Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Tatizo langu juu ya hizi kanuni za bunge ni kwamba katiba ya Jamhuri ya Tanzania inampa mbunge mmoja mmoja uwanja mpana wa kuisimamia serikali iliyoko madarakani; uwanja huo mpana anaopewa mbunge chini ya katiba, unaminywa na kanuni za bunge zilizotungwa na bunge lenyewe. Jambo linalonitatiza ni je inakuwaje kanuni hizo zinachukuliwa kuwa juu ya katiba? Kwangu mimi, kanuni yeyote ambayo mahudhui yake yanapingana na mahudhui ya katiba, ni batili. Kwa mantiki hiyo madaraka makubwa aliyopewa spika ya kuminya mijadala hapo bungeni ni kinyume na sheria