Mathias Lyamunda
JF-Expert Member
- Apr 4, 2013
- 1,369
- 558
Jana Chadema Arusha ilifanya uzinduzi wa kihistoria wa uchaguzi wa kata ya Sombetini na le Captain Mawazo alitoa Hotuba kali iliyowaliza wana Sombetini wakikumbuka jinsi alivyowatumikia kwa uaminifu.
Jana akisikilizwa na Maelfu ya wananchi wa Sombetini Captain Mawazo alimpa wosia mzito Bananga kuwa anakwenda kuwatumikia watu masikini kwahiyo watoto wa masikini ni watoto wake, wakifukuzwa shule kwa kukosa Ada wasiende nyumbani kwa wazazi wao waende kwa Ally Bananga, yeye ndo baba na Mama wa watoto wa Sombetini.
Hotuba yake ili acha Visio kwa watoto na akina mama waliokuwepo kwa wengi mkutano. Nukuu: "Leo kwa moyo wa UJASIRI na unyenyekevu mkubwa na kumkabidhi Bananga kitu pekee kilichonifanya nijulikane kama mwanasiasa Arusha na nje ya Arusha, na kumkabidhi heshima ya kuigwa Mh. Diwani, MAMLAKA siyo kitu kidogo, nimeshuhudia watu wakiloga na kuua ili kuwa madiwani, hiyo na kuacha maana najua wewe ni diwani sasa, pili na kuacha posho wewe na wa wananchi wote WANAJUA kwamba sina hela na nina familia na mahitaji mengine, lakini hivyo vyote haviniumi, kinachoniuma kabisa ni kukua chia MPENZI wangu wa pekee ambayo ni kata ya Sombetini, MACHOZI ya kina mama hawa si kwasababu NYINGINE Bali ni upendo walionao kwangu uliotokana na utumishi na upendo usio na ubinafsi kamwe, niliwahi kutangaza watoto wote wa Sombetini ni watoto wangu, wakifukuzwa shule wasiende nyumbani kwa wazazi wao WAJE kwangu na divyo ilivyokuwa na wananchi ni mashahidi" mwisho wa kunukuu.
Alimsihi Bananga Avae viatu vyake kisawasawa.
Pia aliwashangaa WANASIASA wanaohutubia udini na ukabila aliwauliza wananchi ni nani anayeteseka nchi hii zaidi ya mkulima na mfugaji? Alikumbushia matukia ya kiteto ya wafugaji na wakulima walivyo uana kutokana na chuki za kikatil a zinazopandikizwa na watawala wa CCM, ni SERIKALI ya ccm ndio iliyoua Ng'ombe za wamasai kwenye operation tokomeza ujangili, alisema, nanukuu:
"Tanzanite iko kwenu, mbuga za wanyama ZIKO kwenu, mbaya zaidi wamewageuza kuwa Sehemu ya utaki kwa kuwapiga picha na kupiga picha umasikini wenu, na imewapelekea vijana wenu KUKIMBILIA mjini kuwa walinzi wao kwa kukosa ardhi ya kulima na mails na malisho ya Ng'ombe kwahiyo ndugu zangu wa Maasai adui yenu siyo MCHAGA wala mdengeleko adui yenu ni CCM".
Aliwaomba wananchi wote wa sombetini wamchague Bananga na waichague Chadema.
Jana akisikilizwa na Maelfu ya wananchi wa Sombetini Captain Mawazo alimpa wosia mzito Bananga kuwa anakwenda kuwatumikia watu masikini kwahiyo watoto wa masikini ni watoto wake, wakifukuzwa shule kwa kukosa Ada wasiende nyumbani kwa wazazi wao waende kwa Ally Bananga, yeye ndo baba na Mama wa watoto wa Sombetini.
Hotuba yake ili acha Visio kwa watoto na akina mama waliokuwepo kwa wengi mkutano. Nukuu: "Leo kwa moyo wa UJASIRI na unyenyekevu mkubwa na kumkabidhi Bananga kitu pekee kilichonifanya nijulikane kama mwanasiasa Arusha na nje ya Arusha, na kumkabidhi heshima ya kuigwa Mh. Diwani, MAMLAKA siyo kitu kidogo, nimeshuhudia watu wakiloga na kuua ili kuwa madiwani, hiyo na kuacha maana najua wewe ni diwani sasa, pili na kuacha posho wewe na wa wananchi wote WANAJUA kwamba sina hela na nina familia na mahitaji mengine, lakini hivyo vyote haviniumi, kinachoniuma kabisa ni kukua chia MPENZI wangu wa pekee ambayo ni kata ya Sombetini, MACHOZI ya kina mama hawa si kwasababu NYINGINE Bali ni upendo walionao kwangu uliotokana na utumishi na upendo usio na ubinafsi kamwe, niliwahi kutangaza watoto wote wa Sombetini ni watoto wangu, wakifukuzwa shule wasiende nyumbani kwa wazazi wao WAJE kwangu na divyo ilivyokuwa na wananchi ni mashahidi" mwisho wa kunukuu.
Alimsihi Bananga Avae viatu vyake kisawasawa.
Pia aliwashangaa WANASIASA wanaohutubia udini na ukabila aliwauliza wananchi ni nani anayeteseka nchi hii zaidi ya mkulima na mfugaji? Alikumbushia matukia ya kiteto ya wafugaji na wakulima walivyo uana kutokana na chuki za kikatil a zinazopandikizwa na watawala wa CCM, ni SERIKALI ya ccm ndio iliyoua Ng'ombe za wamasai kwenye operation tokomeza ujangili, alisema, nanukuu:
"Tanzanite iko kwenu, mbuga za wanyama ZIKO kwenu, mbaya zaidi wamewageuza kuwa Sehemu ya utaki kwa kuwapiga picha na kupiga picha umasikini wenu, na imewapelekea vijana wenu KUKIMBILIA mjini kuwa walinzi wao kwa kukosa ardhi ya kulima na mails na malisho ya Ng'ombe kwahiyo ndugu zangu wa Maasai adui yenu siyo MCHAGA wala mdengeleko adui yenu ni CCM".
Aliwaomba wananchi wote wa sombetini wamchague Bananga na waichague Chadema.