Katibu mkuu Wizara ya Afya aitwa Ikulu

Vyombo vya habari vinapotosha umma wa Watanzania kwa malengo wanayoyajua wao
-Muhimbili leo Madaktari waligoma na hao waliosema shuhgli zinaendelea, ni wanafunzi waliokuwa wakionekana(kwa mwananchi wa kawaida yoyote aliyevaa koti hospitalini ni Dr0
-MOI leo ilifungwa kabisa, hakuna mgonjwa aliyeonwa (huyu Bonge wa clouds aliona wanafunzi wa IMTU wakielekea huko)
-Ocean Road ndio kama mlivyosikia TBC1-specialist wachache ndo walibaki kuona wagonjwa wa ndani
-Bugando wameanza vikao endelevu leo na shughuli zilisuasua leo, kuanzia kesho-HAKUNA KAZI
-Mbeya REFFERALwameanza vikao leo-KUANZIA KESHO, TOOLS DOWN (Yule aliyehojiwa Mbeya ni mganga mkuu wa hospitali ya Mkoa-SIO RUFAA ambayo ni ndogo sana na inaona wagonjwa wengi wa nje tu
-DODOMA regional Hospital, wamekaa vikao leo, TOOLS DOWN KESHO

Enyi waandishi wa habari hizi si ndio habari za uchunguzi mnazotakiwa mzifuatilie na kuhoji wahusika (madaktari katika sehemu husika) ili mziandike?? MNAENDEKEZA NJAA TATIZO LENU NA HAMKO PROFFESSIONAL!!
Nendeni kwenye hizi sehemu kesho muone!
 
Waandishi ndo naona wanatumia muda huu kula bahasha. duh haya maisha ya kufa kufaana balaa tupu.
 
Nasikia alivyofika pale ikuru mh.akamwambia...''we mama,changanya na za kwako''
 
Hivyo vyombo vya habari vigome tu lakini chamoto wananchi watakipata na kuwahadithia tu wenzao wao waitane tu sisitunataka madai yetu yatekelezwe wakuu.

hata vyombo vya habari vikigoma kuripoti hata sisi tutashindwa kusimuliana?
 
Ukiona vyombo vya habari vimegomea kuandika ukweli, basi ujue wakiana Pasco washalamba Vibahasha vyao kutoka kwa Mafisadi
Haaahaaa! Kazi ipo...nothing goes without some kind of influence. Ndio maana kuaminiana kunakuwa kudogo.
 
Komaeni tu vijana Sekta ya afya inadharauriwa sana, nakumbuka miaka ya 1992, Ulianzishwa mugomo na wauuguzi baada ya mkutano mrefu pale Mwembeni mbele ya jengo Kibasila, vitisho vikaanza wauguzi wakakomaa, Ma-intern wakaunga mkono, Ma-resident na Ma-specialist wakafuatia, Maprofesa, (Wakabaki wakuu wa Idara wauguzi na Madaktari) Uliendelea kwa wiki nzima hali ikawa mbaya sana sana wagonjwa wakanyenyuka na urinals, ma pop, wheel chair wakaandamana kwenda Ikulu kumuomba Raisi Mwinyi awape hao wafanyakazi wa Afya wanachotaka ndio vitu kama sabuticle leave zikaanza, mikopo ya magari, fungu likaongezwa kwenye vifaa vya kutendea kazi, mortuary ikaboreshwa kwani ilikuwa inatoka funza,walimu vyuo vyote pale Muhimbili wakaboreshewa maeneo ya utendaji.

La muhimu muwe pamoja na muwe na lengo moja

...........umesahau na katikati ya mgomo MzeeMwinyi akaenda kucheza ISAMBE la KANDA BONGOMAN pale shamba la bibi

Kanda-Bongo-Man-Le-Rendez-Vous-De-499602.jpg
 
hawa waandishi wa habari watanzania hawana hekima, wanapenda sana kuabudiwa na cha kushangaza wanatangaza mgomo pasipo kutumia chama chao ambapo mwenyekiti wao ana treason charge mahakamani, swali langu wanasababu gani ya kususia, eti walikatazwa kuingia mkutano wa ndani, hivi hii ni ajabu si watu wote duniani wanajua kwamba kuna mikutano ya ndani ambapo waandishi hawaingii mpaka itakapomalizika na wao kuitwa, yaani wao wallitaka kuonyesha wasemaji wa kupanga resolutions kwenye camera? crap, nini basi maana ya kuwa na leakers, wanaotoa habari za ndani, hawa waandishi wa press release ndio tatizo lao, wavivu, hawana mbinu wamejaa kiburi kama nini, sasa ni sawa wakati madkatari wako katika wakati mgumu kama huu kudai mnasusia kuandika habari za mgomo huu? si ujuha, yaani na nyie mko upande wa serikali kuwapiga vita na kuwatengenezea madakatari wakati mgumu, haya kama wenzetu mna bima za afya lakini wengi wenu ni kama sisi tutakaoishia kufia kwenye reception za hospitalini tukisubiri huduma, waulizeni wale waliokua wanawalamba miguu mafisadi na kudharau kila kitu walipoumwa kama walipata huduma yote toka kwa mafisadi, waliozea makwao na kugeuzwa matonya
 
Mazungumzo ni njia nzuri ya kutatua matatizo kiustarebu ndio maana hata Rais Kikwete aliwaalika CDM Ikulu kuwasikiliza, laiti kama Wizara ya afya ingekubali kuwasikiliza ma Dr. naamini hali isingefika hapa, e Mungu tusaidie watanzania hasa wenye kipato cha chini
 
hakuna kukata tamaa watumishi wa afya mpaka kieleweke. huyo katibu mkuu mpaka aondolewe pmafu zake.
 
Hata kama ameitwa, kwa mawazo yangu sitegemei kama wito huo utakuwa na msaada mkubwa kwa wafanyakazi wa idara ya afya nchini, tatizo ni viburi vilivyotawala ndani ya mioyo ya wakuu hao kwa sababu wao wanamaslahi mazuri mpaka wanafikia kufanya harusi zinazogharimu mabilioni ya fedha.
 
Blandina nyoni ni kilaaza sana.Nimemsikia akihojiwa BBC leo amenisikitisha kwani hata anachokiongea hakijui.Mwanzo kaulizwa akasema hajapelkewa malalamiko ya madakitari akaulizwa swali lenye mtego kujua kama jibu la kwanza ni sahihi akajichanganya kuwa chanzo ni madakitari intern...swali hilo amelijuaje mwanzo alisema hajawahi pelekewa madai ya madakitari!
 
Hao vilaza hawawezikuona uchungu kwa sababu wao wanatibiwa nje tu wao na familia zao yetu wakina sie ndiyo maana kwao hili jambo halisumbui hata kidogo
 
Back
Top Bottom