Polisi wa kutuliza ghasia wamewapiga mabomu ya machozi wanafunzi wa UDSM. Mkasa huo umekuja mara baada ya kumalizika kikao cha wanachuo na waziri wa Elimu. baada ya wageni wote kuondoka ilikuja zamu ya FFU kuondoka kwenye eneo la tukio lakini wanafunzi kwa vile walikuwa wamepania kulipiza kisasi walianza kuwarushia chupa za maji FFU hivyo nao FFU kuanza kujibu mapigo kwa kupiga mabomu ya moshi kuwatawanya wanafunzi. Hivi ninavyoandika maeneo ya kampasi na uandisi na swimming pool hakutamaniki kwa moshi na watu wametawanyika wakikimbia ovyo.
Ni hayo kwa sasa kutoka mlimani.
Waziri Shukuru katoka salama jamani?
Tanzania chuo ni UDSM tu...
Hivyo vingine ni vyuo vya Kata kama zilivyo Sekondari za Kata
Yaani anachomoka tu nyuma mabomu yakaanzwa kupigwa sijajua reaction ya wanafunzi wanaendela na mgomo au la!
Jana usiku order ilishatoka kwa waiziri kuwa wakiendelea hivi leo basi, most likely chuo kifungwe.... polisi wa chuo hawana nguvu tena kuzuia....
Mwili unasisimka natamani vyanzo hivi vya migomo vitumiwe vizuri kumshinikiza Kikwete aondoke madarakani!!
Chupa za maji kwa mabomu? Duh.. Tunaelekea pabaya..
Viongozi na wahusika wa clouds FM, tafadhali tunawaomba muondoeni Kibonde kwenye JAHAZI, watu waliolalamika kuhusu huyu bwana ni wengi sana. Ninapendekeza mpelekeni kwenye Africa Bambataa au Taarabu.
Tanzania chuo ni UDSM tu...
Hivyo vingine ni vyuo vya Kata kama zilivyo Sekondari za Kata
ktk watu wenye ubongo usiofanya kazi basi nawe ni mmoja wapo.unaongelea chuo mnachopita kwa 40%,choo SUA tuone kama utanusa hata mwaka wa pili utaishia kulamba pesa ya bodi na kukimbia chuoTanzania chuo ni UDSM tu...
Hivyo vingine ni vyuo vya Kata kama zilivyo Sekondari za Kata
Naomba wenye taarifa za ziada watupe manake mimi nilikutwa kwenye safari zangu za mishemishe za kujitaftia riziki, pale UCC palikuwa tulivu sana ila gafla pakaaribika sikujua timbwili lilianzaje.
Wanafunzi wametawanyika , wamekanyagana sana, wamejaribu kutupa mawe, ila kutokuwa wamoja kumewaponza , Engineering ndio wanaonekana bado wana nguvu, kwani wao wana ka-mgomo kao ka tofauti na wenzao, wao wanashinikiza mwanafunzi wa mwake wa nne aliyedisco arudishwe!
machozi tumetoa hata members of staff, tumetafuta maji na kunawa bila kupenda, wanafunzi wamekimbilia maofisini ,mwetu hapa ninao akina dada wanne hivi wanalia tu!!! mapinduzi gharama sana kwa nchi za kiafrika.
Dowans..dowans iliimbwa live....
sijajua chanzo cha mabomu...ila nilisikia shukuru kawambwa akiongea nao naona hawakuelewana , mwanzisha thread atatusaidia.
Madai ya elfu kumi yameanza tangu 2007!