kwani kwa akili yako mtu hata akifanya fujo anastahili kufa??? Polisi hawakutakiwa kuua hata kama Slaa ndiye kawatuma hao watu. Kwanini haikuwakamata na kuwafungulia mashtaka ya kufanya fujo kituoni? Kwani hao watu walienda na silaha ili tuseme polisi walikuwa wanajihami?? Hakuna sababu ya polisi kuua watu!! Hao polisi wanatoa wapi mamlaka ya kutoa uhai wa mtu?? Polisi wa Tanzania siwaelewi kabisa!! Hivi wanamwogopa Mungu kweli???
Ndugu wanajamvi, Leo katika kupitia kumbukumbu zangu, nimekutana na kitu ambacho kimenifanya nitafakari na kuunganisha dots na ku cross ts na kupata jibu juu ya vifo vya watz katika mikutano ya CDM.
Katika pekua yangu nikakutana na Slaa akiwahutubia na kuwataka wananchi waende Polisi kuwatoa viongozi wa CDM waliokuwa wamekamatwa na Polisi wa Arusha kwa kufanya maandamano haramu. Ni kutokana na kauli hiyo, watu wakaelekea kituoni na matokeo yake, watu 2 wakafa.
Lau kama isingekuwa kauli hiyo, nchi isingeshuhudia mauaji hayo.
Kauli nyingine chonganishi, zilizotolewa na huyo Slaa, ni ile ya Moro pamoja na Iringa na matokeo yake yanajulikana. Ni kutokana na ukweli huo, ninadiriki kutamka kwamba Mikono ya Slaa ina damu za watz waliouwawa katka shughuli za CDM na ninaamini kuwa katika umri wake pamoja na historia yake ya kupitia kwenye utumishi wa mungu, anapaswa kutubu na kuomba msamaha kwa mungu wake pamoja na watz kwa ujumla.