Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,815
- 11,991
Mgogoro wa ardhi ambao umekuwa ukiendelea kwa muda umesababisha Kanisa Katoliki Jimbo la Kigoma kuamua peleka Mahakamani mashitaka dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Shitaka hilo lililofunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma, Kanisa limewashtaki Bodi ya Wadhamini wa CCM, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halmashauri ya Uvinza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuchukua eneo lao wanalodai kulimiliki tangu Mwaka 1920.
Wamewasilisha shitaka hilo chini ya hati ya dharura na yamepangwa kusikilizwa mbele ya Jaji Lameck Mlacha.
Askofu Joseph Mlola wa Jimbo Katoliki la Kigoma
Waombaji katika shauri hilo wanadai mjibu maombi namba mbili Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Halmashauri ya Uvinza wamepanga kuchukua eneo lao kuwapa CCM bila ridhaa yao kwa ajili ya kujenga madarasa ya Shule ya Sekondari ya Chumvi.
Kupitia kwa Method R.G Kabuguzi ambaye ni Wakili wa Kujitegemea, Kanisa linaomba Mahakama izuie kwa muda uendelezwaji wa eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 39.6 hadi shauri la msingi litakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.
Kanisa limewasilisha hati 3 za viapo zilizosainiwa na Christopher Mibanda, Emmanuel Kimpanti na Padri Esperius Hamenyande. Mahakama imepanga shauri hilo litajwe Februari 15, 2023
Padri Hamenyande ni Mweka hazina wa Jimbo Katoliki la Kigoma na Christopher Mibanda ni Katekista mstaafu huku Emmanuel Mibanda akiwa ni Mzee maarufu Uvinza.
Shitaka hilo lililofunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma, Kanisa limewashtaki Bodi ya Wadhamini wa CCM, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halmashauri ya Uvinza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuchukua eneo lao wanalodai kulimiliki tangu Mwaka 1920.
Wamewasilisha shitaka hilo chini ya hati ya dharura na yamepangwa kusikilizwa mbele ya Jaji Lameck Mlacha.
Askofu Joseph Mlola wa Jimbo Katoliki la Kigoma
Waombaji katika shauri hilo wanadai mjibu maombi namba mbili Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Halmashauri ya Uvinza wamepanga kuchukua eneo lao kuwapa CCM bila ridhaa yao kwa ajili ya kujenga madarasa ya Shule ya Sekondari ya Chumvi.
Kupitia kwa Method R.G Kabuguzi ambaye ni Wakili wa Kujitegemea, Kanisa linaomba Mahakama izuie kwa muda uendelezwaji wa eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 39.6 hadi shauri la msingi litakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.
Kanisa limewasilisha hati 3 za viapo zilizosainiwa na Christopher Mibanda, Emmanuel Kimpanti na Padri Esperius Hamenyande. Mahakama imepanga shauri hilo litajwe Februari 15, 2023
Padri Hamenyande ni Mweka hazina wa Jimbo Katoliki la Kigoma na Christopher Mibanda ni Katekista mstaafu huku Emmanuel Mibanda akiwa ni Mzee maarufu Uvinza.