinkers wa JF. Respect your self, JF members you gona be great thinker. Kuporomosha matusi si jadi yetu JF, hapa kisima cha busara.
 
Umeandika vyema lakini fanya utafiti wa kutosha utakuwa na maoni zaidi mfano:
1)Je wajua kuwa LNG Plant itajengwa kati ya Mtwara au Lindi?
2)Je wajua kuwa gesi inayoletwa Dar ambayo ndiko kwenye miundo mbinu ya uzalishaji umeme inatoka kwenye visima vichache tu vya onshore? Umesikia karibuni kuhusu uwezekano wa kuongezeka gharama za umeme? Kujenga miundombinu Mtwara huoni kuwa kuna kikwazo cha muda na fedha wakati kuna miundombinu ya IPTL ambayo yaweza kuwa suluhisho sahihi kwa nyakati hizi?
3)Je wajua kuwa DAngote inaanza ujenzi wa kiwanda chao 2013, project hii inaprospect ya kuajiri maelfu, pamoja na kiwand cha mbolea ambacho kitakuwa huku kusini?
4)Usalama, kwa akili ya haraka tu kuweka kila kitu sehemu moja huoni kuna risk hapo?
5)Je wajua kuwa bandari ya mtwara itapanuliwa kwa ajili ya gesi na bulk exportation cargo?

Maswali haya yanajaribu kufungua mjadala wa kufikiri kwa mapana zaidi....tusikurupuke kutetea matatizo
 
Kama umeishiwa hoja tuachie wastaarabu majadiliano, matusi si sera ya great thinkers wa JF. Respect your self, JF members you gona be great thinker. Kuporomosha matusi si jadi yetu JF, hapa kisima cha busara.
Hamna tusi hapo ubinafsi si tusi bali hulka na mawazo yako yana chechembe hizo maana kwa mwenendo wako huu taifa linaweza meguka na akili matope ni akili inayoshindwa kufikiri kutokana na ukweli wa mambo (kifupi lazy thinking). Samahani kama nimekuudhi ila hata wewe uandishi wako una uchochezi na vitisho huwezi kutumia masuala kama vita au ugaidi kulazimisha viwanda vya umeme viwe Mtwara bila ya kuangalia ukweli
 
Umeandika vyema lakini fanya utafiti wa kutosha utakuwa na maoni zaidi mfano:
1)Je wajua kuwa LNG Plant itajengwa kati ya Mtwara au Lindi?
2)Je wajua kuwa gesi inayoletwa Dar ambayo ndiko kwenye miundo mbinu ya uzalishaji umeme inatoka kwenye visima vichache tu vya onshore? Umesikia karibuni kuhusu uwezekano wa kuongezeka gharama za umeme? Kujenga miundombinu Mtwara huoni kuwa kuna kikwazo cha muda na fedha wakati kuna miundombinu ya IPTL ambayo yaweza kuwa suluhisho sahihi kwa nyakati hizi?
3)Je wajua kuwa DAngote inaanza ujenzi wa kiwanda chao 2013, project hii inaprospect ya kuajiri maelfu, pamoja na kiwand cha mbolea ambacho kitakuwa huku kusini?
4)Usalama, kwa akili ya haraka tu kuweka kila kitu sehemu moja huoni kuna risk hapo?
5)Je wajua kuwa bandari ya mtwara itapanuliwa kwa ajili ya gesi na bulk exportation cargo?

Maswali haya yanajaribu kufungua mjadala wa kufikiri kwa mapana zaidi....tusikurupuke kutetea matatizo

Naona katika maswali yako yana kitu cha kufikiria pande zote. Ndio maana binafsi sioni kama kuleta bomba Dar es Salaamu ni tatizo, lakini ninachofikiria kutegemea mitambo ya kukodi ya IPTL si suluhisho la kudumu kwani itakuwa ni zima moto tu. Bora kungekuwa na mipango ya kuagiza mitambo yetu wenyewe hata kama itakuwa ni mipango itakayochukua zaidi ya mwaka kwani kitu kuwa kitu chetu.

Nipe muda kidogo nitalijadili hili, umeleta hoja za msingi ambazo nahitaji kuzifanyia kazi.
 
Kuna kitu bado sielewi kwenye hili swala mkuu Candid Scope, kwani hiyo GAS Mtwara haitumiki inaletwa yote DAR?. Nadhani kuleta Dar siyo tatizo, maana haizuii investment kufanyika huko Mtwara pia ili ku-maximize matumizi yake.
 
Mawazo ya Geza Ulole ni sawa na jamaa ambao bado wanaamini viwanda vyote lazima viwe Pugu road, na ambao wanaamini kuwa kila kitu na maendeleo ya kila jambo lazima yawe Dar es salaam na kama yatafanyika kwingine basi itakuwa ni laana na dhambi kubwa, wamekariri, Dar es salaam imechoka na imejaa inatakiwa kupuguziwa mzigo, hivi Mtwara au Lindi hakuna bandari, hakuna uwanja wa ndege au barabara? ambako bidhaa zinaweza safirishwa kirahisi kwenye SADC? Hivi gharama ya kusafirisha hio gesi nadhani inaweza kuwa half the price ya kujenga plant ya umeme ambao utasambazwa southern corridor hadi Malawi na kwingineko? hio gesi haiwezi kuwa exported to abroad via bandari ya Mtwara na Lindi?

Please elewa mada, viwanda vilivyoko Esseni ni vile vinavyotokana na machimbo ya madini yaliyokuwa yanapatikana huko, haina maana eneo jingine la Ujerumani halina viwanda. Madini kama chuma na makaa ya mawe yaliyokuwa yanapatikana hapo yalichochea uanzishwaji wa viwanda hivyo.

Kumbuka viwanda katika nchi za magharibi havifanyi kila kitu kwa sababu ya mfumo wa industrialization, process za awali hufanyika zinakopatikana raw material na kisha products husafirishwa kulisha viwanda vingine. Essen ilikuwa ni viwanda vya ku-process raw material na products zake zilipelekwa kwenye viwanda vingine. Hawakusafirisha mabongo ya madini ya chuma yaliyochimbuliwa ardhini kupelekwa huko unakosema ila processed products.
 
KIla kitu Bagamoyo! Si mnakumbuka mshikemshike wa kuhamisha makao makuu ya Hifadhi ya Saadan ilivyo leta tibwilitibwili na wazee wa Pangani kipindi kile? Kwamba yahamie wilaya ya Bagamoyo!!!!??? Na wazee wa Pangani wakatia mpira kwapani.

Kusini komaeni. Msimuangalie shemeji usoni, bhaa!!!!!

Mkuu hii mpya unaweza ukaianzishia uzi na kuifafanua kiundani?
 
Umeandika vyema lakini fanya utafiti wa kutosha utakuwa na maoni zaidi mfano:
1)Je wajua kuwa LNG Plant itajengwa kati ya Mtwara au Lindi?
2)Je wajua kuwa gesi inayoletwa Dar ambayo ndiko kwenye miundo mbinu ya uzalishaji umeme inatoka kwenye visima vichache tu vya onshore? Umesikia karibuni kuhusu uwezekano wa kuongezeka gharama za umeme? Kujenga miundombinu Mtwara huoni kuwa kuna kikwazo cha muda na fedha wakati kuna miundombinu ya IPTL ambayo yaweza kuwa suluhisho sahihi kwa nyakati hizi?
3)Je wajua kuwa DAngote inaanza ujenzi wa kiwanda chao 2013, project hii inaprospect ya kuajiri maelfu, pamoja na kiwand cha mbolea ambacho kitakuwa huku kusini?
4)Usalama, kwa akili ya haraka tu kuweka kila kitu sehemu moja huoni kuna risk hapo?
5)Je wajua kuwa bandari ya mtwara itapanuliwa kwa ajili ya gesi na bulk exportation cargo?

Maswali haya yanajaribu kufungua mjadala wa kufikiri kwa mapana zaidi....tusikurupuke kutetea matatizo

Mkuu,
ninakubaliana na wewe, Serikali na wanasiasa inabidi wabebe lawama katika hili.

Haya yote yanatokea kwa sababu ya wanachi kutokuwa na information zenye ukweli na pia jamii kutokufanya juhudi ya kupata information zilizo za kweli. Kutokana na haya, hata hitimisho katika fikra kama hizi zilizoletwa hapa zinakuwa hazina ukweli au zinakuwa na nusu ukweli.

Kama wananchi wa mtwara wangeelezwa na wanasiasa na serikali nini kinachofanyika na kile kitakachofanyika na sababu za kufanya hivyo, nafikiri kusingekuwa na mawazo kama haya yanayoonekana kuuungwa mkono na jamii ambayo haijasikia upande wa pili ukitoa sababu zote za kufanya hivyo.
 
Nilishawai kusoma kitabu cha mfalme jua nikacheka sana na kusema hakuna mtu anayeweza kufanya maaamuzi kama aliyefanya mfalme jua. Hata hivyo pia mwaka 2007 nilisoma aticle moja ya mwanasayansi mmoja wa kimalekani ambaye ni mmoja wa wagunduzi ambaye alifanya risechi yake mwenyewa akagundua ubongo wa mtu mweusi (africa) unamatatizo katika maswala ya kufikiri kuliko mtu mweupe (mzungu). Kwangu mimi nilipinga na sasa naelekea kukubali.

Ndugu zangu tuseme ukweli mimi nipo dar kweli huwa naogopa napopita ubungo power plant sikuzote, huwa nawaza siku moja pakipata itarafu sijui maisha ya watu wa ubungo watakuwaje?, pili wakati watu wanaomba ubungo power plant iamishwe iende mbali na makazi ya watu, serekari inaongeza mradi mwingine kutoka mtwara ambao nio mkubwa katika historia ya umeme tanzania.
Kama serikari inaona sawa kufanya hivyo tusubili hiyo siku ya kiama itakapo fikia watu wa ubungo. Poleni wakazi wa mtwara hii sio tanzania bali ni tanzagiza.
 
Back
Top Bottom