chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 12,003
- 20,662
Kwa mujibu wa sheria za nchi, Mahakama haimiliki kesi, kwa msingi kwamba mahakama inapokea tu malalamiko (kesi), mahakama haitafuti kesi mitaani ili ije izisajili. Mahakama ni kama mtoto mchanga anayelishwa chakula, mahakama "inalishwa" kesi zinazoletwa ndipo ifanye kazi.
Hata kama wananchi watapigana mitaani, watauana, lakini kama mgogoro haujapelekwa mahakamani, mahakama haiwezi kufungua kesi yenyewe.
Kesi za jinai zinaweza kufunguliwa na mtu binafsi, hasa mahakama ya mwanzo, lakini kuanzia mahakama ya wilaya, jamhuri ndio inafungua shitaka. Lakini mashtaka yote ya jinai, DPP ndiye anayaratibu, na anaweza kuingia katika shitala lolote lile, katika mahakama yoyote ile, na akaliendeleza au kuliondoa.
Kesi inapokuwa chini ya DPP, mtu aliyefanyiwa kosa anakuwa shahidi tu, sio mlalamikaji, inalalamika jamhuri kwamba mtu wake katendewa kosa.
Pale DPP anapoingia katika shitaka, yule aliyelifungua kwa jina binafsi mamlaka yake yanakoma, kesi mzima inaendeshwa na DPP. Hata Madeleka pia, inashangaza kwamba anakata rufaa katika kesi ambayo si ya mteja wake,kwa kuwa DPP ameshaichukua, ni kesi ya serikali kupitia DPP, mteja wa Madereka ni shahidi tu. Tangu lini shahidi akakata rufaa?
Hata kesi ya gaidi maarufu, Mbowe, wenye kesi waliamua kuiondoa.
Hii pia inaenda katika mashauri ya madai, Mwanasheria Mkuu ana mamlaka ya kuingia katika shauri lolote pale ambapo anaona kuna maslahi ya umma(maslahi ya umma sio lazima yawe maslahi ya serikali).
Kwa hiyo tusiilalamikie mahakama, wao mi simba wa kufugwa, hawawindi.
Hata kama wananchi watapigana mitaani, watauana, lakini kama mgogoro haujapelekwa mahakamani, mahakama haiwezi kufungua kesi yenyewe.
Kesi za jinai zinaweza kufunguliwa na mtu binafsi, hasa mahakama ya mwanzo, lakini kuanzia mahakama ya wilaya, jamhuri ndio inafungua shitaka. Lakini mashtaka yote ya jinai, DPP ndiye anayaratibu, na anaweza kuingia katika shitala lolote lile, katika mahakama yoyote ile, na akaliendeleza au kuliondoa.
Kesi inapokuwa chini ya DPP, mtu aliyefanyiwa kosa anakuwa shahidi tu, sio mlalamikaji, inalalamika jamhuri kwamba mtu wake katendewa kosa.
Pale DPP anapoingia katika shitaka, yule aliyelifungua kwa jina binafsi mamlaka yake yanakoma, kesi mzima inaendeshwa na DPP. Hata Madeleka pia, inashangaza kwamba anakata rufaa katika kesi ambayo si ya mteja wake,kwa kuwa DPP ameshaichukua, ni kesi ya serikali kupitia DPP, mteja wa Madereka ni shahidi tu. Tangu lini shahidi akakata rufaa?
Hata kesi ya gaidi maarufu, Mbowe, wenye kesi waliamua kuiondoa.
Hii pia inaenda katika mashauri ya madai, Mwanasheria Mkuu ana mamlaka ya kuingia katika shauri lolote pale ambapo anaona kuna maslahi ya umma(maslahi ya umma sio lazima yawe maslahi ya serikali).
Kwa hiyo tusiilalamikie mahakama, wao mi simba wa kufugwa, hawawindi.