Katiba Mpya: Serikali Inajikanganya!; Kukusanya Maoni Ki-Msiba Msiba!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wana bodi, leo asubuhi, nimelisoma tangazo la Ofisi ya Bunge, kwenye magazeti ya leo kuwaalika wadau na wananchi kuja kutoa maoni yao juu ya Muswada huu wa Mapitio ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 kwa iku za kesho na keshokutwa, Tarehe 7 na 8 katika kumbi za Karimjee (Dar es Salaam) na Pius Msekwa (Dodoma). Tangazo hilo halikounyesha kuwa maoni hayo pia yatakusanywa Zanzibar, ila leo asubuhi kwenye TBC, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba, Mhe Pindi Chana, ametangaza rasmi kamati yake, itakusanya maoni Zanzibar siku ya keshokutwa, bila kutaja ukumbi.

Kwenye jambo nyeti kama hili, hii ni zimamoto ya ajabu, huku serikali ikijikanganya na kujikanyaga kanyaga as if kumetokea msiba!.

Najiuliza maswali yafuatayo...

1. Hii zimamoto ya ghafla hivi inatokea wapi?.
2. Muswada wenyewe bado uko katika lugha ya Kiingereza na ulihitaji just a day (One Day), kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Sheria, kuutafisiri kwa Kiswahili, haraka hii ya nini?.
3. Hay tu asume wananchi wanaojua kiingereza watawafasiria wenzao wasiojua, haya, jee Muswaada huo uko public, uko wapi?, umechapishwa lini, wapi for public consuption ili hao wananchi wauone, wausome, wautafakari, ndipo waje watioe maoni?!.
4. Leo ndio tangazo linatoka kuwa kesho ndio siku ya kukusanya maoni, yaani hao wananchi, wealikuwa hawana shuguli nyingine zozote walizo jipangia, walikuwa wanasubiri kwa hamu tangazo la kwenda kutoa maoni ili watoe maoni yao!. Yaani siku ya kutoa maoni imegeuka dharura kama dharuza za misiba, hujapanga, ukipata taarifa ya msiba, unavunja shughuli zako zote, ili kuhudhuria mazishi, hii siku ya kukusanya maoni, ina udharura huu kweli, wa 'kimsiba msiba' ?!.
5. Serikali yatu imeshazoe ku watake Watanzania for 'granted' and gives them a ride kwenye mambo serious na ya msingi kama hili la mchakato wa katiba mpya!. Here is onother ride, should we just take it as we are much used to be given a ride?!..
 
Back
Top Bottom