'Karume Hakuyakimbia Mapinduzi ya ZnZ'- Karume Jnr

najiuliza sina jibu, je kama kweli karume hakuwa na mchango wowote katika mapinduzi ya zanzibar kama baadhi ya post zinavyoashiria, ilikuwaje akaweza kumuondoa okello bila resistance kubwa kutoka kwa waliomuunga mkono okello? kwani kwa kuongoza mapinduzi kwenye "field" nina hakika alikuwa anao watu ambao walikuwa tayari kupoteza maisha yao kwa kumuunga mkono yeye. kwani nijuavyo mimi "bond" inayojengeka katika uwanja wa vita ni kubwa sana.

Kuna mambo inabidi uyaelewe. Kwanza, pamoja na Okelo kuunda serikali na kumteua Raisi Karume na baraza la mawaziri, hiyo serikali bado iliwajibika kwake. Neno lake lilikuwa la mwisho na yeyote ambaye hakutii, alishughulikiwa. Kwa mfano, Januari 13,1964, alitoa ujumbe huu kwenye redio:
The government is now run by us....should you be stubborn and disobey orders I will take measures 88 times stronger than at present." and, "If anyone fails to comply... and locks himself in a house, as others have done...I have no alternative but to use heavy weapons. We, the army have the strength of 99,099,000.
Huu ulikuwa utawala wa kijeshi ambao haukuvumilia aina yoyote ya uasi. Januari 14, 1964 aliposikia kuna watu sehemu iliyoitwa Mtendeni, wanalalamikia sheria za ukandamizaji alitoa tangazo hili:
Here is the Field Marshall of Zanzibar and Pemba....I am thinking of going to Mtendeni (village) to destroy it if the people there do not obey orders. After 40 minutes I am coming to finish you off, especially the Comorians". And "To all Arab youths living in Malindi; I will pass through Malindi armed with weapons of which I alone know. I want to see everyone stripped to his underpants and laying down. I want to hear them singing...father of Africans. God bless him in his task and that of the Field Marshall."
Huyo ndiye Okelo, aliogopwa labda zaidi ya Idi Amin wa Uganda baadaye na tamko lake lilikuwa kama sheria. Hakuna Mzanzibari aliyeweza kukohoa mbele ya Okelo. Kufanikiwa kwa haya mapinduzi kulileta hali ya hofu kubwa kwa serikali zote tatu za Afrika Mashariki Tanganyika, Kenya na Uganda. Hata hivyo Okelo alimheshimu sana kiongozi wa Tanganyika na hata alipopewa mwaliko kuja Dar es Salaam alikubali bila wasiwasi.
Okello3.jpg

Hapa anaonekana Field Marshall wa Zanzibar na Pemba John G. Okelo siku alipofika Dar es Salaam

Kitu ambacho hakukijua ni kuwa huu ulikuwa ni mpango wa kumkamata na moja wa wasaliti wake ni Abeid Karume aliyeteuliwa Raisi lakini asiye na madaraka ya mwisho. Haya ndiyo nayaita mapinduzi ndani ya mapinduzi. Bila Tanganyika Zanzibar haingekuwa Zanzibar tunayoiona leo kwani juhudi kubwa ilibidi zifanyike kuifuta historia ya Okelo hadi kitabu alichoandika kupigwa marufuku ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Field Marshall wa Zanzibar na Pemba John G. Okelo alitisha ati.
 
kutokana na kauli zake inaelekea field marshal okelo alikuwa anaamini
kwamba anaungwa mkono kwa kiasi kikubwa na "jeshi la mapinduzi".
inawezekana kabisa huo ndio ulikuwa ukweli na hivyo palihitajika mtu
mwengine ambaye naye anakubalika na "jeshi la mapinduzi" ili kuweza kumuondoa. hivyo sidhani kama nakosea nikisema kiongozi wa namna hiyo alikuwa karume.
hapa naweza fananisha kiasi na hali iliyotokea burkina faso kati campaore na sankara. hawa viongozi wa mapinduzi wote walikuwa maarufu ndio maana campaore akamuwahi sankara.

aidha inawezekana kutokana na ukatili wake basi "viongozi wa mapinduzi" waliona ni bora kumuondoa okelo mapema kabla uongozi wake haujashika mizizi.

hapa nafananisha na juhudi za akina chisiza wa malawi kujaribu kumuondoa banda kabla uongozi wake haujashika mizizi baada ya kuona mzee anawegeuzia kibao wale "waliomualika" katika uongozi. bahati mbaya chisiza hakufanikiwa ila zanzibar walifanikiwa.
 
Mag 3, Your account of what happened in Zanzibar is more accurate. We on the mainland need not distort history.

The fact is that soon afterwards Nyerere and Kawawa arranged for a contingent of Police Officers who went to Zanzibar to restore some element of peace and order. They worked under Eddington Kisasi whom I personally knew from childhood.

Jamshid was helped by Nyerere to go to England as a refugee, of course. Nyerere also helped to curb the excesses of "Field Marshall" John Okelo, and when he could not be restrained, he was tricked to go to Nairobi and subsequently returned to his native Uganda.

It is good that Amani Karume concedes that when matters were hot in Zanzibar, he and his brother were basking in Malawian sun and schooling.

I agree with those JF Members who urge that revolutions should be avoided at all costs. And join those who wish Rashid Mfaume Kawawa's soul to rest in eternal peace. May God give strength to the Kawawa family to recover soon from this great loss.
 
ina maana mwandishi hajui wakina okello,natepe, darwesh, mfaranyaki na bakari ni makabila gani? mbona kataja kisasi (mchaga), na kaujore ( mmakonde) na ingen (mjaluo). je kuna kitu anajaribu kuficha hapa au ni mtindo tu wa uandishi? jee mwinyi nae ni mzanzibar? kwani karume tayari inasemekana ni mmalawi.

inakuwaje muandishi autambue uhuru wa 10 disemba 1963 na sultani kama mzanzibar kisha akane uzanzibar wa akina natepe?

naamini kulaani mapinduzi na mauaji yaliyoambatana nayo ni tofauti na kukana uraia wa wahusika wa mapinduzi kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kusema "yale hayakuwa mapinduzi bali ni uvamizi kutoka nje".
Kafara, nadhani mwandishi naye alidurufu maandishi, by the way siasa za Zanzibar ngumu kama ilivyo historia ya visiwa hivyo.

Hakuna maandishi kuonyesha kabla ya ujio wa Sultan Said Said, wenyeji walikuwa kina nani, karibu wote waliopo sasa ni wahamiaji kwa namna moja ama nyingine.

Weusi wote ni vizalia vya watumwa waliotoka bara, ama wahamiaji kiuchumi. Waarabu wote, ni vizalia vya mwarabu na waliobaki ni majirani, wacomoro, wangazija etc, who is really a Zanzibari?.
 
Kuna mambo inabidi uyaelewe. Kwanza, pamoja na Okelo kuunda serikali na kumteua Raisi Karume na baraza la mawaziri, hiyo serikali bado iliwajibika kwake. Neno lake lilikuwa la mwisho na yeyote ambaye hakutii, alishughulikiwa. Kwa mfano, Januari 13,1964, alitoa ujumbe huu kwenye redio:

Huu ulikuwa utawala wa kijeshi ambao haukuvumilia aina yoyote ya uasi. Januari 14, 1964 aliposikia kuna watu sehemu iliyoitwa Mtendeni, wanalalamikia sheria za ukandamizaji alitoa tangazo hili:Huyo ndiye Okelo, aliogopwa labda zaidi ya Idi Amin wa Uganda baadaye na tamko lake lilikuwa kama sheria. Hakuna Mzanzibari aliyeweza kukohoa mbele ya Okelo. Kufanikiwa kwa haya mapinduzi kulileta hali ya hofu kubwa kwa serikali zote tatu za Afrika Mashariki Tanganyika, Kenya na Uganda. Hata hivyo Okelo alimheshimu sana kiongozi wa Tanganyika na hata alipopewa mwaliko kuja Dar es Salaam alikubali bila wasiwasi.
Okello3.jpg


Hapa anaonekana Field Marshall wa Zanzibar na Pemba John G. Okelo siku alipofika Dar es Salaam


Kitu ambacho hakukijua ni kuwa huu ulikuwa ni mpango wa kumkamata na moja wa wasaliti wake ni Abeid Karume aliyeteuliwa Raisi lakini asiye na madaraka ya mwisho. Haya ndiyo nayaita mapinduzi ndani ya mapinduzi. Bila Tanganyika Zanzibar haingekuwa Zanzibar tunayoiona leo kwani juhudi kubwa ilibidi zifanyike kuifuta historia ya Okelo hadi kitabu alichoandika kupigwa marufuku ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.​



Field Marshall wa Zanzibar na Pemba John G. Okelo alitisha ati.


Asante Mag3, unazama deep vizuri, nimekuja jistukia kumbe napenda history zaidi ya ninachofanya sasa. Ukiondoa hao wahamiaji, wenyeji halisi wa Zanzibar na Pemba, yaani natives kabla ya ujio wa waarabu, ni kina nani?.
 
Mag 3, Your account of what happened in Zanzibar is more accurate. We on the mainland need not distort history.

Eddington Kisasi whom I personally knew from childhood.

eternal peace. May God give strength to the Kawawa family to recover soon from this great loss.
Kilasara, kwa mujibu wa jina lako na Kisasi ni kule kule, kwa vile umemjua tangu utotoni, jee ulimjulia huko huko Zenj ama naye alikuwa bara akahamia ZnZ?.
 
ina maana mwandishi hajui wakina okello,natepe, darwesh, mfaranyaki na bakari ni makabila gani? mbona kataja kisasi (mchaga), na kaujore ( mmakonde) na ingen (mjaluo). je kuna kitu anajaribu kuficha hapa au ni mtindo tu wa uandishi? jee mwinyi nae ni mzanzibar? kwani karume tayari inasemekana ni mmalawi.

inakuwaje muandishi autambue uhuru wa 10 disemba 1963 na sultani kama mzanzibar kisha akane uzanzibar wa akina natepe?

naamini kulaani mapinduzi na mauaji yaliyoambatana nayo ni tofauti na kukana uraia wa wahusika wa mapinduzi kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kusema "yale hayakuwa mapinduzi bali ni uvamizi kutoka nje".

Uvamizi kutoka nje ndivyo ulivyokuwa huo, penda usipende naamini kabisa hao wana makabila yao japo mwandishi hajayaweka hapo kwenye makala hiyo.

Kwa kukusaidia na huyo Mzee Rukhsa (mzaramo).

Ni jambo la kawaida kuwa na raia wenye kutokea sehemu mbali mbali za dunia, kwa Zanzibar ndio kabisa huwezi kuepuka hilo.Kuna wahindi, waarabu, waafrika, na wazanzibari wasiojua asili zao.

Hoja ya nani mzanzibari halisia au nani ana haki zaidi?Naona kama tutakuwa tunajadili pumba....hili ni jambo la kawaida kabisa kuwa na makabila tofauti ndani ya nchi!

All in all hata wana mapinduzi wangelikuwa waarabu, BADO MAPINDUZI NA UONGOZI WA KIJESHI HAUKUBALIKI!!!
 
Uvamizi kutoka nje ndivyo ulivyokuwa huo, penda usipende naamini kabisa hao wana makabila yao japo mwandishi hajayaweka hapo kwenye makala hiyo.

Kwa kukusaidia na huyo Mzee Rukhsa (mzaramo).

Ni jambo la kawaida kuwa na raia wenye kutokea sehemu mbali mbali za dunia, kwa Zanzibar ndio kabisa huwezi kuepuka hilo.Kuna wahindi, waarabu, waafrika, na wazanzibari wasiojua asili zao.

Hoja ya nani mzanzibari halisia au nani ana haki zaidi?Naona kama tutakuwa tunajadili pumba....hili ni jambo la kawaida kabisa kuwa na makabila tofauti ndani ya nchi!

All in all hata wana mapinduzi wangelikuwa waarabu, BADO MAPINDUZI NA UONGOZI WA KIJESHI HAUKUBALIKI!!!

taratibu hapa tunaeleweshana tuu.

natumaini kwa maelezo yako hapo juu unakubali kwamba kiasi kikubwa wahusika wa mapinduzi walikuwa wazanzibari (kwani umesema zanzibar inao mchanganyiko wa raia wa asilia mbali mbali, yaani hata mwinyi pamoja na uasilia ya uzaramo bado ni mzanzibari). kwa mantiki hii ule haukuwa uvamizi kutoka nje bali yalikuwa matumizi ya nguvu ya kuleta mabadiliko ya serikali aka mapinduzi.

nadhani suala la kukubalika au kutokubalika mapinduzi ni hoja pana na inayohitaji thread yake yenyewe.

mada hapa ni jee karume alikimbia au hakuyakimbia mapinduzi?
 
Uvamizi kutoka nje ndivyo ulivyokuwa huo, penda usipende naamini kabisa hao wana makabila yao japo mwandishi hajayaweka hapo kwenye makala hiyo.

Hoja ya nani mzanzibari halisia au nani ana haki zaidi?Naona kama tutakuwa tunajadili pumba....hili ni jambo la kawaida kabisa kuwa na makabila tofauti ndani ya nchi!

All in all hata wana mapinduzi wangelikuwa waarabu, BADO MAPINDUZI NA UONGOZI WA KIJESHI HAUKUBALIKI!!!

MrFroast, maadam umekubali kuwa
Hoja ya nani mzanzibari halisia au nani ana haki zaidi?Naona kama tutakuwa tunajadili pumba....hili ni jambo la kawaida kabisa kuwa na makabila tofauti ndani ya nchi!

Hii hoja yako ya Uvamizi kutoka nje ndivyo ulivyokuwa huo, penda usipende naamini kabisa hao wana makabila yao japo mwandishi hajayaweka hapo kwenye makala hiyo. Haina mashiko.

Ila hoja yako hii All in all hata wana mapinduzi wangelikuwa waarabu, BADO MAPINDUZI NA UONGOZI WA KIJESHI HAUKUBALIKI! ni hoja ya msingi sana. Ni kweli mapinduzi ya kijeshi, hayakubaliki, lakini serikali za kijeshi, zinatambulika ndio maana tuna mifumo miwili ya serikali za dunia hii, nazo ni De Jure-kwa mujibu wa sheria na De Facto, za kimabavu. Zanzibar ilikuwa De Facto tangu baada ya mapinduzi enzi za Karume Baba. Serikali ya Mapinduzi iliyopo sasa, inatumia tuu jina la De Facto kwa kujiita ni serikali ya Mapinduzi, but in fact its De Jure kwa sababu imefanya uchaguzi wa kidemokrasia, suala la kama uchaguzi ilikuwa huru na wa haki, hili ni jingine.
 
.

mada hapa ni jee karume alikimbia au hakuyakimbia mapinduzi?
Kafara, Rais wa Zanzibar mwenyewe kasema kuwa Babaye, hakuyakimbia Mapinduzi, bali alikuja bara, kuwasindikiza yeye na Ali warejee shule Malawi baada ya likizo.

Kwa vile ni kawaida ya wazazi kutowaambia watoto ukweli, na Kama Karume mtoto, hakuwahi kumuuliza baba, "hivi ile safari ya siku ile ya Mapinduzi, kwenda bara kwa mtumbwi, kushukia mbweni, kuomba lifti ya bittle, kuvamia kwa Kawawa, kukutaliwa kufunguliwa mpaka aliposhuka Kawawa mwenyewe, ilikuwa ni kurejea shule tuu baada ya likizo?.

Then, naomba tuyaamini maneno ya Rais Karume, Karume hakuyakimbia Mapinduzi.
 
Serikali ya Mapinduzi iliyopo sasa, inatumia tuu jina la De Facto kwa kujiita ni serikali ya Mapinduzi, but in fact its De Jure kwa sababu imefanya uchaguzi wa kidemokrasia, suala la kama uchaguzi ilikuwa huru na wa haki, hili ni jingine.
Hapo tutakwenda nje ya maada, lakini serekali iliopo nayo ni ya De Facto.Hawajawahi kushinda uchaguzi, na wala CCM haitoshinda uchaguzi Zanzibar bila ya kutumia mabavu.Wengi wa supporters wa CCM, ni hao hao ambao walikuwa ni minority na huwa hawashindi chaguzi.Ndio wakafanya mapinduzi badala ya kushindwa kwenye njia za demokrasia.

Ndio maana kila uchaguzi Zanzibar ni vurugu tupu, kama wanashinda basi ingekuwa kila kitu smooth.

Ukiona serekali inalazimika kutia jeshi mitaani kufumba midomo ya wananchi, ujue hapo kuna faulu.Mbona Tanganyika uchaguzi kila kitu kiko shuari?

By the way, Karume Jr anababaisha historia.Kama walivyojaribu kwa miaka yote baada ya mapinduzi kujaribu kuipindisha.Lakini kukaja mfumo wa vya vingi ndio sasa hivi tuko hapa JF na kwengineko free tunapiga soga na kufadili masuala magumu ya nchi.

Lakini kama ingelikuwa ni zile zama za Mwalimu, sote ni wahaini tuko jela tunaozeana!
 
Hapo tutakwenda nje ya maada, lakini serekali iliopo nayo ni ya De Facto.Hawajawahi kushinda uchaguzi, na wala CCM haitoshinda uchaguzi Zanzibar bila ya kutumia mabavu.Wengi wa supporters wa CCM, ni hao hao ambao walikuwa ni minority na huwa hawashindi chaguzi.Ndio wakafanya mapinduzi badala ya kushindwa kwenye njia za demokrasia.

Ndio maana kila uchaguzi Zanzibar ni vurugu tupu, kama wanashinda basi ingekuwa kila kitu smooth.!
Mzee wa Mzalendo Net, hiyo ni kweli, hali ya kisiasa Zanzibar ni ile ile ya 1963 na matokeo ni yale yale miaka nenda miaka rudi.

CCM imekuwa ikishinda kwa hila siku zote. Karume sasa amelielewa hilo ndio maana ameshikana mikono na Maalim, sasa mambo yenu super.

Tena ngoja nikudokezee siri, lakini usimwambie mtu. Juzi kwenye mkutano wa Redet hapo Zanzibar, nilinong'ona na Maalim Seif kidogo kuhusu mazungumzo yake na Amani, nikamuuliza, mikoni mmeshikana, mmekubali yamekwisha, mbona hajawaamuru wafuasi wake kujitokeza kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura?.

Akasema mambo hayajesha, kushikana mikono ni ishara tuu za mwanzo. Mambo mazuri yanakuja na wakati muafaka mtatangaziwa ili pia mjitokeze kujiandikisha. Uchaguzi wenu safiri hii utakuwa huru na wa haki sawia na matokeO yaliyoleta uhuru wenu. Serikali ya Mapinduzi mwisho mwaka huu, inaingia serikali ya mseto, itaweka tume ya maridhiano kuponya makovu ya mapinduzi na kuutambua rasmi uhuru wa Dec 63.

Ukiona serekali inalazimika kutia jeshi mitaani kufumba midomo ya wananchi, ujue hapo kuna faulu.Mbona Tanganyika uchaguzi kila kitu kiko shuari?
!
Kwenye demokrasia afadhali kwenu Zanzibar, CUF angalau wanamatumaini, Tanganyika uchaguzi shwari kwa sababu sultani CCM, ameshika kisawasawa, hutu hatufurukuti, yeye atatawala milele, labda kama na sisi tutafanya mapinduzi.
 
Serikali ya Mapinduzi mwisho mwaka huu, inaingia serikali ya mseto, itaweka tume ya maridhiano kuponya makovu ya mapinduzi na kuutambua rasmi uhuru wa Dec 63.

Hii itakuwa ni dreams come true kwa wazanzibari waliowengi na wapenda amani duniani.Japokuwa ndio tunavyoomba demokrasia iachiwe ipite...

lakini mzanzibari mie siamini chochote kutoka chama cha mafisadi, hadi nione kwa macho yangu ndio niamini...:D
 
Hii itakuwa ni dreams come true kwa wazanzibari waliowengi na wapenda amani duniani.Japokuwa ndio tunavyoomba demokrasia iachiwe ipite...

lakini mzanzibari mie siamini chochote kutoka chama cha mafisadi, hadi nione kwa macho yangu ndio niamini...:D

Wala usitie shaka, hilo ni wazi, mambo yenu super, labda tatizo kwetu bara ni wasiwasi, Wanzanzibari mkishikamana, ni hatari kwa hatma ya muungano, weza vtokea watu makini wakaishauri serikali yenu isiendelee kuburuzwa, bali kuzirejea zile original articles of union za Nyerere na Karume, na Wanzanzibari kufumbuliwa macho kuhusu nyungeza zote kwenye original articles ni kinyume cha sheria, hivyo ni batil, mkiidai haki hiyo, bara itawafanza tena kama Aboud Jumbe alivyofanzwa kwa kutaka kutetea haki ya Zanzibar ndani ya Muungano.
 
Sidhani kama kuundwa kwa serikali ya mseto kutotoa nafasi ya kutotambua Mapinduzi ya 64.
 
Sidhani kama kuundwa kwa serikali ya mseto kutotoa nafasi ya kutotambua Mapinduzi ya 64.
Kibunango, kwanza ukumbuke ni serikali ya mseto, sio tena serikali ya CCM. Siyo kuwa hawatayatambua Mapinduzi ya 64, bali watatibu makovu ya mapinduzi hayo ambayo yangalipo mpaka leo, na pia kuutambua uhuru wa Desemba 63, maana wale waliopinduliwa ile Januari 64, ndio walioshinda uchaguzi, na ndio hawa hawa wanaopiga kele kupokwa ushindi kila kukicha, wasiwasi ni hatma tuu ya muungano.
 
Kibunango, kwanza ukumbuke ni serikali ya mseto, sio tena serikali ya CCM. Siyo kuwa hawatayatambua Mapinduzi ya 64, bali watatibu makovu ya mapinduzi hayo ambayo yangalipo mpaka leo, na pia kuutambua uhuru wa Desemba 63, maana wale waliopinduliwa ile Januari 64, ndio walioshinda uchaguzi, na ndio hawa hawa wanaopiga kele kupokwa ushindi kila kukicha, wasiwasi ni hatma tuu ya muungano.

Hapa kwetu tunaita KIZUNGUMKUTI,,naam kizungumkuti ndio....Kutibu makovu ya Mapinduzi ndio kupi!??
Walioporwa mashamba na kugawiwa eka tatu tatu watarejeshewa? hivi hayo mashamba wao waliyapata wapi kabla hawajang'anywa?
AU Walioliwa ndugu zao watafutwa machozi kwa kulipwa fidia?
waliobakwa jee!?
kama hawa waliopinduliwa ndio walioshinda uchaguzi Na vipi wale waliofanya mapinduzi ambao wanadia kwamba pia walikua wanashinda katika changuzi lakini wananyimwa,,,wao walidhani mapinduzi ndio yamekuja kutibu makovu yao..kumbe walika waongo! walafi tu wa madaraka...loh!
Pasco tufafanulie,,mwaka huu nami nataka nipige kura eti!! INSHALLAH
 
Hapa kwetu tunaita KIZUNGUMKUTI,,naam kizungumkuti ndio....Kutibu makovu ya Mapinduzi ndio kupi!??
Walioporwa mashamba na kugawiwa eka tatu tatu watarejeshewa? hivi hayo mashamba wao waliyapata wapi kabla hawajang'anywa?
AU Walioliwa ndugu zao watafutwa machozi kwa kulipwa fidia?
waliobakwa jee!?
kama hawa waliopinduliwa ndio walioshinda uchaguzi Na vipi wale waliofanya mapinduzi ambao wanadia kwamba pia walikua wanashinda katika changuzi lakini wananyimwa,,,wao walidhani mapinduzi ndio yamekuja kutibu makovu yao..kumbe walika waongo! walafi tu wa madaraka...loh!
Pasco tufafanulie,,mwaka huu nami nataka nipige kura eti!! INSHALLAH

Tunaposema kuwa supporters wa CUF wana uhusiano na waliopinduliwa, hapo sio literally.Chama cha CUF hakina direct relation na vyama vya kihistoria kabla ya mapinduzi.

Na wazanzibari wameamua kukiunga mkono na kuondosha CCM, basi demokrasia iachwe ifanye kazi yake?

Kuponesha makovu ya mapinduzi kwa akili yangu mie ni kama kufuta sherehe za mapinduzi, kubadilisha jina la serekali kutoka SMZ na kuwa serekali ya umoja au shirikisho la watu wa Zanzibar.Na kujitokeza raisi au kiongozi kutoa speech kama aliyotoa kiongozi wa uingereza kuwaomba radhi waafrika kutokana na makovu ya utumwa.

Lakini sio kurudishiana mashamba, hiyo itakuwa vurugu mpya!!!

Historia:
Aidha ASP ilikuwa ikishinda uchaguzi kwenye ukoloni wa muingereza, mie siamini hivyo hadi nitakufa.Muingereza namuamini zaidi kama uchaguzi wake ulikuwa wa haki kushinda hiyo ZEC!!!

Kwa hiyo mapinduzi yalipindua wazanzibari waliochagua serekali wanayoitaka, na muingereza akakubali kama hawa ndio waliowengi nawaachia visiwa vyao narudi kwetu UK.

ASP wakaamua kutumia Mapinduzi kuiondosha serekali halali....na haya mapinduzi ndio chimbuko la matatizo mengi, yametokea ndio yashatokea....sasa its time to move on,and forget that dark past!!!

Au wasemaje Mshirazi?:confused:
 
Back
Top Bottom