Kanuni hizi za bunge zipitiwe upya kwa manufaa ya taifa

Tatizo langu juu ya hizi kanuni za bunge ni kwamba katiba ya Jamhuri ya Tanzania inampa mbunge mmoja mmoja uwanja mpana wa kuisimamia serikali iliyoko madarakani; uwanja huo mpana anaopewa mbunge chini ya katiba, unaminywa na kanuni za bunge zilizotungwa na bunge lenyewe. Jambo linalonitatiza ni je inakuwaje kanuni hizo zinachukuliwa kuwa juu ya katiba? Kwangu mimi, kanuni yeyote ambayo mahudhui yake yanapingana na mahudhui ya katiba, ni batili. Kwa mantiki hiyo madaraka makubwa aliyopewa spika ya kuminya mijadala hapo bungeni ni kinyume na sheria
 
Ahali yangu nimekubainishia wazi kama Utapunguza USHABIKI na KULALAMIKA na kutulia kitako kusoma vizuri Katiba yenu utajifunza mengi sana. Kumbuka kuwa katika dhana ya Rules of Law, utaona kila muhimili una kazi zake.

Kazi za Bunge ni kutunga sharia
Kazi za Mahakama ni kutafsiri Sharia zinazotungwa na Bunge.
Kazi za Serikali ni Kusimamia sharia zinazotungwa na Bunge.

Na hata ukisoma Katiba hiyo hiyo inasema wazi Serikali inawajibika kwa wananchi kwa sababu Serikali ni ya watu. Soma Katiba yya JMTz katika kuona Serikali na watu sharia namba 15 Ibara ya 6 ya mwaka 1984. Imebainisha hivyo.

Lakin vile vile angalia Sharia hiyo iliyotungwa na Bunge kuhusu separation of Power.
Utekelezaji wa shughuli za Mamlaka ya Nchi Sheria namba Na.15 ib.6 ya 1984, kifungu cha 4

4
.-
(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri

ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili

vyenye mamlaka ya utendaji, vyombo viwili vyenye mamlaka

ya kutekeleza utoaji haki, na pia vyombo viwili vyenye

mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa

shughuli za umma.


(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni

Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki

vitakuwa ni Idara ya Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya

Muungano na Idara ya Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na

kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni

Bunge na Baraza la Wawakilishi.


Mkuu kama ni kuzingatia sheria na kanuni,katiba na kwa ujumla hiyo separation of power tafakari yafuatayo:-
1.Raisi wa nchi kusamehe wezi wa EPA tena mbele ya bunge.Hivi raisi anasamehe watu waliokwisha kuhukumiwa tu au hata watuhumiwa ambao hata hawajapelekwa mahakamani?
2.Raisi kuzungumzia mgomo wa madaktari ktk hotuba yake kwa taifa na bado kuna kesi juu ya jambo hilo mahakamani
3.Serikali kuwasimamisha kazi madaktari wakati kesi bado iko mahakamani
4.Wabunge wa ccm na mwanasheria mkuu wa seikali kuwahusisha chadema na mauaji yenye sura ya kisiasa ya Singida jana trh 16/07/2012 bungeni wakati kesi iko mahakamani na waliruhusiwa na kiti cha spika.
Mkuu, nchi hii kuna walio juu ya sheria na ndio watakaovuruga amani ya nchi siku si nyingi, kwani uvumilivu una mwisho kama ilivyotokea Misri,Libya,Yemeni na sasa Siria.
 
Mkuu kama ni kuzingatia sheria na kanuni,katiba na kwa ujumla hiyo separation of power tafakari yafuatayo:-
1.Raisi wa nchi kusamehe wezi wa EPA tena mbele ya bunge.Hivi raisi anasamehe watu waliokwisha kuhukumiwa tu au hata watuhumiwa ambao hata hawajapelekwa mahakamani?
2.Raisi kuzungumzia mgomo wa madaktari ktk hotuba yake kwa taifa na bado kuna kesi juu ya jambo hilo mahakamani
3.Serikali kuwasimamisha kazi madaktari wakati kesi bado iko mahakamani
4.Wabunge wa ccm na mwanasheria mkuu wa seikali kuwahusisha chadema na mauaji yenye sura ya kisiasa ya Singida jana trh 16/07/2012 bungeni wakati kesi iko mahakamani na waliruhusiwa na kiti cha spika.
Mkuu, nchi hii kuna walio juu ya sheria na ndio watakaovuruga amani ya nchi siku si nyingi, kwani uvumilivu una mwisho kama ilivyotokea Misri,Libya,Yemeni na sasa Siria.

Ndio maana nakwambia punguza ushabiki wa kisiasa utajifunza mengi sana kutoka kwenye Katiba yenu kuhusu hayo ulonena.

Hebu pitia Kipengelle cha Wajibu wa kutii sharia kwenye Katiba ya JMtz iliyotungwa na hao hao wabunge Sharia namba 15 Ibara ya 6 ya mwaka 1984 Inayonena
kifungu cha 26.
26​
.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii Katiba hii na
sheria za Jamhuri ya Muungano.(2) Kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibu uliowekwa nasheria, kuchukua hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba​
na sheria za nchi.

sasa jiulize je umeshachukua hatua au ndio kama kawaida unalalamika.

nakupa pole sana


 
Ndio maana nakwambia punguza ushabiki wa kisiasa utajifunza mengi sana kutoka kwenye Katiba yenu kuhusu hayo ulonena.

Hebu pitia Kipengelle cha Wajibu wa kutii sharia kwenye Katiba ya JMtz iliyotungwa na hao hao wabunge Sharia namba 15 Ibara ya 6 ya mwaka 1984 Inayonena
kifungu cha 26.
26​
.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii Katiba hii na
sheria za Jamhuri ya Muungano.(2) Kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibu uliowekwa nasheria, kuchukua hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba​
na sheria za nchi.

sasa jiulize je umeshachukua hatua au ndio kama kawaida unalalamika.

nakupa pole sana



wewe mropokaji si ulishaaga jf .... nini kinakuwasha tena
 
mnasumbuliwa udhaifu wa kujenga hoja na ukosefu wa nidhamu2, hakuna ziada

Mkuu nadhani kwa maamuzi ya spika ya leo juu ya muongozo wa Hamadi Rashidi bungeni na baadae waziri ambae ndio mtoa hoja kuomba kuondoa hoja yake juu ya swala hilo hilo umepata jibu juu ya mawazo yangu kuhusu mapungufu ya kanuni za bune ikiwa ni pamoja na madaraka ya spika na upendeleo unaoneshwa na kiti cha spika.
Penye ukweli uongo hujitenga.
 
Tanzania tuna safari ndefu, kwani kuna mamilioni hata hawajui na wala hawafuatili nchi inakwendaje na hata inaendeshwa vipi.Wao wanasubiri kupiga kura tu na si kufuatilia utendaji wa hao wanaowachagua.
Hata hili bunge wengi hawana habari nalo, wao wanachojali ni maigizo kwenye TV na magazeti ya udaku.Pita kwenye bar,migahawa na mahotel uangalie ni wangapi wanafuatilia bunge hata kama TV mahali hapo inaonyesha kipindi cha bunge.
Namalizia kwa kusema wanaofuatilia bunge ni sehemu ndogo sana ya watanzania na bila kelele za umma wa watanzania tusitarajie mabadiliko yoyote ya maana bungeni,kwenye mahakama na wala serikalini.
 
Tanzania tuna safari ndefu, kwani kuna mamilioni hata hawajui na wala hawafuatili nchi inakwendaje na hata inaendeshwa vipi.Wao wanasubiri kupiga kura tu na si kufuatilia utendaji wa hao wanaowachagua.
Hata hili bunge wengi hawana habari nalo, wao wanachojali ni maigizo kwenye TV na magazeti ya udaku.Pita kwenye bar,migahawa na mahotel uangalie ni wangapi wanafuatilia bunge hata kama TV mahali hapo inaonyesha kipindi cha bunge.
Namalizia kwa kusema wanaofuatilia bunge ni sehemu ndogo sana ya watanzania na bila kelele za umma wa watanzania tusitarajie mabadiliko yoyote ya maana bungeni,kwenye mahakama na wala serikalini.

True hata viongozi wameshagundua hilo na ndioo maana kiongoz anafanya anavotaka. Watz 26% ndio wanaofatilia mwenendo wa serikal hii ndio sababu ya kuchelewa zaid kupata maendeleo
 
Kumekuwepo mtindo wa kutumia kanuni za bunge, kuwabama wabunge, hasa wa kambi la upinzani, wanapoibua hoja za kuibana serikali kwa kushindwa kuteleza majukumu yake. Mfano mzuri wa jambo hili, ni hatua batili iliyochukuliwa na spika jana ya kuzuia kutolewa kwa hoja binafsi katika kikao cha bunge kinachoendele. Ikumbukwe kazi ya bunge ni kuisimamia serikali katika utendaji wake. Na hivyo, wabunge wanawajibika kuleta hoja binafsi kila wanapobaini kuwepo mapungufu makubwa wa serikali katika utekelezaji wa majukumu yake. Katika hali hiyo, haingii akilini hata kidogo, ni kwa sheria ipi ya nchi, spika anapata hiyo jeuri ya kuzuia bunge lisitimize jukumu lake!

Kwa maoni yangu, hatua iliyochukuliwa na spika jana ya kuzuia bunge kutimiza wajibu wake, huku likiendelea kutumbua fedha za walipa kodi masikini, kujilipe posho nono kwa kulala usingizi pono, ni usaliti mkubwa kwa taifa letu, ambao unapashwa kulaaniwa na watu wote wenye mapenzi mema na taifa hili, bila ya kujari ushabeki wao wa kisiasa. Rai yangu ni kwamba, sasa wakati umefika wa kumpasha Anne Makinda na naibu wake Ndugai kwamba, kama hawawezi kujizuia kutanguliza ukada wao wa CCM katika kusimamia shughuli za bunge, ni vema wakaachia ngazi.
 
Ni kweli mkuu huyu spika na naibu wake wanakera sana kwa nini mambo yenye manufaa kwa wananchi wanaweka pingamizi nyingi hatuwaelewi hawa watu je wako pale wanawawakilishaje watu wao?au ndio waliwachagua wakawe wapinga hoja za maendeleo hawa maspika hawatufahi hata kidogo.
 
Kwa hakika kabisa naliona anguko kubwa sana la CCM. Yanayofanywa na Spika Makinda na Naibu wake Job Ndugai ni kusafisha njia kwa CDM 2015. Tusisikitike inawezekana ni mpango wa Mungu wa kutuondolea MaCCM bila yenyewe kujua kuwa yanajitayarishia safari.
 
Kanuni na taratibu ndani ya bunge la tanzania bado hazitambuliki n wabunge kwa asilimia 90 kwa uchunguzi nilioufanya ambao sio rasmi umenipa majibu haya!!Imeonekana dhairi kabisa kwa pande zote zilizopo bungeni zinashindwa wazi kutumia lakini pia hata kuzitafsiri kanuni za bunge wabunge wengi wameonekana kwenda kinyume kabisa na taratibu..

NINI KIFANYIKE?
1:kuanzishwe darasa huru la kuwafundisha wabunge jinsi ya kutafsiri na kuzitumia kanuni vile ipasavyo!!!!
2;kuanzishwe tena kamati ya kanuni na taratibu za bunge yaani yakusimami pembeni yakua kanuni na taratibu zinafuatwa!!!
 
Atakayetaka kuzungumzia yanayojiri bungeni basi asome kwanza Kanuni (Standing Orders) then achangie badala ya kuongea kama kasuku afu bila ushahidi hapa!! MODs msiziondoe tafadhali!!
KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE, TOLEO LA
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
1-. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007.
2-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba, Kanuni hizi zitatumika kwa mambo yote yanayohusu utaratibu wa uendeshaji wa Shughuli za Bunge.
(2) Iwapo jambo au shughuli yoyote haikuwekewa masharti katika Kanuni hizi, Spika ataamua utaratibu wa kufuata katika jambo au shughuli hiyo, kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturi za uendeshaji bora wa Shughuli za Bunge na uamuzi huo utaingizwa katika Kitabu cha Maamuzi ili kuongoza mwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa Shughuli za Bunge.
3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo yatahitaji vinginevyo:-
“Akidi” ni idadi ya Wabunge inayoruhusu kufanya maamuzi ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni za 77, 78 na 79 za Kanuni hizi; “Bendera” ni Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ina rangi ya bluu iliyoiva iliyo katika umbo la mstatili na yenye umbo dogo la bendera ya Taifa ndani yake katika
Matumizi
Jina
Tafsiri
2
pembe juu ya upande wa kushoto na Siwa, chini kukiwa na utepe wenye maneno “Bunge la Tanzania”; “Bunge” ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 62 ya Katiba; “Bunge Jipya” ni Mkutano wa Kwanza wa Bunge ulioitishwa na Rais kwa mujibu wa Ibara ya 90(1) baada ya kutangazwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu; “Chama” ni Chama cha Siasa chenye uwakilishi Bungeni; “Gazeti” ni Gazeti la Serikali ya Jamhuri ya Muungano; “Hoja ya Kamati” ni hoja iliyokubaliwa na Kamati ya Bunge baada ya majadiliano ya Kamati husika; “Hoja ya Mbunge” ni hoja inayotolewa na Mbunge asiyekuwa Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali; “Jamhuri ya Muungano” ni eneo lote lililokuwa ndani ya Mipaka ya Jamhuri ya Tanganyika na eneo lote lililokuwa ndani ya Mipaka ya Jamhuri ya Zanzibar kabla ya tarehe 26 Aprili, 1964; “Kamati” ni Kamati yoyote ya Bunge iliyoundwa kwa mujibu wa Kanuni hizi; “Kamati ya Bunge Zima” ni Kikao cha Wabunge wote wanapokaa kama Kamati wakati wa:-
(a) kupitisha Muswada wa Sheria; (b) kujadili taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuhusu mashtaka dhidi ya Rais au Makamu wa Rais; (c) kujadili hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu; au (d) kujadili hoja ya kumwondoa madarakani Spika au Naibu Spika.
“Kamati ya Matumizi” ni kikao cha Wabunge wote wanapokaa kama Kamati kushughulikia Makadirio ya Matumizi ya Fedha za Serikali; “Kamati ya Mipango” ni kikao cha Wabunge wote wanapokaa kama Kamati katika Mkutano wa mwezi Februari ili kujadili na kushauri kuhusu mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali katika mwaka wa fedha unaofuata; “Katiba” ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977; “Katibu” ni Katibu wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 87 ya Katiba na inajumuisha pia mtumishi mwingine yeyote wa Bunge aliyeidhinishwa kutekeleza kazi yoyote ya Katibu; “Kikao cha Bunge” ni kikao cha siku moja kinachoanza kwa kusomwa Dua na kumalizika kwa kuahirisha Bunge hadi siku itakayotajwa;
Sura ya 2, Toleo la 2002
3
“Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni” ni Mbunge aliyeteuliwa au kuchaguliwa na Wabunge wanaounda Kambi Rasmi ya Upinzani ili kuwa Kiongozi wa Kambi hiyo na inajumuisha Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni; “Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni”ni Waziri Mkuu kama ilivyoainishwa katika Ibara ya 52(2) ya Katiba; “Kitabu cha Maamuzi” ni kumbukumbu ya maamuzi mbalimbali ya Spika kuhusu suala lolote la utaratibu Bungeni; “Madaraka ya Bunge” ni haki na madaraka ya Bunge kama yalivyofafanuliwa katika Ibara ya 100 ya Katiba na katika Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge; “Maisha ya Bunge” ni muda wote unaoanzia tarehe ambapo Bunge Jipya limeitishwa na Rais kukutana kwa mara ya kwanza baada ya Uchaguzi Mkuu na kuishia tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge kama ilivyoelekezwa na Ibara ya 65 ya Katiba; “Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri ya Muungano; “Mkutano wa Bunge” ni mfululizo wa vikao vya Bunge, kuanzia kikao cha kwanza hadi cha mwisho; “Mgeni” maana yake ni mtu yeyote ambaye si Rais, Mbunge, Katibu au mtumishi yeyote na ambaye hatekelezi kazi rasmi zinazohusu Bunge; “Mpambe wa Bunge” ni mtumishi wa Ofisi ya Bunge anayetekeleza majukumu yaliyoainishwa katika Kanuni ya 20 ya Kanuni hizi; “Mwenyekiti” ni Mbunge aliyechaguliwa kuongoza Shughuli za Bunge na pia lina maana ya Spika, Naibu Spika au Mbunge mwingine anapokuwa anaongoza Kamati ya Bunge Zima, Kamati ya Matumizi au Kamati ya Mipango na vilevile inajumuisha Mbunge yeyote anayeongoza Kamati ya Kudumu, Kamati Ndogo ya Kamati ya Kudumu, Kamati Teule au Mkutano wa Uchaguzi wa Spika; “Naibu Spika” ni Mbunge aliyetajwa kuwa Naibu Spika wa Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 85 ya Katiba na kuchaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 10 ya Kanuni hizi; “Naibu Waziri” ni Mbunge aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu wa Ibara ya 55(2) na (3) ya Katiba; “Orodha ya Shughuli” ni karatasi mahususi zinazoonesha mpangilio wa Shughuli za Bunge katika kila kikao cha Bunge; “Rais” ni mtu aliyechaguliwa kushika Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyoelekezwa katika Ibara ya 33 ya Katiba; “Shughuli za Serikali” ni shughuli zinazowasilishwa Bungeni na Waziri au na Mwanasheria Mkuu wa Serikali;
Sura ya 296, Toleo la 2002
4
“Siwa” ni rungu la dhahabu linalotumika kama kielelezo cha mamlaka ya Bunge ambalo hubebwa na Mpambe wa Bunge akimtangulia Spika wakati wa kuingia na kutoka kwenye Ukumbi wa Bunge kabla na baada ya kikao cha Bunge; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 84 ya Katiba na kuchaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 9 ya Kanuni hizi; “Taarifa Rasmi” ni taarifa za majadiliano ya Bunge zilizotajwa katika Kanuni hizi; “Tume ya Huduma za Bunge” ni Tume iliyoanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Tume ya Huduma za Bunge, Sura ya 115, Toleo la 2002; “Waziri” ni Mbunge aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu wa Ibara ya 55 ya Katiba; “Wimbo wa Taifa” ni Wimbo wa Taifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
SEHEMU YA PILI
UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA BUNGE
Uongozi wa Bunge
4. Spika atachaguliwa na Wabunge kwa mujibu wa Kanuni ya 9 na kushika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba na Kanuni hizi.
5.-(1) Katika kutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika Ibara ya 84 ya Katiba, Spika ataongozwa na Kanuni hizi na pale ambapo Kanuni hazikutoa mwongozo, basi Spika atafanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturi za Mabunge mengine yenye utaratibu wa kibunge unaofanana na utaratibu wa Bunge la Tanzania.
(2) Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, na Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifu Spika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.
(3) Spika anaweza kumtaka Mbunge yeyote anayekiuka Kanuni hizi kujirekebisha mara moja.
(4) Mbunge yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika anaweza kuwasilisha sababu za kutokuridhika kwake kwa Katibu wa Bunge ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.
Spika
Mamlaka ya Spika
5
(5) Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na Kamati hiyo.
(6) Spika au Naibu Spika hatakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni za Bunge inapokaa kujadili uamuzi unaolalamikiwa, bali wajumbe watachagua Mwenyekiti wa muda kwa asilimia 50 ya kura za siri.
(7) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, wakati wowote ambapo Spika hayupo Bungeni au kwa sababu nyingine yoyote hawezi kutekeleza madaraka au majukumu ya Spika, basi madaraka au majukumu ya Spika yatatekelezwa na Naibu Spika.
6.-(1) Naibu Spika aliyetajwa katika Ibara ya 85(1) ya Katiba, atachaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 10 kutoka miongoni mwa Wabunge na kushika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba na Kanuni hizi.
(2) Naibu Spika atakuwa msaidizi wa Spika katika kuliongoza Bunge na atatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Kanuni hizi.
(3) Spika anaweza wakati wowote bila kutoa taarifa rasmi kwa Bunge kumtaka Naibu Spika au Mwenyekiti kuongoza Shughuli za Bunge.
(4) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, wakati wowote ambapo Spika na Naibu Spika wote hawapo Bungeni au kwa sababu nyingine yoyote, hawawezi kutekeleza madaraka au majukumu yao, basi madaraka au majukumu hayo yatatekelezwa na Mwenyekiti wa Bunge.
(5) Naibu Spika anaweza wakati wowote, bila kutoa taarifa rasmi kwa Bunge, kumtaka Mwenyekiti wa Bunge kuongoza Shughuli za Bunge.
7.-(1) Kutakuwa na Wenyeviti watatu wa Bunge ambao watachaguliwa na Wabunge kutoka miongoni mwao kwa kuzingatia jinsia na pande za Muungano.
(2) Kamati ya Uongozi itapendekeza majina ya Wabunge sita ambayo yatawasilishwa Bungeni ili kupigiwa kura.
(3) Wenyeviti wa Bunge wanaweza kuongoza shughuli za Bunge kwa utaratibu na maelekezo ya Spika au Naibu Spika kwa mujibu wa Kanuni hizi.
Majukumu ya Wenyeviti wa Bunge
Majukumu ya Naibu Spika
6
(4) Endapo Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge wote hawapo, Wabunge watamchagua mmoja wa Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge kuendesha Shughuli za Bunge kufuatana na utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi.
8. Kwa kuzingatia matakwa na masharti yaliyowekwa na kiapo cha kazi zake na kwa madhumuni ya utoaji wa maamuzi na uendeshaji wa Shughuli za Bunge kwa haki na bila upendeleo, Spika:-
(a) Ataendesha shughuli za Bunge na kutoa maamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki wala upendeleo wowote, kwa kuongozwa na Katiba, Sheria za nchi, Kanuni hizi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya maspika wa Bunge waliotangulia na pia kwa kuzingatia uzoefu pamoja na mila na desturi za mabunge mengine yanayofuata utaratibu wa kibunge unaofanana na unaofuatwa na Bunge la Tanzania;
(b) Hatafungwa na msimamo utakaowekwa au makubaliano yatakayofikiwa na Kamati yoyote ya Chama cha Siasa kinachowakilishwa Bungeni.
Uchaguzi wa Viongozi wa Bunge
9.-(1) Kutakuwa na Uchaguzi wa Spika utakaofanyika kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 84 (1) ya Katiba pamoja na Kanuni hizi.
(2) Kila Chama cha Siasa kitakuwa na haki ya kupendekeza jina moja la Mbunge wa Chama hicho ambaye atakuwa mgombea wa nafasi ya Spika, kwa mujibu wa Katiba.
(3) Majina ya wagombea wasio Wabunge yatawasilishwa na vyama husika kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi siku tano kabla ya uchaguzi.
(4) Baada ya kupokea majina hayo, Tume itayachambua na kisha itawasilisha majina ya wagombea wenye sifa kwa Katibu siku mbili kabla ya uchaguzi.
(5) Endapo wamependekezwa wagombea wawili au zaidi, uchaguzi utafanyika kwa kufuata utaratibu ulioainishwa katika fasili zinazofuata za Kanuni hii.
Uadilifu kwa Kiongozi wa Bunge
Uchaguzi wa Spika
7
(6) Mgombea yeyote anaweza kumtaarifu Katibu kwa maandishi kwamba anajitoa kugombea, kabla ya shughuli za kupiga kura kuanza Bungeni, na Katibu atalifuta jina la mgombea huyo katika karatasi za kura.
(7) Mwanzoni mwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, mara baada ya Katibu kusoma Tangazo la Rais na Kikao kujigeuza kuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Spika, Katibu atamwomba Mbunge asiye mgombea wa nafasi ya Spika kutoka miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa Wabunge kwa mfululizo kwa muda mrefu, awe Mwenyekiti wa Mkutano huo wa Uchaguzi.
(8) Kabla ya kikao cha Bunge cha kumchagua Spika kuanza, Katibu ataandaa karatasi za kura zitakazoonesha majina ya wagombea wote waliopendekezwa na wakati wa kupiga kura atatoa karatasi moja tu ya kura kwa kila Mbunge.
(9) Mbunge ambaye kabla ya shughuli za uchaguzi kumalizika atakosea katika kuweka alama kwenye karatasi ya kura ataruhusiwa kumrudishia Katibu karatasi hiyo, na papo hapo Katibu ataifuta na kuiharibu kisha kumpa Mbunge huyo karatasi nyingine.
(10) Kila Mbunge atapiga kura ya siri kwa kuweka katika karatasi ya kura alama ya “V” katika mraba pembeni mwa jina la Mgombea anayemtaka awe Spika, na ataitumbukiza karatasi hiyo katika sanduku la kura.
(11) Baada ya Katibu kuridhika kwamba Wabunge wote waliomo Bungeni wamepiga kura na kutumbukiza karatasi zao za kura kwenye masanduku ya kura, masanduku yote yatakusanywa na kuwekwa mahali panapoonekana na baada ya hapo masanduku hayo ya kura yatapelekwa kwenye chumba maalumu na kura hizo zitahesabiwa chini ya usimamizi wa wawakilishi walioteuliwa na wagombea, mmoja mmoja kwa kila mgombea.
(12) Endapo zoezi hili la uchaguzi litaendeshwa kwa mfumo wa elektroniki wa upigaji kura basi upigaji na uhesabuji kura utakuwa wa papo kwa papo na matokeo yake yatakuwa halali.
(13) Mgombea atakuwa amechaguliwa kuwa Spika kama atapata zaidi ya nusu ya kura za Wabunge wote na iwapo hakutakuwa na mgombea aliyepata zaidi ya nusu ya kura hizo, uchaguzi utarudiwa lakini ni wagombea wawili tu waliopata kura nyingi zaidi ndio
8
watakaopigiwa kura, na katika hatua hiyo, mgombea atakayepata kura nyingi zaidi atatangazwa kuwa mshindi.
(14) Endapo wagombea wawili au zaidi watapata kura sawa katika nafasi ya mwanzo, basi wagombea hao tu ndiyo watakaopigiwa kura na mgombea atakayepata kura nyingi zaidi atakuwa ndiye mshindi.
(15) Iwapo wagombea wawili au zaidi watapata kura sawa katika nafasi ya pili na yule wa kwanza hajapata zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa, basi wagombea hao wawili pamoja na yule wa kwanza ndio watakaopigiwa kura na mgombea atakayepata kura nyingi zaidi atakuwa ndiye mshindi.
(16) Endapo awamu ya pili ya upigaji kura itashindwa kumpata mshindi, basi Mwenyekiti atapiga kura yake ya uamuzi ili mshindi apatikane.
(17) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja tu basi mgombea huyo atapigiwa kura ya “Ndiyo” au “Hapana” na atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa Spika iwapo atapata kura za “Ndiyo” za idadi ya zaidi ya nusu ya kura za Wabunge wote.
(18) Mara baada ya mshindi kupatikana, Katibu atamtangaza Spika aliyechaguliwa na Spika huyo Mteule ataapa viapo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni hizi.
(19) Muda wa Spika Mteule kuapishwa utakapowadia, Mwenyekiti atamwita Spika Mteule ajongee mbele ya Bunge ili aape viapo vinavyohusika.
(20) Mtu au Mbunge yeyote aliyechaguliwa kuwa Spika, kabla ya kushika madaraka yake, ataapa mbele ya Bunge Kiapo cha Utii na Kiapo cha Spika vitakavyokuwa na maneno yafuatayo:
Kiapo cha Utii:
“Mimi, …………..….. naapa kwamba, nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wangu wote na kwamba, nitaihifadhi, nitailinda na kuitetea Katiba ya Tanzania kwa mujibu wa Sheria iliyowekwa. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”
9
Kiapo cha Spika:
“Mimi, …………., naapa kwamba, nitaitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangu kama Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheo hicho nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuni za Bunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano na kwa vyovyote vile sitatoa siri za Bunge. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”
(21) Wakati wa kuapa, Spika anayeamini kuwa kuna Mungu, atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifu kinachotambuliwa na imani ya dini yake.
(22) Iwapo Spika haamini kuwa kuna Mungu, basi hatashika Biblia au Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno “Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkono wake wa kuume juu.
10.-(1) Kutakuwa na uchaguzi wa Naibu Spika wa Bunge katika nyakati zilizowekwa na Ibara ya 86(1) ya Katiba na utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi.
(2) Uchaguzi wa Naibu Spika utafanyika katika Mkutano wa Kwanza wa Bunge jipya, au mapema iwezekanavyo baada ya wakati huo au katika kikao cha kwanza cha Bunge mara baada ya nafasi ya Naibu Spika kuwa wazi, au mapema iwezekanavyo baada ya kikao hicho.
(3) Uchaguzi wa Naibu Spika utaendeshwa kwa utaratibu ule ule unaotumika kumchagua Spika, isipokuwa kwamba, Mbunge hawezi kushiriki katika uchaguzi wa Naibu Spika iwapo hajaapa Kiapo cha Uaminifu.
(4) Mbunge yeyote atakayechaguliwa kuwa Naibu Spika, kabla ya kushika madaraka yake, ataapishwa na Spika Kiapo cha Naibu Spika ambacho kitakuwa na maneno yafuatayo:-
“Mimi, …………., naapa kwamba, nitaitumikia vema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangu kama Naibu Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheo hicho nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuni za Bunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano na kwa vyovyote vile sitatoa siri za Bunge. “Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.”
Uchaguzi wa Naibu Spika
10
(5) Wakati wa kuapa, Naibu Spika anayeamini kuwa kuna Mungu, atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifu kinachotambuliwa na imani yake ya dini.
(6) Iwapo Naibu Spika haamini kuwa kuna Mungu, hatashika Biblia au Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno“Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkono wake wa kuume juu.
11.-(1) Uchaguzi wa Wenyeviti wa Bunge utafanyika kwa kuzingatia jinsia na pande za Muungano na kwa kufuata utaratibu kwamba:-
(a) karatasi ya kura itakuwa na majina ya Wabunge sita ambao wamependekezwa na Kamati ya Uongozi kupigiwa kura kutoka miongoni mwa Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge;
(b) kila Mbunge atapiga kura kwa kuchagua majina matatu katika orodha hiyo; na
(c) wagombea watatu watakaopata kura nyingi zaidi kuliko wenzao ndio watakuwa wamechaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge.
(2) Wenyeviti wa Bunge waliochaguliwa kwa mujibu wa masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii watashika madaraka yao kwa muda ambao wataendelea kuwa Wenyeviti au Makamu Wenyeviti wa Kamati zao za Kudumu za Bunge mpaka mwisho wa Mkutano unaofuata mara baada ya Mkutano wa Kumi wa Bunge (ambao ndio hukamilisha nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge) utakaofanyika baada ya kuchaguliwa kwao, lakini wanaweza kuchaguliwa tena kuwa Wenyeviti wa Bunge katika kipindi cha pili kilichobaki cha maisha ya Bunge la kipindi kinachohusika iwapo watachaguliwa tena kuwa Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge.
12. Uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katika vyombo vingine ambavyo kwa mujibu wa Sheria zilizounda vyombo hivyo vinatakiwa viwe na wawakilishi wa Bunge na uchaguzi wa kuwachagua Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki utafanywa kwa kuzingatia, kwa kadri iwezekanavyo, uwiano wa idadi ya Wabunge wa Vyama mbalimbali vya Siasa vinavyowakilishwa Bungeni, uwakilishi wa jinsia na uwakilishi wa pande zote mbili za Muungano.
Uchaguzi wa Wabunge wanao- kwenda kwenye vyombo vingine vya uwakilishi
Uchaguzi wa Wenyeviti wa Bunge
11
13. Endapo Waziri Mkuu ambaye ndiye Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni hatakuwepo Bungeni kwa kipindi kinachozidi siku moja, basi atamteua Waziri mwingine kuwa Kiongozi wa muda wa Shughuli za Serikali Bungeni.
14.-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwa chini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasili za Kanuni hii zinazofuata.
(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge wote.
(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya Wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge wote.
(4) Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimoja ambavyo kila kimoja kina Wabunge asilimia kumi na mbili na nusu au zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kuliko vingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwili au zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimia kumi na mbili na nusu, Wabunge wa vyama vinavyohusika watachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibu watakaokubaliana wenyewe.
15.-(1) Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
(2) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateua Wabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.
16.-(1) Chama kinachounda Serikali na Chama chenye haki ya kuchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, vitateua Wanadhimu wa vyama hivyo Bungeni ambao watajulikana kwa jina la Mnadhimu wa Serikali na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. (2) Vyama hivyo vitateua pia Wanadhimu Wasaidizi ambao idadi yao itaamuliwa na vyama vyenyewe.
Uteuzi wa Wana- dhimu wa vyama Bungeni
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni
Kiongozi wa muda wa Shughuli za Serikali Bungeni
12
(3) Mnadhimu wa Serikali atakuwa kiungo cha mawasiliano kati ya Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni na Wabunge wa Chama kinachounda Serikali na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani atakuwa ni kiungo cha mawasiliano kati ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Wabunge wa Upinzani.
(4) Vyama vya Siasa vyenye uwakilishi Bungeni vinaweza kutunga Kanuni za vyama kwa ajili ya uendeshaji bora wa shughuli za vyama hivyo Bungeni.
17.-(1) Katibu wa Bunge kama alivyotajwa kwenye Ibara ya 87(1) ya Katiba, atawajibika kuhakikisha utekelezaji bora wa Shughuli za Bunge na kwa madhumuni hayo:-
(a) atahudhuria au atawakilishwa katika vikao vyote vya Bunge na vya Kamati ya Bunge Zima na vikao vya Kamati nyingine yoyote ya Bunge;
(b) atawajibika kuweka kumbukumbu zinazotakiwa ziwekwe kwa mujibu wa Kanuni hizi;
(c) atatayarisha Taarifa Rasmi za majadiliano ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni hizi;
(d) atatayarisha siku hadi siku, Kitabu cha Shughuli za Bunge na kukihifadhi Ofisini kwake, kikiwa kinaonesha:
(i) maagizo yote yaliyotolewa na Bunge;
(ii) shughuli zote zilizopangwa kufanywa siku yoyote ya baadaye;
(iii) taarifa zote za maswali na hoja zilizokubaliwa na Spika.
(2) Katibu atawajibika kutunza Kitabu cha Maamuzi ya Spika, Kitabu cha Shughuli, Taarifa Rasmi, Miswada ya Sheria na Hati nyingine zilizowasilishwa Bungeni, na Mbunge au mtu yeyote anaweza kukagua kumbukumbu hizo wakati wowote unaofaa kwa kufuata utaratibu utakaowekwa na Spika.
(3) Katibu ataweka kumbukumbu za maamuzi ya mara kwa mara ya Spika kuhusu masuala ya utaratibu Bungeni.
Majukumu ya Katibu wa Bunge
13
(4) Katibu atawajibika kuhakikisha kuwa, Ukumbi wa Mikutano ya Bunge na mazingira yake, huduma kwa Wabunge na vifaa vingine vinavyohusika na Shughuli za Bunge, viko katika hali inayofaa kuliwezesha Bunge kutekeleza wajibu wake ipasavyo.
18.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi kuhusu uwekaji wa nafasi na ngazi za utumishi katika Ofisi ya Bunge, Ofisi hiyo itakuwa na Idara, Sehemu na Vitengo mbalimbali kwa namna na idadi ambayo itaiwezesha kutoa huduma bora na kamilifu kwa Bunge, Wabunge na Kamati za Bunge.
(2) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, kutakuwa na Makatibu Wasaidizi wa Bunge, kwa idadi na ngazi mbalimbali kadri itakavyoamuliwa na Tume ya Huduma za Bunge iliyoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Uendeshaji wa Bunge.
(3) Kutakuwepo na watumishi wengine wa Bunge ambao nyadhifa, kazi na idadi yao vitaamuliwa na Tume ya Huduma za Bunge.
19. Kutakuwa na Mpambe wa Bunge ambaye atatekeleza shughuli mbalimbali za Bunge kwa kufuata maagizo atakayopewa na Spika, Naibu Spika, Mwenyekiti au Katibu, kwa kadri itakavyokuwa.
20.- (1) Pamoja na kutekeleza shughuli mbalimbali kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 19, Mpambe wa Bunge:-
(a) atasimamia masuala yote ya ulinzi na usalama wa ofisi, mali, vifaa na majengo yote ya Bunge;
(b) atahakikisha utulivu na amani katika sehemu wanayokaa wageni na atawawekea utaratibu maalum wa kuingia na kutoka Bungeni; na
(c) atamtangulia Spika, akiwa amebeba Siwa, wakati Spika anapoingia na anapotoka kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Bunge.
(2) Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake wakati wa vikao vya Bunge, Mpambe wa Bunge anaweza kutoa maagizo anayoona yanastahili kutolewa kwa wahudumu wa Bunge, na wahudumu hao watawajibika kutekeleza maagizo hayo.
(3) Mpambe wa Bunge atawajibika kuratibu na kushauri juu ya usalama wa Ukumbi, majengo na vyumba vyote vya Bunge na pia
Ofisi ya Bunge
Mpambe wa Bunge
Majukumu ya Mpambe wa Bunge
14
sehemu zote za majengo yote yanayotumiwa na Bunge au Kamati za Bunge au Wabunge au watumishi wa Bunge.
(4) Mpambe wa Bunge atakuwa na uwezo wa kutoa maagizo kwa askari mwingine yeyote aliyekabidhiwa kutekeleza majukumu kwenye Ukumbi wa Bunge na mazingira yake au kwenye majengo, vyumba au sehemu nyingine zinazotumiwa kwa ajili ya kutekeleza shughuli za Bunge kwa mujibu wa Kanuni hizi.
21.-(1) Kutakuwa na Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria ambaye atakuwa Msaidizi Mkuu wa Katibu wa Bunge kwa masuala yote yanayohusu Sheria. Pamoja na kazi nyingine, Mshauri wa Bunge wa Mambo ya Sheria atashughulikia mambo yafuatayo:- (a) kutoa ushauri wa kisheria kuhusu Miswada yote ya Sheria inayowasilishwa Bungeni;
(b) kuchambua Miswada ya Sheria inayowasilishwa Bungeni na kuwasaidia Wabunge kupata uelewa sahihi wa Miswada hiyo;
(c) kutoa ushauri kwa Bunge kupitia Kamati ya Kanuni za Bunge kuhusu marekebisho yoyote yanayohitajika kufanyika katika Kanuni za Kudumu za Bunge;
(d) kutoa huduma za ushauri wa kisheria kwa Kamati za Bunge na Wabunge kila atakapohitajika kufanya hivyo;
(e) kuandaa Miswada ya Sheria ya Kamati, Miswada Binafsi ya Sheria na Hoja Binafsi za Wabunge;
(f) kusaidia Wabunge kutayarisha marekebisho ya Muswada wa Sheria unaowasilishwa Bungeni;
(g) kuwa ndiye mwakilishi rasmi wa Bunge katika masula yote ya kisheria na kwa madhumuni hayo, anaweza kushirikiana na wanasheria wengine kuliwakilisha Bunge au Tume ya Huduma za Bunge endapo Bunge au Tume ya Huduma za Bunge itashtaki au itashtakiwa;
(h) kuhakikisha kuwa Muswada wowote wa Sheria uliopitishwa na Bunge unachapishwa kama
Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria na majukumu yake
15
ulivyopitishwa na Bunge na kuwasilishwa kwa Rais kwa ajili ya kupata kibali cha Rais na nakala moja kupelekwa kwa Spika; na
(i) kushughulikia masuala yote ya Sheria yatakayopelekwa kwake na uongozi wa Bunge.
(2) Masuala ya Sheria yanayotoka kwa Mbunge mmoja mmoja au Kamati yoyote ya Bunge yatapelekwa kwa Katibu wa Bunge ambaye atayakabidhi kwa Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria ili kuyafanyia kazi katika kipindi atakachoelekezwa.
(3) Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria atateuliwa na Tume ya Huduma za Bunge kutoka miongoni mwa wanasheria waandamizi.
SEHEMU YA TATU
MIKUTANO NA VIKAO VYA BUNGE
22.-(1) Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya utafanyika mahali, tarehe na saa ambayo Rais atatamka wakati akiitisha Mkutano wa Bunge Jipya.
(2) Bila ya kuathiri Masharti ya Kanuni hizi kuhusu kuanza na kufungwa kwa vikao vya Bunge, Mkutano wa Kwanza wa Bunge utaendelea kwa muda wowote ambao utahitajika kwa ajili ya kutekeleza na kukamilisha shughuli zote za Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya.
23.-(1) Shughuli za Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya zitakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Kusomwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge; (b) Uchaguzi wa Spika; (c) Kiapo cha Spika; (d) Wimbo wa Taifa na Dua; (e) Kiapo cha Uaminifu kwa Wabunge wote; (f) Hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu; (g) Uchaguzi wa Naibu Spika; (h) Ufunguzi rasmi wa Bunge Jipya utakaofanywa na Rais; (i) Hoja ya kujadili Hotuba ya Rais; na (j) Shughuli yoyote ambayo Bunge litaona inafaa kushughulikiwa kwa wakati huo.
Mkutano wa kwanza wa Bunge
Shughuli za Mkutano wa Kwanza wa Bunge
16
(2) Mwanzoni mwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, Katibu atasoma Tangazo la Rais la kuitisha Bunge Jipya.
(3) Mara baada ya Tangazo la Rais kusomwa, Kikao kitajigeuza kuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Spika.
(4) Katibu atamwomba Mbunge asiye mgombea wa nafasi hiyo ya Spika kutoka miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa Wabunge kwa mfululizo kwa muda mrefu awe Mwenyekiti wa Mkutano huo wa Uchaguzi.
(5) Katibu wa Bunge atagawa karatasi za kura kwa Wabunge, na uchaguzi wa Spika utafanywa kwa kuzingatia utaratibu na Kanuni hizi.
(6) Baada ya Uchaguzi wa Spika kumalizika na mshindi kutangazwa, Mwenyekiti atasitisha Mkutano wa Uchaguzi wa Spika na kutaja muda ambao Spika Mteule ataapishwa.
(7) Baada ya Spika Mteule kuapishwa atakalia kiti chake na kutoa hotuba fupi ya shukrani kwa Bunge na kisha ataliahirisha Bunge hadi wakati mwingine atakaoutaja ambapo shughuli za kuapisha Wabunge wote Kiapo cha Utii zitaanza.
24.-(1) Kila Mbunge ataapa Kiapo cha Utii kitakachokuwa na maneno yafuatayo:
“Mimi,…………….., naapa kwamba, nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wangu wote na kwamba, nitaihifadhi, nitailinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Sheria iliyowekwa. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”
(2) Wakati wa kuapa, Mbunge anayeamini kuwa kuna Mungu, atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifu kinachotambuliwa na imani ya dini yake.
(3) Iwapo Mbunge yeyote haamini kuwa kuna Mungu, hatashika Biblia au Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno, “Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkono wake wa kuume juu.
25.-(1) Baada ya shughuli ya kuwaapisha Wabunge kukamilika, Spika atasoma Taarifa ya Rais inayotaja jina la Mbunge
Kiapo cha utii kwa Wabunge
Kuthibi- tisha Uteuzi wa Waziri Mkuu
17
anayempendekeza kuwa Waziri Mkuu ili aweze kuthibitishwa na Bunge.
(2) Baada ya Spika kutaja jina la Mbunge anayependekezwa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali atatoa hoja ya kuliomba Bunge lithibitishe uteuzi wa Mbunge husika kuwa Waziri Mkuu.
(3) Baada ya kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu, Bunge litamchagua Naibu Spika.
(4) Iwapo Bunge litakataa kumthibitisha Waziri Mkuu, Spika atamjulisha Rais kuhusu uamuzi huo wa Bunge.
26.-(1) Baada ya uchaguzi wa Naibu Spika, Spika atalitangazia Bunge mahali, siku na muda ambao Rais atalihutubia na kulifungua rasmi Bunge Jipya na baada ya Tangazo hilo, Spika anaweza:-
(a) kuahirisha Shughuli za Bunge hadi wakati huo; au (b) kuahirisha Kikao cha Bunge hadi siku na muda atakaoutaja.
(2) Rais atakapowasili katika viwanja vya Bunge, atapokelewa na Spika akifuatana na Waziri Mkuu na kisha atakaribishwa ili alihutubie na kisha kulifungua Rasmi Bunge Jipya.
(3) Baada ya hotuba ya Rais, Waziri Mkuu atatoa hoja ya kuahirisha Bunge hadi mahali, siku na muda atakaoutaja.
27.-(1) Isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo, kila Mkutano wa Bunge utafanyika katika ukumbi wa Bunge Dodoma.
(2) Wimbo wa Taifa utapigwa na kuimbwa katika kila kikao cha kwanza na cha mwisho kwa Mikutano yote ya Bunge kufuatana na utaratibu utakaowekwa na Bunge.
(3) Bila ya kuathiri masharti yanayofuata ya Kanuni hii, kila Mkutano isipokuwa Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, utaanza tarehe itakayowekwa na Bunge.
(4) Endapo manufaa ya Taifa yatahitaji kuwa Bunge lisikutane tarehe ile iliyowekwa kwa Mkutano utakaofuata, bali likutane tarehe ya mbele zaidi au ya nyuma zaidi, basi Spika anaweza, baada ya kushauriana na Kamati ya Uongozi, kuliita Bunge likutane tarehe hiyo ya mbele zaidi au nyuma zaidi.
Ufunguzi Rasmi wa Bunge Jipya
Mikutano ya kawaida ya Bunge
18
(5) Iwapo Bunge litatakiwa kukutana tarehe ya mbele zaidi kuliko tarehe iliyotangazwa awali, basi tarehe hiyo mpya haitakuwa mbele zaidi ya siku kumi na nne kutoka tarehe iliyotangazwa hapo awali.
28.-(1) Vikao vya Mikutano ya Bunge, isipokuwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, vitaanza saa 3.00 asubuhi, ila tu, kama Bunge litaamua vinginevyo.
(2) Bunge litakutana hadi saa 7.00 mchana ambapo Spika ataahirisha shughuli yoyote itakayokuwa inafanyika hadi saa 11.00 jioni, isipokuwa kama Spika akiona inafaa, Bunge linaweza kuendelea kukutana kwa muda usiozidi dakika 30 au kusitishwa wakati wowote kabla ya saa 7.00 mchana baada ya kuwahoji Wabunge.
(3) Hoja ya kubadilisha nyakati za vikao itatolewa na Waziri na itaamuliwa kama hoja nyingine yoyote na haitahitaji kutolewa taarifa.
(4) Bunge litaendelea kukaa hadi saa 1.45 usiku wakati ambapo Spika atasitisha shughuli na kuliahirisha hadi kesho yake au siku nyingine atakayoitaja.
(5) Iwapo shughuli zilizopangwa kwa siku hiyo zimemalizika kabla ya saa 1.45, Spika ataliahirisha Bunge bila kuhoji, lakini iwapo zimesalia dakika kumi kabla ya kufikia muda wa kuahirisha kikao, na Bunge au Kamati ya Bunge Zima au Kamati ya Matumizi bado haijamaliza shughuli zake, Spika anaweza kuongeza muda usiozidi dakika thelathini, bila kulihoji Bunge au Kamati ya Bunge Zima au Kamati ya Matumizi ili kukamilisha shughuli zilizobaki.
(6) Iwapo wakati wa kusitisha shughuli umefika na Spika atakuwa analihoji au yupo karibu kulihoji Bunge, basi hatasitisha shughuli mpaka hoja iwe imeamuliwa.
(7) Baada ya hoja kuamuliwa, Waziri atatoa hoja ya kuahirisha Kikao cha Bunge hadi kesho yake au siku nyingine itakayotajwa.
(8) Endapo Spika atakuwa amepokea taarifa ya Mbunge yeyote anayetaka kutoa maelezo binafsi, basi Spika hataliahirisha Bunge bali ataongeza muda usiozidi dakika thelathini bila ya kulihoji Bunge ili kutoa nafasi kwa Mbunge huyo aweze kutoa maelezo yake, isipokuwa kwamba, maelezo hayo sharti yawe
Muda wa Vikao vya Bunge
19
yameandikwa na kuwasilishwa kwa Spika angalau siku moja kabla hayajatolewa na Mbunge anayehusika atalazimika kuyasoma kama yalivyowasilishwa.
(9) Baada ya kusitisha Shughuli za Bunge, hakuna shughuli nyingine yoyote itakayofanywa katika kikao hicho na Spika ataliahirisha Bunge hadi kesho yake au siku nyingine itakayotajwa.
(10) Endapo majadiliano yoyote katika Bunge au katika Kamati ya Bunge Zima yatasitishwa na Spika kwa mujibu wa masharti ya Kanuni hii, wakati yatakaporudiwa katika Bunge au katika Kamati, yataendelezwa kuanzia hapo yalipositishwa na Mbunge yeyote ambaye hotuba yake ilikatizwa na Spika atakuwa na haki ya kuendelea na maelezo yake katika marudio ya mjadala huo na endapo Mbunge hakuitumia haki yake hiyo, basi atahesabiwa kuwa alikuwa amemaliza hotuba yake.
(11) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni hii, wakati Spika anapotaka kuliahirisha Bunge, wakati huo unaweza kutumiwa kama fursa kwa Mbunge yeyote kutaka ufafanuzi utolewe na Waziri juu ya jambo lolote lililo chini ya madaraka ya Waziri huyo au kuanzisha mjadala juu ya jambo lolote la dharura kwa idhini ya Spika, isipokuwa kwa jambo ambalo haliwezi kujadiliwa bila hoja maalumu kutolewa kwanza kwa ajili hiyo.
(12) Jambo lolote haliwezi kuwasilishwa na kujadiliwa kwa mujibu wa Kanuni hii, isipokuwa tu kama Mbunge amewasilisha kwa Spika Taarifa ya maandishi siyo chini ya saa ishirini na nne kabla ya kutolewa kwa jambo hilo Bungeni akieleza kwa ufupi msingi wa jambo analotaka kuzungumzia.
(13) Jumla ya dakika zisizozidi thelathini zitatumika kwa mtoa hoja kuwasilisha Bungeni hoja yake pamoja na majadiliano na maamuzi ya Bunge kwa hoja husika.
(14) Iwapo dakika thelathini zitapita tangu Spika alipotaka kuliahirisha Bunge chini ya fasili ya (7) na (10) ya Kanuni hii, basi Spika atasitisha majadiliano yanayoendelea.
(15) Iwapo shughuli zote zilizopangwa kwa ajili ya kikao hazijamalizika, Spika atalihoji Bunge kuhusu hoja ya kuahirisha kikao cha Bunge na baada ya hoja hiyo kuafikiwa, atakiahirisha kikao hicho hadi kikao kinachofuata ambacho, kama Bunge halikuamua
20
vinginevyo, kitakuwa ni siku itakayofuata, isipokuwa tu kama itakuwa ni siku ya Jumamosi, Jumapili au siku ya mapumziko.
(16) Pale inapotokea dharura yoyote ndani ya Ukumbi wa Bunge, Spika anaweza kusitisha Shughuli za Bunge bila kulihoji Bunge.
29.-(1) Kila Mkutano wa Bunge utafungwa kwa kuliahirisha Bunge hadi Mkutano utakaofuata.
(2) Endapo shughuli zote zilizowekwa kwenye Orodha ya Shughuli kwa ajili ya Mkutano huo zimemalizika, hoja ya kuahirisha Bunge itakayotolewa na Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni itataja siku, mahali na saa ambapo Mkutano unaofuata utaanza.
(3) Mara tu baada ya Bunge kupitisha hoja ya kuahirisha Mkutano wa Bunge, Wimbo wa Taifa utapigwa na kuimbwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Bunge.
SEHEMU YA NNE
SHUGHULI ZA BUNGE
30.-(1) Rais anaweza kulihutubia Bunge siku yoyote ambayo Bunge linakutana na wakati mwingine wowote kwa mujibu wa Ibara ya 91 ya Katiba.
(2) Wakati wa kuanza Kikao cha Kwanza cha Mkutano wowote wa Bunge baada ya Wimbo wa Taifa kupigwa na kuimbwa na Dua kusomwa au kwa vikao vinavyofuata, Dua pekee kusomwa na Spika kukalia kiti chake:-
(a) kama Spika amepata taarifa kuwa Rais anakusudia kulihutubia Bunge siku hiyo, Spika atalitangazia Bunge ni wakati gani Rais atafanya hivyo;
(b) wakati uliopangwa kwa ajili ya Rais kulihutubia Bunge utakapofika, Spika atampokea Rais na kumkaribisha alihutubie Bunge; na
(c) baada ya hotuba ya Rais, Spika anaweza ama kusitisha kikao kwa muda ili amsindikize Rais au kuliahirisha Bunge hadi siku nyingine itakayotajwa.
Kuahirisha Bunge
Mpangilio wa Shughuli za Bunge
21
(3) Baada ya kushauriana na Kamati ya Uongozi, Spika atatenga muda kwa ajili ya kujadili hotuba ya Rais.
(4) Shughuli za Bunge zitaendeshwa kwa mpangilio ufuatao:-
(a) kuwaapisha Wabunge wapya Kiapo cha Uaminifu; (b) taarifa ya Rais; (c) taarifa ya Spika; (d) kuwasilisha Maombi; (e) hati za kuwasilisha Bungeni; (f) maswali kwa Waziri Mkuu; (g) maswali ambayo taarifa zake zimetolewa; (h) hoja za kuahirisha shughuli ili kujadili mambo muhimu ya dharura; (i) kauli za Mawaziri; (j) maelezo binafsi ya Mbunge; (k) mambo yahusuyo haki za Bunge, ikiwa ni pamoja na kuzifanyia mabadiliko Kanuni za Bunge; (l) shughuli za Serikali; (m) hoja au taarifa za Kamati; (n) hoja binafsi za Wabunge; na (o) shughuli yoyote ambayo Bunge litaona inafaa kushughulikiwa kwa wakati huo.
(5) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii na baada ya kushauriana na Kamati ya Uongozi, katika kila Mkutano wa Bunge Spika atatenga muda mahususi kwa ajili ya Bunge kushughulikia Hoja Binafsi na Miswada ya Kamati na Miswada Binafsi ya Wabunge kama itakuwepo.
(6) Shughuli za Bunge katika kila kikao zitatekelezwa kwa kufuata Orodha ya Shughuli za siku hiyo au kwa kufuata utaratibu mwingine ambao Spika ataagiza ufuatwe kwa ajili ya uendeshaji bora wa shughuli za Bunge.
31. Dua ya kuiombea nchi yetu na kuliombea Bunge itasomwa na Spika, itakuwa na maneno yafuatayo:-
“Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba Mbingu na Dunia, Umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu na Mabunge ya Mataifa ili haki yako itendeke. Twakuomba, uibariki nchi yetu idumishe uhuru, umoja, haki na amani, Umjalie Rais wetu hekima, afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri,
Dua ya kuio- mbea nchi yetu na kulio- mbea Bunge
22
wadumishe utawala bora. Utuongezee hekima na busara, sisi Wabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na utupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbele yetu leo, ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa nchi yetu. Amina.”
32.-(1) Taarifa ya Rais, kama ipo, itasomwa na Spika.
(2) Kila inapowezekana, taarifa ya Rais itasomwa Bungeni kwa kufuata mpangilio wa Shughuli za Bunge, lakini Spika anaweza, wakati wowote, kusitisha shughuli za Bunge kwa madhumuni ya kuwezesha taarifa hiyo isomwe.
33.-(1) Spika atatoa taarifa Bungeni kuhusu Miswada yote iliyopitishwa na Bunge katika Mkutano wake uliotangulia, yaani kama imekubaliwa na Rais au kama Rais ametoa uamuzi mwingine.
(2) Wakati wa kikao, Spika anaweza kutoa taarifa nyinginezo kadri atakavyoona inafaa.
34.-(1) Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha Bungeni maombi kuhusu jambo lolote kwa niaba ya watu wanaotoa ombi hilo, na ombi hilo halitawasilishwa Bungeni mpaka kwanza taarifa ya ombi hilo iwe imetolewa kwa maandishi na kupokelewa na Katibu si chini ya siku mbili za kazi kabla ya Mkutano ambapo ombi hilo linakusudiwa kuwasilishwa.
(2) Ombi lolote linaweza kuwasilishwa Bungeni na Mbunge, likionesha jina la Mbunge anayeliwasilisha.
(3) Mbunge anayewasilisha ombi atatoa maelezo mafupi ya kutambulisha watu wanaotoa ombi hilo, idadi yao, saini zilizoambatanishwa kwenye ombi hilo, madai ya msingi yaliyomo, na madhumuni ya ombi hilo.
(4) Baada ya kutimiza masharti ya fasili ya (3) ya Kanuni hii, Mbunge anayewasilisha ombi anaweza kutoa hoja kwamba, Bunge lijadili ombi hilo, isipokuwa kwamba hoja hiyo haitahitaji kutolewa taarifa na inaweza kuamuliwa bila mjadala wowote.
(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kuwasilisha ombi linalomhusu yeye mwenyewe au ambalo yeye amelitia saini yake au ambalo linakiuka masharti yanayohusiana na utaratibu wa kutunga Sheria kuhusu mambo ya fedha.
Taarifa ya Rais
Taarifa ya Spika
Kuwasili sha maombi na taarifa ya ombi
23
35. Ombi lolote halitawasilishwa Bungeni isipokuwa tu kama Spika ataridhika kuwa limezingatia masharti yafuatayo:- (a) limeandikwa katika lugha ya Kiswahili au Kiingereza; na
(b) limeandikwa kwa lugha fasaha, ya heshima na linahitimishwa kwa maelezo ya jumla kuhusu madhumuni ya ombi hilo.
36. Nakala ya kila ombi itawasilishwa kwa Katibu si chini ya siku zisizopungua mbili za kazi kabla ya siku ya kuwasilishwa Bungeni.
37.-(1) Hati inaweza kuwasilishwa Bungeni wakati wa vikao vya Bunge na:- (a) Waziri; au (b) Mwanasheria Mkuu wa Serikali; au (c) Kamati yoyote ya Bunge; au (d) Mbunge yeyote.
(2) Nakala za matoleo yote ya Gazeti pamoja na Nyongeza zake zilizochapishwa tangu kikao cha mwisho cha Mkutano wa Bunge uliopita, zitawasilishwa Bungeni na Waziri na kugawiwa kwa Wabunge.
(3) Hati zote zitawasilishwa Bungeni bila kutolewa hoja yoyote kwa ajili hiyo.
(4) Baada ya hati kuwasilishwa Bungeni, Waziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali au Mbunge, anaweza kutoa hoja kwamba Bunge lijadili hati hiyo.
(5) Hoja inayotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii haitahitaji kutolewa taarifa na itaamuliwa bila ya mabadiliko au mjadala wowote.
(6) Hoja ya kujadili hati iliyowasilishwa Bungeni ikikubaliwa, itashughulikiwa kwa kufuata Mpangilio wa Shughuli za Bunge.
(7) Taarifa zinazowasilishwa Bungeni na Kamati yoyote ya Kudumu, Kamati Teule, Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali pamoja na Mapendekezo ya Matumizi ya Nyongeza ya Fedha zitatengewa muda wa kujadiliwa Bungeni bila hoja kutolewa.
(8) Taarifa ambazo Sheria inaelekeza ziwasilishwe Bungeni zitajadiliwa na Kamati husika za Kudumu za Bunge.
Masharti kuhusu Maombi
Nakala ya Maombi
Hati za kuwasili- sha Bungeni
24
(9) Mjadala unaweza kuzingatia kila jambo lililomo katika hati, isipokuwa kama Spika, kwa kuzingatia uendeshaji bora wa shughuli za Bunge, ataamua vinginevyo.
38.- (1) Waziri Mkuu anaweza kuulizwa maswali na Mbunge yeyote ambayo yatazingatia masharti kuhusu maswali ya Bunge pamoja na Mwongozo uliowekwa na Nyongeza ya Sita ya Kanuni hizi.
(2) Maswali atakayoulizwa Waziri Mkuu hayatakuwa na taarifa ya awali kama maswali mengine.
(3) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kitakuwa kila siku ya Alhamisi na hakitazidi dakika thelathini.
(4) Waziri Mkuu anaweza kutumia Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kutoa taarifa au ufafanuzi kuhusu suala lolote linalohusiana na shughuli za Serikali na lenye maslahi kwa umma kwa muda usiozidi dakika kumi, ikifuatiwa na maswali ya Wabunge kwa dakika ishirini kuhusu taarifa yake au masuala mengine yoyote ya Serikali.
(5) Iwapo siku hiyo, kwa sababu maalum, Waziri Mkuu hatakuwepo Bungeni hakutakuwa na maswali kwa Waziri Mkuu.
(6) Maswali kwa Waziri Mkuu yatafuatiwa na maswali mengine kwa Mawaziri kwa dakika sitini kama yatakavyokuwa yamepangwa kwenye Orodha ya Shughuli ya siku hiyo.
39.-(1) Waziri anaweza kuulizwa maswali kuhusu masuala yoyote ya umma au jambo lingine lolote ambalo linasimamiwa na Ofisi yake, na vilevile Mbunge yeyote anaweza kuulizwa maswali kuhusu mambo yoyote anayohusika nayo kutokana na kuteuliwa na Bunge kushughulikia mambo hayo.
(2) Maswali yanayoulizwa kwa mujibu wa Kanuni hii yatakuwa mafupi kwa kadri inavyowezekana na kila swali litahusu jambo moja tu mahususi.
(3) Madhumuni halali ya swali lolote yatakuwa kutekeleza Ibara ya 63(2) na (3)(a) ya Katiba.
(4) Taarifa ya swali itatolewa kwa maandishi na itapelekwa na
Maswali kwa Waziri Mkuu
Maswali na taarifa ya Maswali
25
kumfikia Katibu si chini ya siku ishirini na moja kabla ya tarehe ambayo jibu linahitajiwa kutolewa.
(5) Taarifa haitatolewa Bungeni kwa mdomo, isipokuwa kwamba, taarifa zote za maswali zitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli za Bunge kuonesha kuwa zimepokelewa na maswali yote yaliyopangwa kujibiwa yatawekwa kwenye Orodha ya Shughuli za siku inayohusika.
(6) Waziri aliyeulizwa swali atatoa jibu lake papohapo wakati wa kipindi cha Maswali.
(7) Endapo swali halikuwahi kujibiwa siku hiyo kwa sababu ya muda wa maswali kumalizika, litapangiwa nafasi ya kujibiwa baadaye katika Mkutano huo unaoendelea. Kama siku inayohusika ndiyo siku ambapo Mkutano wa Bunge unafungwa, swali hilo litajibiwa katika Mkutano unaofuata.
(8) Bunge linapovunjwa, maswali yote ambayo hayakuwahi kujibiwa yatajibiwa kwa maandishi.
(9) Kwa madhumuni ya fasili ya (1), endapo swali lililoulizwa limeelekezwa kwa Mbunge, basi kwa idhini ya Spika, Mbunge ambaye swali limeelekezwa kwake atapewa fursa ya kujibu swali hilo.
(10) Maswali yatajibiwa Bungeni kwa mdomo. Lakini endapo Mbunge mwenye swali hayupo Bungeni kuuliza swali lake, na Spika hakutoa ruhusa kwa swali hilo kuulizwa na Mbunge mwingine, basi Waziri aliyeulizwa swali atapeleka kwa Katibu jibu la maandishi naye Katibu ataliingiza jibu hilo kwenye Taarifa Rasmi.
(11) Katika hali ya kawaida, Mbunge haruhusiwi kuuliza zaidi ya maswali manne yanayohitaji majibu ya mdomo katika Mkutano mmoja wa Bunge.
(12) Endapo kwa maoni ya Spika, swali lililoulizwa na Mbunge siyo la sera na majibu yake ni marefu au linahitaji takwimu, basi swali hilo litajibiwa kwa maandishi na litaorodheshwa kwenye Orodha ya Shughuli na kuonyesha kwamba limejibiwa kwa maandishi na Wabunge wote watagawiwa nakala.
26
(13) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (11) ya Kanuni hii, swali aliloulizwa Waziri mmoja laweza kujibiwa na Waziri mwingine au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
(14) Maswali yote katika Mkutano mmoja yatapewa namba zinazofuatana kwa mfululizo na namba zilizotolewa kwa kila swali zitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli za Bunge.
(15) Maswali yote ambayo yamepangwa kujibiwa katika Kikao kimoja, yanaweza kuwekwa pamoja kwenye Orodha ya Shughuli na kujibiwa kwa zamu kadri itakavyooneshwa kwenye Orodha ya Shughuli.
40. Swali lolote la Bunge halitaruhusiwa kuulizwa Bungeni kama:-
(a) linakiuka Kanuni yoyote ya Bunge;
(b) linashutumu tabia au mwenendo wa mtu yeyote ambaye mwenendo wake unaweza tu kujadiliwa kwa hoja maalumu;
(c) linahitaji habari ambazo zinapatikana katika hati ambazo Mbunge anaweza kujisomea mwenyewe kama vile nakala za Sheria au maandiko ya kumbukumbu za kawaida.
(d) limekusudiwa kupata maoni ya kisheria ya kinadharia au kutoa mapendekezo juu ya jambo la kubahatisha tu;
(e) lina maelezo ya dhihaka, uongo, sifa zisizolazimu, au linatokana na habari za kubahatisha tu;
(f) lina madhumuni ya kutoa habari, au linaulizwa kwa njia inayoonesha jibu lake au kutambulisha mkondo fulani wa maoni;
(g) linahusu jambo zaidi ya moja na ni refu kupita kiasi; au
(h) linamtaja mtu yeyote kwa jina au kutoa maelezo mahususi juu yake ila tu kama ni lazima ili kulifanya lieleweke.
Masharti kuhusu Maswali ya Bunge
27
41. Mbunge anayeuliza swali anaweza kuliondoa swali lake wakati wowote kabla halijajibiwa-
(a) kwa kuwasilisha barua ya kufanya hivyo kwa Katibu iwapo siku iliyopangwa kwa swali hilo kujibiwa haijafika; au
(b) iwapo swali husika tayari limewekwa kwenye Orodha ya Shughuli, kwa kusimama mahali pake jina lake linapoitwa wakati wa maswali na kutamka kuwa analiondoa swali lake na kueleza kwa kifupi sababu za kufanya hivyo.
42.-(1) Wakati swali linalohusika litakapofikiwa katika Orodha ya Shughuli, Spika atamwita Mbunge mwenye swali hilo au kama hayupo, Spika atamwita Mbunge mwingine yeyote aulize swali hilo kwa niaba ya Mbunge mwenye swali.
(2) Mbunge atakayeitwa atasimama na kuuliza swali, pamoja na masahihisho (kama yapo), kwa kutamka maneno yafuatayo bila ya kuongeza jambo lingine lolote:-
“Naomba swali langu (atataja namba ya swali lake lililopo kwenye Orodha ya Shughuli) sasa lijibiwe.”
43.-(1) Muda wa Maswali Bungeni utakuwa dakika tisini, isipokuwa katika Mkutano wa Bunge la Bajeti, ambapo muda utakuwa dakika sitini.
(2) Spika anaweza kuweka kiwango cha juu cha maswali yatakayowekwa katika Orodha ya Shughuli ambayo anaona yanaweza kujibiwa katika muda uliowekwa.
44.-(1) Maswali ya nyongeza yanaweza kuulizwa na Mbunge yeyote kwa madhumuni ya kupata ufafanuzi zaidi juu ya jambo lolote lililotajwa katika jibu lililotolewa.
(2) Mbunge anayeuliza swali la msingi ataruhusiwa kuuliza maswali ya nyongeza yasiyozidi mawili na Mbunge mwingine yeyote atakayepewa nafasi ataruhusiwa kuuliza swali moja tu la nyongeza.
(3) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, swali ambalo litawekwa katika vifungu vya (a) na (b) litahesabiwa kuwa ni maswali mawili.
Maswali ya Nyongeza
Kuondoa Maswali
Jinsi ya Kuuliza Maswali
Muda wa Maswali
28
(4) Isipokuwa kama Spika ataelekeza vinginevyo, Wabunge watakaouliza maswali ya nyongeza hawatazidi watatu kwa swali moja la msingi, na Mbunge hataruhusiwa kusoma swali lake.
45.-(1) Swali lolote la nyongeza ambalo linaleta mambo yasiyotokana au kuhusiana na swali la msingi au linakiuka masharti yanayohusiana na taratibu za kuulizwa maswali litakataliwa.
(2) Endapo Spika atakataa swali la nyongeza kwa kukiuka masharti ya Kanuni hizi, swali hilo halitajibiwa wala halitaoneshwa kwenye Taarifa Rasmi.
(3) Iwapo Spika ataridhika kuwa, swali la msingi au la nyongeza halijapata majibu ya kuridhisha, ataagiza lijibiwe kwa ufasaha zaidi katika kikao kingine cha Bunge.
46.-(1) Waziri anayeulizwa swali atakuwa na wajibu wa kulijibu swali hilo kwa ukamilifu kama lilivyoulizwa, isipokuwa kwamba, kama jibu linalohusika ni refu au lina takwimu nyingi, Waziri atampa Mbunge muuliza swali nakala ya jibu mapema baada ya kikao kuanza, kabla ya muda wa kujibu swali hilo haujafikiwa.
(2) Endapo Mbunge muuliza swali atamwomba Waziri ampatie nakala ya jibu la swali lake kabla ya muda wa kujibu swali hili haujafikiwa basi Waziri anaweza kumpa Mbunge muuliza swali nakala ya jibu kama lilivyoombwa.
(3) Waziri Mkuu au Waziri mwingine yeyote au Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza kutoa majibu ya nyongeza kwa majibu yaliyotolewa na Waziri.
47.-(1) Baada ya Muda wa Maswali kwisha, Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja kuwa Shughuli za Bunge kama zilivyooneshwa kwenye Orodha ya Shughuli ziahirishwe ili Bunge lijadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa umma.
(2) Hoja ya namna hiyo itakuwa ni maalumu na inaweza kutolewa wakati wowote hata kama majadiliano yatakuwa yanaendelea.
(3) Hoja itatolewa na Mbunge kwa kusimama mahali pake na kuomba idhini ya Spika kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge kwa madhumuni ya kujadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa umma.
Maswali kujibiwa kikamilifu
Kuahirisha Shughuli za Bunge ili Kujadili Jambo la Dharura
Maswali ya nyongeza yasiyo- ruhusiwa
29
(4) Iwapo Spika ataridhika kwamba jambo hilo ni la dharura, halisi na lina maslahi kwa umma, basi ataruhusu hoja hiyo itolewe kwa muda usiozidi dakika tano na mjadala juu ya hoja hiyo utaendelea kwa muda ambao Spika ataona unafaa kwa kuzingatia mazingira ya suala linalojadiliwa.
48.-(1) Masharti ya jumla yafuatayo yatatumika vilevile kuhusu hoja ya kujadili suala la dharura:-
(a) hoja hiyo haitaruhusiwa iwapo inahusu jambo ambalo kwalo taarifa ya hoja imekwisha kutolewa au jambo ambalo limekwisha kuwekwa kwenye Orodha ya Shughuli;
(b) hoja zaidi ya moja katika kikao kimoja zenye kutaka kuahirisha Shughuli za Bunge kwa kutumia Kanuni hii hazitaruhusiwa; au
(c) jambo ambalo litakuwa limejadiliwa katika hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge iliyotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii, halitaletwa tena Bungeni katika Mkutano ule ule kwa kutumia Kanuni hii.
(2) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa tu kuwa ni jambo halisi, iwapo:-
(a) ni jambo mahususi;
(b) halikuwekwa katika lugha ya jumla mno au lina mambomengi mchanganyiko;
(c) halikutolewa kwa kutegemea habari zisizo za uhakika au habari halisi juu ya jambo hilo hazipatikani; au
(d) halihusu mambo ya kinadharia.
(3) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa kuwa ni jambo la dharura, iwapo:-
(a) athari zake ni dhahiri na linaweza kutokea wakati wowote;
Masharti ya jumla kuhusu Jambo la Dharura
30
(b) limetokea siku hiyo au siku za karibuni na limeletwa bila kuchelewa; au
(c) hakutatokea fursa ya kulijadili siku za karibuni kwa njia ya kawaida ya kushughulikia mambo ya Bunge.
(4) Jambo lolote litahesabiwa kuwa ni lenye maslahi kwa umma iwapo utatuzi wake unategemea hatua zaidi kuliko zile za utekelezaji wa kawaida wa sheria peke yake.
49.-(1) Waziri anaweza kutoa kauli Bungeni kuhusu jambo lolote linaloihusu Serikali.
(2) Kauli za aina hiyo zinaweza kutolewa kwa idhini ya Spika katika wakati unaofaa kufuatana na mpangilio wa Shughuli za Bunge na zitahusu jambo mahususi, halisi na zisizozua mjadala na muda wa kusema utakuwa ni dakika zisizozidi thelathini.
(3) Waziri mwenye kutoa kauli atawajibika kutoa nakala ya kauli yake kwa Wabunge wote wakati anapoiwasilisha Bungeni.
50.-(1) Mbunge yeyote anaweza, kwa idhini ya Spika kutoa maelezo binafsi Bungeni yanayolenga kufafanua kuhusu jambo lolote linalomhusu na lililoifikia jamii.
(2) Mbunge anayekusudia kutoa maelezo binafsi atapaswa kuwasilisha maelezo hayo mapema kwa Spika na muda wa kusema utakuwa ni dakika zisizozidi kumi na tano, na maelezo hayo hayatakuwa na mjadala kuhusu jambo hilo.
51.-(1) Mbunge anayetaka kuwasilisha jambo ambalo anaamini linahusiana na haki za Bunge atafanya hivyo wakati unaofaa kufuatana na mpangilio wa Shughuli za Bunge uliowekwa na Kanuni hizi na atakuwa amemwarifu Spika mapema kuhusu kusudio lake hilo na jambo ambalo anataka kuliwasilisha.
(2) Spika akimwita Mbunge anayetaka kuwasilisha jambo ambalo anaamini linahusiana na haki za Bunge, Mbunge huyo ataeleza kwa kifupi sababu zinazofanya aamini kwamba jambo analoliwasilisha linahusu haki za Bunge zilizotajwa kwenye Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.
Masuala yanayo- husu Haki za Bunge
Sura ya 296, Toleo la 2002
Maelezo Binafsi ya Wabunge
Kauli za Mawaziri
31
(3) Endapo Spika ataamua kwamba jambo hilo linahusu haki za Bunge, basi atampa nafasi Mbunge mhusika kutoa hoja yake kisha hoja hiyo itapewa kipaumbele katika kupanga shughuli nyingine zote za kikao kinachohusika.
(4) Mambo yanayohusu haki za Bunge yatawasilishwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa katika Kanuni hizi na endapo wakati wa kikao chochote cha Bunge jambo lolote litazuka ghafla ambalo litaonekana linahusu haki za Bunge, shughuli zitasitishwa kwa madhumuni ya kuliwezesha jambo hili kuwasilishwa na kuamuliwa, isipokuwa tu kama wakati huo kura inapigwa.
52.-(1) Shughuli za Serikali zitaanza wakati Spika atakapomwita Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyetoa taarifa ya kuwasilisha Muswada au ya kutoa hoja Bungeni baada ya Katibu kusoma jambo linalohusika kwenye Orodha ya Shughuli.
(2) Baada ya Spika kutoa wito huo, Mbunge yeyote binafsi hataruhusiwa kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge wala kuuliza swali.
53.-(1) Isipokuwa kama Kanuni hizi zimeagiza vinginevyo, hakuna mjadala wowote utakaoendeshwa Bungeni ila tu kuhusu shughuli iliyoingizwa kwenye Kitabu cha Orodha ya Shughuli za Bunge na kuwekwa kwenye Orodha ya Shughuli za kikao hicho.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, Waziri au Mbunge mwingine anaweza, kwa kutoa hoja, kupendekeza kwamba, suala lolote lijadiliwe Bungeni na hoja hiyo itaamuliwa kwa mujibu wa masharti ya Kanuni hizi.
(3) Isipokuwa kama Spika ataamua vinginevyo, kila hoja ambayo taarifa yake imekubaliwa itapelekwa kwanza kwenye Kamati inayohusika.
(4) Endapo hoja itapelekwa kwenye Kamati inayohusika, Kamati hiyo itaanza kuishughulikia hoja hiyo mapema iwezekanavyo, na haitatolewa Bungeni mpaka Mwenyekiti wa Kamati hiyo atakapokuwa amemtaarifu Spika kwamba, Kamati imemaliza kuishughulikia hoja hiyo.
(5) Kamati iliyopelekewa hoja kwa mujibu wa Kanuni hii inaweza kufanya mabadiliko katika hoja hiyo kwa kushauriana na mtoa hoja husika.
Hoja zitakazo- tolewa Bungeni
Shughuli za Serikali
32
(6) Endapo hoja haikupelekwa kwenye Kamati na imewekwa kwenye Orodha ya Shughuli au kama ilipelekwa kwenye Kamati na Kamati hiyo imemaliza kuishughulikia na imewekwa kwenye Orodha ya Shughuli, hoja itawasilishwa na kuamuliwa Bungeni kwa kufuata masharti yafuatayo:-
(a) baada ya hoja kutolewa na inapobidi kuungwa mkono Spika ataomba hoja hiyo ijadiliwe;
(b) mara baada ya mtoa hoja kuwasilisha hoja yake, Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa hoja hiyo atatoa maoni ya Kamati; na
(c) kama hoja inayohusika ni hoja ya Serikali, msemaji wa Kambi ya Upinzani atapewa nafasi ya kutoa maoni juu ya hoja hiyo na kama hoja inayohusika siyo ya Serikali, msemaji wa Serikali atapewa nafasi ya kutoa maoni ya Shughuli za Serikali juu ya hoja hiyo. Isipokuwa masharti ya fasili hii hayatahusu hoja za Kamati.
(7) Baada ya mjadala kumalizika, Spika atawahoji Wabunge ili kupata uamuzi wa Bunge.
(8) Mbunge yeyote hataruhusiwa kufufua jambo lolote ambalo Bunge lilikwisha kuliamua ama katika Mkutano huo uliopo au ule uliotangulia, wala kuwahisha shughuli ya Mkutano huo unaoendelea, isipokuwa kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi au kuwahisha shughuli ambayo itazingatiwa katika Mkutano unaoendelea.
54.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba au ya Kanuni hizi, Mbunge yeyote anaweza kupendekeza jambo lolote lijadiliwe Bungeni kwa kuwasilisha hoja, yaani kwa kutoa pendekezo lililokamilika ili lipate uamuzi wa Bunge.
(2) Jambo lolote litakalowasilishwa kwa mujibu wa Kanuni hii litawekwa katika lugha ambayo italiwezesha Bunge kufanya uamuzi ambao ni bayana.
(3) Isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi, mfumo wa maneno ya hoja inayowasilishwa Bungeni utakuwa kama ifuatavyo:-
Jinsi ya Kuwasi- lisha Hoja
33
“KWA KUWA, .................................................. NA KWA KUWA, ............................................ KWA HIYO BASI, Bunge linaazimia kwamba ...”
(4) Hoja ambayo, kwa maoni ya Spika ina lengo la kutaka jambo ambalo lilikwisha amuliwa na Bunge katika kipindi cha miezi kumi na miwili iliyopita kabla ya kikao kinachoendelea lifikiriwe tena, haitakubaliwa na Spika, isipokuwa tu kama ni hoja ya kutaka uamuzi wa Bunge uliokwisha fanyika ubadilishwe.
(5) Taarifa yoyote ya hoja ambayo inakiuka masharti ya Katiba au ya Kanuni hizi haitakubaliwa.
55.-(1). Isipokuwa kama Kanuni hizi zitaruhusu vinginevyo au kama Spika atatoa idhini yake kwa kutilia maanani udharura wa jambo lenyewe, hoja yoyote haitatolewa Bungeni mpaka iwe imewasilishwa na kupokelewa na Katibu angalau siku moja ya kazi kabla ya Mkutano ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa.
(2) Hoja yoyote itatolewa kwa maandishi na itawekwa saini na Mbunge anayeitoa kabla ya kupokelewa na Katibu kufuatana na masharti ya Kanuni hizi.
(3) Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa:-
(a) kutengua Kanuni yoyote kati ya Kanuni hizi;
(b) kuahirisha Bunge au kuahirisha mjadala;
(c) kutaka wageni waondoke Bungeni;
(d) kutaka ombi lililowasilishwa Bungeni lijadiliwe;
(e) kuahirisha Shughuli za Bunge zinazoendelea ili kujadili jambo la dharura;
(f) kuhusu jambo lolote linalohusiana na haki za Bunge; na
(g) kutaka Hati iliyowasilishwa Bungeni ijadiliwe.
(4) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (2) ya Kanuni hii, iwapo anayetoa taarifa ni Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, taarifa hiyo itawekwa saini na Waziri anayehusika au Mwanasheria Mkuu
Taarifa ya Hoja
34
wa Serikali, lakini hoja hiyo inaweza kuwasilishwa na Waziri mwingine yeyote au Naibu Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
(5) Endapo hoja ambayo kwayo taarifa iliyotolewa haitajadiliwa katika Mkutano alioutaja mtoa hoja, basi taarifa ya hoja hiyo itatenguka lakini inaweza kutolewa tena katika Mkutano mwingine.
(6) Isipokuwa tu kwa idhini maalumu ya Spika, taarifa kuhusu jambo lolote linalohitaji taarifa itolewe kwa mujibu wa Kanuni hizi, lazima taarifa hiyo itolewe.
(7) Hoja zitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli mapema baada ya kupokelewa na Katibu, na zitawekwa kwenye Orodha ya Shughuli ya kikao cha Bunge kulingana na maelekezo ya Spika.
(8) Kila hoja itawekwa kwenye Orodha ya Shughuli ikiwa kama ilivyowasilishwa au kama ilivyofanyiwa marekebisho au mabadiliko ambayo Spika ataagiza yafanyike.
(9) Spika hataruhusu hoja yoyote inayokiuka Katiba au Sheria au Kanuni za Bunge na Katibu atairudisha hoja hiyo pamoja na vielelezo vyake vyote kwa Mbunge mhusika na maelezo ya sababu za kukataliwa kwa hoja hiyo.
(10) Iwapo Mbunge anapenda kufanya mabadiliko ya maneno aliyoyatumia katika hoja anayokusudia kuitoa, anaweza kufanya hivyo kwa kutoa taarifa ya kutaka kufanya mabadiliko angalau siku moja kabla ya siku ile ambapo hoja hiyo imewekwa kwenye Orodha ya Shughuli ili ijadiliwe.
(11) Mbunge ambaye hakutoa taarifa ya kutaka kufanya marekebisho au mabadiliko katika hoja yake, anaweza kumwomba Spika afanye marekebisho au mabadiliko katika hoja hiyo wakati anawasilisha hoja yake bila ya kutoa taarifa.
(12) Pamoja na kuwa taarifa ya kutaka kufanya marekebisho au mabadiliko itakuwa imetolewa, marekebisho au mabadiliko yoyote hayatakubaliwa kama, kwa maoni ya Spika, mabadiliko hayo yanabadilisha mambo ya msingi yaliyomo katika hoja au yanabadilisha makusudio au upeo wa hoja hiyo.
56.-(1) Mbunge atakapoitwa na Spika kutoa hoja, atasimama mahali pake na kutoa hoja yake.
Utaratibu wa kujadili Hoja
35
(2) Hoja au marekebisho au mabadiliko ya hoja yoyote, yatahitaji kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua kumi na endapo hayataungwa mkono hoja au marekebisho au mabadiliko hayo yatatenguka na Katibu ataweka kumbukumbu kwenye Taarifa Rasmi kwamba, kwa kuwa hoja au marekebisho au mabadiliko hayo hayakuungwa mkono, basi hayakujadiliwa.
(3) Mbunge anaweza kuunga mkono hoja kwa kusimama tu mahali pake bila kusema lolote kuhusu hoja hiyo, kisha akakaa; lakini Mbunge aliyefanya hivyo bado atakuwa na haki ya kuizungumzia hoja hiyo hapo baadaye.
(4) Iwapo hoja imewekwa katika Orodha ya Shughuli na Mbunge mtoa hoja anapoitwa na Spika anashindwa kuitoa, hoja hiyo itatenguka, isipokuwa kama kuna Mbunge mwingine aliyeidhinishwa na mtoa hoja, anaweza kuitoa kwa niaba yake au kama mtoa hoja ametoa taarifa ya kutaka kuiahirisha, hoja hiyo itaahirishwa.
(5) Hoja inayohusu shughuli za Serikali inaweza kutolewa na Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
(6) Hoja iliyotenguka yaweza kutolewa tena baadaye, baada ya taarifa mpya kutolewa kwa mujibu wa Kanuni hizi.
(7) Endapo hakuna Mbunge zaidi anayependa kuzungumzia hoja iliyotolewa, Spika atampa mtoa hoja nafasi ya kuhitimisha hoja yake.
(8) Ikiwa muda uliotengwa umekwisha wakati Bunge liko kwenye Kamati ya Bunge Zima kujadili vifungu vya Muswada wa Sheria au katika Kamati ya Matumizi kujadili Makadirio ya Matumizi ya Serikali, basi Mwenyekiti, bila kulihoji Bunge, ataongeza muda usiozidi dakika thelathini kwa ajili ya kukamilisha kazi ya kupitisha Ibara za Muswada wa Sheria au mafungu ya fedha yaliyobaki.
57.-(1) Hoja ikishatolewa ili iamuliwe inaweza kubadilishwa kwa:- (a) kuondoa maneno fulani kwa ajili ya kuingiza maneno mengine;
(b) kuondoa maneno fulani bila kuongeza mengine; au
(c) kuingiza au kuongeza maneno mapya.
Kubadili- sha Hoja
36
(2) Kabla ya kutoa hoja hiyo, mtoa hoja atamkabidhi Katibu maandishi yenye saini yake na yanayoonesha mabadiliko anayotaka yafanywe.
(3) Kila badiliko linalopendekezwa sharti liwiane na hoja inayokusudiwa kufanyiwa mabadiliko na pia liungwe mkono na lisiingize jambo lolote ambalo, kwa maoni ya Spika, linaweza kuwasilishwa kwa hoja maalumu.
(4) Badiliko lolote halitaruhusiwa kama, kwa maoni ya Spika, linapingana moja kwa moja na hoja ya msingi iliyotolewa.
(5) Iwapo hoja ya mabadiliko inapendekeza kuondoa maneno fulani na kuingiza maneno mengine, basi mjadala juu ya suala la kufanya mabadiliko unaweza kuangalia kwa pamoja yale maneno yanayopendekezwa yaondolewe na maneno ambayo yanapendekezwa yaingizwe.
(6) Iwapo hoja inapendekeza kuondoa au kuingiza maneno, mjadala utahusu tu uondoaji au uingizaji wa maneno mapya, kadri itakavyokuwa.
(7) Hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja nyingine ya mabadiliko sharti ihusiane na hoja ya kwanza ya mabadiliko na itatolewa, itajadiliwa na kuamuliwa kabla ya ile hoja ya kwanza ya mabadiliko kufanyiwa uamuzi.
58.-(1) Endapo Mbunge anapenda kupendekeza mabadiliko yafanywe katika hoja kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi, anaweza kutoa hoja yake ya kufanya mabadiliko wakati wowote baada ya hoja anayotaka kuibadilisha kutolewa, lakini kabla Bunge halijahojiwa liifanyie uamuzi.
(2) Endapo kuna mapendekezo mawili au zaidi ya kubadilisha hoja moja, Spika atawaita watoa hoja hizo kwa kufuata mpangilio atakaoamua.
(3) Iwapo mapendekezo yote ya mabadiliko yameamuliwa, Spika ataitoa tena hoja ya awali ili ijadiliwe kama itakavyokuwa imebadilishwa.
(4) Hoja yoyote inaweza kuondolewa wakati wowote kabla hoja hiyo haijafikishwa Bungeni iwapo Mbunge mtoa hoja atatoa kwa Katibu, taarifa ya maandishi ya kuiondoa hoja hiyo.
Mabadi- liko ya Hoja na Kuondoa Hoja
37
(5) Endapo hoja imefikishwa Bungeni, mtoa hoja anaweza tu kuiondoa hoja yake kwa kusimama mahali pake na kusema “Ninaomba ruhusa kuondoa hoja” na papo hapo Spika ataliuliza Bunge kama linaafiki hoja hiyo kuondolewa na inapotokea Wabunge walio wengi watakubali, Spika atasema “Hoja inaondolewa kwa idhini ya Bunge” na hoja hiyo itakuwa imeondolewa na Bunge litaendelea na shughuli inayofuata.
SEHEMU YA TANO
KANUNI ZA MAJADILIANO
59.- Kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyote anaweza kusimama na kuchangia Bungeni katika nyakati zifuatazo:- (a) wakati wa kuchangia mjadala wa hoja yoyote iliyowasilishwa Bungeni ambayo Kanuni zinaruhusu ijadiliwe;
(b) wakati anatoa hoja ili ijadiliwe;
(c) wakati anawasilisha mabadiliko yoyote ya hoja;
(d) wakati amesimama kutaka kuzungumzia jambo lolote linalohusu utaratibu;
(e) wakati amesimama kuzungumzia jambo linalohusu haki za Bunge;
(f) wakati wa kutoa hoja ya kuahirisha shughuli za Bunge kwa madhumuni ya kujadili jambo la dharura na muhimu kwa Umma;
(g) wakati wa kutoa Maelezo Binafsi;
(h) wakati wa kuuliza au kujibu swali;
(i) wakati wa kutoa taarifa baada ya kupewa idhini ya Spika kufanya hivyo.
60.-(1) Mbunge akitaka kusema anaweza:-
(a) kumpelekea Spika ombi la maandishi; (b) kusimama kimya mahali pake; au (c) kutumbukiza kadi ya elektroniki.
Jinsi ya kupata nafasi ya kusema Bungeni
Nyakati za Mbunge kusema Bungeni
38
(2) Isipokuwa kwamba, Mbunge yeyote hataanza kuzungumza hadi aitwe na Spika ama kwa jina au wadhifa wake na kumruhusu kusema na wakati wa kusema ataelekeza maneno yake kwa Spika.
(3) Mbunge akimaliza kutoa maelezo yake atakaa kwenye nafasi yake na hapo Spika atamwita Mbunge mwingine aliyempelekea ombi la maandishi au kama Spika hakupata ombi lolote la maandishi, basi Mbunge mwingine yeyote anayetaka kujadili hoja anaweza kusimama mahali pake na kusubiri Spika amwone.
(4) Iwapo Wabunge wawili au zaidi watasimama wakati mmoja, Spika atamwita Mbunge atakayemwona kwanza.
(5) Endapo maombi ya kuchangia hoja fulani yatakuwa mengi zaidi ya muda uliotengwa kwa hoja hiyo, Spika atatoa nafasi ya kwanza kwa Wabunge ambao:-
(a) hawajachangia katika hoja zilizotangulia kujadiliwa katika Mkutano unaoendelea; au
(b) wamechangia mara chache.
(6) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (5) ya Kanuni hii, Spika atahakikisha kuwa, nafasi za kuchangia zinatolewa kwa uwiano unaofaa baina ya aina zote za Wabunge walioomba kuchangia hoja hiyo.
(7) Masharti yaliyotangulia katika Kanuni hii, hayatamzuia Spika kutoa nafasi ya kuchangia kwa Mbunge mwingine yeyote iwapo ataona kuwa, taaluma au uzoefu fulani wa Mbunge huyo utaboresha hoja inayojadiliwa.
(8) Mbunge hatasoma maelezo, isipokuwa, kwa madhumuni ya kutilia nguvu maelezo yake, anaweza kusoma dondoo kutoka kwenye kumbukumbu zilizoandikwa au kuchapishwa na anaweza pia kujikumbusha kwa kuangalia kwenye kumbukumbu alizoziandika.
(9) Kila Mbunge atasema akiwa amesimama na atatoa maelezo yake kwa kutumia vyombo vilivyowekwa kwa madhumuni ya kutafsiri, kukuza na kurekodi sauti.
(10) Kwa ruhusa ya Spika, Mbunge yeyote aliye na ulemavu au ugonjwa anaweza kuzungumza akiwa ameketi.
39
(11) Endapo Spika atasimama wakati Waziri au Mbunge anatoa hotuba Bungeni au atakuwa amesimama mahali pake akisubiri kuanza kuzungumza, Waziri au Mbunge huyo ataketi mahali pake na Bunge litabaki kimya ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake.
(12) Mbunge hataruhusiwa kuzungumzia suala lililokuwa likijadiliwa baada ya Spika kuwahoji Wabunge na hoja hiyo kutolewa maamuzi.
(13) Mbunge yeyote anaweza pia kutoa maoni yake kwa maandishi na kumpelekea Waziri au Mbunge mtoa hoja inayohusika, wakati ambapo hoja inaendelea kujadiliwa.
(14) Mtoa hoja atayakabidhi maoni hayo kwa Katibu ili yaweze kuingizwa katika Taarifa Rasmi za Bunge.
(15) Katika mjadala wowote, Mawaziri watatajwa kwa majina ya nyadhifa zao na Wabunge watatajwa kwa kutumia neno “Mheshimiwa” kabla ya majina yao.
61.-(1) Wakati wa majadiliano Bungeni au kwenye Kamati yoyote ya Bunge, Mbunge hataruhusiwa kuzungumzia jambo lolote ambalo yeye mwenyewe ana maslahi binafsi nalo ya kifedha, isipokuwa baada ya kusema jinsi anavyohusika nalo na kutaja kiwango cha maslahi hayo, na kwa sababu hiyo, itakuwa ni lazima kwa Mbunge yeyote anayetaka kuzungumzia jambo hilo Bungeni au kwenye Kamati yoyote ya Bunge, kusema kwanza jinsi anavyohusika na jambo hilo na kutaja kiwango cha maslahi ya kifedha aliyonayo kuhusiana na jambo hilo kabla ya kuanza kuzungumzia jambo hilo.
(2) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, Mbunge au mwananchi yeyote anaweza kumwarifu Spika, kwa maandishi, akitoa na ushahidi kuwa, Mbunge amezungumzia jambo ambalo ana maslahi binafsi nalo ya kifedha bila kusema jinsi anavyohusika nalo wala kutaja kiwango cha maslahi hayo.
(3) Baada ya kupokea taarifa iliyowasilishwa kwake kwa mujibu wa fasili ya (2) ya Kanuni hii, Spika ataipeleka taarifa hiyo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.
(4) Baada ya kupokea taarifa iliyopelekewa na Spika chini ya fasili ya (3) ya Kanuni hii, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaichunguza taarifa hiyo na endapo itadhihirika kwamba ni kweli Mbunge amezungumzia jambo ambalo ana maslahi binafsi nalo ya
Kuto- zungumzia jambo ambalo lina maslahi binafsi ya kifedha
40
kifedha bila kusema jinsi anavyohusika nalo wala kutaja kiwango cha maslahi hayo, Kamati hiyo ya Bunge inaweza kulishauri Bunge kwamba, Mbunge huyo aadhibiwe kwa ukiukwaji wa Kanuni hii kama ifuatavyo:- (a) ikiwa hilo ni kosa lake la kwanza, asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi;
(b) ikiwa hilo ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;
(5) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowote uliotolewa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu adhabu anayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka masharti ya Kanuni hii.
(6) Kabla ya Bunge kupitisha Azimio la kumwadhibu Mbunge kwa kuzingatia ushauri wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge utakaotolewa chini ya fasili ya (4) na (5) ya Kanuni hii, Mbunge mhusika atapewa nafasi ya kutoa utetezi wake mbele ya Bunge.
62.-(1) Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo kwenye Kanuni hizi:- (a) kila Mbunge anayejadili hoja, ataruhusiwa kusema kwa muda usiozidi dakika kumi na tano;
(b) Waziri anayetoa hoja ataiwasilisha hoja yake kwa muda usiozidi dakika thelathini na wakati anahitimisha hoja yake atasema kwa muda usiozidi dakika sitini;
(c) Mwenyekiti anayewasilisha maoni ya Kamati atayawasilisha kwa muda usiozidi dakika thelathini;
(d) Msemaji wa Upinzani anayewasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani atayawasilisha maoni hayo kwa muda usiozidi dakika thelathini; na
(e) Mbunge anayetoa hoja binafsi ataiwasilisha hoja yake kwa muda usiozidi dakika thelathini na wakati wa kuhitimisha hoja yake atasema kwa muda usiozidi dakika sitini.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii, Mbunge anayejadili hoja ataruhusiwa kusema kwa muda unaoruhusiwa na Kanuni hizi.
Muda wa kusema Bungeni
41
63.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge, ni marufuku kabisa kusema uongo Bungeni na kwa sababu hiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni ana wajibu wa kuhakikisha kwamba anatoa kauli au maelezo kuhusu jambo au suala ambalo yeye mwenyewe anaamini kuwa ni la kweli na siyo jambo la kubuni au la kubahatisha tu.
(2) Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni hatachukuliwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu jambo fulani lililotangazwa au lililoandikwa na vyombo vya habari.
(3) Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama mahali pake na kutamka “kuhusu utaratibu” na baada ya kuruhusiwa na Spika, kudai kwamba, Mbunge aliyekuwa anasema kabla yake ametoa maelezo ya uwongo kuhusu jambo au suala alilokuwa analisema Bungeni.
(4) Mbunge anayetoa madai kwa mujibu wa fasili ya (3) ya Kanuni hii atakuwa na wajibu wa kutoa na kuthibitisha ukweli kuhusu jambo au suala hilo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge.
(5) Bila ya kuathiri masharti ya fasili zilizotangulia za Kanuni hii, Spika au Mbunge mwingine yeyote, baada ya kutoa maelezo mafupi ya ushahidi unaotilia mashaka ya dhahiri kuhusu ukweli wa kauli au usemi au maelezo juu ya jambo au suala ambalo Mbunge amelisema Bungeni, anaweza kumdai Mbunge huyo atoe uthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi au maelezo yake na kama atashindwa kufanya hivyo, afute kauli au usemi au maelezo yake hayo.
(6) Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha ukweli wa kauli au usemi au maelezo yake aliyoyatoa Bungeni, atawajibika kutoa uthibitisho huo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge, papo hapo au katika muda atakaopewa na Spika kwa ajili ya kufanya hivyo.
(7) Endapo Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha kauli au usemi au maelezo yake aliyoyatoa Bungeni atashindwa kufanya hivyo, anaweza kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yake hayo, papo hapo au katika muda atakaokuwa amepewa na Spika kwa ajili ya kuthibitisha kauli au usemi au maelezo yake.
(8) Endapo hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa, Mbunge aliyetakiwa kutoa uthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi au
Kutosema uongo Bungeni
42
maelezo yake aliyoyatoa Bungeni atakataa au atashindwa kutoa uthibitisho huo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge na kama atakataa kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yake, basi Spika atamwadhibu kwa kumsimamisha Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi vitano.
(9) Endapo Mbunge mwingine yeyote ataona kwamba uwongo uliosemwa na Mbunge huyo Bungeni ni mkubwa kiasi cha kuathiri heshima ya Bunge, anaweza kutoa hoja kwamba, Mbunge huyo: -
(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza, asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi;
(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;
(c) achukuliwe hatua nyingine za kinidhamu zitakazotajwa katika hoja yake.
(10) Hoja ya aina hiyo inaweza kutolewa bila taarifa na itajadiliwa na kuamuliwa kwa utaratibu ufuatao:-
(a) Mtoa hoja atatoa hoja yake;
(b) Mbunge anayetuhumiwa kusema uongo Bungeni chini ya fasili ya (9) ya Kanuni hii atapewa nafasi ya kujitetea;
(c) Wabunge, kwa idadi itakayoamuliwa na Spika kulingana na muda uliopo, watachangia hoja hiyo kwa dakikazitakazopangwa;
(d) Mtoa hoja atahitimisha hoja yake;
(e) Mbunge anayetuhumiwa kusema uwongo Bungeni au Mbunge mwingine yeyote anaweza kutoa maombi ya adhabu iliyopendekezwa kwa kosa la kusema uongo Bungeni ipunguzwe kwa kiwango au namna atakayoipendekeza;
(f) Spika atawahoji Wabunge ili kupata uamuzi wa Bunge kuhusu ombi la kupunguziwa adhabu kama litatolewa na Mbunge anayetuhumiwa au Mbunge mwingine yeyote.
43
(g) Iwapo pendekezo la kupunguziwa adhabu litakataliwa, basi Spika atalihoji Bunge ili kupata uamuzi kuhusu adhabu iliyopendekezwa na Mtoa hoja.
64.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge, Mbunge:-
(a) hatatoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazina ukweli;
(b) hatazungumzia jambo ambalo haliko kwenye mjadala;
(c) hatazungumzia jambo lolote ambalo linasubiri uamuzi wa Mahakama au jambo lolote ambalo lilijadiliwa na kutolewa maamuzi kwenye Mkutano uliopo au uliotangulia na ambalo halikuletwa rasmi kwa njia ya hoja mahususi na vilevile hatapinga uamuzi wowote uliofanywa na Bunge, isipokuwa tu kwa kutoa hoja mahususi inayopendekeza kuwa uamuzi huo uangaliwe upya;
(d) hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katika mjadala, au kwa madhumuni ya kutaka kulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwa namna fulani;
(e) hatazungumzia mwenendo wa Rais, Spika, Mbunge, Jaji, Hakimu au mtu mwingine yeyote anayeshughulikia utoaji wa haki, isipokuwa tu kama kumetolewa hoja mahususi kuhusu jambo husika;
(f) hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusi kwa Mbunge au mtu mwingine yeyote;
(g) hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilisha watu wengine.
(2) Mbunge yeyote anayeamini kuwa Mbunge mwingine amevunja au amekiuka masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, atasimama
Mambo yasiyo- ruhusiwa Bungeni
44
mahala pake na kumwambia Spika wa Bunge “Kuhusu utaratibu” na atakaporuhusiwa na Spika kusema, atalazimika kutaja masharti ya Kanuni hii yaliyovunjwa au kukiukwa na Mbunge huyo mwingine, na kama Mbunge huyo mwingine atakuwa anasema wakati huo, atakaa chini kusubiri maelekezo na mwongozo wa Spika kuhusu jambo hilo.
65.-(1) Isipokuwa tu kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyote hataruhusiwa kusema zaidi ya mara moja juu ya hoja, ila tu kama:- (a) wakati huo Bunge liko kwenye Kamati ya Bunge Zima au Kamati ya Matumizi;
(b) anatumia haki yake ya kujibu; au
(c) anasema kuhusu utaratibu.
(2) Mbunge ambaye amezungumza juu ya hoja anaweza kuzungumza tena juu ya hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja aliyoisemea; na Mbunge ambaye amependekeza kufanya mabadiliko katika hoja ya awali, anaweza kuzungumza tena juu ya hoja ya awali baada ya mabadiliko kufanyika.
(3) Mbunge mtoa hoja ya msingi au mtoa hoja ya kutaka kufanya mabadiliko katika hoja iliyokwisha kutolewa, atakuwa na haki ya kujibu kabla uamuzi juu ya hoja hiyo haujatolewa.
(4) Wakati wa kujibu, mtoa hoja atapaswa kujibu mambo yale tu yaliyozungumzwa na Wabunge waliochangia hoja yake na hataruhusiwa kutoa maelezo yoyote mapya, isipokuwa kama maelezo hayo ni ya lazima kwa madhumuni ya kufafanua jambo lililochangiwa na Wabunge.
(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kusema Bungeni baada ya Spika kuwahoji Wabunge na kura ya sauti ama ya elektroniki au ya siri ya “ndiyo” au “siyo” au ya “kutokukubaliana” au kura ya uamuzi ya aina nyingine yoyote kupigwa, isipokuwa pale ambapo itaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura kwa kufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya 5 ya Kanuni ya 79 ya Kanuni hizi.
66.-(1) Wakati wa Vikao vya Bunge, Spika anapokuwa anaingia au kutoka katika Ukumbi wa Bunge, Wabunge na wageni wote waliopo kwenye Ukumbi huo watasimama kwa utulivu mahali pao na kubaki kimya hadi Spika atakapokuwa ameketi katika Kiti chake au atakapokuwa ametoka kwenye Ukumbi wa Bunge.
Staha ndani ya Bunge
Kuzungu- mza zaidi ya mara moja
45
(2) Wakati Bunge linaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima au katika Kamati ya Matumizi, Wabunge na wageni wote waliopo kwenye Ukumbi wa Bunge watasimama kwa utulivu mahali pao na kubaki kimya ili kutoa heshima kwa mchakato wa Bunge kuingia kwenye Kamati ya Bunge Zima au kwenye Kamati ya Matumizi na baadaye Bunge kurejea.
(3) Mbunge aliyepo Bungeni wakati wa mjadala atatakiwa:-
(a) kuingia au kutoka kwenye Ukumbi wa Bunge kwa staha na atainamisha kichwa kuelekea kwa Spika au kufanya mkunjo wa magoti kwa heshima, kila mara Mbunge huyo atakapokuwa akienda au kutoka mahali pake;
(b) kutulia na kukaa kwa heshima mahali pake, na hatatangatanga kwenye ukumbi wa Mikutano bila sababu;
(c) kutopita kati ya Kiti cha Spika na Mbunge anayesema;
(d) kutosoma kitabu chochote, gazeti au barua, isipokuwa kama vitu hivyo vinahusu shughuli za mjadala unaoendelea wakati huo; na
(e) kuzima simu ya mkononi na kwa namna yoyote kutotumia simu.
67.-(1) Spika anaweza kulihutubia Bunge wakati wowote na kwa ajili hiyo, anaweza kumkatiza Mbunge yeyote anayezungumza.
(2) Endapo Spika atasimama wakati wa mjadala, na kuanza kuzungumza, Mbunge yeyote ambaye atakuwa anazungumza wakati huo au ambaye atakuwa amesimama mahali pake akisubiri kuanza kuzungumza, ataketi mahali pake, na Bunge litabaki kimya ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake.
68.-(1) Mbunge anaweza kusimama wakati wowote na kusema maneno “kuhusu utaratibu”, ambapo Mbunge yeyote ambaye wakati huo atakuwa anasema atanyamaza na kukaa chini na Spika atamtaka Mbunge aliyedai utaratibu ataje Kanuni au sehemu ya Kanuni iliyokiukwa.
Mamlaka ya Spika kukatiza majadiliano
Taarifa kuhusu utaratibu na Mwongozo
46
(2) Mbunge aliyedai utaratibu atalazimika kutaja Kanuni au sehemu ya Kanuni ya Bunge iliyokiukwa.
(3) Baada ya kutaja Kanuni au sehemu ya Kanuni ya Bunge iliyokiukwa Mbunge aliyesimama kuhusu utaratibu, ataketi mahali pake kusubiri maelekezo na uamuzi wa Spika.
(4) Spika anaweza, ama papo hapo kutoa uamuzi wake juu ya jambo la utaratibu lililotajwa au kuahirisha uamuzi ili alifikirie zaidi jambo hilo na kutoa uamuzi baadaye au kutoa uamuzi na baadaye kutoa sababu za uamuzi huo, vyovyote atakavyoamua.
(5) Katika kufikia uamuzi wake, Spika anaweza kuitaka Kamati ya Kudumu ya Kanuni za Bunge au Kamati nyingine yoyote ya Bunge impe ushauri kuhusu jambo husika.
(6) Mbunge aliyekuwa anazungumza wakati jambo la utaratibu lilipohojiwa anaweza kuendelea na hotuba yake baada ya Spika kutoa uamuzi juu ya jambo hilo.
(7) Hali kadhalika, Mbunge anaweza kusimama wakati wowote ambapo hakuna Mbunge mwingine anayesema na kuomba “Mwongozo wa Spika” kuhusu jambo ambalo limetokea Bungeni mapema, ili Spika atoe ufafanuzi kama jambo hilo linaruhusiwa au haliruhusiwi kwa mujibu wa Kanuni na taratibu za Bunge na majibu ya Spika yatatolewa papo hapo au baadaye, kadri atakavyoona inafaa.
(8) Vilevile, Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kusema “taarifa” na kwa ruhusa ya Spika, atatoa taarifa au ufafanuzi kwa Mbunge anayesema, ambapo Spika atamtaka Mbunge anayesema aketi kusikiliza taarifa hiyo.
(9) Mtoa taarifa atakapomaliza na kuketi, Spika atamuuliza Mbunge aliyekuwa akisema mwanzo kama anaikubali au haikubali taarifa hiyo kabla ya kumruhusu kuendelea kuchangia hoja.
(10) Uamuzi wa Spika kuhusu suala lolote la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.
69.- (1) Mbunge anayependa mjadala unaoendelea juu ya hoja yoyote uahirishwe hadi wakati wa baadaye, anaweza kutoa hoja “Kwamba mjadala sasa uahirishwe” na atataja mjadala huo
Hoja ya kuahirisha Mjadala
47
uahirishwe hadi wakati gani na pia atalazimika kutoa sababu kwa nini anataka mjadala uahirishwe.
(2) Kama Spika atakuwa na maoni kwamba kuwasilishwa kwa hoja hiyo ni kinyume cha uendeshaji bora wa shughuli za Bunge, atakataa kuitoa ili iamuliwe; vinginevyo, papo hapo atawahoji Wabunge juu ya hoja hiyo kadri atakavyoona inafaa.
(3) Endapo hoja iliyowasilishwa haitapata kibali cha Bunge, mjadala kuhusu hoja iliyoko mbele ya Bunge utaendelea.
(4) Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja iliyotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii.
70.-(1) Utaratibu utakaotumika kufunga mjadala ni kutoa hoja ya kufunga mjadala endapo bado kuna Wabunge wanaopenda kuzungumza juu ya jambo lililoko katika mjadala lakini muda uliotengwa umekwisha au endapo Bunge limewekewa kiwango cha juu cha muda wa kujadili hoja inayohusika na muda huo bado haujaisha.
(2) Hoja ya kufunga mjadala inaweza kutolewa baada ya hotuba yoyote kukamilika au ikiwa Spika ataruhusu hoja ya kufanya mjadala, mara tu au muda mfupi baada ya hoja hiyo kutolewa ili iamuliwe.
(3) Mbunge anayetoa hoja ya kufunga mjadala, anaweza kusimama mahali pake na kutoa hoja “Kwamba mtoa hoja sasa apewe nafasi ya kujibu”.
(4) Endapo Spika ataona kuwa hoja ya kufunga mjadala inakiuka mwenendo bora wa Shughuli za Bunge au inavunja haki za Wabunge, basi ataikataa.
(5) Endapo hoja “Kwamba mtoa hoja sasa apewe nafasi ya kujibu” itakubaliwa, mtoa hoja atajibu kama akipenda na baada ya hotuba ya kujibu kukamilika au kama mtoa hoja hapendi kujibu basi Spika atawahoji Wabunge ili kuamua hoja hiyo.
71.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 na 101 ya Katiba, mtu yeyote asiye Mbunge ambaye atajisikia kuwa amepata athari hasi kutokana na kauli au maneno au shutuma zilizotolewa Bungeni kumhusu yeye binafsi, anaweza kupeleka malalamiko pamoja na maelezo yake ya kujitetea kwa Spika:-
Hoja ya Kufunga Mjadala
Haki ya raia kujitetea na kujisafisha dhidi ya kauli zinazoto- lewa Bungeni
48
(a) yawe yameandikwa kwa lugha fasaha na ya heshima na yanahitimishwa kwa maelezo ya jumla kuhusu madhumuni yake;
(b) yawe yamewasilishwa katika kipindi cha siku kumi nanne baada ya kauli au maneno yanayolalamikiwa kutolewa;
(c) yawe yamewasilishwa na mtu binafsi ambaye ni raia wa Tanzania na hayajawasilishwa na au kwa niaba ya Kampuni, Shirika au Taasisi;
(d) yaonyeshe wazi kuwa, kwa dhahiri mhusika aliathirika yeye binafsi kutokana na kauli au maneno au shutuma zilizotolewa Bungeni.
(e) yaeleze kwa ufasaha ni jinsi gani mhusika amepata athari hasi, kama vile kuchafuliwa jina lake na heshima yake katika jamii au kuharibu sifa, mahusiano na ushirikiano wake na wengine au kazi yake anayoifanya katika jamii au kuingilia uhuru na maisha yake binafsi na familia yake isivyo halali kutokana na kauli au shutuma zilizotolewa Bungeni.
(f) yatoe ombi kwamba, endapo kwa utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi yatakubalika, basi maelezo ya utetezi au ufafanuzi yaliyotolewa na muhusika kwa ajili ya kusafisha jina na kurejesha heshima yake yachukuliwe na Bunge kuwa ndiyo majibu sahihi ya kauli au shutuma zilizotolewa Bungeni.
(2) Mara baada ya kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwake kwa mujibu wa fasili ya (1) ya Kanuni hii na kujiridhisha kuwa malalamiko hayo yameandikwa katika lugha ya heshima na ya kistaarabu na yanatoa hoja mahususi na ambayo si ya uzushi, uongo, uchochezi au chuki binafsi; na kwamba yanastahili kufikiriwa au kufanyiwa kazi na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Spika atayapeleka malalamiko hayo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili kuyatafakari na kulishauri Bunge.
(3) Katika kuyafanyia kazi malalamiko yaliyopelekwa kwake na Spika kwa mujibu wa fasili ya (3) ya Kanuni hii, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge:-
49
(a) itakutana katika kikao cha faragha;
(b) inaweza kumhoji mtu aliyewasilisha malalamiko yake kwa Spika au Mbunge au Waziri aliyetoa Bungeni kauli au shutuma zinazolalamikiwa;
(c) haitajadili wala kutoa uamuzi kuhusu ukweli wa kauli au shutuma zilizotolewa Bungeni au ukweli wa maelezo yaliyotolewa kwenye malalamiko husika;
(d) haitatangaza maelezo yaliyomo kwenye malalamiko husika wala mwenendo wa majadiliano yake kuhusiana na malalamiko husika;
(4) Baada ya kukamilisha kazi yake, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itawasilisha Bungeni, taarifa ya uamuzi wake kuhusu malalamiko husika, pamoja na maelezo yote au sehemu ya maelezo ya malalamiko husika, kwa ajili ya kuridhiwa na Bunge.
(5) Taarifa itakayowasilishwa Bungeni na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge inaweza kupendekeza mojawapo ya yafuatayo:-
(a) maelezo ya utetezi au ufafanuzi wa mlalamikaji, kama yalivyoelezwa kwenye taarifa hiyo, yaingizwe kwenye Taarifa Rasmi za Bunge; au
(b) Bunge lisichukue hatua yoyote nyingine.
SEHEMU YA SITA
AMANI NA UTULIVU BUNGENI
72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.
(2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi anaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu na vilevile Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama na kumfahamisha Spika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katika kufanya hivyo, atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyoweka utaratibu uliokiukwa.
Mamlaka ya Spika kusimamia utaratibu
50
(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa jambo au suala alilolisema Bungeni na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anaweza kumsimamisha Mbunge huyo kuhudhuria vikao vya Bunge visivyozidi vitano.
(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahi kuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spika atalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 71 ya Kanuni hizi ili Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu hatua za kinidhamu zinazostahili kuchukuliwa dhidi ya Mbunge huyo.
73.-(1) Mbunge au Waziri atakayezungumzia jambo au mambo ambayo hayaruhusiwi na Kanuni hizi, anaweza kuamriwa na Spika au Naibu Spika au Mwenyekiti akatishe hotuba yake na kukaa mahali pake.
(2) Endapo Mbunge au Waziri atatumia maneno au lugha isiyotakiwa Bungeni, yaani lugha ya matusi, usafihi, uchokozi au lugha ya maudhi na akitakiwa na Spika ajirekebishe kwa kufuta maneno au lugha hiyo atakataa kufanya hivyo, Spika anaweza kumwamuru Mbunge huyo atoke mara moja nje ya Ukumbi wa Bunge na abaki huko nje kwa muda wote uliosalia wa kikao cha siku hiyo.
(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa maneno aliyoyasema na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa, amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anaweza kumsimamisha Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi vitano.
(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahi kuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spika atalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa kwa Mbunge mhusika.
74.-(1) Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau Mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa:-
(a) kwa maneno au vitendo, Mbunge huyo anaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au
Adhabu zinazo- weza kuto- lewa na Spika kwa ukiukaji wa Kanuni
Adhabu zinazo- weza kutolewa na Bunge kwa ukiukaji wa Kanuni
51
(b) Mbunge huyo atafanya kitendo chochote cha makusudi cha kudharau Shughuli ya Bunge au Mbunge yeyoteanayeongoza shughuli hiyo.
(2) Ikiwa maneno au vitendo vya Mbunge vilivyoainishwa katika fasili ya (1) ya Kanuni hii vimetokea wakati Bunge likiwa katika Kamati ya Bunge Zima, basi Mwenyekiti atasimamisha shughuli za Kamati na ataagiza Bunge kurudia ili kumpatia Spika fursa ya kutoa taarifa kwa Bunge kuhusu mwenendo wa Mbunge huyo na kuwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.
(3) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itajadili suala hilo na ikithibitika kuwa Mbunge husika ametenda kosa inaweza kushauri kwamba:-
(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi; au
(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;
(4) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowote utakaotolewa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu adhabu anayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka masharti ya Kanuni hii.
(5) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, Bunge linaweza kumchukulia hatua nyinginezo za kinidhamu, ikiwa ni pamoja na kumsimamisha kazi Mbunge yeyote aliyetenda kosa chini ya Kanuni hii.
(6) Adhabu yoyote itakayotolewa kwa Mbunge aliyekiuka masharti ya Kanuni hii itatolewa kupitia Azimio la Bunge ambalo litataja adhabu hiyo pamoja na sababu zake.
75.- Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge na hataingia tena katika sehemu yoyote ya Ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa, na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana na mshahara huo.
76.-(1) Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani ya Ukumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumia
Masharti kwa Mbunge aliyesima- mishwa kazi
Udhibiti wa fujo Bungeni
52
nguvu, basi anaweza kuahirisha Shughuli za Bunge bila ya hoja yoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujo hiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge.
(2) Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababisha kutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la Mbunge au majina ya Wabunge waliohusika na fujo hiyo ili Kamati hiyo iweze kulishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa.
SEHEMU YA SABA
UHALALI WA SHUGHULI
77.-(1) Akidi kwa kila kikao cha Bunge wakati wa kufanya maamuzi itakuwa ni nusu ya Wabunge wote, kama ilivyofafanuliwa katika Ibara ya 94 ya Katiba, isipokuwa kwamba, idadi hiyo haitahusu hoja kuhusu uamuzi wa kubadilisha masharti yoyote ya Katiba kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba.
(2) Mbunge yeyote aliyehudhuria anaweza kumjulisha Spika kwamba, Wabunge waliopo ni pungufu ya akidi inayohitajika kwa ajili ya shughuli inayoendelea.
(3) Endapo Spika ataridhika kwamba ni kweli idadi ya Wabunge walio ndani ya Ukumbi wa Bunge ni pungufu ya akidi inayohitajika, basi atasimamisha Shughuli za Bunge kwa muda atakaoutaja na atamwagiza Katibu kupiga kengele.
(4) Bunge litakaporudia baada ya wakati uliotajwa kukamilika, Spika atahakikisha kama idadi ya Wabunge waliopo inafikia akidi inayohitajika ili kuruhusu uamuzi kufanyika.
(5) Endapo Spika ataridhika kwamba bado idadi ya Wabunge waliomo ndani ya Ukumbi wa Bunge haifikii akidi inayohitajika basi ataahirisha Shughuli za Bunge hadi muda mwingine atakaoutaja.
78.-(1) Shughuli za Bunge hazitakuwa batili kwa sababu tu kwamba nafasi yoyote ya Mbunge ipo wazi.
79.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara za 46A, 50(3), 53A na 98 za Katiba, mambo yote yanayohitaji kuamuliwa na Bunge yataamuliwa kwa kufuata maoni ya Wabunge walio wengi waliohudhuria na kupiga kura Bungeni.
Uhalali wa maamuzi ya Bunge
Akidi ya Vikao vya Bunge
Uamuzi wa Bunge
53
(2) Spika, wakati amekalia kiti cha Spika, hatakuwa na kura ya kawaida bali atakuwa na kura ya uamuzi endapo kura za “Ndiyo” na “Siyo” zitalingana.
(3) Wakati mjadala juu ya hoja unapomalizika, Spika atawahoji Wabunge ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo kama ilivyo au baada ya kufanyiwa marekebisho au mabadiliko, Spika kwanza atataka uamuzi wa wale wanaoafiki kwa kusema: “Wale wanaoafiki waseme Ndiyo” na baadaye atataka uamuzi wa Wabunge wasioafiki kwa kusema: “Wale wasioafiki waseme Siyo.”
(4) Isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi, uamuzi juu ya mambo yote utapatikana kwa kufuata wingi wa sauti za Wabunge za “Ndiyo” au “Siyo” na Spika atatangaza matokeo ya kura kwa kusema “Naamini Walioafiki Wameshinda” au “Naamini Wasioafiki Wameshinda.”
(5) Endapo itaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura kwa kufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya (4) ya Kanuni hii, Spika ataruhusu muda upite ili kutoa nafasi kuhakikisha uamuzi wa Bunge juu ya jambo hilo na kwa muda huo, ikiwa inaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura, Mbunge yeyote anaweza kusimama na kusema “Kura zihesabiwe.”
(6) Endapo hakuna Mbunge aliyeomba kura zihesabiwe, Spika atatoa kauli ya uamuzi wa mwisho kwa kusema “Walioafiki Wameshinda” au “Wasioafiki Wameshinda”, kulingana na hali itakavyokuwa.
(7) Endapo Mbunge yeyote ataomba kura zihesabiwe, basi Spika ataamuru kura zihesabiwe ikiwa Wabunge wengine kumi au zaidi watasimama mara moja kuunga mkono maombi ya kura kuhesabiwa.
(8) Endapo Spika ataamuru kura zihesabiwe, Katibu atapiga kengele ya kuwaita Wabunge kwa muda wa dakika moja na baada ya muda huo, Spika atamwagiza Katibu kumwita Mbunge mmoja mmoja kwa jina lake na kumuuliza anapiga kura yake upande gani na kurekodi kura hiyo.
(9) Baada ya Katibu kukamilisha shughuli ya kuhesabu kura, atamjulisha Spika kuhusu kura zote za wanaoafiki, wasioafiki na wasiokuwa na upande wowote na Spika atatangaza matokeo ya hesabu hiyo ya kura.
54
(10) Orodha kamili itaandaliwa ikionyesha namna kura zilivyopigwa na itarekodiwa katika Taarifa Rasmi kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya uamuzi wa Bunge.
SEHEMU YA NANE
KUTUNGA SHERIA – MASHARTI YA JUMLA
80.-(1) Kila Muswada wa Sheria utatangazwa kwenye Gazeti katika matoleo angalau mawili, kukiwa na kitambo kisichopungua siku saba kamili kati ya toleo la kwanza na la pili.
(2) Tangazo la Kwanza la Muswada wa Sheria litatolewa na kumfikia Katibu katika muda usiopungua siku 21 kabla ya Muswada huo kusomwa Bungeni kwa Mara ya Kwanza, na litaonesha Muswada mzima, ikiwa ni pamoja na maelezo kuhusu madhumuni ya Muswada husika yaliyotiwa saini na Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
(3) Muswada wa Serikali utahesabiwa kuwa umetangazwa mara ya pili endapo itatolewa taarifa katika Gazeti inayotaja jina la Muswada, nambari na tarehe ya Gazeti ambapo Muswada ulitangazwa mara ya kwanza.
(4) Muswada wowote wa Sheria wa Serikali wa dharura hautaingizwa kwenye shughuli za Bunge bila ya kuwa na hati iliyowekwa saini na Rais inayoeleza kuwa Muswada uliotajwa katika hati hiyo ni wa dharura.
(5) Muswada huo utawasilishwa kwanza kwenye Kamati ya Uongozi ukiwa umeambatishwa na hati ya dharura ili Kamati hiyo iweze kujiridhisha iwapo Muswada husika wa sheria unastahili kuwasilishwa kwa dharura au la.
(6) Iwapo Kamati ya Uongozi itaona kuwa Muswada wa Sheria wa Serikali uliowasilishwa kwa hati ya dharura haustahili kuwasilishwa kwa dharura, Kamati hiyo itaishauri Serikali ipasavyo.
(7) Haitakuwa lazima kwa Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutoa taarifa ya Muswada wa Serikali ambao unakusudiwa kuwasilishwa Bungeni iwapo Muswada huo umekwisha kutangazwa kwenye Gazeti.
(8) Katibu atagawa kwa kila Mbunge nakala ya kila Muswada wa Sheria kama ulivyochapishwa na kutangazwa kwenye Gazeti.
Utanga- zaji wa Miswada ya Serikali
55
81.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamati yoyote ya Kudumu ya Bunge au Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha Bungeni Muswada Binafsi wa Sheria.
(2) Taarifa ya kuwasilisha Muswada Binafsi wa Sheria na Muswada wa Sheria wa Kamati itapelekwa kwa Katibu na taarifa hiyo itaeleza jina la Muswada unaopendekezwa pamoja na madhumuni na sababu zake.
(3) Baada ya taarifa kutolewa, Muswada Binafsi wa Sheria au Muswada wa Sheria wa Kamati utatangazwa katika Gazeti kama ilivyo kwa Miswada ya Sheria ya Serikali, isipokuwa kwamba, madhumuni na sababu yatawekwa saini na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge au Mbunge anayehusika.
(4) Muswada Binafsi wa Sheria utahesabiwa kuwa umetangazwa mara ya pili endapo itawekwa taarifa kwenye Gazeti inayotaja jina la Muswada, nambari na tarehe ya Gazeti ambapo Muswada ulitangazwa Mara ya Kwanza.
(5) Masharti kuhusu muda wa utangazaji wa Miswada ya Sheria yanaweza kuwekwa kando na kutenguliwa kwa hoja kutolewa na kuamuliwa kama kutawasilishwa Bungeni hati iliyowekwa saini na theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Kamati kama ni Muswada wa Kamati na kwa Muswada wa Mbunge hati iliyowekwa saini na Wabunge wasiopungua kumi inayoeleza kuwa Muswada Binafsi uliotajwa katika hati hiyo ni wa dharura.
(6) Masharti ya kujadili hoja hii yatakuwa kama yalivyo kwa upande wa Miswada ya Sheria ya Serikali.
82.-(1) Muswada wa Sheria wa Serikali utawasilishwa Bungeni na Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
(2) Muswada Binafsi wa Sheria unaweza kuwasilishwa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati yoyote ya Kudumu ya Bunge au Mbunge yeyote ambaye si Waziri.
83.-(1) Muswada wowote wa Sheria ambao umetangazwa kwenye Gazeti, unaweza kuwasilishwa Bungeni kufuatana na Orodha ya Shughuli ili Kusomwa Mara ya Kwanza na katika hatua hiyo Katibu atasoma jina refu la Muswada wa Sheria unaohusika bila hoja yoyote kutolewa kwa ajili hiyo.
Uwasili- shaji wa Muswada
Utaratibu kuhusu Miswada Binafsi
Muswada Kusomwa Mara ya Kwanza
56
(2) Hakutakuwa na mjadala wowote wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Kwanza.
84.-(1) Spika atapeleka Muswada wa Sheria kwenye Kamati inayohusika na Kamati itaanza kuujadili Muswada huo mapema iwezekanavyo
(2) Kamati iliyopelekewa Muswada itatoa matangazo au itatoa barua ya mwaliko kumwalika mtu yeyote afike kutoa maoni yake mbele ya Kamati hiyo kwa lengo la kuisaidia katika uchambuzi wa Muswada huo.
(3) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamati iliyopelekewa Muswada itakuwa na uwezo wa kufanya marekebisho katika Muswada wa Sheria kwa kumshauri Waziri au Mbunge anayehusika na Muswada huo kufanya mabadiliko, vilevile Serikali itakuwa na uwezo wa kuishauri Kamati ya Kudumu ya Bunge kuhusu kufanya marekebisho au mabadiliko juu ya Muswada Binafsi.
(4) Kabla Muswada wa Sheria uliofanyiwa mabadiliko haujawasilishwa Bungeni kwa ajili ya Kusomwa Mara ya Pili, utapelekwa kwenye Kamati inayohusika kwa madhumuni ya kuzingatia mabadiliko hayo.
85.-(1) Kamati iliyopelekewa Muswada wa Sheria itakapokamilisha kuujadili Muswada huo Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika kwa maandishi kwamba, Kamati imemaliza kujadili Muswada husika.
(2) Spika ataagiza Muswada huo uwekwe kwenye Orodha ya Shughuli kwa ajili ya kusomwa Mara ya Pili.
86.-(1) Siku ambayo Muswada wa Sheria uliokwisha kujadiliwa na Kamati umepangwa kwenye Orodha ya Shughuli, Waziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mwenyekiti wa Kamati au Mbunge mwenye Muswada husika atawasilisha hoja kwamba Muswada wa Sheria ambao atautaja kwa jina Kusomwa Mara ya Pili.
(2) Hoja ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili itakuwa kama ifuatavyo:-
“Kwamba, Muswada wa Sheria uitwao….. sasa usomwe mara ya pili”. Au kadri itakavyokuwa;
Muswada kupele- kwa kwenye Kamati
Taarifa ya Kamati
Muswada Kusomwa Mara ya Pili
57
“Kwamba, Muswada uitwao ……………… kama ulivyorekebishwa kwa mujibu wa jedwali la marekebisho au kama ulivyochapishwa upya sasa usomwe mara ya Pili.”
(3) Haitakuwa halali katika hatua hii kuleta hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja isipokuwa tu kwamba:-
(a) mabadiliko bila kutoa sababu yanaweza kutolewa kwa kusema: “Kwamba, Muswada huu usisomwe mara ya Pili sasa na badala yake usomwe baada ya ….. kuanzia …..”, na hapo muda ambao Muswada huo unaokusudiwa kusomwa utatajwa.
(b) mabadiliko yenye kutoa sababu yanaweza kutolewa kwa kusema: “Kwamba, Bunge hili likatae Muswada huu Kusomwa Mara ya Pili kwa sababu zifuatazo …….”, na hapo sababu za kupinga Muswada Kusomwa Mara ya Pili zitatajwa kwa ukamilifu.
(4) Iwapo hoja itatolewa chini ya fasili ya 3(a) na (b) ya Kanuni hii, Spika atalihoji Bunge ili kufikia uamuzi.
(5) Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa Muswada wa Sheria au Mjumbe mwingine wa Kamati aliyeteuliwa kwa ajili hiyo, atatoa maoni ya Kamati kuhusu Muswada husika.
(6) Ikiwa Muswada wa Sheria unaohusika ni Muswada wa Serikali, basi Msemaji wa Kambi ya Upinzani atatoa maoni yake juu ya Muswada husika na endapo ni Muswada Binafsi au Muswada wa Kamati, basi msemaji wa Serikali atatoa maoni yake.
(7) Mjadala wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili utahusu ubora na misingi ya Muswada huo tu.
(8) Majadiliano juu ya hoja kuhusu Muswada kama yapo yatahusu maneno yanayohusiana na hoja tu.
(9) Mbunge yeyote au Waziri anaweza, wakati wa mjadala huo, kumshauri Mtoa hoja afanye mabadiliko katika Muswada, ama mabadiliko ya jumla au yale atakayoyataja Mbunge.
58
(10) Katika hatua hii iwapo mtoa hoja anataka kufanya marekebisho au mabadiliko katika Muswada wa Sheria kutokana na ushauri uliotolewa ama katika Kamati au wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili au kwa sababu nyingine yoyote, iwapo Muswada huo ni wa Serikali atamjulisha Mwandishi Mkuu wa Sheria na iwapo Muswada husika ni wa Kamati au Binafsi atamjulisha Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria ili atayarishe na kumkabidhi Katibu ambaye atagawa kwa kila Mbunge nakala ya:-
(a) Muswada wa Sheria uliochapishwa upya ukiwa na marekebisho au mabadiliko yanayokusudiwa kufanyika; au
(b) Jedwali la Marekebisho au mabadiliko yanayokusudiwa kufanyika.
(11) Kamati au Mbunge anaweza kuwasilisha kwa Katibu, kwa maandishi, mabadiliko anayokusudia kuyafanya katika Muswada huo wakati wa Kamati ya Bunge Zima akionesha bayana mabadiliko yanayokusudiwa kufanyika katika kila Ibara inayohusika.
87.-(1) Endapo Muswada ulikwishasomwa mara ya Pili na haukuwa na mabadiliko, lakini kuna jambo au suala jipya limetokea na linahitaji kuzingatiwa, Mtoa hoja anaweza kumwomba Spika wakati wowote kabla Muswada haujapelekwa katika Kamati ya Bunge Zima kwamba, Muswada huo urejeshwe tena kwenye Kamati inayohusika.
(2) Endapo Muswada wa Sheria utapelekwa tena kwenye Kamati inayohusika, Mbunge yeyote ambaye wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili alimwomba mtoa hoja kufanya mabadiliko katika Muswada huo, anaweza kuhudhuria mkutano wa Kamati na kushiriki katika majadiliano, isipokuwa kwamba, Mbunge huyo hatakuwa na haki ya kupiga kura kuhusu uamuzi wowote wa Kamati hiyo.
(3) Kamati itakutana mapema iwezekanavyo ili kujadili mabadiliko yaliyopendekezwa.
(4) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamati inayohusika itakuwa na mamlaka ya kufanya mabadiliko katika Muswada uliopelekwa kwake kwa mujibu wa Kanuni hii kwa:-
Kureje- sha Muswada katika Kamati
59
(a) kumshauri Waziri, Kamati au Mbunge anayehusika na Muswada kufanya mabadiliko katika Muswada huo; au
(b) kupitisha Azimio la kutoa Bungeni, taarifa maalumu kuhusu Muswada huo.
(5) Baada ya Kamati kukamilisha kuujadili Muswada kwa mara ya pili, Muswada huo utapelekwa katika Kamati ya Bunge Zima.
(6) Endapo Kamati iliyojadili Muswada kwa mara ya pili itaazimia kuwa taarifa maalumu juu ya Muswada huo itolewe Bungeni, basi Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika na taarifa hiyo itatolewa na Mwenyekiti au Mjumbe mwingine wa Kamati kwa niaba ya Mwenyekiti, kabla Muswada huo haujawasilishwa katika Kamati ya Bunge Zima.
88.-(1) Mtoa hoja au Mbunge mwingine anayekusudia kuwasilisha mabadiliko katika Muswada unaojadiliwa, anaweza kumwomba Spika kwamba, hatua ya kuingia katika Kamati ya Bunge Zima iahirishwe hadi wakati atakaoutaja katika ombi lake na Spika atatoa uamuzi wake kadri atakavyoona inafaa.
(2) Mabadiliko yote yaliyopendekezwa kufanyika katika Muswada wa Sheria sharti yawekwe katika Jedwali la Mabadiliko litakaloandaliwa kwa ajili hiyo na kugawiwa kwa Wabunge na katika kujadili na ama kuyapitisha au kutoyapitisha, vyovyote itakavyokuwa, mabadiliko hayo yatashughulikiwa kwa mpangilio utakaofuata na kwa kuzingatia mtiririko wa Ibara za Muswada wa Sheria unaohusika.
(3) Kwa madhumuni ya Bunge kujadili na ama kupitisha au kutopitisha, mabadiliko yaliyopendekezwa, Mtoa hoja atapewa fursa ya kwanza kueleza mapendekezo yake kabla ya mabadiliko mengine yatakayokuwa yamependekezwa na Wabunge wengine.
(4) Mabadiliko yoyote yaliyopendekezwa kufanyika katika Muswada wa Sheria na kuwekwa katika Jedwali la Mabadiliko hayataondolewa na Mtoa hoja, isipokuwa tu kwa idhini ya Spika.
(5) Mtoa hoja anayependekeza mabadiliko kufanywa katika Muswada wa Sheria atawasilisha hoja yake ya mabadiliko hayo kwa muda wa dakika tano.
Muswada katika Kamati ya Bunge Zima
60
(6) Endapo kuna mabadiliko mengine yamependekezwa kufanyika katika Jedwali la Mabadiliko, basi mabadiliko hayo yaliyopendekezwa awali na ambayo yamo katika Jedwali la Mabadiliko hayatahesabiwa kwamba yameondolewa hadi majadiliano juu ya mabadiliko hayo yatakapokuwa yamefikia mwisho au Waziri, Kamati ya Bunge au Mbunge aliyetoa mapendekezo yaliyomo katika Jedwali la Mabadiliko atakapoomba kwa Spika mapendekezo yake yaondolewe.
(7) Mtoa hoja aliyependekeza mabadiliko yoyote kufanyika katika Muswada wa Sheria na mapendekezo hayo kuwekwa katika Jedwali la mabadiliko atapewa nafasi ya kuwasilisha na kufunga hoja yake ya mabadiliko.
(8) Baada ya Mtoa hoja kuhitimisha hoja yake ya mabadiliko, Spika atalihoji Bunge ili kupata uamuzi kuhusu hoja hiyo ya mabadiliko.
(9) Muda wa kusema katika Kamati ya Bunge Zima kwa wachangiaji mbalimbali wanaounga mkono hoja ya kufanya mabadiliko utakuwa dakika tatu.
(10) Kamati ya Bunge Zima itajadili na kupitisha au kufanya mabadiliko na kupitisha Muswada wa Sheria Ibara moja baada ya Ibara nyingine, isipokuwa kwamba, Mwenyekiti, akiona inafaa, anaweza kuihoji Kamati itoe uamuzi wake kwa sehemu moja yenye Ibara kadhaa au Ibara zote zilizomo katika sehemu moja ya Muswada.
89.-(1) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi ya kupitia Muswada wa Sheria, Bunge litarejea na Mtoa hoja atatoa taarifa Bungeni kwa maneno yafuatayo:-
“Kamati ya Bunge Zima imeupitia Muswada wa Sheria, Ibara kwa Ibara na kuukubali bila mabadiliko, naomba kutoa hoja.” au kama kuna mabadiliko yaliyofanywa kwa maneno yafuatayo:-
“Kamati ya Bunge Zima imeupitia Muswada wa Sheria, Ibara kwa Ibara na imeukubali pamoja na marekebisho yaliyofanyika, naomba kutoa hoja” na kisha atatoa hoja:
“Kwamba, Muswada wa Sheria wa ……………… sasa ukubaliwe”.
Taarifa baada ya Muswada Kusomwa Mara ya Pili
61
au kama kuna mabadiliko yaliyofanywa katika Muswada kwa maneno yafuatayo:- “Kwamba, Muswada wa Sheria wa …. Kama ulivyorekebishwa au kubadilishwa katika Kamati ya Bunge zima, sasa ukubaliwe.”
(2) Hoja ya kupitisha Muswada wa Sheria wa mabadiliko ya Katiba itaamuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba. Kwa sababu hiyo, kura zitapigwa kwa kuita jina la Mbunge mmoja mmoja katika hatua ya Muswada huo Kusomwa Mara ya Pili.
90.- Mtoa hoja anayewasilisha Muswada wa Sheria anaweza kuuondoa Muswada wakati wowote kabla ya Bunge kuhojiwa kutoa uamuzi wake, baada ya kutoa taarifa kwa Spika.
91.- Baada ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Tatu, utahesabika kuwa umepitishwa na Bunge.
92.-(1) Muswada kama ulivyopitishwa na Bunge, utatayarishwa chini ya uangalizi na usimamizi wa Katibu kwa kuingiza mabadiliko yote yaliyofanyika na atawasilisha nakala moja ya Muswada huo kwa Rais mapema ili Rais atoe kibali chake kwa mujibu wa Ibara ya 97 (1) ya Katiba na pia nakala moja kwa Spika kwa taarifa.
(2) Nakala halisi ya Sheria iliyopata kibali cha Rais itahifadhiwa na Katibu.
93.-(1) Bunge halitashughulikia hatua zaidi ya moja kwa Muswada wowote wa Sheria katika Mkutano mmoja wa Bunge.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Bunge linaweza kushughulikia Muswada wa Sheria katika hatua zaidi ya moja endapo:-
(a) hoja mahususi itatolewa kwamba Muswada huo ushughulikiwe katika hatua zaidi ya moja;
(b) Spika ataridhika na hoja hiyo; na
(c) Bunge litaafiki hoja hiyo kwa kupiga kura.
Utaratibu wa Kusoma Miswada ya Sheria
Kuondoa Muswada Bungeni
Muswada Kusomwa Mara ya Tatu na kupitishwa na Bunge
Ridhaa ya Rais na hifadhi ya Sheria
62
(3) Masharti ya Fasili ya (1) ya Kanuni hii hayatatumika kwa Muswada wa Sheria ya Fedha, Muswada wa Matumizi ya Fedha na Muswada wowote unaowasilishwa kwa hati ya dharura.
SEHEMU YA TISA
UTARATIBU WA KUTUNGA SHERIA KUHUSU MAMBO YA FEDHA
94. Ili kutekeleza majukumu yaliyoainishwa katika Ibara ya 63(3)(c) ya Katiba, Bunge litakaa kama Kamati ya Mipango katika Mkutano wake wa mwezi wa Februari ili kujadili na kushauri kuhusu mapendekezo ya mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali katika mwaka wa fedha unaofuata.
95.- Bunge halitashughulikia Muswada, hoja au ombi lolote endapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali atathibitisha kwamba, matokeo ya Muswada, hoja au ombi hilo yatakuwa ni:-
(a) kuweka masharti yanayoanzisha au kuongeza kodi yoyote au yanayoweza kuongeza kiwango cha matumizi ya fedha zitakazotolewa kutoka katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Jamhuri ya Muungano au yanayofuta au kupunguza deni lolote linalodaiwa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano; au
(b) kubadilisha mishahara, marupurupu au masharti ya utumishi, ikiwa ni pamoja na likizo, usafiri na kupandishwa cheo kwa mtumishi yeyote wa umma au kufanya mabadiliko katika Sheria, Kanuni au taratibu zinazohusu pensheni, kiinua mgongo au marupurupu mengineyo ya mtumishi wa umma au ya mjane, watoto wanaomtegemea au wawakilishi wake.
96.-(1) Waziri atapeleka kwa Katibu Makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Maendeleo ya Serikali ya Mwaka wa Fedha unaohusika na nakala ya Makadirio hayo itapelekwa na kumfikia kila Mbunge angalau siku ishirini na moja kabla ya Mkutano ambao utashughulikia Makadirio hayo.
(2) Makadirio ya Fedha za Matumizi ya Serikali yatawasilishwa Bungeni na Waziri wa Fedha kwa Hotuba kuhusu Makadirio hayo
Masharti kuhusu Miswada, Hoja na Maombi ya Fedha
Bunge kukaa kama Kamati ya Mipango
Kuwasi- lisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Serikali
63
itakayoitwa Hotuba ya Bajeti ambayo itatolewa kabla ya tarehe 20 ya mwezi Juni kwa kila mwaka.
(3) Muda wa kusoma Hotuba ya Bajeti utaamuliwa na Spika kadri atakavyoona inafaa.
(4) Hoja ya kuwasilisha Makadirio hayo itakuwa katika maneno yafuatayo; “Kwamba Bunge likubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha wa….”
(5) Siku ya kuwasilisha Bungeni Hotuba ya Bajeti, nafasi pia itatolewa kwa Waziri anayehusika na mipango au uchumi kutoa maelezo kuhusu hali ya uchumi kwa ujumla.
(6) Hotuba ya Bajeti na ya Waziri anayehusika na Mipango zitafuatiwa na hotuba za Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge inayohusika na masuala ya fedha na uchumi na Msemaji wa Kambi ya Upinzani.
(7) Muda wa kusoma maoni ya Kamati na ya Kambi ya Upinzani utakuwa dakika zisizozidi thelathini kwa kila hotuba.
97.-(1) Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti utaendelea kwa siku zisizozidi tano ambapo dakika zisizozidi kumi na tano zitatolewa kwa kila Mbunge anayetaka kuchangia Hotuba ya Bajeti.
(2) Katika hatua hii majadiliano yatahusu mambo ya jumla kuhusiana na hali ya uchumi na Mbunge yeyote hataruhusiwa kupendekeza mabadiliko katika Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali.
98.-(1) Mjadala juu ya Hotuba ya Bajeti utakapomalizika, Spika atalihoji Bunge litoe uamuzi wake wa kupitisha au kutokupitisha Bajeti ya Serikali ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 90(2)(b) ya Katiba.
(2) Uamuzi wa Bunge wa kupitisha au kutokupitisha Bajeti ya Serikali utafanywa kwa kupiga kura ya wazi kwa kuita jina la Mbunge mmoja mmoja.
99.-(1) Jumla ya siku zisizozidi hamsini zitatengwa kwa ajili ya Bunge kujadili utekelezaji wa Wizara zote kwa mujibu wa Ibara ya 63(3)(b) ya Katiba.
Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti
Utaratibu wa kuidhinisha Makadirio ya Matumizi ya Serikali
Kujadili utekele- zaji wa Bajeti za Wizara
64
(2) Shughuli za Bajeti ya Serikali zitapewa nafasi ya kwanza kabla ya shughuli nyingine yoyote, na zitawekwa kwanza kwenye Orodha ya Shughuli za Kikao kila siku hadi pale zitakapokuwa zimemalizika, isipokuwa kama Bunge litaamua vinginevyo.
(3) Asubuhi ya siku ambayo Waziri amepangiwa kuwasilisha hoja ya Makadirio ya Wizara yake, Waziri huyo, Mwenyekiti wa Kamati inayohusika au Mjumbe yeyote atakayeteuliwa kwa niaba yake, na Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara husika watawasilisha Mezani nakala ya taarifa zao kwa kuzingatia mpangilio wa Shughuli za Bunge.
(4) Pamoja na kuwasilisha mezani nakala ya hotuba ya hoja ya Makadirio ya Wizara yake, Waziri mhusika atawasilisha pia randama ya makadirio hayo, siku moja kabla ya siku ambayo hotuba yake imepangwa kutolewa Bungeni.
(5) Wakati utakapofika wa kuwasilisha taarifa ya Wizara inayohusika, hoja itatolewa kwa maneno yafuatayo:- “Kwamba sasa Bunge likubali kujadili na kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Wizara yangu.”
(6) Isipokuwa kwa Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, muda wa Waziri anayewasilisha Hotuba ya Makadirio ya Wizara yake utakuwa ni dakika zisizozidi sitini.
(7) Waziri atafuatiwa na Mwenyekiti wa Kamati iliyopitia Makadirio husika na Msemaji wa Kambi ya Upinzani ambao watatoa maoni yao kwa muda usiozidi dakika thelathini kila mmoja.
(8) Mbunge anayejadili Makadirio ya Matumizi ya Wizara mbalimbali ataruhusiwa kusema kwa muda usiozidi dakika kumi na tano.
(9) Endapo Spika ataona kuwa muda uliotengwa kwa ajili ya kujadili Bajeti ya Wizara inayohusika umekaribia kwisha, atafunga mjadala ili kumpatia Waziri mtoa hoja nafasi ya kujibu ndani ya muda wa dakika sitini.
100.-(1) Mjadala wa jumla kuhusu Makadirio ya Matumizi kwa Wizara utakapomalizika Bunge litaingia katika Kamati ya Matumizi ili kupitisha Makadirio ya Wizara husika kifungu kwa kifungu.
Kamati ya Matumizi
65
101.-(1)Katika Kamati ya Matumizi, Mwenyekiti atawahoji Wajumbe kuhusu kifungu kimoja kimoja cha Makadirio ya Matumizi ya Mwaka na kila kifungu kitaafikiwa peke yake.
(2) Mbunge yeyote anaweza kuomba ufafanuzi au maelezo zaidi katika Kifungu chochote cha Fungu linalohusika, wakati Kifungu hicho kitakapofikiwa na Kamati ya Matumizi.
(3) Mbunge atakayeamua kutumia kifungu chenye mshahara wa Waziri, ataruhusiwa tu iwapo ataomba ufafanuzi wa suala mahususi la sera na hatazungumzia zaidi ya mambo mawili ya aina hiyo.
(4) Kwa idhini ya Mwenyekiti, Mbunge anayetaka ufafanuzi anaweza kuzungumza si zaidi ya mara mbili juu ya suala hilo.
(5) Muda wa kusema katika Kamati ya Matumizi kwa ajili ya kutoa ufafanuzi hautazidi dakika tano.
102.-(1) Katika Kamati ya Matumizi Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja ya kutaka kufanya mabadiliko katika Makadirio ya Matumizi ya Serikali iwapo mabadiliko hayo hayatabadili madhumuni ya Fungu au sehemu yoyote ya Fungu husika.
(2) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kupunguza kifungu fulani katika Fungu lolote haijapitishwa, hoja nyingine bado inaweza kutolewa kwa madhumuni ya kupunguza kifungu kingine cha Fungu hilo hilo.
103.-(1) Kwa kuzingatia utaratibu wa majadiliano uliowekwa na Kanuni hizi, Mbunge yeyote anaweza kuomba ufafanuzi au maelezo zaidi katika Kifungu chochote cha Fungu linalohusika, wakati Kifungu hicho kitakapofikiwa na Kamati ya Matumizi.
(2) Vilevile Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja ya kuondoa shilingi moja katika kifungu chochote cha Fungu hilo.
(3) Madhumuni halisi ya hoja ya aina hiyo ni kumwezesha Mbunge aliyeitoa aweze kueleza kutoridhika kwake na utekelezaji wa jambo fulani mahususi ambalo dhahiri linahusika na kifungu hicho.
(4) Hoja ya aina hiyo itatolewa kwa muda wa dakika tano.
Kubadili- sha Makadirio ya Matumizi katika Kamati ya Matumizi
Mjadala katika Kamati ya Matumzi
Hoja ya kuondoa shilingi kwenye Makadirio
66
(5) Wabunge wanaweza kuchangia hoja ya kuondoa shilingi moja iliyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) kwa muda usiozidi dakika tatu kila mmoja.
(6) Waziri anayehusika atapewa nafasi ya kutoa majibu ya hoja hiyo.
(7) Mbunge aliyetoa hoja ya kuondoa shilingi ndiye atakayefunga mjadala wa hoja hiyo.
(8) Endapo Mbunge atashikilia hoja yake ya kuondoa shilingi moja katika kifungu hicho, basi kura itapigwa.
(9) Endapo hoja ya kuondoa shilingi moja katika kifungu chochote itakubaliwa, basi kifungu hicho kitakuwa kimepitishwa kikiwa pungufu ya hiyo shilingi moja.
(10) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kuondoa shilingi moja katika kifungu chochote cha Fungu linalohusika imekataliwa, hoja nyingine yenye madhumuni ya kuondoa shilingi moja katika Kifungu kingine cha Fungu hilo hilo bado inaweza kutolewa.
104.-(1) Iwapo zimesalia dakika kumi kabla ya kufikia muda wa kuahirisha kikao cha Bunge na Kamati ya Matumizi bado haijamaliza kupitisha mafungu, Mwenyekiti anaweza kuongeza muda usiozidi dakika thelathini bila kuihoji Kamati ili kumaliza shughuli ya kupitisha mafungu yaliyobakia.
(2) Baada ya Kamati ya Matumizi kumaliza kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Wizara inayohusika na Bunge kurudia, Waziri mtoa hoja atatoa taarifa kwamba:-
(a) “Mheshimiwa Spika, Bunge lako likikaa kama Kamati ya Matumizi limekamilisha kazi zake”; na kuomba kwamba:
(b) “taarifa ya Kamati ya Matumizi ikubaliwe na Bunge”; na atamaliza kwa kusema: “naomba kutoa hoja.”
(3) Spika atawahoji Wabunge kwa kuuliza, “Wanaoafiki waseme ndiyo” na “Wasioafiki waseme siyo.”
Kukamilika mjadala katika Kamati ya Matumizi
67
105.-(1) Baada ya Bunge kukamilisha kazi ya kujadili na kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Wizara zote kwa mwaka unaohusika, Muswada wa Fedha za Matumizi utawasilishwa Bungeni na kupitishwa mfululizo katika hatua zake zote.
(2) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, “Muswada wa Fedha za Matumizi” maana yake ni Muswada wa Sheria wenye Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Serikali kwa Mwaka wa Fedha unaofuatia.
(3) Muswada wa Fedha za Matumizi hautapelekwa kwenye Kamati yoyote ya Kudumu wala Kamati ya Bunge Zima, na masharti kuhusu Miswada Kusomwa Mara ya Kwanza hayatatumika.
(4) Muswada wa Fedha za Matumizi hautatangazwa kwenye Gazeti kabla haujawasilishwa Bungeni.
106. Baada ya Bunge kukamilisha kazi ya kupitisha Muswada wa Fedha za Matumizi, Muswada wa Sheria ya Fedha utajadiliwa na kupitishwa kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na Sehemu ya Nane ya Kanuni hizi.
107. Mapendekezo yoyote kwa ajili ya Matumizi ya Nyongeza ya Fedha za Serikali au kwa ajili ya kutoa fedha yoyote ya nyongeza zaidi ya Fedha za Matumizi ya Mwaka huo:- (a) yataitwa Makadirio ya Nyongeza ya Matumizi;
(b) yatapelekwa kwenye Kamati ya Matumizi kufuatana na masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba; na
(c) yatafuata masharti ya Kanuni zote zinazohusu Makadirio ya Mwaka ya Matumizi ya Serikali.
SEHEMU YA KUMI
KAMATI ZA BUNGE
108.-(1) Kutakuwa na Mkutano wa Wabunge wote ambao unaweza kuitishwa na Spika siku moja kabla au wakati wa Mkutano wowote wa Bunge.
(2) Mkutano wa Wabunge wote utajadili masuala yote yenye maslahi kwa Wabunge na utaipa Serikali fursa ya kutoa taarifa mbalimbali kwa Wabunge kuhusu hali ya nchi kwa ujumla.
Muswada wa Sheria ya Fedha
Makadirio ya Matumizi ya Nyongeza
Muswada wa Fedha za Matumizi
Mkutano wa Wabunge wote
68
(3) Mwenyekiti wa Kikao cha Mkutano wa Wabunge wote atakuwa Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni.
109.-(1) Wabunge wa kila Chama cha Siasa kinachowakilishwa Bungeni wanaweza kuunda Kamati ya Wabunge wa Chama kwa kuzingatia Katiba, Kanuni na Taratibu za Chama kinachohusika.
(2) Endapo makubaliano yamefikiwa baina ya Vyama viwili au zaidi vya Upinzani vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimia kumi na mbili na nusu basi Wabunge wa Kambi ya Upinzani wanaweza kuunda Kamati ya Wabunge wote wa Kambi hiyo.
110.-(1) Kamati za Vyama vya Siasa Bungeni zitajiwekea utaratibu kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli.
(2) Majadiliano yote kwenye mikutano ya Kamati pamoja na mambo mengine yote yanayohusu Kamati hizo yatakuwa na hadhi, kinga na nafuu zote zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria kuhusu majadiliano, kumbukumbu na mambo mengineyo ya Bunge na vikao vyake kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 100 (1) na (2) ya Katiba na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.
111. Kwa kufuata yaliyomo kwenye Orodha ya Shughuli au kwa mujibu wa Kanuni hizi, ukifika wakati wa Bunge au Bunge likihitajiwa kuingia katika Kamati ya Bunge Zima, Spika ataondoka kwenye Kiti chake bila hoja yoyote kutolewa.
112.-(1) Masharti ya Kanuni ya 77 yatatumika kuhusu Kamati ya Bunge Zima, ila tu kama idadi ya Wabunge waliohudhuria itakuwa bado haifikii nusu ya Wabunge wote baada ya kipindi kilichowekwa na Kanuni ya 77(3), Mwenyekiti ataondoka kwenye Kiti, Bunge litarudia na Katibu atahesabu idadi ya Wabunge waliohudhuria na kama idadi yao itakuwa bado haifikii nusu ya Wabunge wote, basi Spika ataahirisha Bunge.
(2) Kanuni za Bunge zinazohusu mwenendo wa Bunge zitatumika katika Kamati ya Bunge Zima isipokuwa kwamba katika Kamati hiyo:-
(a) hoja ikitolewa haitahitaji kuungwa mkono;
(b) Kwa idhini ya Mwenyekiti, Mjumbe anayetaka ufafanuzi anaweza kuzungumza mara mbili juu ya suala hilo.
Mikutano ya Kamati za Vyama vya Siasa
Kamati ya Bunge Zima
Kamati za Vyama vya Siasa
Akidi na Utaratibu katika Kamati ya Bunge Zima
69
(3) Mjumbe yeyote anaweza kuchangia katika hoja ya kutaka ufafanuzi iliyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) (b).
(4) Muda wa kusema katika kuchangia hoja ya ufafanuzi hautazidi dakika tano.
(5) Mjumbe yeyote anayetaka kutoa hoja kwamba majadiliano ya Kamati ya Bunge Zima yaahirishwe mpaka wakati mwingine, anaweza kutoa hoja hiyo wakati wowote, kwa maneno yafuatayo:
“Kwamba Waziri au Mbunge atoe taarifa kwa Bunge juu ya maendeleo ya kazi ya Kamati hii na kuomba ruhusa Kamati hii ikutane tena baadae.”
(6) Bunge litakaporudia, Waziri au Mbunge aliyehusika na shughuli zilizokuwa zikifanywa na Kamati atasimama mahali pake na kuliarifu Bunge kwamba Kamati imeshughulikia maendeleo lakini haikukamilisha kazi yake.
(7) Mara tu baada ya Waziri au Mbunge aliyehusika na shughuli zilizokuwa zikifanywa na Kamati kuliarifu Bunge kutokamilika kwa kazi yake, Spika atalitaarifu Bunge siku na wakati ambapo Kamati itaendelea na kazi yake.
(8) Kamati ya Bunge Zima itafikiria mambo yale tu yatakayopelekwa na Bunge kwenye Kamati hiyo.
(9) Kamati ya Bunge Zima, inaweza kuamua, baada ya hoja kutolewa kwamba shughuli iliyo mbele yake wakati huo irudishwe au ipelekwe kwenye Kamati ya Kudumu inayohusika.
(10) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha shughuli zake, Mwenyekiti ataondoka kwenye Kiti na kurejea kwenye Kiti cha Spika ambapo Bunge litarudia.
113.-(1) Mbunge yeyote ambaye si Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge yoyote ambayo inahusika na Kanuni hii na Waziri mwenye dhamana ya jambo lolote linalopelekwa au kujadiliwa na Kamati, pamoja na Naibu Waziri aliyeteuliwa kumsaidia Waziri huyo, watakuwa wajumbe wa Kamati wakati Kamati itakapokuwa inashughulikia jambo hilo.
(2) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Mbunge
Muundo wa Kamati za Kudumu za Bunge
70
yeyote ambaye ni Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya hatachaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
(3) Wajumbe wa Kamati zote watateuliwa na Spika kwa namna ambayo itawezesha kila Mbunge kuwekwa kwenye Kamati mojawapo.
(4) Wajumbe walioteuliwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Kamati ya Masuala ya Ukimwi, wanaweza pia kuteuliwa kwenye Kamati nyingine.
(5) Wakati wa kuteua Wabunge kuwa Wajumbe wa Kamati mbalimbali, Spika:-
(a) atateua idadi ya Wabunge inayolingana kwa kila Kamati, isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi;
(b) atazingatia aina zote za Wabunge na kuwateua Wabunge wa aina mbalimbali kwa kila Kamati, akiongozwa na kigezo cha asilimia ya kila aina ya Wabunge hao ilivyo Bungeni;
(c) kwa kadri inavyowezekana, atayapa kipaumbele matakwa ya Wabunge wenyewe, lakini hatalazimika kutosheleza kila takwa au ombi;
(d) atazingatia haja kwa kila Kamati kuwa na Wabunge wenye uzoefu au ujuzi maalumu kuhusu kazi za Kamati hiyo.
(6) Katibu atahakikisha kuwa Wabunge wote wanapewa orodha inayoonesha jinsi walivyoteuliwa katika Kamati mbalimbali.
(7) Ujumbe katika Kamati za Kudumu za Bunge utadumu mpaka mwisho wa Mkutano wa Kumi wa Bunge ambao ni nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge.
(8) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (7) ya Kanuni hii, Mbunge yeyote anaweza kuteuliwa tena katika Kamati aliyokuwa anaitumikia katika nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge.
71
(9) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (7) ya Kanuni hii, Mbunge atakoma kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge endapo atateuliwa kuwa Waziri au kuchaguliwa kuwa Spika au Naibu Spika.
(10) Wajumbe wa kila Kamati watawachagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti kutoka miongoni mwao ambao kwa muda wote watakaokuwa Wabunge, wataendelea kushika nafasi hizo mpaka mwisho wa kipindi kilichotajwa katika fasili ya (7) ya Kanuni hii, lakini wanaweza kuchaguliwa tena.
(11) Wenyeviti wa Kamati za Bunge zinazosimamia matumizi ya fedha za Umma ambazo ni Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma watachaguliwa kutoka miongoni mwa Wajumbe wa Kamati hizo ambao wanatoka katika Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
114.-(1) Masharti ya Kanuni hii yatatumika kwa Kamati zote za kudumu.
(2) Mwenyekiti ataongoza vikao vyote vya Kamati na endapo Mwenyekiti hayupo kwenye kikao, Makamu Mwenyekiti ataongoza shughuli za kikao hicho na ikiwa Mwenyekiti na Makamu wake wote hawapo, wajumbe waliohudhuria watamchagua mmojawapo miongoni mwao kuongoza kikao hicho.
(3) Kamati ya Kudumu itakutana kila inapoitwa na Spika, Naibu Spika au na Mwenyekiti wake baada ya kupata idhini ya Spika.
(4) Mikutano ya kawaida ya Kamati za Kudumu itafanyika Dodoma, Dar es Salaam au Zanzibar.
(5) Kila Kamati itafanya vikao vyake kwa kuzingatia bajeti ya Kamati husika ambayo imeidhinishwa kwa mwaka huo wa fedha.
(6) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati ya Kudumu itakuwa theluthi moja ya Wajumbe wote wa Kamati.
(7) Mambo yote yatakayojadiliwa na Kamati yataamuliwa kwa kufuata maoni ya walio wengi kati ya Wajumbe wa Kamati waliohudhuria na kupiga kura.
(8) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, kila Kamati itajiwekea utaratibu wake, na Kamati inaweza kuwaruhusu Wabunge ambao si Wajumbe wa Kamati au watu ambao si
Utaratibu katika Kamati za kudumu za Bunge
72
Wabunge kuhudhuria na kushiriki katika shughuli za Kamati, lakini hawatakuwa na haki ya kupiga kura.
(9) Shughuli za kawaida za Kamati zitaendeshwa kwa uwazi ambapo Kamati itaalika wadau ili kupata maoni na ushauri wao kwa ajili ya kuboresha Muswada au jambo ambalo litakuwa linashughulikiwa na Kamati hiyo.
(10) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (9) ya Kanuni hii, shughuli zote za Kamati zinazohusu kuandaa na kutoa mapendekezo ya kuwasilishwa Bungeni zitafanywa kwa faragha.
(11) Maoni ya Kamati yatakuwa ni yale yaliyokubaliwa na wajumbe walio wengi na kuwasilishwa Bungeni na Mwenyekiti au Mjumbe mwingine.
(12) Mjumbe yeyote wa Kamati hataruhusiwa kuzungumzia hadharani maoni ya Kamati kuhusu Muswada au jambo lolote litakalokuwa linashughulikiwa na Kamati kabla maoni hayo hayajawasilishwa rasmi Bungeni.
(13) Mwanasheria Mkuu wa Serikali na au mwakilishi wake, atahudhuria kila mkutano wa kila Kamati ya Kudumu inapokuwa inachambua Muswada wa Sheria.
(14) Kamati yoyote ambayo Spika atapeleka kwake kwanza Muswada au jambo lingine lolote, itahesabiwa kuwa ndiyo Kamati inayohusika kushughulikia Muswada huo au jambo hilo.
(15) Itakuwa ni lazima kwa kila Kamati ya Kudumu ya Bunge kuwasilisha Bungeni taarifa ya mwaka ya shughuli zake kwa madhumuni ya kujadiliwa katika Mkutano wa mwisho kabla ya Mkutano wa Bajeti.
(16) Taarifa ya Kamati inapowasilishwa Bungeni, itashughulikiwa kwa kufuata mpangilio wa Shughuli za Bunge.
(17) Spika ataweka utaratibu wa kujadili taarifa za Kamati na endapo Kamati yoyote katika kutekeleza majukumu yake, itaona kuwa kuna mambo ya utekelezaji ambayo yanahitaji kurekebishwa, inaweza kutoa taarifa maalumu ya ushauri kwa Waziri mwenye dhamana juu ya mambo hayo ili Waziri aweze kuchukua hatua zinazostahili.
73
(18) Kamati yoyote inaweza kuunda Kamati Ndogo kwa ajili ya utekelezaji bora wa Shughuli zake, kadri itakavyoona inafaa na kila Kamati Ndogo itapangiwa kazi zake na Kamati ya Kudumu inayohusika.
(19) Mjumbe wa Kamati yoyote hataruhusiwa kuzungumzia au kushughulikia jambo lolote lililofikishwa katika Kamati iwapo ana maslahi binafsi katika jambo hilo au idara hiyo isipokuwa anaweza kufanya hivyo baada ya kutaja jinsi anavyohusika na kiwango cha maslahi hayo.
115.-(1) Kutakuwa na Kamati za Kudumu za Bunge kama zilivyoainishwa kwenye Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.
(2) Muundo na majukumu ya Kamati za Kudumu za Bunge yameainishwa kwenye Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.
116. Mbali na majukumu ya msingi ambayo yameorodheshwa kwa kila Kamati ya Kudumu, Kamati yoyote inaweza kupendekeza kwa Spika ipewe majukumu ya nyongeza ambayo yatatajwa katika pendekezo hilo na vilevile Spika anaweza kukabidhi jambo lingine lolote kwa Kamati yoyote kadri atakavyoona inafaa, kwa ajili ya kushughulikiwa na Kamati hiyo.
117.-(1) Kamati Teule inaweza kuundwa na Bunge kwa madhumuni maalumu kwa hoja mahsusi itakayotolewa na kuafikiwa.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, baada ya kujadili hoja yoyote, Bunge linaweza kuunda Kamati Teule kwa madhumuni ya kushughulikia jambo lolote lililotokana na hoja hiyo kwa utaratibu ufuatao:-
(a) Baada ya hoja iliyokuwa ikijadiliwa kuamuliwa, Mbunge yeyote mwenye nia ya kutoa hoja chini ya Kanuni hii anaweza kusimama mahali pake na kutoa taarifa ya mdomo kwamba anakusudia kutoa hoja ya kuunda Kamati Teule;
(b) Mbunge ambaye anakusudia kutoa hoja ya kuunda Kamati Teule atawasilisha taarifa ya hoja
Kamati za Kudumu za Bunge
Majukumu ya jumla ya Kamati za Kudumu za Bunge
Utaratibu wa Kuunda Kamati Teule
74
yake kwa maandishi kwa Katibu na hoja hiyo itashughulikiwa wakati unaofaa kwa kuzingatia mpangilio wa shughuli kama ulivyoainishwa chini ya Kanuni ya 30 (4).
(3) Bunge litapeleka jambo linalotokana na hoja iliyokuwa ikijadiliwa Bungeni kwenye Kamati Teule.
(4) Wajumbe wa Kamati Teule watateuliwa na Spika na watamchagua Mwenyekiti wa Kamati hiyo kutoka miongoni mwao.
118.- (1) Kila Kamati Teule itakuwa na Wajumbe wasiozidi watano.
(2) Akidi ya vikao vya Kamati Teule itakuwa ni theluthi mbili ya wajumbe wake.
(3) Kamati Teule itafanya kikao chake cha kwanza mahali na saa atakayoamua Mwenyekiti na vikao vinginevyo vitafanyika kwa wakati na mahali popote itakapoamua.
(4) Mwenyekiti ataongoza vikao vyote vya Kamati Teule, na iwapo Mwenyekiti hayupo katika kikao chochote, Wajumbe waliohudhuria watamteua mmoja wao kuwa Mwenyekiti wa kikao hicho.
(5) Endapo kwa sababu yoyote Mjumbe yeyote wa Kamati Teule atashindwa kufanya kazi yake, Spika atamteua Mbunge mwingine kushika nafasi yake.
(6) Majadiliano ya Kamati Teule yatahusu tu mambo yaliyopelekwa kwake na Bunge na yatakuwa ya wazi au siri kufuatana na Kamati itakavyoamua kulingana na masuala husika.
119.-(1) Kamati Teule itatoa taarifa Bungeni kuhusu maoni na uchunguzi wake pamoja na kumbukumbu za ushahidi uliopokelewa na vilevile inaweza kutoa taarifa maalumu juu ya mambo yoyote ambayo itaona yanafaa kuwasilishwa Bungeni.
(2) Taarifa ya Kamati Teule itawasilishwa Bungeni na Mwenyekiti.
(3) Iwapo baada ya hoja kutolewa, Bunge litaamua kujadili taarifa hiyo, hoja itakayotolewa Bungeni itakuwa ni kwa madhumuni ya kuliomba Bunge likubali mapendekezo yaliyomo katika taarifa hiyo.
Akidi na utaratibu wa Vikao vya Kamati Teule
Taarifa ya Kamati Teule
75
(4) Bunge linaweza kuamua vinginevyo kwa kutumia utaratibu wa kubadilisha hoja ambao umeelezwa katika Kanuni ya 57 ya Kanuni hizi.
(5) Katibu wa Kamati Teule ataweka kumbukumbu zinazoonesha majina ya Wajumbe waliohudhuria mikutano ya Kamati na maamuzi yaliyofanyika.
(6) Kumbukumbu zitakazowekwa kwa mujibu wa masharti ya fasili ya (5) ya Kanuni hii zitawekwa saini na Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati na zitaambatishwa kwenye Taarifa ya Kamati na kuwasilishwa Bungeni pamoja na taarifa hiyo.
120.- Taarifa yoyote ya Kamati inayowasilishwa Bungeni itakuwa katika muundo ufuatao:-
(a) Sehemu ya Utangulizi, ambayo itaonesha hadidu za rejea ambazo Kamati ilipewa; maelekezo yoyote yaliyotolewa kwa Kamati, njia au mbinu zilizotumika na Kamati katika kutekeleza majukumu yake, pamoja na mambo mengine, kama yapo, ambayo yalijitokeza wakati wa uchunguzi;
(b) Sehemu ya Katikati, ambayo itatoa maelezo kamili kuhusu jambo au mambo yote yaliyofanyiwa Uchunguzi na Kamati; na
(c) Sehemu ya Mwisho, ambayo itatoa maoni na mapendekezo ya Kamati ya Bunge.
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
UTARATIBU WA KUMWONDOA RAIS MADARAKANI
121.- Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha kwa Spika taarifa ya Hoja ya kumshtaki Rais kwa madhumuni ya kumwondoa Rais madarakani kupitia Azimio la Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 46A ya Katiba ikiwa inadaiwa kwamba Rais -
(a) ametenda vitendo ambavyo kwa ujumla vinavunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
Muundo wa Taarifa za Kamati
Taarifa ya Hoja ya Kumwo- ndoa Rais,
Sura ya 2, Toleo la 2002
76
(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa Vyama vya Siasa yaliyotajwa katika Ibara ya 20(2) ya Katiba; au
(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano. Isipokuwa kwamba, hoja ya namna hiyo haitatolewa, ndani ya miezi kumi na miwili tangu ilipotolewa na kukataliwa na Bunge.
122.-(1) Bunge halitajadili wala kushughulikia hoja ya kumshtaki Rais, isipokuwa tu kama: –
(a) taarifa ya maandishi, iliyowekwa saini na kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya Wabunge wote itatolewa;
(b) taarifa hiyo itawasilishwa kwa Spika, siku thelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa Bungeni;
(c) taarifa hiyo pia itafafanua makosa aliyoyatenda Rais; na
(d) taarifa hiyo vile vile itapendekeza kuwa, Kamati Maalumu ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze mashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Rais.
(2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwa saini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.
(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo.
123.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Rais itaungwa mkono na Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Spika atatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi, kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 46A(4) ya Katiba.
(2) Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa na wajumbe wafuatao:-
Sura ya 398, Toleo la 2002
Masharti ya hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi
Wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi,
Sura ya 2, Toleo la 2002
77
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo; (b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na (c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwa kuzingatia uwiano wa uwakilishi baina ya Vyama vya Siasa vinavyowakilishwa Bungeni.
(3) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalumu ya Uchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, na kwa sababu hiyo, kazi na madaraka ya Rais yatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 37(3) ya Katiba hadi Spika atakapomfahamisha Rais juu ya Azimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.
124.-(1) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi ya Rais na itampatia Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake kwa mujibu wa masharti na utaratibu uliowekwa na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge na Kanuni hizi.
(2) Mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile katika muda usiozidi siku tisini, Kamati Maalumu ya Uchunguzi itatoa taarifa yake kwa Spika.
(3) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa ni Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar na Wajumbe wengine wanne kutoka Bungeni.
(4) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi.
125.-(1) Endapo kwa mujibu wa Orodha ya Shughuli za Bunge utafika wakati wa Bunge kujadili taarifa ya Kamati hiyo Maalumu ya Uchunguzi, basi Bunge litaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima ili kushughulikia taarifa hiyo na Bunge linaweza kumruhusu Mwenyekiti na mjumbe mwingine ambaye siyo Mbunge wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuwasilisha na kuelezea uamuzi wa Kamati yake kwenye Kamati ya Bunge Zima.
(2) Baada ya taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuwasilishwa Bungeni, Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.
Sura ya 296, Toleo la 2002
Utaratibu katika Kamati ya Bunge Zima kuhusu mashtaka dhidi ya Rais
Sura ya 2, Toleo la 2002
Utaratibu wa kazi ya Kamati Maalumu ya uchunguzi
78
126.-(1) Baada ya kusikiliza utetezi wa Rais, Wabunge watapiga kura ya siri ili kupata uamuzi wa Bunge iwapo mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika au mashtaka hayo hayakuthibitika.
(2) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi zake na Bunge kurudia, Mbunge aliyetoa hoja ya kumshtaki Rais atatoa taarifa ya kukamilika kwa shughuli za Kamati ya Bunge Zima na endapo mashtaka dhidi ya Rais yatakuwa yamethibitika, kwa kuungwa mkono na kura za Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, papo hapo atatoa hoja kwamba, Bunge lipitishe Azimio la kumwondoa Rais madarakani, kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 46A(5) ya Katiba.
(3) Endapo Bunge litapitisha Azimio la kumwondoa Rais madarakani, Spika atawafahamisha Rais na Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi juu ya Azimio hilo la Bunge na Rais atawajibika kujiuzulu katika kipindi cha siku tatu tangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo.
(4) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika na Bunge kupitisha Azimio la kumwondoa madarakani, Rais hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya pensheni.
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
UTARATIBU WA KUMWONDOA MAKAMU WA RAIS MADARAKANI
127.-(1) Rais anaweza kuwasilisha Bungeni hati ya kuliomba Bunge lipitishe Azimio la kumwondoa Makamu wa Rais madarakani ikiwa Makamu wa Rais ameacha au ameshindwa kutekeleza kazi za Makamu wa Rais kwa mujibu wa Ibara ya 50(3) ya Katiba.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha Bungeni hoja ya kutaka kumwondoa Makamu wa Rais madarakani ikiwa Makamu wa Rais:-
(a) ametenda vitendo ambavyo kwa ujumla vinavunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
Sura ya 2, Toleo la 2002
Sura ya 2, Toleo la 2002
Azimio la kumwo- ndoa Rais
Sura ya 398, Toleo la 2002
Utaratibu wa kumwo- ndoa Makamu wa Rais Madarakani,
79
(b) ametenda vitendo vinavyokiuka maadili yanayohusu uandikishaji wa Vyama vya Siasa vilivyotajwa kutoka Ibara ya 20 (2) ya Katiba; au
(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano au Kiti cha Makamu wa Rais. Isipokuwa kwamba, hoja ya namna hiyo haitatolewa ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja ya namna hiyo ilipotolewa na kukataliwa na Bunge.
128.-(1) Bunge halitajadili wala kushughulikia hoja ya kumshtaki Makamu wa Rais isipokuwa tu kama: -
(a) taarifa ya maandishi, iliyowekwa saini na kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya Wabunge wote imetolewa;
(b) taarifa hiyo itawasilishwa kwa Spika, siku thelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa Bungeni;
(c) taarifa hiyo pia itafafanua makosa aliyoyatenda Makamu wa Rais; na
(d) taarifa hiyo pia itapendekeza kuwa, Kamati Maalumu ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze mashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Makamu wa Rais.
(2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwa saini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.
(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo.
129.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Makamu wa Rais itaungwa mkono na Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Spika atatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi, kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 46A(4) ya Katiba:-
Sura ya 2, Toleo la 2002
Masharti ya hoja ya kuunda Kamati Maalumu ya Uchunguzi
Wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi
80
(2) Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa na wajumbe wafuatao:-
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo;
(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na
(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwa kuzingatia uwiano wa Uwakilishi baina ya vyama vya siasa vinavyowakilishwa Bungeni.
(3) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalumu ya Uchunguzi, Makamu wa Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, na kwa sababu hiyo, kazi na madaraka ya Makamu wa Rais yatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 37(3) ya Katiba hadi Spika atakapomfahamisha Makamu wa Rais juu ya Azimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.
130.-(1) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi ya Makamu wa Rais na itampatia Makamu wa Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake kwa mujibu wa masharti na utaratibu uliowekwa na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge na Kanuni hizi.
(2) Mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile katika muda usiozidi siku tisini, Kamati Maalumu ya Uchunguzi itatoa taarifa yake kwa Spika.
(3) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa ni Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar na Wajumbe wengine wanne kutoka Bungeni.
(4) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi.
131.-(1) Endapo kwa mujibu wa Orodha ya Shughuli za Bunge utafika wakati wa Bunge kujadili taarifa ya Kamati hiyo Maalumu ya Uchunguzi, basi Bunge litaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima ili kushughulikia taarifa hiyo na Bunge linaweza kumruhusu Mwenyekiti na mjumbe mwingine ambaye siyo Mbunge wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuwasilisha na kuelezea uamuzi wa Kamati yake kwenye Kamati ya Bunge Zima.
Sura ya 2, Toleo la 2002
Sura ya 296, Toleo la 2002
Sura ya 2, Toleo la 2002
Utaratibu Katika Kamati ya Bunge Zima kuhusu mashtaka dhidi ya Makamu wa Rais
Utaratibu wa kazi ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi,
81
(2) Baada ya taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuwasilishwa Bungeni, Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Makamu wa Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.
132.-(1) Baada ya kusikiliza utetezi wa Makamu wa Rais, Wabunge watapiga kura ya siri ili kupata uamuzi wa Bunge iwapo mashtaka dhidi ya Makamu wa Rais yamethibitika au mashitaka hayo hayakuthibitika.
(2) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi zake na Bunge kurudia, Mbunge aliyetoa hoja ya kumshtaki Makamu wa Rais atatoa taarifa ya kukamilika kwa shughuli za Kamati ya Bunge Zima na endapo mashtaka dhidi ya Makamu wa Rais yatakuwa yamethibitika, kwa kuungwa mkono na kura za Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, papo hapo atatoa hoja kwamba, Bunge lipitishe Azimio la kumwondoa Makamu wa Rais madarakani, kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 46A(5) ya Katiba.
(3) Endapo Bunge litapitisha Azimio la kumwondoa Makamu wa Rais madarakani, Spika atawafahamisha Rais, Makamu wa Rais na Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi juu ya Azimio hilo la Bunge na Makamu wa Rais atawajibika kujiuzulu katika kipindi cha siku tatu tangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo.
(4) Endapo Makamu wa Rais ataacha kushika kiti cha Makamu wa Rais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika na Bunge kupitisha Azimio la kumwondoa madarakani, Makamu wa Rais, hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya pensheni.
SEHEMU YA KUMI NA TATU
HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA WAZIRI MKUU
133.-(1) Mbunge yeyote anaweza kutoa taarifa ya maandishi kwa Spika ya kutaka kuleta hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu kwa mujibu wa Ibara ya 53A ya Katiba.
(2) Hoja yoyote ya kutaka kupitisha Azimio la kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu haitatolewa Bungeni endapo:-
Sura ya 2, Toleo la 2002
Azimio la kumwo- ndoa Makamu wa Rais madarakani
Taarifa ya Hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu
Sura ya 2, Toleo la 2002
82
(a) haina uhusiano na utekelezaji wa majukumu ya Waziri Mkuu yaliyoainishwa katika Ibara ya 52 ya Katiba;
(b) hakuna madai kwamba Waziri Mkuu amevunja Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
(c) haijapita miezi sita tangu alipoteuliwa; au
(d) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyo ilipotolewa Bungeni na Bunge likakataa kuipitisha.
(3) Hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu haitajadiliwa na Bunge isipokuwa tu kama:-
(a) taarifa ya maandishi iliyowekwa saini na kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya Wabunge wote itatolewa kwa Spika, siku zisizopungua kumi na nne kabla ya siku inayokusudiwa kuwasilishwa Bungeni;
(b) Spika ataridhika kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuleta hoja hiyo yametimizwa.
(4) Hoja inayotolewa chini ya Kanuni hii na iliyotimiza masharti ya Katiba, itawasilishwa Bungeni mapema iwezekanavyo na itaamuliwa kwa kura za siri.
(5) Hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwa tu iwapo inaungwa mkono na Wabunge walio wengi.
(6) Endapo hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwa na Bunge kwa kupigiwa kura na Wabunge walio wengi, Spika atawasilisha Azimio hilo kwa Rais na mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile ndani ya siku mbili tangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo, Waziri mkuu atajiuzulu na Rais atamteua Mbunge mwingine kuwa Waziri Mkuu.
Sura ya 398, Toleo la 2002
Sura ya 2, Toleo la 2002
83
SEHEMU YA KUMI NA NNE
KUMWONDOA SPIKA AU NAIBU SPIKA MADARAKANI
134.-(1) Mbunge yeyote anayetaka kuwasilisha hoja ya kumwondoa Spika madarakani chini ya Ibara ya 84(7)(d) ya Katiba, atawasilisha taarifa ya maandishi ya kusudio hilo kwa Katibu akieleza sababu kamili ya kutaka kuleta hoja hiyo.
(2) Mara tu baada ya kupokea taarifa ya maandishi ya kusudio la kumwondoa Spika kwenye madaraka, Katibu ataipeleka taarifa hiyo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kuijadili.
(3) Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaridhika kuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Spika zinazohusu uvunjaji wa masharti ya Ibara ya 84(7)(a), (b), (e), (f), (g) na (h) ya Katiba, Sheria au Kanuni zinazoongoza shughuli za Bunge, basi Kamati hiyo itaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe Bungeni ili iamuliwe.
(4) Naibu Spika, atakalia Kiti cha Spika wakati wa kujadili hoja ya kutaka kumwondoa Spika madarakani na Spika atakuwa na haki ya kujitetea wakati wa mjadala.
(5) Spika atakuwa ameondolewa kwenye madaraka endapo zitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya Wabunge wote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bunge utafanywa kwa kuzingatia kura za siri.
(6) Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kutoa maelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzi juu ya hoja ya kumwondoa madarakani.
135.-(1) Utaratibu wa kumwondoa Naibu Spika madarakani chini ya Ibara ya 85(4)(c) ya Katiba utakuwa kama ule wa kumwondoa Spika, isipokuwa tu taarifa ya kusudio la kumwondoa Naibu Spika madarakani inayoeleza sababu kamili za kuleta hoja hiyo, itapelekwa kwa Spika ambaye ataiwasilisha kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kuijadili.
(2) Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaridhika kuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Naibu Spika zinazohusu uvunjaji wa Katiba, Sheria au Kanuni zinazoongoza Shughuli za Bunge, basi
Taarifa ya Hoja ya kumwondoa Spika madarakani
Utaratibu wa kumwo- ndoa Naibu Spika Madarakani
Sura ya 2,Toleo la 2002
Sura ya 2, Toleo la 2002
84
Kamati hiyo itaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe Bungeni ili iamuliwe.
(3) Spika atakalia Kiti wakati wa kujadili hoja ya kutaka kumwondoa Naibu Spika madarakani na Naibu Spika atakuwa na haki ya kujitetea wakati wa mjadala.
(4) Naibu Spika atakuwa ameondolewa kwenye madaraka endapo zitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya Wabunge wote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bunge utafanywa kwa kuzingatia kura za siri.
(5) Naibu Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kutoa maelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzi juu ya hoja ya kumwondoa madarakani.
SEHEMU YA KUMI NA TANO
WAGENI BUNGENI
136.-(1) Wageni wanaweza kuruhusiwa kuingia kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Bunge katika sehemu yoyote ya Ukumbi huo ambayo itatengwa kwa ajili hiyo.
(2) Wageni wakiwa ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge watalazimika kufuata na kuzingatia masharti yafuatayo:-
(a) Watakaa kimya na kwa heshima inayostahili hadi watakapotoka nje ya Ukumbi huo;
(b) Wanapaswa wawe wamevaa mavazi ya heshima;
(c) Wataingia na kutoka Ukumbini kwa staha;
(d) Wasisome kitabu chochote, gazeti, barua au hati nyingineyo ambayo si Orodha ya Shughuli za Bunge;
(e) Wasiandike wala kurekodi jambo lolote linalozungumzwa, isipokuwa tu kama ni wawakilishi wa vyombo vya habari;
Ruhusa kwa wageni Bungeni
85
(f) Inapolazimu kuzungumza, wasizungumze kwa sauti ya juu;
(g) Wasivute sigara au kiko wakati wowote wakiwa ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge au mahali popote nje ya Ukumbi huo ambapo kuna mahali pa kukaa wageni;
(h) Wazime simu zao za mikononi;
(i) Wasiingie na kamera wala kupiga picha;
(j) Wasishangilie wala kuzomea wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge; na
(k) Wasifanye jambo au kitendo chochote ambacho kinaweza kuvuruga amani na utulivu Bungeni.
(3) Spika anaweza kumwamuru mgeni yeyote aondoke kwenye Ukumbi wa Bunge endapo atavunja lolote kati ya masharti yaliyotajwa katika fasili ya (2) ya Kanuni hii.
137.-(1) Katibu anaweza kutoa ruhusa maalumu au ya jumla kwa mwakilishi wa chombo chochote cha habari kuhudhuria vikao vya Bunge katika sehemu ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge iliyotengwa kwa ajili hiyo.
(2) Ruhusa yoyote itakayotolewa na Katibu inaweza kuwekewa masharti yafuatayo:-
(a) Chombo husika kitoe maombi rasmi;
(b) Chombo husika kiteue Waandishi wenye sifa na maadili ya kuweza kuandika habari za Bunge.
(3) Katibu anaweza wakati wowote kuondoa ruhusa aliyotoa kwa mwakilishi wa chombo chochote cha habari, iwapo chombo hicho kitatoa taarifa yoyote kuhusu Shughuli za Bunge ambayo, kwa maoni ya Bunge, inapotosha ukweli au vinginevyo inakiuka Kanuni, taratibu au haki za Bunge.
Ruhusa Kwa Waandishi wa Habari
86
Utaratibu wa kukaa kwa Wabunge, Watumishi na Wageni Bungeni
138.-(1) Spika anaweza kuamuru wageni watoke nje ya sehemu yoyote ya Ukumbi na maeneo yake na anaweza kuamuru milango ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge ifungwe.
(2) Endapo wakati wa kikao chochote Mbunge atatoa hoja kuwa wageni watoke nje, Spika atalihoji Bunge papo hapo na hoja itaamuliwa bila ya mjadala au mabadiliko yoyote, wakati wowote atakapoona inafaa kufanya hivyo.
(3) Mtumishi yeyote wa Bunge hataruhusiwa kumtoa nje mgeni au kuagiza mgeni atolewe nje ya Ukumbi wa Bunge endapo Katibu amemruhusu mgeni huyo kuwa ndani ya Ukumbi wa Bunge.
139.- (1) Spika anaweza kuwatambulisha wageni wote wa kitaifa na kimataifa waliomo katika Ukumbi wa Bunge.
(2) Spika vilevile anaweza kuwatambulisha wageni wengine waliomo katika Ukumbi wa Bunge ambao:-
(a) wanahusika moja kwa moja na shughuli za Majimbo;
(b) wanatembelea Bunge kwa ajili ya ziara za mafunzo; na
(c) wametoa mchango wa kitaifa unaohitaji kuenziwa.
SEHEMU YA KUMI NA SITA
UKAAJI NDANI YA BUNGE
140.- Spika ataweka utaratibu maalumu wa ukaaji wa Wabunge ndani ya Bunge, bila ya kuathiri mpangilio ufuatao:-
(a) Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni atakaa kiti cha kwanza akifuatiwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mawaziri, upande wa kulia wa Spika.
(b) Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni atakaa kiti cha kwanza akifuatiwa na Wasemaji Wakuu wa Upinzani upande wa kushoto wa Spika.
Mamlaka ya kuwao- ndoa wageni Bungeni
Utambu- lisho wa Wageni
87
(c) Endapo hakuna Kiongozi wa Upinzani aliyechaguliwa na chama chenye haki ya kuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni lakini Wabunge wa Upinzani wapo, basi Wabunge hao watakaa upande wa kushoto wa Spika.
(d) Wapambe wa Bunge, watumishi wa Ofisi ya Bunge, wahudumu wa Bunge, Watumishi wa Serikali wenye shughuli maalumu Bungeni, waandishi wa vyombo vya habari na wageni wengine watakaa sehemu ambazo zimetengwa kwa ajili yao.
(e) Wageni wa Wabunge na wageni wengine wanaweza kutengewa sehemu maalumu ya kukaa.
(f) Wageni mashuhuri, Mabalozi na Viongozi wengine watakaa sehemu maalumu ya Spika.
SEHEMU YA KUMI NA SABA
USALAMA WA MAENEO YA BUNGE
141.-(1) Spika ataweka utaratibu wa kutoa vitambulisho kwa Wabunge, watumishi wa Bunge, watumishi wa Serikali na kwa mtu mwingine yeyote anayeingia kwenye Ukumbi wa Bunge au maeneo mengine ya Bunge.
(2) Katibu atatoa vitambulisho vya aina tofauti kwa ajili ya Wabunge, watumishi wa Bunge, watumishi wa Serikali na wageni wanaokaribishwa katika Ukumbi wa Bunge au maeneo mengine ya Bunge.
142.-(1) Kutakuwa na utaratibu wa kumkagua mtu yeyote anayeingia katika maeneo ya Bunge kwa kuzingatia:-
(a) staha na heshima; na
(b) tofauti ya jinsia.
(2) Endapo katika kufanya ukaguzi mtu yeyote atapatikana na kifaa ambacho kwa asili yake ni cha hatari, kifaa hicho atakiacha kwa walinzi waliopo mlangoni.
Utaratibu wa kuingia Maeneo ya Bunge
Ukaguzi
88
Lugha Rasmi Bungeni
Taarifa Rasmi za Bunge
(3) Mbunge, mtumishi au mgeni yeyote atakayekataa kukaguliwa au kukabidhi kitu chochote ambacho walinzi wataona kwamba ni cha hatari, hataruhusiwa kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge au maeneo ya Bunge.
SEHEMU YA KUMI NA NANE
MENGINEYO
143.-(1) Kuhudhuria vikao vya Bunge na Kamati zake ni wajibu wa kwanza wa kila Mbunge.
(2) Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria Mikutano ya Bunge mitatu mfululizo bila ruhusa ya Spika iliyotolewa kwa maandishi, atapoteza Ubunge wake kwa mujibu wa Ibara ya 71(1)(c) ya Katiba na Spika ataiarifu Tume ya Uchaguzi.
(3) Mbunge atakapokosa kuhudhuria nusu ya vikao vya Mkutano mmoja bila ya sababu ya msingi atapewa onyo.
(4) Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria vikao vya Bunge na Kamati zake kwa sababu maalumu atatakiwa kupata kibali cha Spika.
(5) Kwa madhumuni ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, kibali kitatolewa katika Ofisi za Bunge za Dodoma au Dar es Salaam au Zanzibar.
144.-(1) Shughuli za Bunge zitaendeshwa katika lugha ya Kiswahili au Kiingereza, bila tafsiri ya lugha hizo kutolewa.
(2) Kwa kadri itakavyowezekana, Mbunge atajitahidi kutochanganya lugha zote mbili wakati anasema Bungeni, isipokuwa tu pale anaponukuu.
145.-(1) Taarifa Rasmi ya Majadiliano Bungeni, ikiwa katika lugha iliyotumiwa na msemaji, yakiwa ni maneno halisi aliyoyatamka, itatayarishwa chini ya usimamizi wa Katibu wa Bunge kwa kufuata maagizo yatakayotolewa na Spika kwa ajili hiyo.
(2) Kila Mbunge aliyetoa hotuba Bungeni atapewa nakala ya hotuba yake mapema iwezekanavyo, ili aweze kusahihisha makosa ya uchapaji, kama yatakuwepo ila hataruhusiwa kubadilisha maana halisi ya maneno aliyoyasema Bungeni.
Wajibu wa Mbunge kuhudhuria Vikao vya Bunge Sura ya 2, Toleo la 2002
89
146.-(1) Mbunge anayeingia kwenye Ukumbi wa Bunge atawajibika kuvaa mavazi ambayo ni safi na yenye kuhifadhi heshima yake, hadhi ya Bunge na utamaduni wa nchi, kama ilivyoainishwa katika Kanuni hii.
(2) Vazi Rasmi la Spika na Naibu Spika litakuwa ni joho lenye kuonesha rangi za Bendera ya Taifa, Nembo ya Taifa na baadhi ya mazao makuu nchini, lililoshonwa maalumu kwa ajili hiyo, ambalo litavaliwa juu ya vazi lolote ambalo ni vazi rasmi kwa Wabunge.
(3) Vazi rasmi kwa Wabunge litakuwa lolote kati ya yafuatayo:-
(a) Kwa Wabunge wanawake:- (i) vazi lolote la heshima yaani ambalo si la kubana mwili, lisiloonesha maungo ambayo kwa mila na desturi za kitanzania hayapaswi kuoneshwa na ni refu kuvuka magotini;
(ii) gauni la kitenge au blauzi inayovaliwa na kitenge au sketi ya rangi yoyote;
(iii) kilemba cha kadri au mtandio;
(iv) suti ya kike; na
(v) vazi linalovaliwa wakati wa eda.
(b) Kwa Wabunge wanaume:- (i) suti ya Kiafrika au safari ya mikono mirefu au mifupi yenye ukosi au shingo ya mviringo na yenye fulana au bila fulana ndani, ya rangi moja, isiyokuwa na nakshi, pamoja au bila baragashia;
(ii) vazi la kimwambao yaani kanzu rasmi na nadhifu, koti, baraghashia na makubadhi au viatu;
(iii) suti kamili ya kimagharibi ya rangi kadri isiyomeremeta;
(iv) koti aina ya blazer na tai, pamoja na suruali yoyote ya heshima; au
Mavazi Rasmi
90
(v) tarbushi na kilemba cha Singasinga, au kilemba chochote kinachovaliwa kwa mujibu wa masharti ya imani au mila.
(4) Vazi Rasmi la Katibu na Wasaidizi wake Bungeni litakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Kwa Makatibu wanaume:
(i) suti kamili ya kiafrika au safari, yenye ukosi au shingo ya mviringo na mikono mirefu au mifupi ya rangi nyeusi au bluu; au
(ii) suti kamili ya kimagharibi ya rangi nyeusi au bluu na shati jeupe na tai.
(b) Kwa Makatibu wanawake:
Suti ya rangi nyeusi au ya bluu na shati jeupe na tai.
(c) Makatibu na Wahudumu watavaa mavazi maalumu wakati wa shughuli maalumu za Bunge.
(5) Mpambe wa Bunge na Wasaidizi wake ndani ya Ukumbi wa Bunge watavaa mavazi rasmi ambayo yataamuliwa na Spika.
(6) Spika anaweza kwa sababu maalumu, kumruhusu mtu mwingine anayehusika na shughuli za Bunge kuvaa viatu ambavyo sio rasmi.
(7) Mbunge yeyote anaweza kutoa taarifa Bungeni iwapo Mbunge mwingine ataingia kwenye Ukumbi wa Bunge akiwa na mavazi yasiyoruhusiwa kwa mujibu wa Kanuni hii.
(8) Spika atakaporidhika kuwa Mbunge aliyetolewa taarifa kwa mujibu wa fasili ya (7) ya Kanuni hii hajavaa mavazi rasmi ataamuru Mbunge huyo atoke nje ya Ukumbi wa Bunge.
(9) Mbunge aliyetolewa nje kwa mujibu wa fasili ya (8) ya Kanuni hii hataingia ndani ya Ukumbi wa Bunge hadi pale atakapokuwa amevaa mavazi rasmi.
147. Kutakuwa na Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayoitwa Bendera ya Bunge, ambayo:-
Bendera ya Bunge
91
(a) itakuwa katika umbo la mstatiri na rangi ya bluu iliyoiva na pembeni itakuwa na umbo dogo la bendera ya Taifa ndani yake katika pembe ya juu upande wa kushoto.
(b) itakuwa pia na Siwa ya Bunge yenye rangi ya dhahabu, chini kukiwa na utepe wenye maneno “Bunge la Tanzania.”
148.-(1) Bendera ya Bunge itapepezwa kwenye maeneo yafuatayo:-
(a) Katika Ofisi za Bunge Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar.
(b) Nje ya Ofisi za Wabunge zilizopo Makao Makuu ya Mkoa, Wilaya na katika Majimbo ya Uchaguzi.
(c) Ndani ya Ofisi ya Mbunge juu ya meza anayofanyia kazi.
(d) Katika magari binafsi ya Wabunge ambapo Bendera hiyo itapepezwa ikiwa mbele upande wa kushoto wa gari la Mbunge wakati Mbunge mwenyewe anapokuwa ndani ya gari hilo, na akiwa anaendeshwa na dereva mwingine, siyo anapokuwa anaendesha mwenyewe.
(2) Mbunge hatapepeza Bendera kwenye gari lake awapo katika Miji ya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, na anapokuwa anatumia gari la kukodi au la kuazima.
(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, Bendera ya Bunge itapepezwa kuanzia saa 12.00 asubuhi na kuteremshwa mara ifikapo saa 12.00 jioni kila siku.
(4) Bendera ya Bunge itaendelea kupepezwa katika gari la Mbunge baada ya saa 12.00 jioni endapo anayepepeza Bendera hiyo atakuwa safarini hadi pale atakapomaliza safari yake.
Utaratibu wa kupepeza Bendera
92
Kufanya Mabadi- liko katika Kanuni
149.- Endapo Mbunge atafariki wakati Bunge likiwa katika shughuli zake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili ya maombolezo.
150.-(1) Kwa idhini ya Spika, Kanuni yoyote inaweza kutenguliwa kwa madhumuni mahususi baada ya Waziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali au Mbunge yeyote kutoa hoja kwa ajili hiyo.
(2) Hoja ya kutengua Kanuni za Bunge haitahitaji kutolewa taarifa.
(3) Maelezo ya hoja ya kutaka kutengua Kanuni yoyote itakuwa ni pamoja na maelezo kuhusu madhumuni ya kutaka Kanuni hiyo itenguliwe.
(4) Kanuni hiyo itatenguliwa kwa madhumuni yaliyokusudiwa tu na siyo kwa madhumuni mengine yoyote.
151.-(1) Endapo litatokea jambo lolote ambalo muhusika wake au mwathirika wa jambo hilo anastahili kupewa pongezi au pole na Wabunge basi Spika atatoa pongezi au pole kwa mhusika au mwathirika wa jambo hilo kwa niaba ya Wabunge wote . (2) Baada ya Spika kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote, kwa ajili ya kuokoa muda wa majadiliano, Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakati wowote wa majadiliano Bungeni.
(3) Kwa upande wa Serikali, Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni atatoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote kwa niaba ya Serikali.
(4) Baada ya Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote, kwa ajili ya kuokoa muda wa majadiliano, Waziri yeyote hataruhusiwa kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakati wowote wa majadiliano Bungeni.
152.-(1) Bunge linaweza kupitisha Azimio la kufanya mabadiliko katika Kanuni yoyote kutokana na mapendekezo ya Kamati ya Kanuni za Bunge.
(2) Mabadiliko yoyote ya Kanuni za Bunge yatawasilishwa Bungeni na Naibu Spika.
Salamu za Pongezi na Pole
Utaratibu baada ya kifo cha Mbunge
Kutengua Kanuni za Bunge
93
(3) Spika, kwa kushauriana na Kamati ya Kanuni za Bunge, atakuwa na madaraka ya kuzifanyia marekebisho au mabadiliko Nyongeza za Kanuni hizi, kulingana na mahitaji ya wakati, kadri atakavyoona inafaa.
153.-(1) Mabadiliko yaliyopitishwa hayataanza kutumika mpaka yatakapochapishwa na kuingizwa katika Toleo la Kanuni za Bunge litakalofuata.
(2) Endapo Kanuni za Bunge zitafanyiwa mabadiliko, Spika ataagiza zichapishwe upya kwenye Gazeti kwa madhumuni ya kuingiza mabadiliko yaliyofanyika.
(3) Nakala za Kanuni za Bunge zilizochapishwa kwa kufuata utaratibu uliofafanuliwa katika Kanuni hii itahesabiwa kuwa nakala halisi za Kanuni za Kudumu za Bunge zilizofanyiwa mabadiliko.
154.-(1) Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2004 zinafutwa.
(2) Bila kujali masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii jambo lolote, amri yoyote, uteuzi wowote, agizo au suala jingine lolote lililofanyika kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2004 halitakuwa batili na litaendelea kuwa halali hadi litakapobadilishwa, kufutwa au kuagizwa vinginevyo kwa mujibu wa Kanuni hizi.
Kanuni kuanza kutumika
Kufutwa kwa Toleo la 2004 na hifadhi ya mambo yaliyo- fanyika
94
________
NYONGEZA _________
NYONGEZA YA KWANZA ________________
KANUNI ZA UCHAGUZI WA SPIKA NA NAIBU SPIKA _________
(Chini ya Kanuni ya 9 na 10) _________
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Uchaguzi wa Spika na Naibu Spika.
2. Kanuni hizi zitatumika katika mchakato wa Uchaguzi wa Spika na Naibu Spika.
3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale maelezo yatakapohitaji vinginevyo:- “Chama” ni Chama cha Siasa chenye usajili wa kudumu; “Chombo cha Uteuzi” ni Chama kinachopendekeza mgombea au wagombea wake; “Katibu” ni Katibu wa Bunge; “ Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri ya Muungano; “Mgombea” ni mtu aliyejitokeza au aliyependekezwa na Chama cha Siasa kuwa mgombea wa uchaguzi; “Msimamizi wa Uchaguzi” ni mtu ambaye kwa mujibu wa Kanuni hizi amepewa mamlaka ya kuendesha na kusimamia Uchaguzi; “Nafasi” ni nafasi wazi ya Spika au Naibu Spika, iliyotokea ama kutokana na kuvunjwa kwa Bunge au kutokana na nafasi itokeayo kwa nasibu; “Nafasi ya nasibu” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabunge isiyotokana na kuvunjwa kwa Bunge; “Naibu Spika” ni Naibu Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 85 ya Katiba;
Jina
Matumizi
Tafsiri
95
“Siku ya uteuzi” ni siku ambayo imetangazwa na msimamizi wa uchaguzi kwamba ndiyo siku ya mwisho ya kupokea majina ya wagombea; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 84 ya Katiba; “Uchaguzi” ni Uchaguzi wa Spika au Naibu Spika.
SEHEMU YA PILI MSIMAMIZI WA UCHAGUZI
4. Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo, uchaguzi wa Spika na Naibu Spika utaendeshwa na kusimamiwa na Katibu wa Bunge, kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge pamoja na Kanuni hizi.
SEHEMU YA TATU KUWASILISHA JINA LA MGOMBEA
5.-(1) Inapofika wakati wa uchaguzi wa Spika au Naibu Spika, Chama chochote cha Siasa chenye kusudio la kushiriki kwenye uchaguzi huo kitawasilisha kwa Katibu wa Bunge jina moja tu la ama Mbunge wa Chama hicho au la mtu mwingine yeyote wa Chama hicho mwenye sifa za kuwa Mbunge kuwa mgombea wake.
(2) Mgombea mhusika au Ofisa wa ngazi ya kitaifa wa Chama kilichompendekeza, atawasilisha jina la mgombea huyo kwa Katibu ambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi.
(3) Jina la mgombea huyo linatakiwa limfikie Katibu Ofisini kwake Dodoma, kabla ya saa kumi jioni ya siku ya uteuzi.
SEHEMU YA NNE MASHARTI YA MGOMBEA UCHAGUZI
6. Mtu yeyote anaweza kuteuliwa kugombea kuchaguliwa kuwa Spika au Naibu Spika iwapo tu atakuwa ametimiza masharti yote ya kuwa mgombea wa nafasi hizo, kama yalivyotajwa katika Kifungu cha 38 cha Sheria ya Uchaguzi, Sura 343, Toleo la 2002.
Uendeshaji na usimamizi wa uchaguzi
Kuwasi- lisha majina ya wagombea
Masharti kwa mgombea
96
SEHEMU YA TANO KUCHAGULIWA BILA KUPINGWA
7. Endapo hadi kufikia saa kumi jioni ya siku ya uteuzi kutakuwa na jina moja tu lililowasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi, mgombea huyo atatangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi kuwa amechaguliwa bila kupingwa kuwa Spika au Naibu Spika.
Kuchagu- liwa bila kupingwa
97
_________ NYONGEZA YA PILI _________
KANUNI ZA UCHAGUZI WA WABUNGE WANAOKWENDA KWENYE VYOMBO VINGINE VYA UWAKILISHI _________ (Chini ya Kanuni ya 12) _________
SEHEMU YA KWANZA UTANGULIZI
1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katika vyombo vingine vya uwakilishi au kuwa Wajumbe wa Tume ya Bunge.
2. Kanuni hizi zitatumika kwa uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katika vyombo vingine kuliwakilisha Bunge na pia kwa uchaguzi wa Wabunge wanaogombea kuwa wajumbe wa Tume ya Bunge.
3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale maelezo yanapohitaji vinginevyo:- “Chama” ni Chama cha Siasa chenye uwakilishi Bungeni; “Chombo cha Uteuzi” ni chama kinachopendekeza mgombea au wagombea wake; “Katibu” ni Katibu wa Bunge; “Idadi inayotakiwa” ni idadi ya kura zinazotakiwa kupatikana au idadi ya nafasi zinazotakiwa zijazwe kwenye Uchaguzi; “Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri ya Muungano; “Mgombea” ni mtu aliyejitokeza au aliyependekezwa na Chama cha Siasa kuwa mgombea wa uchaguzi; “Msimamizi wa Uchaguzi” ni mtu ambaye kwa mujibu wa Kanuni hizi amepewa mamlaka ya kuendesha na kusimamia Uchaguzi; “Nafasi” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabunge kutoka miongoni mwa Wabunge iliyotokana na kuvunjwa kwa Bunge au na nafasi itokeayo kwa nasibu; “Nafasi ya nasibu” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabunge isiyotokana na kuvunjwa kwa Bunge;
Tafsiri
Jina
Matumizi
98
“Siku ya uteuzi” ni siku ambayo imetangazwa na Msimamizi wa uchaguzi kwamba ndiyo siku ya mwisho ya kupokea majina ya Wagombea; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyechaguliwa kwa mujibu wa Ibara ya 84 ya Katiba; “Uchaguzi” ni uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katika vyombo vingine kuliwakilisha Bunge au kuwa Wajumbe wa Tume ya Bunge.
SEHEMU YA PILI UTEUZI WA WAGOMBEA
4. Uteuzi wa Wagombea utafuata utaratibu ufuatao:-
(a) Unapofika wakati wa Uchaguzi, kila Mbunge anayetaka kushiriki atawasilisha jina lake kwa Katibu ambaye atakuwa ndiye Msimamizi wa Uchaguzi huo.
(b) Majina ya Wagombea wote yatatakiwa kumfikia Katibu Ofisini kwake Dodoma, siku moja kabla ya siku ya uteuzi.
SEHEMU YA TATU UTARATIBU WA UCHAGUZI
5.-(1) Uchaguzi wa wagombea wa nafasi za Uwakilishi utaendeshwa na kusimamiwa na Katibu kwa utaratibu ufuatao:-
(a) Wakati wa Uchaguzi wa kwanza katika maisha ya Bunge wa nafasi zilizotangazwa, mara tu baada ya Wagombea kuwasilisha majina yao, Spika:-
(i) Ataagiza majina ya wagombea wote waliojitokeza yasambazwe kwa Wabunge;
(ii) Atatangaza Bungeni siku na muda ambapo kura zitapigwa;
(b) Katibu atatoa Taarifa ya maandishi kuhusu saa ya kupiga kura ambayo itatolewa si chini ya saa ishirini na nne kabla ya muda wa kupiga kura.
Uchaguzi wa wagombea wa nafasi za uwakilishi
Uteuzi wa Wagombea
99
(c) Endapo itatokea nafasi miongoni mwa Wabunge waliochaguliwa kwa kufuata Kanuni hizi kutokana na sababu isiyohusiana na kuvunjwa kwa Bunge au kama nafasi ya namna hiyo haikujazwa, Spika atatoa taarifa ya kutokea kwa nafasi hiyo kwa Wabunge wote Bungeni.
(2) Utaratibu wa kujaza nafasi ambazo zimetengwa maalumu kwa ajili ya ama kundi la Wabunge Wanawake au kundi la Wabunge wa Kambi ya Upinzani, utakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Katibu atatangaza siku ya uteuzi ambayo itakuwa si zaidi ya siku tano baada ya tangazo la Spika kutolewa Bungeni kwa mujibu wa fasili ya (1)(c) ya Kanuni hii.
(b) Mbunge yeyote wa kundi linalohusika anayetaka kuwa mgombea wa nafasi hiyo atawasilisha jina lake kwa Katibu, angalau siku moja kabla ya siku ya uteuzi iliyowekwa.
(c) Endapo atajitokeza mgombea mmoja wa nafasi inayohusika, Wabunge watampigia kura za “NDIYO” au “HAPANA.”
(3) Baada ya kupata majina ya wagombea wote, Katibu atatoa matangazo kuhusiana na idadi ya wagombea, siku na muda wa uchaguzi.
(4) Endapo kunatokea nafasi mbili au zaidi za nasibu kwa wakati mmoja, uchaguzi na upigaji kura utaendeshwa kama uchaguzi mmoja.
SEHEMU YA NNE UCHAGUZI WA KUJAZA NAFASI ZA NASIBU
6. Kwa madhumuni ya uchaguzi wa kujaza nafasi yoyote ya nasibu, kutakuwa na karatasi moja tu ya kura ambayo itakuwa na orodha ya majina ya wagombea wote waliojitokeza, inayofuata mfululizo wa alfabeti pamoja na jina la Chama cha mgombea na kutakuwa na nafasi tupu pembeni ya jina la kila mgombea kwa ajili ya kuweka alama ya kupiga kura.
Uchaguzi wa kujaza nafasi za nasibu
100
SEHEMU YA TANO UTARATIBU WA KUPIGA KURA
7.-(1) Kila Mbunge atakayekuwepo ukumbini wakati wa kupiga kura anaweza, katika uchaguzi wa kwanza katika maisha ya Bunge au katika uchaguzi wa kujaza nafasi ya nasibu moja au zaidi:-
(a) kupiga kura moja moja au zaidi kulingana na maelekezo yaliyomo kwenye karatasi ya kura kwa ajili ya wagombea uchaguzi wa nafasi inayoshindaniwa kutoka miongoni mwa wale waliopendekezwa; au
(b) kupiga kura moja kwa kila mgombea Uchaguzi mmoja kwa kufuata idadi ya nafasi za nasibu zilizopo katika Uchaguzi huo.
(2) Mbunge atapiga kura yake kwa kuweka alama ya “V” katika nafasi wazi ya karatasi ya kura pembeni ya jina la mgombea anayetaka kumpigia.
SEHEMU YA SITA KUPIGA KURA
8.-(1) Utakapofika wakati wa kupiga kura, Spika atasitisha majadiliano ya Bunge na kuelekeza kwamba, kura ipigwe.
(2) Wakati huo huo mambo yafuatayo yatafanyika:-
(a) Katibu atatangaza idadi au aina ya Chaguzi zitakazofanyika au nafasi zitakazojazwa;
(b) Kila mgombea atapewa muda wa kujieleza na kuomba kura.
(3) Kabla ya kupiga kura, sanduku la kura litaoneshwa kwenye ukumbi kuwa ni tupu, baada ya hapo kila Mbunge atakayekuwepo ukumbini atapewa karatasi moja ya kupiga kura.
(4) Sanduku la kura litawekwa chini ya usimamizi wa Katibu pamoja na Wabunge waliochaguliwa kusimamia kuhesabiwa kwa kura mpaka wakati wa kuhesabiwa kwa kura, na Katibu pamoja na hao Wabunge watakuwa na madaraka kuhakikisha kwamba, sanduku hilo halifunguliwi mpaka wakati wa kuanza kuhesabu kura na
Utaratibu wa kupiga kura
Kupiga kura
101
kwamba, hakuna kitu kitakachowekwa ndani ya sanduku hilo baada ya karatasi za kura kukusanywa kwa mujibu wa fasili ya (3).
(5) Baada ya Wabunge kupiga kura, karatasi zitakusanywa na kutumbukizwa kwenye sanduku la kura.
(6) Baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika na karatasi za kura kukusanywa, Spika atachagua Wabunge wawili wasimamie kazi ya kuhesabu kura na majadiliano ya Bunge yatarudia kuanzia pale yalipositishwa.
SEHEMU YA SABA KUHESABU KURA
9.-(1) Mapema itakavyowezekana baada ya kupiga kura na kabla ya kumaliza Kikao kilichopo cha Bunge, Katibu, mbele ya Wabunge wawili waliochaguliwa kusimamia zoezi la kuhesabu kura, atalifungua sanduku la kura, kuzihesabu na kuziandika kura alizopata kila mgombea.
(2) Karatasi ya kura itakataliwa na kura hazitahesabiwa katika karatasi hiyo:-
(a) ikiwa karatasi hiyo siyo rangi rasmi ya karatasi ya kupigia kura iliyotolewa na Katibu;
(b) ikiwa mpiga kura amepiga kura zaidi au pungufu ya zile zinazotakiwa kupigwa;
(c) ikiwa kutaonekana kwenye karatasi hiyo maandishi yoyote au alama yoyote iliyowekwa na mpiga kura isiyokuwa ya ile ya “V”;
(d) ikiwa haikuwekwa alama au imewekwa alama isiyoonesha dhahiri ni mgombea yupi ambaye mpiga kura amempigia; isipokuwa kwamba, ikiwa baadhi ya kura kwenye karatasi ya kura ni dhahiri na nyingine si dhahiri, karatasi ya kura hiyo itakataliwa kuhusu tu zile kura zisizokuwa dhahiri na kura zilizo dhahiri zitahesabiwa.
(3) Uamuzi wa Spika juu ya kuwa karatasi ya kura ikataliwe yote au sehemu tu utakuwa ni wa mwisho.
Kuhesabu kura
102
SEHEMU YA NANE KUTANGAZA MATOKEO YA KURA
10.-(1) Baada ya kura kuhesabiwa, Katibu atatangaza matokeo ya kura zote zilizopigwa kisha atatamka majina ya wagombea waliochaguliwa ambao wamepata idadi kubwa zaidi ya kura na kuwatangaza kwamba wamechaguliwa.
(2) Endapo baada ya kuhesabu kura kutakuwa na sababu ya kurudia Uchaguzi kutokana na kutokupatikana mshindi katika nafasi yoyote inayohusika katika uchaguzi huo, Spika ataeleza sababu za kutokupatikana mshindi, kisha ataagiza kura ipigwe tena ili kupata mshindi kwa nafasi hiyo.
(3) Kura ya uamuzi haitatumika kwenye uchaguzi.
(4) Iwapo imeamuliwa ipigwe kura tena kwa mujibu wa fasili ya (2), basi wagombea wanaopigiwa kura watakuwa ni wale tu ambao walipata kura sawa.
(5) Iwapo Spika hawezi kutangaza idadi inayotakiwa ya wagombea waliochaguliwa kwa sababu ya kukosekana kura, basi:-
(a) atatangaza kadri ya wingi wa wagombea waliochaguliwaambao wamepata kura kuwa wamechaguliwa; na
(b) atawaarifu Wabunge wote kuhusu nafasi iliyobakia au zilizobakia na utaratibu wa uchaguzi utaanza upya kwa ajili ya nafasi hiyo au nafasi hizo.
(6) Kila tamko na agizo linalotolewa na Spika kwa mujibu wa Kanuni hii litatolewa Bungeni.
Kutangaza matokeo ya kura
103
SEHEMU YA TISA UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZA KURA
11.-(1) Katibu ataandika maneno “imekataliwa” na “kura iliyokataliwa” kwenye karatasi za kura zilizokataliwa na ataziweka karatasi hizo pamoja na zile zilizokuwa safi kwa muda wa miezi sita baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi.
(2) Baada ya hapo, isipokuwa kama Bunge litaamuru vinginevyo, Katibu ataziharibu karatasi hizo.
(3) Karatasi za kura zilizokwishatumika hazitaonyeshwa kwa mtu yeyote na Katibu, isipokuwa kwa mujibu wa azimio la Bunge baada ya hoja ya kutaka zionyeshwe kupitishwa.
SEHEMU YA KUMI KUPINGA MATOKEO YA KURA
12. Iwapo mgombea yeyote hataridhika na matokeo ya Uchaguzi au jinsi uchaguzi ulivyofanywa, atakuwa na haki ya kupeleka madai yake mahakamani na madai hayo yatashughulikiwa kwa mujibu wa Sheria iliyowekwa na Bunge kwa ajili ya kushughulikia malalamiko ya uchaguzi wa Wabunge.
Utunzaji wa kumbu- kumbu za kura
Kupinga Matokeo ya kura
104
__________
NYONGEZA YA TATU
__________
THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLY ELECTION RULES
______ (Made under Standing Order 12 and Article 50 of the Treaty for the Establishment of East African Community) _______
ARRANGEMENT OF RULES ____________
PART I
PRELIMINARY RULES
1. These Rules may be cited as the East African Legislative Assembly Election Rules.
2. In these rules, all the parliamentary words and expressions used shall have the same meaning assigned to them in the Parliamentary Standing Orders and, unless the context requires otherwise:-
“Candidate” means a person who is nominated to stand for election to the East African Legislative Assembly as provided for in rule 5 of these rules; “Election” means an election to the East African Legislative Assembly; “Nomination” means nomination as a candidate to stand for election to the East African Legislative Assembly; “Returning Officer” means the Clerk of the National Assembly; “Treaty” means the Treaty for the Establishment of the East African Community, 1999; “Voter” means a Member of Parliament present and voting during the election;
Citation
Interpre- tation
105
PART II QUALIFICATION OF CANDIDATES
3. A person shall be qualified to be a candidate for election to the East African Legislative Assembly who he is qualified to be elected in accordance with Article 50(2) of the Treaty.
PART III NOMINATION OF CANDIDATES
4. -(1) Where an election is to be held, the Returning Officer shall by notice published in the Gazette, appoint a nomination day for that election.
(2) The Returning Officer shall give at least fourteen days notice of such nomination day.
5.-(1) In order to be validly nominated as a candidate for the East African Legislative Assembly elections, a person must be nominated in a transparent and democratic manner by the political party which is sponsoring him.
(2) The nomination shall be in the prescribed form, signed by the candidate and by the Secretary General of the party nominating him, and shall contain the following particulars:-
(a) The name, educational qualifications, address and occupation of the candidate;
(b) A certificate by the candidate that he is willing and otherwise qualified to stand for election.
(3) Every nomination paper shall be accompanied by the following documents:-
(a) Proof of citizenship of the United Republic of Tanzania, provided by the Immigration Department;
(b) Detailed biographical information relating to the candidate signed by the candidate himself,
Qualifi- cation of candidates
Nomina- tion of Candida- tes
Validity of nomina- tion
106
which shall enable the Returning Officer to determine whether or not the candidate has proven experience or interest in consolidating and furthering the aims and objectives of the Community in terms of Article 50(2)(e) of the Treaty; and
(c) An extract of the nomination proceedings of the party organ which approved the final nomination of the candidate, signed by the Chairman and Secretary of that Organ which shall enable the Returning Officer to determine whether or not the relevant political party’s proceedings were democratic and transparent in terms of the Political Parties Act.
(4) The candidate or an official of the Party nominating him, shall deliver the nomination papers to the Returning Officer at his office in Dodoma, not later than four o’clock in the afternoon of the nomination day.
(5) Any political party which is entitled to sponsor candidates may submit to the Returning Officer, the names of three candidates for each vacant seat in the following relevant groups:-
Group A: Women Candidates; Group B: Zanzibar Candidates; Group C: Opposition Parties Candidates; Group D: Mainland Candidates.
6. A candidate, or an official of the party nominating him shall, at the time of delivering the nomination paper, deposit a non- refundable deposit of fifty thousand shillings, to cover for the cost of election expenses.
7. Objections may be made by the Returning Officer to the nomination of a candidate, if it is apparent to him from the contents of the nomination papers that the candidate is not qualified to stand for election. In which case the Returning Officer shall forthwith reject the nomination papers of that candidate.
Cap. 258
Non- refunda- ble deposit
Rejection of nomina- tion papers
107
PART IV ELECTION AND VOTING PROCEDURE
8. The Returning Officer shall by notice published in the Gazette, appoint an election day which shall be not more than seven days after nomination day, provided that, such election day shall be a day when the National Assembly is sitting in ordinary session.
9.-(1) A candidate may withdraw his candidature by notice in writing, signed and delivered by him to the Returning Officer and a copy to the Secretary General of the Party sponsoring him, not later than four o’clock in the afternoon of the day following nomination day, thereafter no withdraws shall be accepted.
(2) Where any candidate dies after four o’clock in the afternoon of nomination day and before election day, the election process will continue undisturbed.
10.-(1) An aspiring candidate may introduce himself to the voters and seek their support even before nomination day and may continue to do so after nomination day.
(2) Before the votes are cast on election day, each candidate will be permitted to appear before the voters, duly assembled in an ordinary sitting of the House and address them in English for such length of time and answer such number of questions, if any, as may be determined by the Speaker for that purpose.
11.-(1) The voting shall be conducted under the general supervision of the Returning Officer.
(2) The Returning Officer shall issue only one ballot paper to each voter. (3) The ballot paper shall contain the names of all candidates, arranged alphabetically in the following groups:-
Group A: Women Candidates; Group B: Zanzibar Candidates; Group C: Opposition Parties Candidates; Group D: Mainland Candidates.
Withdra- wal of candida- ture
Campaign by candidates
Election day
Supervi- sion of the Voting process
108
(4) A voter shall be required to cast a specified number of votes, to be announced by the Speaker in each of the groups.
(5) On receiving a ballot paper, each voter shall secretly record his votes by putting a mark against the names of the nine candidates he wishes to vote for.
(6) Each voter shall be required to cast as many votes as there are vacancies, otherwise his whole ballot paper will be regarded as spoilt.
(7) A voter who has accidentally spoiled his ballot paper while the voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paper to the Returning Officer and obtain a replacement thereof.
12.-(1) When all the voters have casted their votes, the Speaker shall appoint two counting agents, one from the ruling party and the other from the opposition benches, to act as counting agents for all the candidates.
(2) Immediately after all the ballots have votes been collected, the Returning Officer, with the assistance of Clerk Assistants and before the two counting agents as witnesses, shall count the votes so casted.
(3) In order to enable the National Assembly to proceed with other business, the counting of votes shall take place outside the Assembly Chamber, in a room designated by the Clerk for that purpose within the precincts of the Assembly.
13. When the votes have already been counted and the results of the election has been ascertained, the Returning Officer shall:-
(a) Report to the Assembly the election results, together with the number of votes recorded for each candidate in each group. (b) Announce to the Assembly the names of nine persons receiving the majority number of votes in each group and shall declare those persons to have been elected as members of the East African Legislative Assembly.
Votes Count- ing agents
Announce- ment of election results
109
14.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of all ballot papers and other documents relating and pertaining to the conduct of the election.
(2) The Returning Officer shall cause all documents to which this paragraph applies to be destroyed after the expiration of six months from the election day, unless otherwise directed by an order of the High Court arising from any proceedings of a petition relating to the election.
PART V ANNULMENT AND AVOIDANCE OF ELECTION
15. Pursuant to the provisions of Article 52(1) of the Treaty, the election of a candidate as a member of the East African Legislative Assembly may be declared null and void only on an Election Petition.
16. The procedure, jurisdiction and grounds for declaring the election of such member null and void shall be the same as those provided by law for election petitions in respect of Members of the Parliament of the United Republic of Tanzania.
PART VI MISCELLANEOUS
17. (1) If any matter or thing arises which is not specifically provided for in these rules, the Speaker shall make a ruling directing what is to be done in respect of that matter or thing.
(2) In making such a ruling, the Speaker shall be guided by the practices and procedures normally followed in similar situations with regard to Parliamentary elections.
18. These rules may be amended at any time by a resolution of the National Assembly on a proposal submitted to it by the Standing Orders Committee.
Custody of ballot papers
Grounds for annulment and avaoid- ance of election
Matters not provided for
Amend- ment of rules
Annulment and avoida- nce of election
110
__________ NYONGEZA YA NNE __________
THE SUBMISSION OF REGULAR REPORTS TO THE PARLIAMENT OF TANZANIA BY THE TANZANIA MEMBERS OF THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLY ___________ [Made under Article 65 of the Treaty for the Establishment of the East African Community] _________
1. These Regulations may be cited as the Submission of Regular Reports to the Parliament of the United Republic of Tanzania by the Members of the East African Legislative Assembly Regulations.
2.-(1) These Regulations are made to provide for a procedure for the Members of the East African Legislative Assembly hailing from Tanzania to submit regular reports to the Parliament of the United Republic of Tanzania.
(2) These Regulations shall apply to members of East African Legislative Assembly hailing from the United Republic of Tanzania.
3. The Members of the East African Legislative Assembly shall present an annual report of the activities of the East African Legislative Assembly for the relevant year, to the Parliament of the United Republic of Tanzania through its Standing Committee responsible for Foreign Affairs, Defence and Security.
4. The annual reports shall be presented at a regular meeting of the Standing Committee at a time to be determined by the Chairman of the Committee.
5. The Tanzania members of the East African Legislative Assembly may, if they consider it desirable to do so, present any special report, or make any appropriate consultations with the Committee, on any matter which is relevant to the work of the East African Legislative Assembly at any other scheduled meeting of the Committee.
Application
Presentation of annual report
Time of presentation
Presenta- tion of special report and consultations
Citation
111
6.-(1) All Tanzania Members of the East African Legislative Assembly shall be present at the time of presentation of any report.
(2) All such reports shall subsequently be laid on the Table of the House and shall be debated.
Attenda- nce and laying of reports on the Table
112
__________ NYONGEZA YA TANO __________ THE PAN-AFRICAN PARLIAMENTARY ELECTION RULES
[Made under Standing Order 12 and Article 2 of the Protocol to the Treaty for Establishing of the African Economic Community Relating to the Pan-African Parliament]
PART I PRELIMINARY RULES
1. These Rules may be cited as the Pan-African Parliamentary Election Rules, and shall come into operation on the day of their adoption by resolution of the National Assembly.
2. In these Rules, unless the context requires otherwise- “Candidate” means a Member of Parliament who is duly nominated to stand for election to the Pan-African Parliament as provided for in rule 5 of these Rules; “Election” means the election to membership of the Pan-African Parliament; “Election day” means the day on which the election of Members of the Pan-African Parliament is set to be conducted; “Nomination” means nomination as a Candidate to stand for election to the Pan-African Parliament; “Nomination day” means the day which shall by notice published by the Returning Officer, be set to be the last day for receiving application forms from Candidates; “Nominator” means a Member of Parliament of the Parliament of the United Republic of Tanzania entitled to vote, who nominates and supports a Candidate who aspires to stand and contest for election to the Pan-African Parliament; “Qualification” means the qualification which entitles a person to stand and contest for election to the Pan-African Parliament; “Returning Officer” means the Clerk of the National Assembly; “Speaker” means the Speaker of the National Assembly; “Voter” means a Member of Parliament of the United Republic of Tanzania present and voting during the election.
Citation
Interpreta- tion
113
PART II QUALIFICATION OF CANDIDATES
3. No person shall be qualified to be a Candidate for election to the Pan-African Parliament unless he or she is a Member of Parliament of the United Republic of Tanzania, and is fluent in any of the languages approved for use in the proceedings of the Pan- African Parliament.
PART III NOMINATION PROCEDURE
4.-(1) Where election of Members of the Pan-African Parliament is to be held, the Returning Officer shall, by written notice circulated to all members of the Parliament of the United Republic of Tanzania, appoint a nomination day for that election, which must be a day during any period when the National Assembly is in ordinary session.
(2) The Returning Officer shall give at least seven days notice of such nomination day.
5. The following shall be the procedure for the nomination of candidates that:-
(a) in the case of a General Election of all the five members of the Pan-African Parliament representing Tanzania, the candidates will be nominated in accordance with the following groups:-
Group A: Women Candidates; Group B: Zanzibar Candidates; Group C: Mainland Candidates; Group D: Opposition Parties Candidates;
Provided that, whereas Group A shall be reserved for Women Candidates only, the remaining Groups shall be open to both men and women Candidates.
(b) the number of candidates to be elected in each group shall be as follows:-
Quqlifica- tion of Candidates
Appoint- ment of nomination day
Nomina- tion procedure
114
Group A: One Candidate; Group B: One Candidate; Group C: Two Candidates; Group D: One Candidate;
(c) in the case of a by-election to fill a casual vacancy, candidates will be nominated only in respect of the group in which the vacancy has occurred;
(d) no candidate may be nominated for more than one specified group.
6.-(1) In order to be validly nominated to stand as a candidate for election to Pan-African Parliament, a person shall be nominated and supported in writing by not less than ten nominators who are entitled to vote at that election. A nominator may nominate up to four candidates, one for each of the four groups.
(2) The nomination shall be in the prescribed form obtainable from the Returning Officer, and shall contain working experience of the candidate.
(3) The time for receipt by the Returning Officer of nomination forms duly completed by the aspiring Candidates shall expire at four o’clock in the afternoon of the nomination day and soon thereafter, the Returning Officer shall give written notification to all Members of Parliament, of the complete list of the all Candidates who have been validly nominated for the election in respect of each of the four groups.
(4) After being validly nominated, a Candidate may withdraw his candidature by notice in writing signed and delivered by him to the Returning Officer, not later than four o’clock in the afternoon of the day following the nomination day, thereafter, no withdrawals shall be accepted.
(5) Where any Candidate dies at any time after nomination day and before election day, the election process shall continue undisturbed.
(6) After being validly nominated, a Candidate may conduct his or her election campaign.
Nomina- tion of Candi- dates
115
PART IV ELECTION PROCEDURE
7. The Returning Officer shall, by written notice circulated to all Members of Parliament, appoint an election day, which must be a day on which the National Assembly is sitting in ordinary session, and shall be not more than five days after nomination day.
8. The voting process shall be conducted under the general supervision of the Speaker, provided that, if the Speaker himself or herself is a Candidate, he or she shall vacate the chair before the commencement of the election proceedings.
9. Before the voting exercise takes place on election day, each Candidate shall be given an opportunity to appear before the voters assembled in an ordinary sitting of the National Assembly and address them in English for such length of time and answer such number of questions, if any, as may be determined by the Speaker for that purpose.
10. Immediately after address of the candidates, voting shall commence and proceed as follows:-
(a) Only one ballot paper shall be issued to each voter.
(b) The ballot paper shall contain all names of the Candidates arranged in alphabetical order for each of the groups.
(c) Each voter shall be required to cast the exact number of votes equal to the number of persons to be elected in each group. Any ballot paper which will show a greater or smaller number of votes than the specified number will be treated as spoilt and will not be counted.
11.-(1) On receiving a ballot paper each voter shall secretly record his or her five votes by placing a tick in the space provide against the nameof each Candidate, and thereafter shall place the ballot paper in the ballot box.
(2) A voter who has accidentally spoiled his or her ballot paper
Election day
Voting process
Candida- tes to address voters
Casting of votes
Voting procedure
116
while voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paper to Returning Officer and obtain a replacement thereof.
12.-(1) Immediately after all the votes have been placed in the ballot boxes and before the ballot boxes are removed from the Assembly Chamber for counting the votes, the Speaker shall appoint one counting agent for the Candidates in each of the groups.
Provided that, any candidate who wishes to appoint his or her own counting agent may do so by submitting the name of that agent to the Speaker immediately after the appointments by the Speaker have been announced.
(2) The counting of Votes shall be done by such number of Officers of the Assembly as may be appointed by the Returning Officer, and shall be witnessed by the counting agents.
13.-(1) In order to enable the National Assembly to proceed with other business scheduled for that day, the counting of votes shall take place in a room designated by the Speaker for that purpose within the precincts of the Assembly.
14. After the counting of votes is complete and the results ascertained and certified by the Returning Officer and the counting agents, the Returning Officer shall immediately submit the results to the Speaker who shall:-
(a) Report to the Assembly the results of the election together with the number of votes recorded for each candidate in each of the Groups.
(b) Announce to the Assembly the names of five Candidates receiving the highest number of votes in each Group, and shall declare those candidates to have been elected as Members of the Pan- African Parliament.
Appoint- ment of Counting Agents and counting of votes
Decla- ration of elec- tion results
Place for count- ing of votes
117
15.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of all ballot papers and other documents pertaining to the election.
(2) The Returning Officer shall cause all documents to which this rule applies to be destroyed after the expiration of six months from the election day.
PART V MISCELLANEOUS
16. Where anything arises which is not specifically provided for in these Rules, the Speaker shall make a ruling directing what is to be done. In making such a ruling, the Speaker shall be guided by the procedures and practices normally followed in similar situations with regard to Parliamentary elections.
17.-(1) These Rules may be amended at any time by a resolution of the National Assembly on a proposal submitted to it by the Standing Orders Committee.
Custody of ballot papers
Matters not provided for
Amend- ment
118
_____________ NYONGEZA YA SITA _____________
MWONGOZO KUHUSU MASWALI KWA WAZIRI MKUU ______________________________
[Chini ya Kanuni ya 38(1)] ____________
1. (1) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kikishaanza Bungeni, hakitakatishwa wala kusitishwa, isipokuwa kutokana na sababu maalum ya dharura.
(2) Maswali yatakayoulizwa kwa Waziri Mkuu wakati wa Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu yatakuwa ni yale yanayohusu Sera za Serikali au jambo lolote lenye manufaa na maslahi kwa jamii na Taifa lililo chini ya madaraka na mamlaka ya kazi ya Waziri Mkuu.
(3) Maswali kwa Waziri Mkuu yatakuwa ni ya papo kwa papo; yaani yataulizwa bila kutolewa taarifa na yatajibiwa kwa mdomo papo kwa papo.
(4) Waziri Mkuu hatalazimika kujibu swali lolote linalohitaji takwimu au majibu yanayohitaji utafiti.
2. Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya 3(1) ya Mwongozo huu, Wabunge wanaotaka kumuuliza Waziri Mkuu swali wakati wa Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, watawasilisha majina yao kwa Katibu, kabla ya saa 2.30 Asubuhi, siku hiyo ya Maswali kwa Waziri Mkuu.
3. (1) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kinapoanza Bungeni, Spika atamwita Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na kumpa fursa ya kwanza ya kumuuliza Waziri Mkuu swali.
(2) Baada ya kuuliza na kujibiwa swali lake la kwanza, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni anaweza kumuuliza Waziri Mkuu swali moja la ziada la kudai ufafanuzi.
Maelezo ya Jumla
Utaratibu wa kupata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuu Swali
Utaratibu wa kuuliza maswali kwa Waziri Mkuu
119
(3) Mbunge yeyote atakayepata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuu swali na kujibiwa, anaweza kumuuliza Waziri Mkuu swali lingine moja la ufafanuzi.
(4) Endapo orodha ya majina ya wauliza maswali kwa Waziri Mkuu kwa siku hiyo itafikia mwisho lakini muda wa Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu bado haujamalizika, Spika anaweza kutoa fursa kwa Mbunge yeyote ambaye hakupangwa katika orodha hiyo kumuuliza Waziri Mkuu swali.
(5) Mbunge anayetaka kupewa fursa na Spika kwa mujibu wa fasili ya (4), atasimama mahala pake ili Spika amwone na kumwita.
(6) Mbunge yeyote aliyepata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuu swali wakati wa Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, atakuwa na haki pia ya kuuliza swali lake lililowekwa kwenye Orodha ya Shughuli za siku hiyo, wakati wa Kipindi cha Maswali ya Bunge kitakapowadia.
4. Maswali na majibu katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu yawe mafupi.
Maswali na majibu kwa maswali kwa Waziri Mkuu
120
________ NYONGEZA YA SABA ________ MWONGOZO WA UTARATIBU KATIKA KAMATI ZA BUNGE _________
[Chini ya Kanuni ya 114(9) na (10)] _________
1. Mwongozo wa upatikanaji wa habari kutoka kwenye Vikao vya Kamati, ikiwa ni mojawapo ya njia za kukuza demokrasia za uwazi kwa shughuli za Kamati za Bunge na kudumisha mahusiano na wananchi kupitia Vyombo vya Habari utatambua aina ya majukumu ambayo yanatekelezwa na Kamati.
2. Majukumu yatakayofanywa kwa uwazi na ambayo yanaweza kutolewa kwa Waandishi wa Habari bila kuleta athari kwenye maamuzi ya Kamati ni yafuatayo:-
(a) mambo ya kawaida ya kuisimamia na kuishauri Serikali, kama vile kutathmini utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo;
(b) mambo yatolewayo na wadau walioalikwa na Kamati ulingana na utaratibu wa ‘Public Hearing’ uliowekwa na Bunge;
(c) majukumu ambayo yanalenga kuwapatia Wabunge elimu, Semina, Makongomano na ziara za mafunzo;
(d) maelezo yanayotolewa na Serikali kwenye Kamati za Bunge kwa lengo la kuwaelimisha Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati kabla ya kufanya kazi ya uchambuzi wa Hoja au jambo lolote na ambayo Waziri ataona hayatakuwa na athari kwa upande wa Serikali, mfano mmojawapo ukiwa ni pale Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji anapotoa taarifa ya Hali ya Uchumi wa nchi.
Maelezo ya jumla
Majukumu yatakayo- fanywa kwa uwazi
121
3.-(1) Majukumu yatakayofanywa kwa faragha yatahusu mambo yote ambayo habari zake zikitolewa kwa Waandishi wa Habari kabla ya wakati wake yanaweza kuathiri maamuzi ya Kamati na pia kusababisha ukiukwaji wa Kanuni za Bunge ni yafuatayo:-
(a) kazi zote zinazopelekwa kwenye Kamati na Mheshimiwa Spika ili baadaye apelekewe taarifa ya mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Bunge au kuyatolea maamuzi.
(b) shughuli zote za uchambuzi wa Hoja mbalimbali zilizoko mbele ya Kamati.
(c) Shughuli zote zinazofanywa kwa utaratibu wa uchunguzi.
(d) shughuli zote za kiuchunguzi zenye utaratibu uliowekewa masharti zinazofanywa na Kamati.
(e) shughuli zote zinazofanywa na Kamati Ndogo zilizoundwa na Mheshimiwa Spika au Kamati husika ili kufanya kazi maalumu.
(f) Kamati zinapofanya ziara za kiuchunguzi.
(2) Kamati zitakazofanya kazi zake kwa faragha ni Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu ya Serikali za Mitaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
4.-(1) Majukumu yenye uwazi wenye mipaka ni yale yanayotekelezwa na Kamati za kiuchunguzi zifuatazo zenye utaratibu uliowekewa masharti :-
(a) Kamati ya Hesabu za Serikali;
(b) Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa;
(c) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge; na
(d) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Majukumu yatakayo- fanywa kwa faragha
Majukumu yenye uwazi wenye mipaka
122
(2) Mfano wa uwazi wenye mpaka ni ufuatao:- (a) taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inapowasilishwa Bungeni inakuwa wazi kwa Vyombo vya Habari; na
(b) mchakato wa Kamati hizi kuanza kuwahoji Maafisa Masuhuli kuhusiana na taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali utakuwa wazi hadi hatuaambayo Kamati inataka kufanya maamuzi ya kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa na Bunge. Katika hatua hiyo ya kutoa mapendekezo Kamati itafanya kazi zake kwa faragha.
(3) Iwapo mchakato wa kuhoji Maafisa Masuhuli utakuwa ni wa kiuchunguzi, mchakato utafanyika kwa faragha.
(4) Kamati zinapofanya ziara kwa lengo la kujifunza au kujielimisha, shughuli zake zitafanywa kwa uwazi na Wajumbe wa Kamati watakuwa na uhuru wa kutoa maoni yao ya jumla kwenye vyombo vya habari.
(5) Maoni ya Kamati yatakuwa ni yale ambayo hayaathiri maamuzi yatakayotolewa kwa faragha na Kamati baada ya ziara yake.
(6) Waandishi wa Habari katika kutoa taarifa za namna hii waeleze wazi kwamba, maoni hayo ni ya Mbunge binafsi na siyo ya Bunge wala Kamati ya Bunge au Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
5.-(1) Kwa kuwa Mawaziri wanapokutana na Kamati kwenye Vikao vilivyopangwa wanakuwa Wajumbe, na kwa kuwa inapotokea wamekutana na Waandishi wa Habari mara baada ya Kikao kuzungumzia suala lolote lililojadiliwa kwenye Kamati; Mwenyekiti wa Kamati au Mwakilishi wake au Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni watakuwa huru kulitolea maoni jambo hilo, ili mradi maelezo yao hayatahusu maamuzi yaliyotolewa na Kamati ambayo yanatakiwa kuwasilishwa Bungeni.
(2) Wenyeviti wa Kamati zote wataandaliwa utaratibu wa kawaida wa kukutana na Waandishi wa Habari kuzungumzia shughuli itakayofanywa au iliyofanywa na Kamati na maelezo hayo yanayotolewa kwenye Vyombo vya Habari, kwa namna yoyote, yasiwe ni mapendekezo ambayo Kamati imeazimia kuyawasilisha Bungeni na ambayo yanaweza kuathiri maamuzi hayo.
Mawaziri wanapo- toa taarifa kwa waandishi wa habari baada ya kukutana na kamati
123
(3) Kama kuna jambo ambalo lina maslahi kwa umma na wananchi wanataka maelezo, Mwenyekiti wa Kamati au Mwakilishi wake atakuwa na uhuru wa kulitolea maelezo ya jumla ili mradi maelezo hayo hayatahusiana na maamuzi ya Kamati ambayo yanatakiwa kuwasilishwa Bungeni.
124
_______
NYONGEZA YA NANE ________
KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE
[Chini ya Kanuni ya 115]
SEHEMU YA KWANZA KAMATI ZA KUDUMU ZISIZO ZA SEKTA
1.- Kamati za Kudumu zisizo za Sekta zitakuwa zifuatazo:-
(a) Kamati ya Uongozi; (b) Kamati ya Kanuni za Bunge; (c) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge; (d) Kamati ya Sheria Ndogo; na (e) Kamati ya Masuala ya Ukimwi;
2.-(1) Kamati ya Uongozi itakuwa na Wajumbe wafuatao:-
(a) Spika, ambaye atakuwa Mwenyekiti; (b) Naibu Spika; (c) Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni au Mwakilishi wake; (d) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni au Mwakilishi wake; (e) Wenyeviti wa Kamati za Kudumu au Makamu wao; (f) Mwanasheria Mkuu wa Serikali;
(2) Katibu atakuwa Katibu wa Kamati.
(3) Majukumu ya Kamati ya Uongozi yatakuwa ni:-
(a) kujadili na kumshauri Spika kuhusu mambo yote yanayohusu Shughuli za Bunge kwa jumla, ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu utakaorahisisha maendeleo ya Shughuli za Bunge au za Kamati yoyote.
Kamati za Kudumu zisizo za Sekta
Muundo na majuku- mu ya Kamati ya Uongozi
125
(b) kupokea hoja zenye maslahi kwa Taifa zinazojitokeza kwenye Kamati za Bunge za kisekta wakati wa kupitia bajeti za Wizara na kuishauri Serikali kuhusu hatua muafaka za kuchukua kabla ya Hotuba ya Bajeti kusomwa Bungeni.
(4) Katika kutekeleza kazi zilizotajwa katika fasili ya 3 ya Kanuni hii, Kamati ya Uongozi itakuwa na uwezo wa kuweka muda ambao shughuli yoyote iliyopelekwa katika Kamati inayohusika sharti ikamilike, na iwapo shughuli iliyopelekwa imewekewa muda kama huo, basi baada ya kwisha muda huo au baada ya kwisha muda wowote ulioongezwa, Kamati inayohusika itahesabiwa kuwa imemaliza shughuli hiyo na shughuli hiyo itaendelea kwenye hatua nyingine kana kwamba Mwenyekiti wa Kamati hiyo amemuarifu Spika kumalizika kwa shughuli hiyo.
3.- (1) Kamati ya Kanuni za Bunge itakuwa na Wajumbe wafuatao:-
(a) Wajumbe watakaoteuliwa na Spika;
(b) Kiongozi wa Upinzani au Mwakilishi wake; na
(c) Mwanasheria Mkuu wa Serikali au Mwakilishi wake.
(2) Spika atakuwa Mwenyekiti na Naibu Spika atakuwa Makamu Mwenyekiti.
(3) Majukumu ya Kamati ya Kanuni za Bunge yatakuwa ni:-
(a) kujadili na kutoa mapendekezo juu ya kufanya mabadiliko katika Kanuni za Bunge;
(b) kuchunguza na kutoa taarifa juu ya pendekezo lolote linalohusu Kanuni za Kudumu za Bunge ambalo limepelekwa kwa Kamati hiyo na Spika au na Mbunge yeyote;
(c) kuchunguza na kutoa taarifa juu ya malalamiko yote kuhusu uamuzi wa Spika ambayo yamepelekwa mbele ya Kamati na Mbunge yeyote.
(d) kuzifanyia marekebisho au mabadiliko Nyongeza za Kanuni hizi.
Muundo na majukumu ya Kamati ya Kanuni za Bunge
126
(4) Akidi ya mikutano ya Kamati ya Kanuni za Bunge itakuwa ni Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti pamoja na nusu ya Wajumbe wengine.
4.-(1) Majukumu ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge yatakuwa:-
(a) kuchunguza masuala yote yahusuyo haki, kinga na madaraka ya Bunge yanayopelekwa kwake na Spika;
(b) kushughulikia mambo yanayohusu maadili ya Wabunge; na
(c) kujadili jambo lingine lolote litakalopelekwa kwake na Spika.
5. Kamati ya Sheria ndogo itakuwa na majukumu ya kuchambua Sheria Ndogo ili kujiridhisha iwapo zimekidhi matakwa na masharti ya Katiba, Sheria Mama na Sheria nyingine za nchi.
6. Kamati ya Masuala ya UKIMWI itatekeleza majukumu yafuatayo:-
(a) kuratibu masuala yanayohusu UKIMWI katika taasisi ya Bunge;
(b) kufuatilia utekelezaji wa Sera na mipango ya Serikali kuhusu UKIMWI;
(c) kujadili na kutoa mapendekezo na ushauri juu ya Sera na mipango ya Serikali kuhusu UKIMWI.
SEHEMU YA PILI
KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZA SEKTA
7.-(1) Kamati za Kudumu za Bunge za sekta zitakuwa zifuatazo:-
(a) Kamati ya Fedha na Uchumi; (b) Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala;
Majukumu ya Kamati ya Sheria Ndogo
Majukumu ya Kamati ya masuala ya UKIMWI
Kamati za Kudumu za Sekta
Majukumu ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge
127
(c) Kamati ya Viwanda na Biashara; (d) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama; (e) Kamati ya Huduma za Jamii; (f) Kamati ya Maendeleo ya Jamii; (g) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira; (h) Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji; (i) Kamati ya Miundombinu; na (j) Kamati ya Nishati na Madini.
8.-(1) Kamati ya Fedha na Uchumi itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Wizara ya Fedha na Uchumi.
(2) Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Ofisi ya Rais:
(i) Utawala Bora; (ii) Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
(b) Ofisi ya Makamu wa Rais: Muungano.
(c) Ofisi ya Waziri Mkuu:
(i) Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI); (ii) Sera na Uratibu.
(d) Wizara ya Katiba na Sheria.
(3) Kamati ya Viwanda na Biashara itasimamia shughuli za Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko.
(4) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa;
(b) Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki;
(c) Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; na
Kamati na shughuli za Wizara
128
(d) Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
(5) Kamati ya Huduma za Jamii itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii;
(b) Wizara ya Mawasiliano, Sayansi naTeknolojia; na
(c) Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
(6) Kamati ya Maendeleo ya Jamii itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto;
(b) Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo; na
(c) Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
(7) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi;
(b) Wizara ya Maliasili na Utalii; na
(c) Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira).
(8) Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji itasimamia shughuli za Wizara zifuatazo:-
(a) Wizara ya Maji na Umwagiliaji;
(b) Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika; na
(c) Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.
(9) Kamati ya Miundombinu itasimamia shughuli za Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu.
(10) Kamati ya Nishati na Madini itasimamia shughuli za Wizara ya Nishati na Madini.
129
9.-(1) Majukumu ya Kamati ya Kudumu ya sekta yatakuwa yafuatayo:-
(a) kushughulikia bajeti ya Wizara inazozisimamia;
(b) kushughulikia Miswada ya Sheria na Mikataba inayopendekezwa kuridhiwa na Bunge iliyo chini ya Wizara inazozisimamia;
(c) kushughulikia Taarifa za kila mwaka za utendaji za Wizara hizo;
(d) kufuatilia utekelezaji unaofanywa na Wizara hizo kwa mujibu wa Ibara ya 65(3) (b) ya Katiba.
(2) Bila ya kuathiri majukumu ya jumla ya Kamati za sekta kama yalivyoainishwa katika fasili ya (1) ya Kanuni hii, Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama itatekeleza pia majukumu yafuatayo:-
(a) kuimarisha ushirikiano na Mabunge ya nchi nyingine;
(b) kushughulikia taarifa za wawakilishi katika Bunge la Afrika Mashariki, SADC na Bunge la Afrika.
SEHEMU YA TATU KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZINAZOSIMAMIA FEDHA ZA UMMA
10.-(1) Kamati za Kudumu za Bunge zinazosimamia fedha za Umma zitakuwa zifuatazo:-
(a) Kamati ya Hesabu za Serikali.
(b) Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa.
(c) Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
11.- Majukumu ya Kamati za Hesabu za Serikali yatakuwa yafuatayo:-
(a) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Umma katika
Kamati za Kudumu za Bunge zinazo- simamia Fedha za Umma
Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali
Majukumu ya Kamati
130
Wizara za Serikali yaliyoainishwa katika taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali;
(b) kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo yaliyokwishatolewa na Kamati hiyo yenye lengo la kuondoa matatizo hayo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Umma katika Wizara za Serikali; na
(c) kutoa mapendekezo na ushauri kwa Wizara za Serikali kuhusu matumizi mazuri ya fedha za Umma.
12.- Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa yatakuwa kama ifuatavyo:-
(a) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Serikali za Mitaa yaliyoainishwa katika Taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali;
(b) kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo yaliyokwishatolewa na Kamati hiyo ili kuondoa matatizo hayo;
(c) kutoa mapendekezo na ushauri kwa Serikali za Mitaa kuhusu matumizi mazuri ya fedha ili kuhakikisha kwamba tatizo la matumizi mabaya ya fedha linapungua katika Serikali za Mitaa.
13. Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma yatakuwa kama ifuatavyo:-
(a) kushughulikia taarifa za kila mwaka za hesabu zilizokaguliwa za Mashirika ya Umma;
(b) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Mashirika ya Umma yaliyoainishwa katika taarifa za kila mwaka za hesabu zilizokaguliwa za Mashirika hayo na kutoa mapendekezo na ushauri wa namna ya kuyaondoa matatizo hayo.
Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa
Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma
131
(c) kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo yaliyokwishatolewa na Kamati hiyo ili kuondoa matatizo hayo.
(d) kutathmini ufanisi wa Mashirika ya Umma.
(e) kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma.
Zimepitishwa kwa mujibu wa Azimio la Bunge tarehe 15 Novemba, 2007.
Dodoma DAMIAN S. L. FOKA Katibu wa Bunge
 
Hongera kwa kazi nzuri. KAMA iko katika softi kopi ungeupload uzi ili iwe na mpangilio na isomeke vizuri. Big up
 
Tunashukuru ndugu kwa kutuletea kanuni hizi ili tuzifahamu kwa undani zaidi.

Hata hivyo, kwa mbunge ambae ni mvivu wa kusoma hawezi kuelewa vizuri kanuni hizi kwani zinahitaji ufanye kazi ya ziada kuzisoma na kuzielewa.
 
unakubaliana na ulipanaji wa posho sio?
Wabunge hawalitumikii bunge, wanawatumikia wapigakura wao, hivyo basi wasilipwe na ofisi za bunge bali walipwe na waajiri wao kupitia halmashauri zao na mishahara yao ipitishwe na madiwani, iandaliwe kwa mapendekezo ya wapigakura na kujadiliwa na wataalam katika mjadala huru, wabunge waruhusiwe kufanya kazi zao za kitaalamu na kupokea mshahara huko.

Wabunge wawajibike kwa wapiga kura wao moja kwa moja na si kwa chama wala bunge!

Mkuu nakubaliana na wewe, sisi wa chini tunaona wenyewe hawaoni kweli tz tuna maDr na Profs ovyoo kabisaa
 
Back
Top Bottom