Katavi: UCSAF yajenga Kituo cha Redio Mpimbwe

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987

Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ambao ndio wafadhili wakuu wa kujenga vituo vya Serikali kupitia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamekamilisha ujenzi wa kituo cha redio ya jamii katika Halmashauri ya Mpimbwe Mkoani Katavi chenye thamani ya zaidi ya Tsh. Milioni 200 ikiwa ni sehemu ya kusogeza huduma kwa Wananchi.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua redio hiyo amewataka watumishi wa Serikali kutumia Vyombo vya Habari hasa redio katika kusikiliza kero na kuzitatua kwa haraka ili kuleta msukumo wa maendeleo.

Baadhi ya wananchi wa maeneo hayo wamefurahishwa navuzinduzi wa redio hiyo ambapo awali hapakua na usikivu wa redio aina yoyote.
 
Kuna maeneo nchi hii kuipata tbc tu ni shughuli pevu, tena ni katikati ya nchi. Masafa ya fm hapo tu manyoni na itigi tbc haipatikani, kuna redio moja inayomilikiwa na dini ndio inasikika tena kwa taabu. Jiji la dodoma redio nyingi za dar zinasikika hapo lakini usikivu haufiki manyoni iliyo karibu na dodoma. Huo mfuko wa mawasiliano ufanye utafiti kuna maeneo mengi tu kupata matangazo ya redio za kitafa hazipatikani
 
Back
Top Bottom