Kampeni chafu zaanza UVCCM

Maneno umesema mengi sana lakini hayana uhusiano wowote na CCM kupokea msaada wa mwananchi, semeni labda tatizo ni kwa sababu ni Mhindi, dataz nilizonazo ni kwamba CCM enzi hizo ilikuwa haina bajeti wala responsibility, ilikuwa inachota tu serikalini bila idhini yetu wananchi, Mwalimu alikuwa na mazuri na mapungufu pia, lakini no way ninataka kurudi kwenye maisha yake tena yale ya foleni za unga wa njano no thank you!

Mhindi ni mwananchi ametoa mchango wake kwa chama cha siasa, kama kuna sheria inakataza isemwe, kama mhindi ni mwizi isemwe wizi wake, tule naye sahani moja, hisia haziwezi kuwa sheria ni just hisia tu!

Tunaelewa kwamba CCM ina ubovu, so is vyama vyote vya siasa, lakini tuwe na sababu ya kumshambulia mwananchi anayetoa msaada kwa taifa.



Mheshimiwa FM ES nakataa mpaka kifo kuwa Wahindi wahindi ni Watanzania. Wanatudanganya kujiita Mtanzania ili aweze ku enjoy ku exploit Danganyika. Nimefanikiwa kuwa karibu na wahindi fulani na inapotokea wanasafiri nje ya Tanzania huwa hawajitambulishi kuwa ni watanzania.Utasikia "I am an Indian but my businesses are in Tanzania. You know the place is attractive to invest, the gays there are easy to handle!!!!! If at all you can win the support of the rulling party then you are assured of the ........". Hata wale watoto wao wanaozaliwa hapa hawajiiti watanzania. But inapokuja issue ya biashara hapa wanajiita watanzania na wanakuja na vijisent vyao kuipa ccm. Mbona sijasikia kuwa wamechangia kujenga shule na mahospitali? Za shule wanapeleka Aghakan Foundation na kuchangia massively kuendeleza hospital zao ambazo user fees zao ni za matajiri tu. Je bibi yangu kule kijijini anafaidika vipi na hilo?

Halafu kuna mabasi yao kabisa ya shule yameandikwa INDIAN SCHOOL????

Mheshimiwa FM ES hata kama leo utafanikiwa kwenda India au mjukuu wako azaliwe India hawezi kutambulika kwa lolote. Pengine atakuwa na uraia tu kama kwa India issue ya kuzaliwa kwao unapata uraia but hataweza kupata even kazi ya maana India!!!!!!!!!! Sembuse ardhi na biashara kubwakubwa??????

Hizo pesa alizochagia CCM si za Mtanzania wa kawaida kama mimi na wengine. Ana print materials na ni sawa zinarudi kwake. Hizo alizotoa kama allowances is not meaningful kwa uchumi anyway, wanachama wataimalizia hukohuko Dodoma. Let me ask you a simple question? Will that money directly bring the impact to our economy??? That is hugely on Consumption!!!!! Angepeleka kwenye investment whether social or economic ningempa big up!!!!!!

Wahindi hawataki tuamke kichumi kwa kuwa wanjua tutawaangusha na ndiyo maana wengi wao wanapigana kufa kuhakikisha wafanyabiashara wazalendo hawaendelei. At the same time, serikali haiwapi kipaumbele wafanyabiashara wetu. Wewe utasikia tu Somaiya amepata tax incentive in one form lakini si kwa mzalendo. No free lunches!!!!! RA alikuwa anachanga vilivyo ila tu kwenye kodi anapata exemption ya bilions wakati amechanga tu millions???

Haya mambo hayaniingi akilini kwa mtu kutetea wahindi unless naye ana uhindi au ka affilition fulani na wahindi au pia niseme ni kada wa ssm maana wanaabudu wahindi kuliko miungu yao wenyewe.
 
Some of us will soon be proved right. unahitaji moyo wa paka kutetea mambo mengine. Hata hivyo kinachogomba hapa nafikiri ni nani anapokea zaidi kuliko anayetoa huo msaada. Angekuwa anapokea dagaa tu duh JF hapangetosha lakini anayepokea, loh.... funika kombe. JF inapoteza hadhi, koleo haliitwi tena koleo, na nyani anaangaliwa kwanza sura lakini thubutu utamke hivyo. Hivi akina Lowassa, Mkono na hata Mkapa wameshitakiwa ? ..ama kweli, wanavyovaliwa njuga humu JF !!! Kichwa kimenasa, juhudi za kuokoa zapamba moto.... kulikoni ? Sasa ni wakati mwafaka wa kutamka wazi kuwa CCM imeoza, full stop.

CCM wameoza na wameoza big time.They need some reformation or otherwise they are done.
 
Wakuu wote mliochangia hapo juu heshima mbele, naomba kukubali kutokubaliana, mnazo hoja zntio sana lakini hakuna inayomfunga huyu mwananchi mwenzetu Mhindi aliyetoa msaada kwa CCM.

Kwamba ninatetea wahindi hapana, sitetei a proven fisadi hata siku moja ila sichukiii wananchi wengine bila sababu eti kwa kuwa ni wahindi tu, hapana hayo Obama ameyamaliza tayari.

Mkuu Wild Card,

Mwalimu was the greatest aver hilo ninaamini kwa 100%, lakini policies zake nilikuwa sikubaliani nazo, ndio maana nikaamua kwenda kupanda meli mapema sana.

Otherwise wakulu wote nimewasikia sana, nilitaka tu kujua huko the otherside kuna nini, yaani what are the arguments kuacha tu hizo name calling wengi mna hoja nzito ingawa nyingi hazina uhusiano wowote na hii ishu, lakini some of them ni worthy ku-take a note.

Respect kwa wote mliochangia.
 
10.11.2008 @21:21 EAT

Trader's Sh400m donation to CCM attracts mixed feelings
By Orton Kiishweko
THE CITIZEN

Opposition politicians and various activists yesterday received with mixed feelings reports that a local businessman had donated Sh400 million to the ruling CCM.

Some saw it as backtracking by CCM on its promise to draw a line between politics and business.

Mr Tanil Somaiya gave the donation in Dodoma on Sunday to facilitate the ruling party's youth wing's elections slated for next month.

Mr Somaiya said he saw it fit to help the CCM youth wing, UVCCM, because he was a staunch supporter of the ruling party.

CCM national chairman President Jakaya Kikwete said the businessman had advertised his business through the donation.

But some opposition politicians and activists criticised the party for accepting the donation, which they viewed as an unacceptably "huge favour" from a single individual.

They recommended that Parliament agitates for the formulation of a law to regulate the funding of political parties.

Some of the existing laws, specifically the Political Parties Act, outline regulations governing private contributions to political parties. The regulations places limits on individual donations to candidates and political parties.

But according to Section 13 of the law, political parties have to declare only contributions coming from outside Tanzania or from non-Tanzanians and organisations based in the country.

The secretary-general of the opposition Chadema, Dr Wilibrod Slaa, said he was surprised that CCM, which had been calling for a law to guard against the influence of money in local politics, had made a swift about-turn in the "hour of need".

CCM has formed a four-member committee led by Dodoma Regional Commissioner William Lukuvi to raise funds ahead of the UVCCM elections.

But Dr Slaa said some wealthy businessmen could use such opportunities to gain favours,particularly when things were not going their way.

He also called for a system to control political party funding that would set limits to how much an individual could donate to a party.

Dr Slaa proposed limits to campaign expenditure, disclosure of donations that were over a certain "acceptable" sum and parties being obliged to publish their accounts.

Whereas some analysts saw it as being transparent since the ruling party had gone public about the donation as the law requires, Dr Slaa said a more pressing issue was the likelihood of compromise in case wealthy individuals flexed their financial muscle by giving "huge" donations to political parties.

He said he was sceptical as to whether a statute which drew a clear line between business and politics would ever be passed and enacted.

However, the outgoing UVCCM chairman, Dr Emmanuel Nchimbi, disputed this in an interview with The Citizen, saying accepting donations from private individuals could not compromise CCM.

"In all fairness, this is a youth wing project which we need money to implement, but this is not to say that the party will be open to manipulation if it accepts donations," he said, adding that UVCCM was an established political institution.

Civic United Front (CUF) head of Foreign Affairs and International Relations Ismail Jussa told The Citizen that he had no qualms about the ruling party accepting such donations.

"As far as I am concerned, there is nothing wrong provided they followed all the required procedures," he said.

He, however, said it was important that the President fulfilled his promise of introducing a law on the funding of political parties "so that no individual will hold any political party to ransom".

Dar es Salaam University don Sengondo Mvungi said in the sum donated by an individual was not important, adding that of concern was the likelihood of wealthy individuals holding the country hostage in the future.
 
The secretary-general of the opposition Chadema, Dr Wilibrod Slaa, said he was surprised that CCM, which had been calling for a law to guard against the influence of money in local politics, had made a swift about-turn in the "hour of need".
Jamaa kwa kulia lia...Mmhm!



Civic United Front (CUF) head of Foreign Affairs and International Relations Ismail Jussa told The Citizen that he had no qualms about the ruling party accepting such donations.

"As far as I am concerned, there is nothing wrong provided they followed all the required procedures," he said.

He, however, said it was important that the President fulfilled his promise of introducing a law on the funding of political parties "so that no individual will hold any political party to ransom".

^^Wenye ufahamu wa mambo
 
Jamaa kwa kulia lia...Mmhm!


^^Wenye ufahamu wa mambo

Huo si ufahamu wa mambo bali ni kutojua kuchambua mambo kwa kina. Leo Somaiya kaipa CCM shilingi millioni 400 ili kukisaidia chama hicho katika uchaguzi wa tawi la vijana. Sidhani kama uchaguzi huo utagharimu pesa nyngi kiasi hicho. Kesho Manji naye anatoa milioni 400 ili zisaidie uchaguzi wa UWT na kesho kutwa Subhash Patel anatoa milioni 400 ili zisaidie uchaguzi wa jumuiya ya Wazazi. Hizi ni pesa nyingi sana na tayari zinaipa advantage kubwa sana CCM ukilinganisha na vyama vingine visivyokuwa madarakani.

Kwa maoni yangu kuwe na limit ya shilingi million 5 tu ambayo itatolewa katika kipindi cha kila miaka miwili na mchangiaji mmoja na pia chama kinachopokea mchango huo kitozwe kodi inayostahili kwa kiasi hicho ilichopokea. Hii itasababisha kupunguza matajiri wawe wa halali ama wa haramu kuipa advantage kubwa sana CCM katika chaguzi zetu maana sidhani kama uchaguzi wowote ule wa moja ya jumuiya za CCM unahitaji shilingi milioni 400 ili kugharamia uchaguzi huo.
 
Thank you Kevo. Ni aibu tupu lakini wengine wanataka kuhalalisha matajiri kupitia ufisadi kutoa michango mikubwa namna hii kwa CCM. Halafu tukisema CCM ni chama cha mafisadi wanakuja juu. Huyo Somaiya alikuwa ni mmoja wa watu wa karibu katika mkataba wa kununua rada ambayo baadaye mkataba huo ulionekana umejaa rushwa tupu na uchunguzi wake bado unaendelea.

Wakati serikali na CCM vimegubikwa na habari za ufisadi wa hali ya juu kupitia EPA, Richmond, ununuzi wa Rada, ununuzi wa ndege ya Rais, magari ya jeshi na helicopters za jeshi na jengo la UVCCM itakuwa ni utaahira kulifumbia macho hili la tajiri anayehusika kwa karibu na tuhuma dhidi ya rushwa katika ununuzi wa rada kutoa pesa nyingi kiasi hicho kwa chama ambacho kuna ushahidi wa kutosha kwamba viongozi wake wa juu wanahusika na ufisadi.

Huu msaada umetolewa na mtuhumiwa katika ununuzi wa rada na kupewa CCM ambayo kuna ushahidi wa kutosha kwamba ilihusika na wizi wa mabilioni ya BOT kupitia Tangold, Meremeta, Deepgreen na ili kuficha ushahidi dhidi ya wizi huo wanathubutu kusema kwamba hilo linahusu usalama wa Taifa!!!! Hili la kupokea pesa hizo linathibitisha kwa mara nyingine tena kwamba CCM ni chama cha mafisadi.

Kuhisiwa pekee yake kwa tuhuma nzito za Radar kunatosha kabisa kuifanya CCM ikatae 'msaada' wake. Na wangekuwa makini huyu angekuwa anachunguzwa alihusika vipi na kashfa ya Rada, lakini bado anapeta tu mtaani!!!!

Hili siyo swala la ubaguzi kwamba tunamjadili huyu kwa kuwa ni mhindi, bali tunamjadili huyo kwa kuwa ana tuhuma nzito dhidhi yake katika ufisadi wa ununuzi wa Rada. Huku ni kukumbatia mafisadi na ndiyo maana ufisadi utaendelea kushamiri Tanzania. Usilifananishe hili na ubaguzi hata kidogo. Utajiri wanaoupata kwa kupitia njia za haramu si utajiri unaostahili kupigiwa makofi hata siku moja.

Huo si ufahamu wa mambo bali ni kutojua kuchambua mambo kwa kina. Leo Somaiya kaipa CCM shilingi millioni 400 ili kukisaidia chama hicho katika uchaguzi wa tawi la vijana. Sidhani kama uchaguzi huo utagharimu pesa nyngi kiasi hicho. Kesho Manji naye anatoa milioni 400 ili zisaidie uchaguzi wa UWT na kesho kutwa Subhash Patel anatoa milioni 400 ili zisaidie uchaguzi wa jumuiya ya Wazazi. Hizi ni pesa nyingi sana na tayari zinaipa advantage kubwa sana CCM ukilinganisha na vyama vingine visivyokuwa madarakani.

Kwa maoni yangu kuwe na limit ya shilingi million 5 tu ambayo itatolewa katika kipindi cha kila miaka miwili na mchangiaji mmoja na pia chama kinachopokea mchango huo kitozwe kodi inayostahili kwa kiasi hicho ilichopokea. Hii itasababisha kupunguza matajiri wawe wa halali ama wa haramu kuipa advantage kubwa sana CCM katika chaguzi zetu maana sidhani kama uchaguzi wowote ule wa moja ya jumuiya za CCM unahitaji shilingi milioni 400 ili kugharamia uchaguzi huo.

Vizuri sana, naona sasa unarudi kinyume, ama umeshafahamu kuwa mchango wa Somaiya katika umoja wa vijana hauna tatizo kisheria. Aidha hofu yako ni juu ya matajiri wengine kuchangia CCM pekee na sio kwa vyama vingine.

Hilo lisikupe shaka, kwani nimesoma sehemu kuwa Chadema tayali wameshaanza kupokea matajiri waliokuwa wakiichangia CCM. Cha msingi ni kwa matajiri hao kuendelea kuchangia Chadema pasipo kuogopa.

Aidha suala la kiwango cha uchangiaji katika jumuiya za chama linazungumzika, kama lile la kuchangia kampeni wakati wa chaguzi. Kwa sasa ni heri kuwa umefahamu nini kinaendelea.
 
Vizuri sana, naona sasa unarudi kinyume, ama umeshafahamu kuwa mchango wa Somaiya katika umoja wa vijana hauna tatizo kisheria. Aidha hofu yako ni juu ya matajiri wengine kuchangia CCM pekee na sio kwa vyama vingine.

Hilo lisikupe shaka, kwani nimesoma sehemu kuwa Chadema tayali wameshaanza kupokea matajiri waliokuwa wakiichangia CCM. Cha msingi ni kwa matajiri hao kuendelea kuchangia Chadema pasipo kuogopa.

Aidha suala la kiwango cha uchangiaji katika jumuiya za chama linazungumzika, kama lile la kuchangia kampeni wakati wa chaguzi. Kwa sasa ni heri kuwa umefahamu nini kinaendelea.

Fumbua macho kaka!!! Hivi unaamini kweli uchaguzi wa Vijana CCM unahitaji shilingi milioni 400 ili kugharimia uchaguzi huo!!!!? Kwa gharama zipi hasa na mahesabu hayo yalifanywa na nani ili kuthibitisha uchaguzi huo unahitaji shilingi milioni 400? :confused:

Kama uchaguzi huo unahitaji kwa mfano shilingi 50 millioni pesa zinazobaki unadhani zitaacha kukombwa na CCM ili kuwapa advantage CCM katika chaguzi zijazo!?

Hao matajiri wa CHADEMA waliotoka CCM wameichangia CHADEMA kiasi gani!? Unasema mchango wa Somaiya kwa umoja wa Vijana hauna tatizo kisheria, kwa sheria zipi unazozizungumzia!!? Sheria hizo zilitungwa lini na nani? :confused:

Aliyekwambia nimefahamu kinachoendelea nani!!!? :confused: usinibambikie maneno ambayo sijayasema.

Mimi naamini kabisa hizi pesa za matajiri ndani ya vyama na jumuiya za vyama inabidi zithibitiwe ili kuhakikisha vyama vyote vinakuwa na nafasi sawa ya kushinda katika chaguzi hizo. Ikitokea mafisadi 4 matajiri wote wakichangia CCM shilingi milioni 400 kila mmoja basi CCM itakuwa na advantage kubwa sana ukilinganisha na vyama vingine.

Transparent ndani ya vyama vya siasa kwa sasa hakuna kabisa hivyo ili kuhakikisha wanasiasa hawanunuliwi na matajiri ili wafanyiwe favours mbali mbali inabidi 'misaada' ithibitiwe barabara.
 
Vizuri sana, naona sasa unarudi kinyume, ama umeshafahamu kuwa mchango wa Somaiya katika umoja wa vijana hauna tatizo kisheria. Aidha hofu yako ni juu ya matajiri wengine kuchangia CCM pekee na sio kwa vyama vingine.

Hilo lisikupe shaka, kwani nimesoma sehemu kuwa Chadema tayali wameshaanza kupokea matajiri waliokuwa wakiichangia CCM. Cha msingi ni kwa matajiri hao kuendelea kuchangia Chadema pasipo kuogopa.

Aidha suala la kiwango cha uchangiaji katika jumuiya za chama linazungumzika, kama lile la kuchangia kampeni wakati wa chaguzi. Kwa sasa ni heri kuwa umefahamu nini kinaendelea.


Kwa mwendo huu hatutaacha kuona kila Rais toka CCM akija na wazo la kuomba omba kwa matajiri kuendesha Nchi maana ndiyo kikomo cha uelewa wao hawa watu .Maana jadi ama sili ya hawa jamaa ndiyo hiyo .Kuanzia Vijana wanao tegemewa na CCM kesho kuwa viongozi wakubwa wote ni omba omba ndiyo maana JK haishi nje ya Nchi kwa jina la kuomba omba maana hana akili ya kuendesha Nchi bila ya kuomba omba .

Hao walio ingia Chadema hawajaenda kuchangia bali wamesema wameamua sasa kujiunga na na upande mwingine wanao uamini kwamba waweza kuwa mbadala wa CCM na si kwamba ni matajiri wa kuchangisha mapesa kama ilivyo CCM .So tofautisha haya mambo .
 
Kwani Jeetu alichanga kiasi gani wakati wa kampeni za CCM/JK 2005? Sasa hivi yuko wapi? JK ni zaidi ya tunavyomfahamu!
Its an insult kumfananisha jeetu Patel na somaiya young man.Kma hujui watu aliochangia kuuleta uhuru wa nchii ni pamoja na somaiya thats why hata wakati wa ktutaifisha viwanda mwalimu aliviacha viwanda vya somaiya.usikurupuke kujifanya Mr Politician.
 
Its an insult kumfananisha jeetu Patel na somaiya young man.Kma hujui watu aliochangia kuuleta uhuru wa nchii ni pamoja na somaiya thats why hata wakati wa ktutaifisha viwanda mwalimu aliviacha viwanda vya somaiya.usikurupuke kujifanya Mr Politician.


Kwani huyo Somaiya ni ndugu na yule Somaiya wa Tanga au yule Somaiya wa Kenya?
 
Mimi naamini kabisa hizi pesa za matajiri ndani ya vyama na jumuiya za vyama inabidi zithibitiwe

Transparent ndani ya vyama vya siasa kwa sasa hakuna kabisa hivyo ili kuhakikisha wanasiasa hawanunuliwi na matajiri ili wafanyiwe favours mbali mbali inabidi 'misaada' ithibitiwe barabara.

Mkuu Bubu, hapa ninakubaliana na wewe kwa 100%, yaani tupo ukurasa mmoja,

Tanzania tuwe na sheria ya kuthibiti zawadi au misaada kwa vyama vyetu vya siasa, lakini hatuwezi kuwa na sheria ya kuwalazimisha watoa misaada kutoa kwa pande ya siasa wasiyoitaka, hapana huo sio ustaarabu wala uhuru wa kisiasa, yaani wa wananchi ku-practice politics as they wish as long as hawavunji sheria za jamhuri,

Habari zote zilizo wazi so far hazionyeshi Somaiya kuwa ni fisadi, unless kuna habari ambayo haipo hapa tayari, kwa sababu kuwa na rafiki fisadi sidhani kama ni dhambi kwa sheria zetu za bongo, binafsi nina tatizo sana na tabia nyingi za Wahindi, lakini sio Wahindi wenyewe, Primary niliyosoma ilikuwa un-official ya Wahindi, na ninakumbuka sana tabia zao darasani, nimeenda Bombay nimewaona tabia zao kule wao wanaamini sisi waa-Africa ni wasi wasi, pamoja na kwamba kila mahali mjini kwao kuna kinyesi cha binadam, kitu ambacho sisi bongo hatujafikia bado,

Lakini still, hawa Wahindi bongo bado ni ndugu zetu Jumamosi nilikuwa ninaongea na mama mmoja wa Kiganda, akanipa darasa sana jinsi Wahindi kwao walivyo na heshima na wazawa toka kile kiboko cha Amin, na ni wachache sana sio kama zamani, sasa kwa kusoma betweeen the lines kwenye hii thread sio siri kwamba Tanzania tuna tatizo kubwa sana na Wahindi in general that hatuwezi kuona Mhindi akitoa hela zote hizi kwa chama cha siasa bila sababu nyuma yake, na kwamba ni lazima iwe sababu ya kifisadi, kwa kweli hakuna wa kulaumiwa kwa hayo mawazo,

Sasa tunafanya nini as a nation ku-deal na hii ishu ya Wahindi, kwa sababu the ishu hapa kama nina-read sawa sawa ni tabia za wahindi bongo, lakini sio Wahindi wenyewe au wote, au?
 
Mkuu Bubu, hapa ninakubaliana na wewe kwa 100%, yaani tupo ukurasa mmoja,

Tanzania tuwe na sheria ya kuthibiti zawadi au misaada kwa vyama vyetu vya siasa, lakini hatuwezi kuwa na sheria ya kuwalazimisha watoa misaada kutoa kwa pande ya siasa wasiyoitaka, hapana huo sio ustaarabu wala uhuru wa kisiasa, yaani wa wananchi ku-practice politics as they wish as long as hawavunji sheria za jamhuri,

Habari zote zilizo wazi so far hazionyeshi Somaiya kuwa ni fisadi, unless kuna habari ambayo haipo hapa tayari, kwa sababu kuwa na rafiki fisadi sidhani kama ni dhambi kwa sheria zetu za bongo, binafsi nina tatizo sana na tabia nyingi za Wahindi, lakini sio Wahindi wenyewe, Primary niliyosoma ilikuwa un-official ya Wahindi, na ninakumbuka sana tabia zao darasani, nimeenda Bombay nimewaona tabia zao kule wao wanaamini sisi waa-Africa ni wasi wasi, pamoja na kwamba kila mahali mjini kwao kuna kinyesi cha binadam, kitu ambacho sisi bongo hatujafikia bado,

Lakini still, hawa Wahindi bongo bado ni ndugu zetu Jumamosi nilikuwa ninaongea na mama mmoja wa Kiganda, akanipa darasa sana jinsi Wahindi kwao walivyo na heshima na wazawa toka kile kiboko cha Amin, na ni wachache sana sio kama zamani, sasa kwa kusoma betweeen the lines kwenye hii thread sio siri kwamba Tanzania tuna tatizo kubwa sana na Wahindi in general that hatuwezi kuona Mhindi akitoa hela zote hizi kwa chama cha siasa bila sababu nyuma yake, na kwamba ni lazima iwe sababu ya kifisadi, kwa kweli hakuna wa kulaumiwa kwa hayo mawazo,

Sasa tunafanya nini as a nation ku-deal na hii ishu ya Wahindi, kwa sababu the ishu hapa kama nina-read sawa sawa ni tabia za wahindi bongo, lakini sio Wahindi wenyewe au wote, au?

Ahsante sana FMES kwa mchango wako mzuri. Mimi siwachukii wahindi hata kidogo ni binadamu wenzetu na inabidi kuwaheshimu, kuwatendea haki na kuhakikisha wanakuwa na haki zote ambazo Watanzania na binadamu wote duniani wanazithamini.

Nisichokipenda ni hii tabia yao ya kutaka kuwanunua wanasiasa kwa kutoa michango mikubwa sana kwa CCM. Kama utakumbuka Mwalimu kabla hajafariki alilizungumzia hili la CCM kuvamiwa na matajiri. Mwalimu hakuwa mbaguzi na ndani ya serikali zake alikuwa na Mzungu Bryson, Wahindi Amir Jamal na Alnoor Kassum lakini wahindi ambao walikuwa wanafiki walikuwa wanamuogopa sana Mwalimu kutokana na principles zake za kuhakikisha chama kinabaki kuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi na si chama cha matajiri.

Sioni ubaya wowote wa Wahindi kuchangia vyama vya siasa, lakini michango hiyo iwe ya kiwango maalum ili kuhakikisha chama kimoja hakina advantage kubwa ukilinganisha na vyama vingine. Pia nchi yetu ina matatizo mengi sana katika mahospitali, mashule n.k. kwa nini wahindi hawa wasihamasishwe kusaidia sehemu kama hizo!!!? au kusponsor wanafunzi pale UDSM au vyuo vingine ambao wanatoka katika familia zenye uwezo mdogo? Hebu fikiria shilingi milioni 400 zingenunua vitanda vingapi vya mahospitali yetu, au madawati mangapi ya mashule yetu au kusomesha wanafunzi wangapi pale UDSM!?

Ni kweli kwa sasa kuna tuhuma tu za ufisadi dhidi ya Somaiya lakini yeye katoa ushahidi unaonyesha hakuhusika na kashfa ya rada, lakini tukisikia upande mwingine wa shilingi kutoka kwa yule Vethalani labda naye ni muhusika mkuu. Pia anahusika kwa karibu na mkataba wa ununuzi wa magari na helicopters za jeshi ambao nao una utata. Pia tukumbuke panapofuka moshi hapakosi moto.
 
naomba nifahamishwe mi nilidhani katoa vifaa vyenye thamani ya 250m(kofia,tshirts ets..) na pesa taslim 150m kwa ajili ya malazi,chakula,posho,etc kwa wajumbe wa jumuiya iyo au?
 
Mbona wafanyabiashara wa Tarime wamejitokeza waziwazi kuunga mkono Chadema?

As long as hakuna sheria ya kudhibiti kiasi na aina ya michango kwa vyama vya siasa sioni tatizo wafanyabiashara kuchangia CCM au Chadema
 
nyie mnapiga kelele zabure.. ni chama gani hapa au association yakibongo itakayokataa 400million zabure..lol.. lets be serious!
 
Date::11/21/2008
Kampeni chafu zaanza UVCCM
Exuper Kachenje
Mwananchi

KAMPENI chafu na za kupakana matope zimezuka miongoni mwa makundi ya wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM imebainika.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi inazo, wagombea hao kwa upande mmoja, wamekuwa wakiendesha kampeni chafu za chuki na kupakana matope kwa misingi ya rangi.

Habari za uhakika zilizoifikia Mwananchi zinaeleza kuwa, kumezuka kundi ambalo kwa makusudi linaendesha kampeni za kumpaka matope mmoja wa wa wagombea wa nafasi hiyo kwa kusambaza ujumbe mchafu kumhusu yeye kwa njia ya simu selula na kueleza kuwa UVCCM, ipo hatarini kutekwa na maharamia.

"Wanafanya hivyo kwa kasi chini ya ufadhili wa mgombea mwinigine wa nafasi hiyo ya juu ya uongozi katika UVCCM," kilieleza chanzo cha habari hizi

Habari zaidi zinabainisha kuwa, anayekusudiwa kupakwa matope na kuchafuliwa ni Hussein Bashe, mgombea mwenye asili ya kisomali ambaye Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ilipitisha jina lake kugombea nafasi hiyo.

Sehemu ya ujumbe huo ulisomeka: " Kama meli za mfuta zinavyotekwa na maharamia ya kisomali vivyo hivyo wana CCM tuwe macho, kwani UVCCM iko hatarini kutekwa na maharamia hao wa kisiasa toka ughaibuni. Shime Watanzania wenzangu tuamke tusikubali kuongozwa na ma-tx."

Akizungumzia tukio hilo, Hussein Bashe alisema kuwa wanaosambaza ujumbe huo wamefilisika kisiasa na kwamba badala ya kupoteza muda kwa kupakana matope waeleze wataisaidia nini UVCCM.

"Wanaosambaza ujumbe huo wamefilisika kisiasa, waeleze wataisaidia nini jumuia. Hata mwalimu Nyerere aliwahi kusema: watu waliofilisika kisiasa hukimbilia mambo madogo madogo yasiyo na msingi," alisema Bashe.
 
Duh..!!
Sasa ndo maneno ya Baba wa Taifa Yanatimia, inaonyesha hao wanaompaka matope Bwana bashe wamesahagundua nguvu yake, na nina imani, ni wafa maji wanaotapatapa,ila namnukuu marehamu Baba wa taifa katika baadhi ya hotuba zake,''UKIONA MWANASIASA ANAANZA KUHOJI UDINI,RANGI,UKABILA BASI UJUE AMEFILISIKA KISIASA'' ,ninavyofikri hoja ni kuisaidia jamii KAMA ALIVYOSEMA Bwn, Bashe na si kuanza mambo ya Ubaguzi n.k
NB:WAPIGA KURA WAWE MAKINI NA WATU HATARI KAMA HAWA..!!!
 
Back
Top Bottom