Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Pole, lakini lazima NIKUAMBIE UKWELII.

Hiyo unayoiita TIBA MBADALA ndio TIBA HALISI, Mimea ya asili yenye nguvu ya kukuponya na kuhuisha mwili dhidi ya maradhi ya aina yoyote.

Hayo MAKEMIKALI ndio yalipaswa kuwa TIBA MBADALA. Ukishafeli kutumia MIMEA SAFI (kitu ambacho hakiwezekani) sasa ndio ukajijaze MAKEMIKALI MACHAFU na MIONZI.

Mkiambiwa MNABEZA, ooohh MIMEA NI UCHAWI! Haya sasa!!!!! Umerudi kule kule!!!

Oooohh, wewe hujui sayansi, wewe mchawiii!! Sayansi yenyewe ndio hiyo, umelipa MAMILIONI ukajazwa MIONZI LUKUKI mpaka mwili ukaharibika zaidi na zaidi.

Najua kuna MAKANJANJA watanivamia hapa, lakini sijali. MIMI NAPASUA UKWELI TU, tukana, bwata, lakini HABARI IMEFIKA.
mimi naomba dawa ya kunitibia na Allergy maana nateseka
 
Aisee mkuu pole,,familia yetu tumewahi oata wagonjwa wawili wa saratani ya shingo ya kizazi. Wa kwanza ni dada yangu ila alifariki na wa pili akawa mtoto wake ajabu dogo alipata saratani akiwa darasa la 7 kwakweli kuuguza mgonjwa wa saratani ni gharama mno ila Mungu amejaalia yule dogo amepon na anaendelea na masomo yake.

M/Mungu akutie nguvu katika nyakati hizi ngumu.
 
HAIJAWA BAHATI KWANGU, SARATANI IMESHINDA VITA YA KUPIGANIA UHAI NA MKE WANGU
Pole sana jamani 😭😭😭😭. Amevipiga vita, mwendo ameumaliza, apumzike kwa amani, Amina. Ndio naona leo nimesikitika sana
 
Moderator mngemsaidia kupandisha juu ile post ya mleta uzi aliyosema kuwa huyo mke wake alishafariki dunia ili kwa msomaji mpya aelewe na hii itasaidia kuondoa mkanganyiko.

Kwani kuna wengine wanatoa pole na wengine wanamtakia mke uponyaji mwema wakati huyo mke mwenyewe hata hayupo tena duniani.
 
Back
Top Bottom