Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,371
Wakati watanzania tuko kwenye mchakato wa katiba mpya naamini ni wakati muafaka na wabunge kupitia upya kanuni na taratibu za kuendesha bunge kwani zina mapungufu makubwa na ni janga la kitaifa kwa kuzingatia umuhimu wa bunge.Nitatoa mifano michche ambayo mimi kwangu hainiridhishi:-
1. Spika,naibu spika na wenyeviti wawe watu huru
Hii ni kutokana na viongozi hawa kusimamia na kuendesha bunge kwa kuzingatia itikadi za vyama vyao badala ya kufuata kanuni na matokea yake ni mambo kama upendeleo na uonevu ktk maamuzi.
2. Kanuni juu ya mwongozo na taarifa
Hii kanuni kwakweli ina upungufu sana kwani inampa spika mamlaka ya kutoa muongozo wakati wowote anaoona unafaa.Nadhani hapa spika anatakiwa awekewe kipengele cha kumbana kwamba ni lazima atoe muongozo ndani ya kipindi fulani na anaposhindwa kufanya hivyo awasilishe sababu bungeni.Vile vile iwe ni lazima kwa spika kupokea muongozo na taarifa kutoka kwa wabunge kwani hivi sasa anaweza kukataa kuruhusu muongozo au taarifa kutolewa.
3. Taarifa za kamati kutegemea ruhusa ya spika
Sina uhakika sana na kanuni hii ila kama kweli taarifa ya kamati ya bunge juu ya uchunguzi wa jambo fulani ni lazima kwanza ipate ruhusa ya spika ndio taarifa hiyo iruhusiwe kusomwa bungeni hili nalo ni tatizo kubwa. Nashauri taarifa yeyote ya kamati ya bunge ni shariti isomwe bungeni na spika apewe taarifa tu juu ya uwasilishaji lakini asiwe muamuzi.
4. Maamuzi yanayohusu mambo mazito kama upitishaji bajeti yawe kwa kura ya siri na sio kwa mtindo wa kuhoji wabunge kwa pamoja.
5. Wabunge walipwe posho baada ya kusaini mara mbili asubuhi na jioni ili kudhibiti utoro na anaesaini mara moja kwa siku alipwe nusu posho.
6. Kanuni zipige marufuku mambo kama pongezi za kifamilia na hata mawaziri wasilazimike kuwataja(kuwatambua)wale wote waliochangia ili kuokoa muda na labda anaweza kuwashukuru kwa ujumla tu.
7. Na kanuni zingine zote ambazo ni kikwazo cha maendeleo kwa taifa letu.
8. Hoja kwamba jambo lilkishajadiliwa na kufanyiwa maamuzi basi jambo hilo ndio limefungwa rasmi kwa maana ya kwamba halitarudishwa bungeni tena. Kanuni hii ni ya ovyo na inalenga kulea uozo serikalini. Athari ya kanuni hii ni kuhusu mambo kadhaa kwa mfano kashifa ya richmond ambayo kwa sasa imeshafungwa rasmi kujadiliwa bungeni na hata swala la uuzaji wa nyumba za serikali.
Hapa cha msingi ni kuzingatia nyakati na kama kuna taarifa au ushahidi mpya unaoweza kusaidia jambo fulani kwa wakati wowote jambo husika lilrudishwe bungeni. Pia inawezekana maamuzi ya nyuma yalifanywa kimakosa kutokana na taarifa zilizokuwepo kwa wakati huo na kuna umuhimu wa kuzingatia taarifa mpya au hata mazingira ya wakati wa sasa.
1. Spika,naibu spika na wenyeviti wawe watu huru
Hii ni kutokana na viongozi hawa kusimamia na kuendesha bunge kwa kuzingatia itikadi za vyama vyao badala ya kufuata kanuni na matokea yake ni mambo kama upendeleo na uonevu ktk maamuzi.
2. Kanuni juu ya mwongozo na taarifa
Hii kanuni kwakweli ina upungufu sana kwani inampa spika mamlaka ya kutoa muongozo wakati wowote anaoona unafaa.Nadhani hapa spika anatakiwa awekewe kipengele cha kumbana kwamba ni lazima atoe muongozo ndani ya kipindi fulani na anaposhindwa kufanya hivyo awasilishe sababu bungeni.Vile vile iwe ni lazima kwa spika kupokea muongozo na taarifa kutoka kwa wabunge kwani hivi sasa anaweza kukataa kuruhusu muongozo au taarifa kutolewa.
3. Taarifa za kamati kutegemea ruhusa ya spika
Sina uhakika sana na kanuni hii ila kama kweli taarifa ya kamati ya bunge juu ya uchunguzi wa jambo fulani ni lazima kwanza ipate ruhusa ya spika ndio taarifa hiyo iruhusiwe kusomwa bungeni hili nalo ni tatizo kubwa. Nashauri taarifa yeyote ya kamati ya bunge ni shariti isomwe bungeni na spika apewe taarifa tu juu ya uwasilishaji lakini asiwe muamuzi.
4. Maamuzi yanayohusu mambo mazito kama upitishaji bajeti yawe kwa kura ya siri na sio kwa mtindo wa kuhoji wabunge kwa pamoja.
5. Wabunge walipwe posho baada ya kusaini mara mbili asubuhi na jioni ili kudhibiti utoro na anaesaini mara moja kwa siku alipwe nusu posho.
6. Kanuni zipige marufuku mambo kama pongezi za kifamilia na hata mawaziri wasilazimike kuwataja(kuwatambua)wale wote waliochangia ili kuokoa muda na labda anaweza kuwashukuru kwa ujumla tu.
7. Na kanuni zingine zote ambazo ni kikwazo cha maendeleo kwa taifa letu.
8. Hoja kwamba jambo lilkishajadiliwa na kufanyiwa maamuzi basi jambo hilo ndio limefungwa rasmi kwa maana ya kwamba halitarudishwa bungeni tena. Kanuni hii ni ya ovyo na inalenga kulea uozo serikalini. Athari ya kanuni hii ni kuhusu mambo kadhaa kwa mfano kashifa ya richmond ambayo kwa sasa imeshafungwa rasmi kujadiliwa bungeni na hata swala la uuzaji wa nyumba za serikali.
Hapa cha msingi ni kuzingatia nyakati na kama kuna taarifa au ushahidi mpya unaoweza kusaidia jambo fulani kwa wakati wowote jambo husika lilrudishwe bungeni. Pia inawezekana maamuzi ya nyuma yalifanywa kimakosa kutokana na taarifa zilizokuwepo kwa wakati huo na kuna umuhimu wa kuzingatia taarifa mpya au hata mazingira ya wakati wa sasa.