Mwenyekiti kamati uchumi na fedha ccm kata ya msalato, dodoma amewekwa ndani jana.

OMUSILANGA

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
384
227
Ndiyo Wakuu , heshima kwenu ! Katika kile kinacho ashiria kuwa mwisho wa utawala wa ccm unafikia mwisho, viongozi na makada wengi wa ccm wame ona kuwa matumizi ya nguvu, vitisho na unyanyasaji ndiyo njia mbadala ya kuki imarisha chama badala ya kutekeleza ahadi ya maisha bora kwa watanzania .

Jana Mwenyekiti wa kamati ya uchumi na fedha wa kata ya msalato amekamatwa na polisi pamoja na wenzake baada ya kumshambulia na kumuumizaa vibaya mzee Benard wa mtaa wa Mwinyi .

Tukio hilo lilitokea juzi baada ya huyo mzee pamoja na wazee wenzake wapatao 20 kuunda kikundi cha kwaya kuipongeza cdm na mgombea wake wa Udiwani kata ya Msalato kamanda Nsubi. Maandalizi ya kikundi hicho cha kwaya ya Wazee yalikuwa yakifanyikia nyumbani hapo kwa Mzee Bernad.

Mzeea Bernad mwenye umri wa miaka 79 ,yuko hoi hospital ya mkoa Dodoma wodi no.1, uongozi kampeini kata ya Msalato chini ya Kamanda Mawazo Alophonce wanatoa huduma kwa mzee tangu juzi.

Hivi CCM kwa vitendo hivi ndo kumu enzi Baba wa Taifa? Hivi kwa vitendo hivi ndo kujivugua gamba? Yetu macho lakini kamwe ubaya hauja wahi shinda wema. Vilevile giza halija wahi shida nuru . Naomba kuwasilisha. SOURCE : MAWAZO MWENYEWE.
 
Hivi ni viashirio vya wazi kuwa CCM haikubaliki hata kwa mabavu. Ndugu wana CHADEMA naomba itambulike kuwa ukombizi si lelemama bali ni lazima. Lazima tutegemee vikwazo lakini tutavuka tu.
 
Watashindana lkn hawataweza, watadhuru miili ila wanaimarisha ujasiri wa wateswa, na Kwa hayo wanaitangaza zaidi cdma. Thanx magamba, ndaga fijo, mwabeja sana, mwalimi, mwasalipa, tuhongidze, msengwine, wakora.
 
Au ndiyo maana Ngeleja kasema hivi:




Ngeleja awabeza wapinzani


na Sitta Tumma, Mwanza
MBUNGE wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), amesema vyama vya upinzani kamwe visiwe na ndoto ya kukiangusha chama tawala katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014 pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Alisema CCM bado ipo imara kuliko inavyotafsiriwa na wapinzani, na kwamba viongozi wake walioingia madarakani kupitia chaguzi za ndani ya chama hicho, ni kielelezo tosha kwamba chama hicho kitaendelea kuongoza dola ifikapo mwaka 2015.

Akizungumza juzi jijini Mwanza, katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM mkoani hapa, Ngeleja aliyepata kuwa Waziri wa Nishati na Madini, alisema chama chake hakitishiki na kelele za wapinzani, kwani mbio za kupokezana vijiti katika uongozi, ukiwamo wa ndani ya chama ni ishala tosha ya kuzidi kuimarika kwa CCM.

“Utaratibu wa kupokezana vijiti katika uongozi ni maandalizi mazuri ya CCM kuendelea kushika dola ifikapo mwaka 2015. Nina uhakika asilimia 100 viongozi wa CCM waliopo madarakani ni imara.

“Kwa uhakika huu, vyama vya upinzani hawaiwezi CCM, waondoe ndoto za kuongoza dola ifikapo mwaka 2015...na hata uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2014, maana chama hiki kipo imara kuliko inavyotafsiriwa na wapinzani,” alisema.

Bila kutaja chama cha upinzani, mbunge huyo alisema majigambo yanayotolewa na wapinzani hayana tija, na kwamba hizo ni propoganda ambazo kamwe haziwezi kufua dafu kwa kukiondoa madarakani chama hicho.
 
Au ndiyo maana Ngeleja kasema hivi:




Ngeleja awabeza wapinzani


na Sitta Tumma, Mwanza


amka2.gif
MBUNGE wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), amesema vyama vya upinzani kamwe visiwe na ndoto ya kukiangusha chama tawala katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014 pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Alisema CCM bado ipo imara kuliko inavyotafsiriwa na wapinzani, na kwamba viongozi wake walioingia madarakani kupitia chaguzi za ndani ya chama hicho, ni kielelezo tosha kwamba chama hicho kitaendelea kuongoza dola ifikapo mwaka 2015.
Akizungumza juzi jijini Mwanza, katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM mkoani hapa, Ngeleja aliyepata kuwa Waziri wa Nishati na Madini, alisema chama chake hakitishiki na kelele za wapinzani, kwani mbio za kupokezana vijiti katika uongozi, ukiwamo wa ndani ya chama ni ishala tosha ya kuzidi kuimarika kwa CCM.
“Utaratibu wa kupokezana vijiti katika uongozi ni maandalizi mazuri ya CCM kuendelea kushika dola ifikapo mwaka 2015. Nina uhakika asilimia 100 viongozi wa CCM waliopo madarakani ni imara.
“Kwa uhakika huu, vyama vya upinzani hawaiwezi CCM, waondoe ndoto za kuongoza dola ifikapo mwaka 2015...na hata uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2014, maana chama hiki kipo imara kuliko inavyotafsiriwa na wapinzani,” alisema.
Bila kutaja chama cha upinzani, mbunge huyo alisema majigambo yanayotolewa na wapinzani hayana tija, na kwamba hizo ni propoganda ambazo kamwe haziwezi kufua dafu kwa kukiondoa madarakani chama hicho.


h.sep3.gif


link4.gif
 
Back
Top Bottom