Wanitakiani
JF-Expert Member
- Apr 18, 2008
- 641
- 135
Kama kuna uchaguzi uliomuongezea mlipakodi Wa Tz mzigo ni huu wa Igunga! Aibu!
Tusubiri maamuzi ya mahakama japo sina imani nazo.
Kwa mfumo wa uchaguzi wa 'ki-ccm', kesi za namna hii hazitakaa kuisha.
Kuna hila, gilba na dhuruma nyingi sana zinafanyika wakati wa uchaguzi. Haya mambo yangetakiwa kushughulikiwa outright before uchaguzi na mgombea anakua disqualified. Lkn tatizo vyombo vya kuyashughulikia haya, e.g. Tume ya uchaguzi, PCCB, msimamizi wa uchaguzi au msajili wa vyama vya siasa, wote hawa wameweka mbele 'u-ccm'. Yani ni matatizo tu.
Tuhuma ni nyingi sana, kuna ununuzi wa shahada ulidhibitishwa na ushahidi upo, uchakachuaji wa Daftari la wapiga kura ushahidi upo kwani kuna baadhi waliorodheshwa kwamba wameishafariki huku waliwa bado hai na ni kwa nini ni wanachama wa CDM pekee ndio walisingiziwa kuwa wamekufa? pia hadi sasa daftari la awali la wapiga kura limepotea wahusika wanajitahidi kutafuta halijapatikana. DC kuingilia mikutano ya Kampeni ya CDM.
Wanajamii nafikiri wengi tungependa kujua nini kinachoendelea kwenye kesi iliyofunguliwa na mgombea wa CHADEMA kupia kwa wakili wake Prof. Safari.
Tafuta gazeti la Nipashe leo limeripoti