MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,090
- 22,370
Mwaka 2015 nilipata Admission ya kwenda kusoma Masters kwenye ujasiriamali pale UDSM. Nilishapokea maelekezo yote ikabakia kulipa tu ada. Nilivyojicheki nikaona hadi wakati ule nilikuwa nina pesa ya kulipa ada na gharama zingine kwa mwaka mmoja tu. Hata kama Masters sio muda mrefu bado pesa ingepelea. Baada ya tafakuri nzito nikaamua niahirishe chuo na kuwekeza pesa yote kwenye biashara. Huo ulikuwa mojawapo ya maamuzi bora kabisa niliyowahi kufanya kwenye maisha yangu.
Ninaandika huu uzi baada ya kuona vijana wengi wakikosa utulivu kwenye haya mambo ya kujisomesha. Kijana uliyemaliza form six au form four na ukawa huna msaada wowote wa kupata pesa za kwenda chuo ni bora kupambana kwanza kutengeneza hela kupitia shughuli yoyote ya halali iliyoko mbele yako badala ya kujipanikisha kutafuta ada ambayo pia hata ukiipata unaweza kujikuta unasoma kwa taabu sana. Wengine wamefikia hatua ya kuomba omba watu pesa. Ninashauri kiasi chochote utakachokipata kwenye mihangaiko yako usikimbilie kulipa ada. Chukua hicho kiasi kizungushe. Mambo yakiwa sawa utasoma baadae.
Kuna watu wanaoweza sema kwamba biashara sio ya kila mtu. Hii sio kweli. Biashara haina mwenyewe. Ni kama vile tunavyoenda shule ambako hata kama wewe ni kipanga lazima kuna wakati unafeli hata zile monthly tests. Sio kwamba utafaulu tu kirahisi. Kwenye biashara nako ni hivyohivyo. Juhudi na kujituma ndo muhimu. Sisi wote kwenye biashara ni kama wanafunzi yaani kila siku tunajifunza na kupitia mambo mengi.
Itakuwa haina maana kijana umepambana ukapata milioni 5 kisha ukaipeleka yote shule ambapo baada ya miaka mitatu unarudi mtaani kuanza upya. Hiyo 5m ungeizungusha ungekuwa mbali kwa miaka 3.
NB: Mimi naheshimu mno elimu ila pia nauchukia sana umaskini. Kwa dunia ya leo unaweza kusoma kimaskini na bado ukarudi kitaa na kuendelea kuwa maskini. Umakini unahitajika
Ninaandika huu uzi baada ya kuona vijana wengi wakikosa utulivu kwenye haya mambo ya kujisomesha. Kijana uliyemaliza form six au form four na ukawa huna msaada wowote wa kupata pesa za kwenda chuo ni bora kupambana kwanza kutengeneza hela kupitia shughuli yoyote ya halali iliyoko mbele yako badala ya kujipanikisha kutafuta ada ambayo pia hata ukiipata unaweza kujikuta unasoma kwa taabu sana. Wengine wamefikia hatua ya kuomba omba watu pesa. Ninashauri kiasi chochote utakachokipata kwenye mihangaiko yako usikimbilie kulipa ada. Chukua hicho kiasi kizungushe. Mambo yakiwa sawa utasoma baadae.
Kuna watu wanaoweza sema kwamba biashara sio ya kila mtu. Hii sio kweli. Biashara haina mwenyewe. Ni kama vile tunavyoenda shule ambako hata kama wewe ni kipanga lazima kuna wakati unafeli hata zile monthly tests. Sio kwamba utafaulu tu kirahisi. Kwenye biashara nako ni hivyohivyo. Juhudi na kujituma ndo muhimu. Sisi wote kwenye biashara ni kama wanafunzi yaani kila siku tunajifunza na kupitia mambo mengi.
Itakuwa haina maana kijana umepambana ukapata milioni 5 kisha ukaipeleka yote shule ambapo baada ya miaka mitatu unarudi mtaani kuanza upya. Hiyo 5m ungeizungusha ungekuwa mbali kwa miaka 3.
NB: Mimi naheshimu mno elimu ila pia nauchukia sana umaskini. Kwa dunia ya leo unaweza kusoma kimaskini na bado ukarudi kitaa na kuendelea kuwa maskini. Umakini unahitajika