Katavi: Wafanyabiashara wamkataa Afisa wa TRA

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Wafanyabiashara wa soko la Majimoto katika Halmashauri ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kumuondoa Afisa Mfawidhi wa Kituo cha Majimoto, Fraseck Mwakalenga kwa madai ya kukusanya kodi kiholela ikiwemo matumizi ya lugha za kukera.

Wakizungumza mbele ya Meneja wa (TRA) Mkoa wa Katavi, Nicholaus Migera wamesema kuwa wamechoshwa na vitendo vya kukadiliwa kodi kubwa kinyume na mapato ya biashara zao, jambo ambalo limepelekea baadhi yao kufunga biashara.

Aidha, wameongeza kwa kusema kuwa kwa muda mrefu wakihoji kuhusu jambo hilo wamekuwa wakijibiwa kuwa ambaye haridhiki na makadirio hayo au faini zinazotozwa na mamlaka hiyo afunge biashara.
TRA.jpg
Akijibu tuhuma hizo Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Katavi Nicholaus Migera amewaomba radhi wafanyabiashara hao kwa changamoto walizopata na kuahidi kuwa mamlaka hiyo inayafanyia kazi changamoto zote zilizo elezwa ili kukuza ustawi wa biashara na kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato.

Migera amesema Mamlaka hiyo itaendelea na program ya elimu kwa mlipa kodi ili kukuza uelewa wa masuala ya kikodi kwa wafanyabishara pamoja na kuwajengea uwezo watumishi wake ili kujiepusha na ukiukwaji wa maadili wakati wa ukusanyaji wa kodi na tozo zingine kwa wananchi.
 
Safi apelekwe musoma huko

Ila na ninyi watu wa majimoto mmeshindwa kudili nae kijadi mbna huko Ni sumbawanga tu
 
Wafanyabiashara wa soko la Majimoto katika Halmashauri ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kumuondoa Afisa Mfawidhi wa Kituo cha Majimoto, Fraseck Mwakalenga kwa madai ya kukusanya kodi kiholela ikiwemo matumizi ya lugha za kukera.

Wakizungumza mbele ya Meneja wa (TRA) Mkoa wa Katavi, Nicholaus Migera wamesema kuwa wamechoshwa na vitendo vya kukadiliwa kodi kubwa kinyume na mapato ya biashara zao, jambo ambalo limepelekea baadhi yao kufunga biashara.

Aidha, wameongeza kwa kusema kuwa kwa muda mrefu wakihoji kuhusu jambo hilo wamekuwa wakijibiwa kuwa ambaye haridhiki na makadirio hayo au faini zinazotozwa na mamlaka hiyo afunge biashara.
Akijibu tuhuma hizo Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Katavi Nicholaus Migera amewaomba radhi wafanyabiashara hao kwa changamoto walizopata na kuahidi kuwa mamlaka hiyo inayafanyia kazi changamoto zote zilizo elezwa ili kukuza ustawi wa biashara na kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato.

Migera amesema Mamlaka hiyo itaendelea na program ya elimu kwa mlipa kodi ili kukuza uelewa wa masuala ya kikodi kwa wafanyabishara pamoja na kuwajengea uwezo watumishi wake ili kujiepusha na ukiukwaji wa maadili wakati wa ukusanyaji wa kodi na tozo zingine kwa wananchi.
Tunaendelea kuboresha huduma kwa walipakodi na kuongeza uadilifu kwa watumishi wetu wa TRA. Na kuhusu suala la Katavi tunaendelea kulishughulikia kama alivyosema meneja wa Mkoa wa Katavi. Msisite kutoa maoni yenu kwenye semina, mikutano, vipindi vya redio na TV, kupiga simu 0800780078/0800750075 kituo cha wateja au kutuma barua pepe huduma@tra.go.tz au kuwasilisha maoni kwenye mitandao yetu ya kijamii.
 
Back
Top Bottom