Le Grand Alexei
Senior Member
- Nov 9, 2011
- 116
- 83
Kucheleweshwa vitabu vya bajeti: Kigwangalla Agomea Kujadili Bajeti Kwny Kamati! : Dr. Hamisi Kigwangalla's Round Table Kucheleweshwa vitabu vya bajeti: Kigwangalla Agomea Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati! : Dr. Hamisi Kigwangalla's Round Table # 5 mins ago
Kumekuwa na mwenendo mbovu wa kuchelewesha nyaraka muhimu za bajeti ya serikali kwenye kamati kuanzia mwaka wa fedha unaoisha. Mwaka jana vitabu vya bajeti viligawiwa kwa wabunge wiki mbili kabla ya Bunge kuanza, kwa maana nyingine katika kipindi cha kamati kujadili na kuandaa mapendekezo kwa Bunge, kwa maana hiyo wabunge walipewa vitabu leo na kesho wakatakiwa kuanza kujadili na kutoa mapendekezo yao. Mwaka jana baadhi ya kamati ziligoma na hivyo kusababisha Spika kuitaka serikali isirudie kuchelewesha tena namna hiyo. Mwaka huu, hali ni mbaya zaidi; kamati zimepewa vitabu mwisho wa wiki ya kwanza (kati ya mbili) ya kamati. Hali hii ni kinyume na utaratibu wa kikanuni wa Bunge ambapo ingepaswa wabunge wapewe vitabu vya bajeti wiki tatu (siku 21) kabla ya tarehe ya kuanza Bunge Dodoma. Kwa maana hiyo wabunge wangekuwa wamepewa vitabu si chini ya siku saba kabla ya kuanza kwa kamati (Ukizingatia kamati hukutana wiki 2 kabla ya Bunge kuanza). Hii ingewawezesha kusoma kwa umakini na kuandaa mapendekezo ya mabadiliko ama ushauri kwenye bajeti hiyo kwa ufanisi unaopaswa.
Kwa kucheleweshewa vitabu kiasi hiki na kwa kuzingatia ukubwa na wingi wa mavitabu haya ya bajeti ni dhahiri hakuna Mbunge mwenye spidi na uwezo wa kuisoma, kuimaliza na kuichambua bajeti hii kwa ufanisi na tija inayostahiki. Kwa maana hiyo wabunge, ambao ni jicho la wananchi kwenye bajeti na utendaji kazi wa serikali, wamenyimwa fursa ya kufanya kazi yao ipasavyo na hivyo wanalipua lipua ili mradi liende tu! Uchunguzi wangu umegundua kuwa haya yamekuwa ni mazoea. Hii inaonesha ni kwa jinsi gani mhimili wa Bunge ulivyokandamizwa na mhimili wa serikali (executive) na inaaakisi maovu na uvundo uliokuwepo kwenye serikali kwa muda mrefu bila kurekebishwa ipasavyo; kumbe ni kwa sababu mhimili Bunge ulikuwa usingizini kwa muda mrefu. Kama hii ni kwa maksudi ili kupunguza kelele na kupitisha bajeti kwa urahisi ama ni bahati mbaya nimeshindwa kuelewa, japokuwa kwa kiasi kikubwa ni harufu ya hila na inda inayotawala hali hii.
Mimi nimeshindwa kuelewa wenzangu wanawezaje kujadili bajeti hizi bila kusoma!
Ili kuweka wazi suala hili, na ili kuishinikiza serikali na viongozi wa Bunge kuona umuhimu wa kuwahisha vitabu ili kutoa fursa kwa wawakilishi wa wananchi kujadili bajeti kwa ufanisi na tija inayostahili, nimeamua kugoma kujadili bajeti katika ngazi ya kamati na badala yake nitajadili katika ngazi ya Bunge zima nitakapokuwa nimesoma na kuridhika kwamba ninapitisha kitu ninachokielewa. Nawashauri wabunge wenzangu waniunge mkono ili muda wa kujadili bajeti hizi katika ngazi ya kamati usogezwe mbele kwa wiki walau moja ili kutoa fursa ya kufanya kazi ya uhakika bila kulipua.
Naelewa kuna sababu nyingi zinatolewa, kuwa eti re-shuffle ya mawaziri imesababisha kuchelewa, sawa, lakini hatuwezi ku-compromise ubora wa kazi nyeti kama kupitisha bajeti bila kutoa fursa ya kutosha kwa wabunge kujadili, kuchambua na kushauri ipasavyo.
Tamko hili limetolewa na Dkt. Hamisi Kigwangalla (MB), Nzega.
Kumekuwa na mwenendo mbovu wa kuchelewesha nyaraka muhimu za bajeti ya serikali kwenye kamati kuanzia mwaka wa fedha unaoisha. Mwaka jana vitabu vya bajeti viligawiwa kwa wabunge wiki mbili kabla ya Bunge kuanza, kwa maana nyingine katika kipindi cha kamati kujadili na kuandaa mapendekezo kwa Bunge, kwa maana hiyo wabunge walipewa vitabu leo na kesho wakatakiwa kuanza kujadili na kutoa mapendekezo yao. Mwaka jana baadhi ya kamati ziligoma na hivyo kusababisha Spika kuitaka serikali isirudie kuchelewesha tena namna hiyo. Mwaka huu, hali ni mbaya zaidi; kamati zimepewa vitabu mwisho wa wiki ya kwanza (kati ya mbili) ya kamati. Hali hii ni kinyume na utaratibu wa kikanuni wa Bunge ambapo ingepaswa wabunge wapewe vitabu vya bajeti wiki tatu (siku 21) kabla ya tarehe ya kuanza Bunge Dodoma. Kwa maana hiyo wabunge wangekuwa wamepewa vitabu si chini ya siku saba kabla ya kuanza kwa kamati (Ukizingatia kamati hukutana wiki 2 kabla ya Bunge kuanza). Hii ingewawezesha kusoma kwa umakini na kuandaa mapendekezo ya mabadiliko ama ushauri kwenye bajeti hiyo kwa ufanisi unaopaswa.
Kwa kucheleweshewa vitabu kiasi hiki na kwa kuzingatia ukubwa na wingi wa mavitabu haya ya bajeti ni dhahiri hakuna Mbunge mwenye spidi na uwezo wa kuisoma, kuimaliza na kuichambua bajeti hii kwa ufanisi na tija inayostahiki. Kwa maana hiyo wabunge, ambao ni jicho la wananchi kwenye bajeti na utendaji kazi wa serikali, wamenyimwa fursa ya kufanya kazi yao ipasavyo na hivyo wanalipua lipua ili mradi liende tu! Uchunguzi wangu umegundua kuwa haya yamekuwa ni mazoea. Hii inaonesha ni kwa jinsi gani mhimili wa Bunge ulivyokandamizwa na mhimili wa serikali (executive) na inaaakisi maovu na uvundo uliokuwepo kwenye serikali kwa muda mrefu bila kurekebishwa ipasavyo; kumbe ni kwa sababu mhimili Bunge ulikuwa usingizini kwa muda mrefu. Kama hii ni kwa maksudi ili kupunguza kelele na kupitisha bajeti kwa urahisi ama ni bahati mbaya nimeshindwa kuelewa, japokuwa kwa kiasi kikubwa ni harufu ya hila na inda inayotawala hali hii.
Mimi nimeshindwa kuelewa wenzangu wanawezaje kujadili bajeti hizi bila kusoma!
Ili kuweka wazi suala hili, na ili kuishinikiza serikali na viongozi wa Bunge kuona umuhimu wa kuwahisha vitabu ili kutoa fursa kwa wawakilishi wa wananchi kujadili bajeti kwa ufanisi na tija inayostahili, nimeamua kugoma kujadili bajeti katika ngazi ya kamati na badala yake nitajadili katika ngazi ya Bunge zima nitakapokuwa nimesoma na kuridhika kwamba ninapitisha kitu ninachokielewa. Nawashauri wabunge wenzangu waniunge mkono ili muda wa kujadili bajeti hizi katika ngazi ya kamati usogezwe mbele kwa wiki walau moja ili kutoa fursa ya kufanya kazi ya uhakika bila kulipua.
Naelewa kuna sababu nyingi zinatolewa, kuwa eti re-shuffle ya mawaziri imesababisha kuchelewa, sawa, lakini hatuwezi ku-compromise ubora wa kazi nyeti kama kupitisha bajeti bila kutoa fursa ya kutosha kwa wabunge kujadili, kuchambua na kushauri ipasavyo.
Tamko hili limetolewa na Dkt. Hamisi Kigwangalla (MB), Nzega.