OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo Wakuu ,heshima kwenu ! Katika kutimilika kwa nukuu ya Rais msitaafu wa Afrika ya kusini, Mzee Mandela isemayo "NO EASY WALK TO FREEDOM AND DEMOCRACY." Jana Kamanda Mawazo,diwani wa zamani wa ccm kata ya Sombetini,Arusha aliye vua gamba na kuhamia Cdm alifanyiwa hujuma baada ya mgombea wa ccm kata ya Msalato kufungulia nyuki toka kwenye mfuko wa Marbolo na kusababisha mtafaruku mkubwa katika kitongoji cha Mazinge kwenye kampeini zinazo endelea za uchaguzi mdogo wa madiwani, kata 29. Pamoja na taharuki hiyo, baadae hali ili rejea shwari ambapo makanda waliendeleza harakati mpaka mwisho. Ki ukweli kama ndo siasa hizi ,ni wazi kuwa ccm imefulia kama si kufilisika ki fikra. Hiki kikombe ccm lazima wakinywee kwani siku zote mjinga akijitambua ni wazi kuwa lazima mwerevu uwe matatani. Naomba kuwasilisha . Source : Mawazo mwenyewe.