omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 145
Date::11/21/2008
Kampeni chafu zaanza UVCCM
Exuper Kachenje
Mwananchi
KAMPENI chafu na za kupakana matope zimezuka miongoni mwa makundi ya wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM imebainika.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi inazo, wagombea hao kwa upande mmoja, wamekuwa wakiendesha kampeni chafu za chuki na kupakana matope kwa misingi ya rangi.
Habari za uhakika zilizoifikia Mwananchi zinaeleza kuwa, kumezuka kundi ambalo kwa makusudi linaendesha kampeni za kumpaka matope mmoja wa wa wagombea wa nafasi hiyo kwa kusambaza ujumbe mchafu kumhusu yeye kwa njia ya simu selula na kueleza kuwa UVCCM, ipo hatarini kutekwa na maharamia.
"Wanafanya hivyo kwa kasi chini ya ufadhili wa mgombea mwinigine wa nafasi hiyo ya juu ya uongozi katika UVCCM," kilieleza chanzo cha habari hizi
Habari zaidi zinabainisha kuwa, anayekusudiwa kupakwa matope na kuchafuliwa ni Hussein Bashe, mgombea mwenye asili ya kisomali ambaye Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ilipitisha jina lake kugombea nafasi hiyo.
Sehemu ya ujumbe huo ulisomeka: " Kama meli za mfuta zinavyotekwa na maharamia ya kisomali vivyo hivyo wana CCM tuwe macho, kwani UVCCM iko hatarini kutekwa na maharamia hao wa kisiasa toka ughaibuni. Shime Watanzania wenzangu tuamke tusikubali kuongozwa na ma-tx."
Akizungumzia tukio hilo, Hussein Bashe alisema kuwa wanaosambaza ujumbe huo wamefilisika kisiasa na kwamba badala ya kupoteza muda kwa kupakana matope waeleze wataisaidia nini UVCCM.
"Wanaosambaza ujumbe huo wamefilisika kisiasa, waeleze wataisaidia nini jumuia. Hata mwalimu Nyerere aliwahi kusema: watu waliofilisika kisiasa hukimbilia mambo madogo madogo yasiyo na msingi," alisema Bashe.
Well, ingawa nachukia sana siasa hizi za kikaburu lakini ni muhimu wasomaji wakajua kuwa Hussein Bashe alikuwa na bado mpambe mzuri sana wa ROSTAM AZIZI ambaye alikuwa bosi wake wakati Hussein akifanya kazi katika kampuni ya Mwananchi Communications inayomiliki gazeti hili liloandika hii habari.
Hussein Bashe mwenye ufadhili mkubwa wa ROSTAM na anayetokea mkoa wa TABORA alihusika kwa namna fulani katika kufanikisha zile siasa chafu za kibaguzi dhidi ya Dr Salim Ahmed SALIM.
Wanasema...........
Tanzanianjema