'Karume Hakuyakimbia Mapinduzi ya ZnZ'- Karume Jnr

Karume hakukimbia mapinduzi kwani alikua hajui kinacho endelea...mambo yalipangwa Tanganyika na watanganyika kuondoa uislam znz.
Karume akapewa na sera ya mwanzo ilikua kuwadhalilisha masheikh wakubwa ....hakuna cha kujivunia hapa
 
Karume hakukimbia mapinduzi kwani alikua hajui kinacho endelea...mambo yalipangwa Tanganyika na watanganyika kuondoa uislam znz.
Karume akapewa na sera ya mwanzo ilikua kuwadhalilisha masheikh wakubwa ....hakuna cha kujivunia hapa
Kumbe lengo la yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 1964, ilikuwa ni kupindua dola la Kiislamu la Sultani na kuweka dola ya Kikisto ya Juliasi?!. Kwa vile mapinduzi yale yalifanikiwa sana ndio maana hadi kesho tunaimba mapinduzi daima, hiyo dola ya Kikristo ndio hii inayotawala Zanzibar?!, na ndio inayomnyima Maalim ushindi?!. Baada ya kufanikiwa kuuondoa Uislamu Zanzibar, kumbe sasa Zanzibar ni taifa la Kikisto!.

Mapinduzi Daima!.

Pasco
 
Maalim Seif alikua vizuri kukaa kimya kuliko lile tangazo alilotoa Mansur Yusuf Himid la kususia sherehe za Mapinduzi matukufu, hii inawapa washindani wake nafasi nzuri ya kumsema kwamba hapendi Muungano na anapinga uwepo wa Baraza la Mapinduzi.

Hata Tangazo lake la jana bado halijampa nafuu ktk siasa amechelewa sana watu wako mashambani.
 
Nawatakia kumbukumbu njema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyovikomboa visiwa hivi.
P
 
Kwanza tuendelee kupeana pole kwa Msiba wa Kawawa.
Leo amezikwa na apumzike kwa amani.
Ila pia msiba huu umefungua baadhi ya mambo ambayo hayakupata kujulikana kabla mongoni mwake ni haya...

Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi.

Akisimulia Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa saa 2 tuu, tangu saa 8:00 usiku mpaka saa10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.
Hivyo kulikucha salama usalmini.

Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kuja Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali shuleni Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?.

Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.

Waliposhuka pwani ya mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?.
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.

Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.

Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuawatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.

My Stake, January mwaka jana nilipata bahati ya kuisikiliza simulizi ya Mjane wa Karume, ambaye ndiye Mama yake Amani, Bi. Fatma Karume akieleza Karume alikuwa wapi wakati wa Mapinduzi, Bi. Fatma alikuwa mkweli zaidi kwa kusema mumewe alijihifadhi mahali, kwa vile hakuwa na uhakika mapinduzi yatafanikiwa, mpaka alipopata uhakika, ndipo akajitokeza. Ikumbukwe iliyeongoza Mapinduzi yale ni Mganda Field Marshal John Okelo na ndie aliyetangaza Mapinduzi kwenye Redio ya Sauti ya Zanzibar alfajiri ya tarehe 12 January,1964.

Hivi jamani, does it really make sense, nchi imepinduliwa usiku wa manane, na wewe alfajiri eti unahangaikia watoto warudi shule baada ya likizo, hivyo mnakosa usafiri, mnapanda mtumbwi, mnashukia Mbeni, mnaomba lifti ya Volkswagon ya watu, mnavamia kwa Kawawa, mnakataliwa kufunguliwa, was it just for watoto Amani na Ali kurejea Shule Malawi?.

Huu ni uthibitisho mwingine jinsi Mzee Kawawa alivyokuwa mtu wa watu. Umati uliojitokeza tangu jana kwenye heshima za mwisho na leo kwenye mazishi, ni uthibitisho wa hili.

RIP Mzee RASHIDI MFAUME KAWAWA, SIMBA WA VITA, UPUMZIKE KWA AMANI.
Tuulize sisi tuliokuwepo Zanzibar, wchana na vijarida vya kubuni story chonganishi.Mzee Thabiti Kombo amelibainisha hilo.
Je wewe na Thabit nani mkweli>?
 
Kwanza tuendelee kupeana pole kwa Msiba wa Kawawa.
Leo amezikwa na apumzike kwa amani.
Ila pia msiba huu umefungua baadhi ya mambo ambayo hayakupata kujulikana kabla mongoni mwake ni haya...

Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi.

Akisimulia Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa saa 2 tuu, tangu saa 8:00 usiku mpaka saa10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.
Hivyo kulikucha salama usalmini.

Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kuja Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali shuleni Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?.

Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.

Waliposhuka pwani ya mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?.
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.

Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.

Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuawatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.

My Stake, January mwaka jana nilipata bahati ya kuisikiliza simulizi ya Mjane wa Karume, ambaye ndiye Mama yake Amani, Bi. Fatma Karume akieleza Karume alikuwa wapi wakati wa Mapinduzi, Bi. Fatma alikuwa mkweli zaidi kwa kusema mumewe alijihifadhi mahali, kwa vile hakuwa na uhakika mapinduzi yatafanikiwa, mpaka alipopata uhakika, ndipo akajitokeza. Ikumbukwe iliyeongoza Mapinduzi yale ni Mganda Field Marshal John Okelo na ndie aliyetangaza Mapinduzi kwenye Redio ya Sauti ya Zanzibar alfajiri ya tarehe 12 January,1964.

Hivi jamani, does it really make sense, nchi imepinduliwa usiku wa manane, na wewe alfajiri eti unahangaikia watoto warudi shule baada ya likizo, hivyo mnakosa usafiri, mnapanda mtumbwi, mnashukia Mbeni, mnaomba lifti ya Volkswagon ya watu, mnavamia kwa Kawawa, mnakataliwa kufunguliwa, was it just for watoto Amani na Ali kurejea Shule Malawi?.

Huu ni uthibitisho mwingine jinsi Mzee Kawawa alivyokuwa mtu wa watu. Umati uliojitokeza tangu jana kwenye heshima za mwisho na leo kwenye mazishi, ni uthibitisho wa hili.

RIP Mzee RASHIDI MFAUME KAWAWA, SIMBA WA VITA, UPUMZIKE KWA AMANI.
Ahsanta mkuu nimekusoma kwa utuvu.
 
Leo tarehe 12 January ni Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, nachukua nafasi hii kuwatakia nyote heri na fanaka za Mapinduzi na kukutakieni maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa watakao shereheka kwa wale wenye kumbukumbu njema, na kwa vile Mapinduzi Matukufu yale pia yaliandamana na umwagaji damu, natoa pole kwa wenye kumbukumbu chungu.
P
 
Akiwa aliyakimbia au hakuyakimbia, mie kama mzanzibari wa leo sioni umuhimu wowote.Ninachojua mie, Zanzibar ilipewa uhuru kama nchi nyengine zilizokuwa zimetawalia hapa barani Afrika.

Baada ya uhuru, gurupu fulani halikuridhishwa na waliokamata serekali wakaamua kutumia njia ya nguvu na vita kuindoa i.e Mapinduzi.

Kwa vile hilo gurupu lililopindua lilipata nguvu au hifadhi kutoka Tanganyika (hoja ya msingi ya kuundwa kwa mungano), imebidi hadi leo tuite Mapinduzi ndio uhuru wa kweli.

Lakini hakuna chochote Mapinduzi HAYAKUBALIKI kwenye ulimwengu wa demokrasia, hivyo Zanzibar haina budi kuyaweka kama ni historia na kuendelea kusherehekea uhuru wake wa 1963 kama ilivyo nchi nyengine yoyote iliokuwa koloni.

Huu ndio ufahamu wangu, mimi ni mzanzibari na kijana wa leo napenda kukabiliana na kila aina ya hoja.Lakini hoja hizi za kihistoria ni lazima viongozi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wakubali ukweli, kama mapinduzi sio jambo jema wala lakuomba.Huu ni uvunjwaji wa haki za kibinadamu!

Walioliwa wote kwenye mapinduzi hayo, walikuwa ni wazanzibari waliopachikwa labels za kibaguzi za kiarabu.Lakini amini usiamini, wafuasi hao waliopinduliwa ni wazanzibari na wengine hata rangi zao ni pure Afrikans au Zanzibaris.Si kweli kwamba Pemba nzima ina waarabu, wenye damu ya kiarabu ni chini ya 10%.Kuna sehemu Unguja pia ambazo zinadaiwa zilikuwa ndio hizo zilizokuwa na wafuasi wa serekali iliyopinduliwa, mfano Uzi, Bumbwini, Stone-Town...hizi sehemu zote haina waarabu, kama wapo ni wachache kama sehemu zengine zozote za Zanzibar.

Nawakilisha...
Wewe si ni Mjukuu wa Masulutani, tuachie tufurahie siye
 
Leo tarehe 12 January ni Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, nachukua nafasi hii kuwatakia nyote heri na fanaka za Mapinduzi na kukutakieni maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa watakao shereheka kwa wale wenye kumbukumbu njema, na kwa vile Mapinduzi Matukufu yale pia yaliandamana na umwagaji damu, natoa pole kwa wenye kumbukumbu chungu.
P

Hivi nawewe huna Babu yako aliyekimbilia Zanzibar kama Magufuli?
 
Okello alikuwa polisi hapo Zanzibar ingawa alikuwa ametokea Uganda.
Sidhani kama Okello alikuwa ndani ya jeshi la polisi kama mtumishi. Kumbuka Okello hata kiswahili kikimsumbua, fuatiliza video za mahojiano kwenye youtube. Lugha ikimsumbua ya kiswahili, huu kwangu ni ushahidi alihamia Zanzibar si zaidi ya miaka michache kutokea Uganda kuelekea Mapinduzi.

Lengo kudadisi waliopanga Mapinduzi sio kuyahalalisha, bali kuondoa upotofu uliopo kuwa mapinduzi yalimwondoa Sultan wakati ukweli iliondolewa serekali halali kwa sheria na taratibu za wakati huo. This is just a fact, hata kama hupendi monarchi style zipo nchi nyingi tuu duniani na nyengine afrika zina wafalme.
 
Just googling Okello alihamia muda gani visiwani Zanzibar, alihamia miaka 4 kabla ya Mapinduzi.
John Okello, a Langi from the present-day Alebtong District in northern Uganda. He had gone to the island four years earlier.
REF:
 
Watu wenye akili za kufikiria nje ya box, Okello hakuhamia as coincidence. He was a men in a mission, a retired military trained in Cuba. Wengine watasema ni speculation kama alifundishwa uharamia kwa Castro. Kwangu siamini bahati mbaya, naconnect dots hadi kwa Julius.
 
Sidhani kama Okello alikuwa ndani ya jeshi la polisi kama mtumishi. Kumbuka Okello hata kiswahili kikimsumbua, fuatiliza video za mahojiano kwenye youtube. Lugha ikimsumbua ya kiswahili, huu kwangu ni ushahidi alihamia Zanzibar si zaidi ya miaka michache kutokea Uganda kuelekea Mapinduzi.

Lengo kudadisi waliopanga Mapinduzi sio kuyahalalisha, bali kuondoa upotofu uliopo kuwa mapinduzi yalimwondoa Sultan wakati ukweli iliondolewa serekali halali kwa sheria na taratibu za wakati huo. This is just a fact, hata kama hupendi monarchi style zipo nchi nyingi tuu duniani na nyengine afrika zina wafalme.
Alikuwa polisi mzee wangu; kuna rekodi nyingi zinathibitisha hivyo. Alikuwa ni polisi aliyeachwa na wakoloni hakuwa wa mapinduzi. Wakati huo waingereza walikuwa wanatawala Kenya, Uganda na Tanganyika na Zanzibar, kwa hiyo kwao wao askari atokee Kenya au Uganda lilikuwa jambo la kawaida sana. Hata idi Amini aliwahi kutumika kwenye jeshi ta KAR kambi ya Tabora
 
Alikuwa polisi mzee wangu; kuna rekodi nyingi zinathibitisha hivyo. Alikuwa ni polisi aliyeachwa na wakoloni hakuwa wa mapinduzi. Wakati huo waingereza walikuwa wanatawala Kenya, Uganda na Tanganyika na Zanzibar, kwa hiyo kwao wao askari atokee Kenya au Uganda lilikuwa jambo la kawaida sana. Hata idi Amini aliwahi kutumika kwenye jeshi ta KAR kambi ya Tabora

Okello hakuwahi kuwa polisi Zanzibar, Yawezekana wewe unamchanganya na Edison Kisasi
 
Alikuwa polisi mzee wangu; kuna rekodi nyingi zinathibitisha hivyo. Alikuwa ni polisi aliyeachwa na wakoloni hakuwa wa mapinduzi. Wakati huo waingereza walikuwa wanatawala Kenya, Uganda na Tanganyika na Zanzibar, kwa hiyo kwao wao askari atokee Kenya au Uganda lilikuwa jambo la kawaida sana. Hata idi Amini aliwahi kutumika kwenye jeshi ta KAR kambi ya Tabora
Utaishi vipi polisi Zanzibar halafu usijue kiswahili ? Kwa kiswahili cha Okello, miaka minne nadhani ni very conservative estimate. It should be much lower than that!
 
Utaishi vipi polisi Zanzibar halafu usijue kiswahili ? Kwa kiswahili cha Okello, miaka minne nadhani ni very conservative estimate. It should be much lower than that!
Siyo kuwa kila aaliyekuwa akiishi Zanzibar alikuwa anajua kiswahili. Okelo alikwenda kwanza Kenya kutafuta kazi, akapata kazi ya hovyo hovyo kwa vile hakuwa na elemu, aliposikia zanzibar kuna kazi za upolisi ndipo akaenda kujaribu na akafanikiwa. Kujua lugha huwa inategemea na kichwa cha mtu, wengine ni wazito na wengine ni wepesi. Tuliwahi kusimuliwa hadithi yote ya mapinduzi yale na Brigedia Yusufu Himid pamoja Kanali Abdallah Natepe mwaka 1976; wao wamo kwenye picha hii pamoja na Okello.

1617912623028.png


Kimoja walichosema wote ni kuwa kwa vile Okello alikuwa haogopi kitu na alikuwa na lugha ya kutisha na sauti ya ukali sana kwa kutumia amri za kipolisi, ndiye aliyekuwa mbele ya mapinduzi yale na aliwatia hofu sana watu wa serikali. In fact alipovamia kituo cha polisi kupora silaha ni kwa vile alikuwa anafanyia kituo hicho hicho na alikuwa anajua silaha ziko wapi.

Ndani ya picha hiyo unaweza kuwaona Abdallah Natepe na nyuma ya Okello, na Yusuf Himid pembeni mwake.
 
Back
Top Bottom