Kesi ya Mbowe: Mbowe na viongozi wa CHADEMA msiposikiliza ushauri wa Godbless Lema anaeshauri muondoe mawakili mahakamani, mtakuja kujiulaumu sana

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,017
144,373
Siku chache zilizopita, nilileta mada hapa niki-suggest Mbowe aacha kujitetea mbele ya hizi mahakama zetu kutokana na mwenendo mzima wa hii kesi. Leo hii kupitia You tube, nimemsikia Godbless Lema akimshauri Mbowe aondoe mawakili na akae kimya mahakamani ili wafanye kile wanachokita. Lema pia kaongea na katibu mkuu wa chama na anapanga kuongea na makamu mwenyekiti wa chama kuhusu jambo hili. Isitoshe, Lema kakumbusha uamuzi wa mke wake kutoa mawakili wakati ule wa kesi ya yake alipokuwa ananyimwa dhamana.

Katika kufafanua, Lema kataja mapungufu kadhaa yanayoonekana katika hii kesi na mfano mmojawapo ni Jaji kutumia mawazo yake(opinion) kufanya maamuzi badala ya kutumia vifungu vya sheria katika kuamua mapingamizi. Mbali na kutaja mapungufu yanayojitokeza, Lema anahoji kama katika hatua hizi za mwanzo taratibu zinakikuwa, tunatarajia kweli hukumu itakuwa fair?(swali la msingi sana hili).

Binafsi naungana na Lema kuwa kuna umuhimu wa kuondoa mawakili na Mbowe akae kimya mahakamani tuwaache wafanye wanalotaka kufanya. Hapa tunarudia kosa lilelile la kuwa wagumu kufanya maamuzi kama tulivyofanya kwenye kususia chaguzi zinazoendeshwa na hii tume ya uchaguzi isiokuwa huru. Na hapa niwaambie tu, wakifanikiwa kumfunga Mbowe halafu tukalalamika kuwa taratibu zilikiukwa, majibu yao(MATAGA) yatakuwa mawili: (1) kwanini hamkujitoa (2)Mkakate rufaa kama hamridhiki na maamuzi ya mahakama.

Kuhusu hili la kusubiri kwenda Mahakama ya Rufaa kupinga kitachoamuliwa, naungana pia na Lema kupinga hoja hii kwani hata hao Majaji wa Mahakama ya Rufaa upatikanaji wao ni ule ule wa kuteuliwa na Raisi,hivyo bado lolote linaweza kutokea. Kwahiyo, nashauri viongozi wa CHADEMA na wana familia ya Mbowe watafakari upya kama ni sahihi kuendelea kuweka mawakili mahakamani au Mbowe akae kimya na awaache waamue wanavyoona inafaa.
 
Isingekuwa hukumu ya kesi hii imeshatolewa na rais (akihojiwa na BBC) na IGP Zirro nisingekubaliana na mawazo ya Lema,Mbowe atoe mawakili na akaye kimya mahakamani maana kinachoendelea sasa ni kumcheleweshea siku za kutumikia kifungo tu.

Kadri tunavyozidi kujitetea ndiyo tunavyorefusha muda wa kukaa gerezani.

Mbowe ashahukumiwa kinachoendelea mahakamani ni maigizo na unajisi wa sheria kama ilivyo kawaida ya CCM.
 
Utafungwa naomba mwenyekiti uwapuuze Hawa mazuzu wewe ndiye unajua adha ya jela wao wataanza kuuana wakigombea KITI chako na watakusahau ndani ya siku 90.

Wewe ndiye nguzo ya chama unapambana kivyako wanajifanya wapo pamoja nawe lakini mioyoni mwao hawapo pamoja nawe.

Hizi siasa za harakati ni ngumu sana na hata ukishinda harakati zinakurudia kwa kiwango kilekile ulichokijenga.
 
Serikali siyo wajinga kumfungulia Mbowe kesi ya ugaidi. Mbowe mwenyewe anajuwa namna alivyolikoroga.

Muulizeni kati ya Desemba 2020 na March 2021 mpaka tunamzika DIKTETA Magufuli alikuwa wapi? Muulizeni ni kitu gani aliomba kwenye ubalozi wa Denmark na alijibiwa nini?

Nendeni na ubalozi wa Canada mkaone status ya papers zake kwa alichokiomba. Mmasingizia alikuwa kwenye biashara zake Dubai, ana biashara gani Dubai?

Kwa nini Serikali ihangaike kumtengeneza Mbowe mashtaka ya kubumba? Ni nguvu gani aliyonayo?

Mbowe alitaka kuweka nchi kwenye status of instability immediately baada ya uchaguzi kukamilika. Serikali ilipogundua njama ndipo akalazimika kukimbia.

Nani kasikia masekondari ya shule za Kisslami yanachomwa tena baada ya Mbowe kuwa mikono salama pale Ukonga?

Na kwa kiasi kikubwa amshukuru Samia ambaye ameacha Mahakama itende haki kwani ingekuwa hajawahi kukimbia nchi wakati wa Mwendazake, saa hizi Mbowe angekuwa na msaidizi wake Ben Saanane huko kuzimu.

Nashangaa Wana CDM mnamtukana Rais SSH eti DIKTETA mwanamke wakati ameacha uhuru wa habari na utawala wa sheria uendelee.
 
Sio wazo baya, ila mimi nashauri waombe mwenendo wa kesi toka kwa jaji, kisha hapo wataona nini jaji anaandika, baada ya hapo watajua nini kinaendelea nyuma ya pazia. Wakiona mwenendo wowote uonaoacha shaka, ambao nina uhakika upo wachukue uamuzi wa kujitoa kwani hawana imani na mahakama. Nasisitiza waseme hawana imani na mahakama na sio jaji tu. Kisha wairuhusu mahakama itekeleze inachoagizwa na serikali.
 
Kwa mara ya kwanza naungana na Lema kwenye hili.

Rais alishatoa hukumu tusitegemee kuna judge atatoa hukumu na kinyume chake.

Case hii ilikwisha kabisa pale kwenye maamuzi ya hukumu ndogo kukubali maelezo ya wale wanajeshi wastaafu.

Pale ndipo palimaliza case hiii haya ya muendelezo yatakuwa na mchango mdogo sana na ukweli ni kwamba lengo ni kumfunga Mbowe na watafanya hivyo kwa njia yeyote ile.

Kila mtu anajua fika Mbowe sio gaidi na awezi tenda vitendo hivyo..... bora kweli waondoe hao mawakili wafanye watakalo.... akiingia mahakamani ake kimya tuuu waamue wao
Hii case Rais alishatoa hukumu na kamwe judge awezi muumbuwa boss wake.

Kibaya zaidi case inaendelea Rais anampandisha cheo msimamizi wa case ambaye anakwenda kuwa mkubwa zaidi na mteuzi wa wasimamizi wa case(majudge).

Mimi binafsi niliacha kufatilia hii case baada ya hukumu ya case ndogo.
 
Mwenyekiti na Mungu pekee ndio wanaojua ukweli, msimpe kichwa kufanya maamuzi atayoyajutia mbele ya safari
 
Wakijitoa sasa hivi MATAGA watasema mawakili wa mboe wameona wamezidiwa na hivyo kuamua kujitoa,kwa hali ilivyo bora wapambane kupAngua ushaidi mpaka mwisho ili wote tuone vioja vinavyoendelea huko mahakamani
 
Serikali siyo wajinga kumfungulia Mbowe kesi ya ugaidi. Mbowe mwenyewe anajuwa namna alivyolikoroga.

Muulizeni kati ya Desemba 2020 na March 2021 mpaka tunamzika DIKTETA Magufuli alikuwa wapi? Muulizeni ni kitu gani aliomba kwenye ubalozi wa Denmark na alijibiwa nini?

Nendeni na ubalozi wa Canada mkaone status ya papers zake kwa alichokiomba. Mmasingizia alikuwa kwenye biashara zake Dubai, ana biashara gani Dubai?

Kwa nini Serikali ihangaike kumtengeneza Mbowe mashtaka ya kubumba? Ni nguvu gani aliyonayo?

Mbowe alitaka kuweka nchi kwenye status of instability immediately baada ya uchaguzi kukamilika. Serikali ilipogundua njama ndipo akalazimika kukimbia.

Nani kasikia masekondari ya shule za Kisslami yanachomwa tena baada ya Mbowe kuwa mikono salama pale Ukonga?

Na kwa kiasi kikubwa amshukuru Samia ambaye ameacha Mahakama itende haki kwani ingekuwa hajawahi kukimbia nchi wakati wa Mwendazake, saa hizi Mbowe angekuwa na msaidizi wake Ben Saanane huko kuzimu.

Nashangaa Wana CDM mnamtukana Rais SSH eti DIKTETA mwanamke wakati ameacha uhuru wa habari na utawala wa sheria uendelee.

Unaamini kwa kuandika propaganda ndefu ndio utatupoteza maboya kwa kinachoendelea huko mahakamani? Huu utoto ulioandika hapa hauendani na ushahidi unaotolewa mpaka sasa mahakamani. Kinachofanyika hivi sasa huko mahakamani ni kupotezeana muda kwa ushahidi wa kulazimisha toka kwa kundi la wahalifu walioko kwenye vyombo vya dola, ili kukidhi matakwa ya siasa chafu. Kufikia Ijumaa ya wiki ijayo, mawakili wachukue hatua za kujiondoa maana ni utoto wa uzeeni unaoendelea kwenye hiyo kesi.
 
Back
Top Bottom