EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
MAHAKAMA KUU ya Kanda ya Tabora leo itaanza kusikiliza kesi ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi Dk Peter Kafumu Mbunge wa Igunga kupitia Tiketi ya CCM katika uchaguzi mdogo uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Shauri hilo lilifunguliwa na mlalamikaji Joseph Kashindye aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Tiketi ya Chadema dhidi ya Peter Kafumu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo.
Mahakama hiyo itaanza kusikiliza hoja za msingi zilizowasilishwa na pande zote ili kupata ufumbuzi wa uamuzi sahihi katika mahakama hiyo.
Hoja 15 ziliwasilishwa na wakili wa upande wa mlalamikaji Profesa Abdalla Safari ikiwamo anayopdai kwamba Waziri wa Ujenzi John Magufuli alifanya mkutano wa kampeni Kata ya Igulubi wilayani Igunga kutumia madaraka yake kuahidi ujenzi wa Daraja la Mbutu kama wananchi hao watampigia kura mgombea wa chama mapinduzi.
Pia Safari anadai waziri huyo aliwatisha wananchi wa kata hiyo kwamba wasipo ichagua CCM daraja hilo halitajengwa na kwamba pia aliwatisha wananchi hao kuwa wasipomchagua Dk Kafumu watashughulikiwa.
Profesa Safari alidai Baraza la Waislamu(Bakwata) Wilaya ya Igunga liliwakataza wasikipigie waumini wasiipigie kura Chadema na kwamba naye Rais mstaafu Benjamini Mkapa alitoa ahadi ya kugawa mahindi kwa wananchi wa Igunga siku mmoja kabla uchaguzi ili waichague CCM.
Jaji Mary Shangali anatarajia kusikiliza kesi hiyo na kwamba tayari mashahadi 80 wanatarajiwa kutoa ushahidi wao kwenye shauri hili.
Shangali alibainisha kuwa upande wa walalamikaji watakuwa na mashahidi wasiopungua 50 huku upande wa wajibu madai chini ya wakili Kamaliza Kayaga watakuwa na mashahidi 20 .
Miongoni mwa mashahidi ni mawaziri, baadhi ya wabunge na kwamba upande wa Serikali utakuwa na mashahidi 10.
Source: Mwananchi
Shauri hilo lilifunguliwa na mlalamikaji Joseph Kashindye aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Tiketi ya Chadema dhidi ya Peter Kafumu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo.
Mahakama hiyo itaanza kusikiliza hoja za msingi zilizowasilishwa na pande zote ili kupata ufumbuzi wa uamuzi sahihi katika mahakama hiyo.
Hoja 15 ziliwasilishwa na wakili wa upande wa mlalamikaji Profesa Abdalla Safari ikiwamo anayopdai kwamba Waziri wa Ujenzi John Magufuli alifanya mkutano wa kampeni Kata ya Igulubi wilayani Igunga kutumia madaraka yake kuahidi ujenzi wa Daraja la Mbutu kama wananchi hao watampigia kura mgombea wa chama mapinduzi.
Pia Safari anadai waziri huyo aliwatisha wananchi wa kata hiyo kwamba wasipo ichagua CCM daraja hilo halitajengwa na kwamba pia aliwatisha wananchi hao kuwa wasipomchagua Dk Kafumu watashughulikiwa.
Profesa Safari alidai Baraza la Waislamu(Bakwata) Wilaya ya Igunga liliwakataza wasikipigie waumini wasiipigie kura Chadema na kwamba naye Rais mstaafu Benjamini Mkapa alitoa ahadi ya kugawa mahindi kwa wananchi wa Igunga siku mmoja kabla uchaguzi ili waichague CCM.
Jaji Mary Shangali anatarajia kusikiliza kesi hiyo na kwamba tayari mashahadi 80 wanatarajiwa kutoa ushahidi wao kwenye shauri hili.
Shangali alibainisha kuwa upande wa walalamikaji watakuwa na mashahidi wasiopungua 50 huku upande wa wajibu madai chini ya wakili Kamaliza Kayaga watakuwa na mashahidi 20 .
Miongoni mwa mashahidi ni mawaziri, baadhi ya wabunge na kwamba upande wa Serikali utakuwa na mashahidi 10.
Source: Mwananchi