Kama Zanzibar, baada ya miaka mingi ya Muungano, iliamua kuunda Katiba yake na kuwa na Bendera yake, kwanini isiwe kwa Tanganyika?

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,075
Mwaka 1964, Rais Nyerere na Karume Walipoamua kuunganisha Taifa la Zanzibar na Tanganyika, kila nchi ilipoteza katiba yake, bendera yake na Wimbo wa Taifa lake.

Wakati wa utawala wa Jakaya Mrisho Kikwete, baada ya kupita zaidi ya miaka 40 tangu kuasisiwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Zanzibar walifanyia marekebisho makubwa ya katiba yao ya mwaka 1984, wakaitisha kura ya maoni, wazanzibari wakapiga kura kuipitisha katiba yao. Marekebisho hayo makubwa ya Katiba ya Zanzibar, ya mwaka 2010, yaliitambua Zanzibar kama nchi yenye katiba yake, bendera yake na wimbo wake wa Taifa. Marekebisho hayo makubwa ya katiba yakaainisha mipaka ya nchi ya Zanzibar. Marejebisho hayo ikayaondoa baadhi ya mambo yaliyokuwa ya Muungano kama bandari, gas na mafuta.

Kwa hiyo, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo, leo Zanzibar ina katiba yake ya nchi iliyoidhinisha bendera ya nchi ya Zanzibar, iliyoidhinisha vikosi vyake vya ulinzi vinavyofanana na polisi, iliyoidhinisha matumizi ya wimbo wake wa Taifa.

Kwa unafiki wa viongozi wetu wa wakati ule, wote walikaa kimya, kama vile hakuna kilichotokea.

Leo hii, sijui ni kwa ujinga au unafiki, mtu akitamka tu Tanganyika, eti ni mbaguzi na mtu mwenye dhamira ya kudhoofisha Muungano.

Tuwaulize hawa viongozi wanafiki na waongo, Zanzibar ilipokuwa inaandika katiba yake na kuitambua Zanzibar kama nchi, yenye alama zote za Taifa linalojitegemea, walikuwa wapi? Hawakuona? Au waliona, lakini waliona ni haki na ni sahihi?

Kama ni sahihi kwa Zanzibar, basi na sisi Tanganyika, tuandike katiba yetu, itakayoitambua Tanganyika kama nchi, katiba itakayorudisha nembo za nchi ya Tanganyika, na kuainisha mipaka yake. Na katiba ya Tanganyika ianishe wazi kuwa masuala yasiyo ya Muungano, na rasilimali za Taifa kama bandari na madini, iwe ni marufuku kwa asiye Mtanganyika kuyafanyia maamuzi.

Viongozi waache unafiki, wafumbe vinywa vyao kama walivyokuwa wamefumba wakati Zanzibar ikiandika katiba yake, na wakae kimya, wasinene lolote.
 
Zanzibar kuna wakati nikiitazama naiona kama "nchi" iliyofunikwa na nchi nyingine, lakini wameachiwa vitu kama jeshi, katiba, bunge, na mahakama ili wajiskie wana mamlaka kamili.

Nasema hivyo kwasababu ukitazama kwa undani, utagundua maamuzi mazito yenye hatma kwa Zanzibar yenyewe huwa yanatokea Dodoma, sasa kama unajinasibu una mamlaka kamili, lakini bado kiongozi wenu mkuu anateuliwa kwa vikao nje ya nchi yenu, ninyi ni watumwa tu.

Hata hizi fursa wanazopata sasa hivi, kama kufutiwa deni na Tanesco, bado naziona kama pipi tu wanazopewa ili kudanganywa kwa utamu wake..

Lakini kimsingi, siku akiondoka Mmakunduchi kwenye utawala, hao wazanzibari wataendelea kuishi kwa matumaini tu, migao mingi wanayoipata sasa, licha ya kwamba ipo kiutaratibu, lakini ukweli asipokuwepo ndugu yao kuongoza Tanganyika, hawaipati kwa uzito kama waipatavyo sasa.

Baada ya kuandika hayo, binafsi sioni kama tuna haja ya kubabaishwa na uwepo wa bunge, mahakama, serikali, majeshi, na katiba kule Zanzibar, kwani hivyo vyote walivyonavyo ni kama pipi tu za kuwazubaisha watoto wazuri ili wasililie kujitoa kwenye muungano.
 
Zanzibar kuna wakati nikiitazama naiona kama "nchi" iliyofunikwa na nchi nyingine, lakini wameachiwa vitu kama jeshi, katiba, bunge, na mahakama ili wajiskie wana mamlaka kamili.

Nasema hivyo kwasababu ukitazama kwa undani, utagundua maamuzi mazito yenye hatma kwa Zanzibar yenyewe huwa yanatokea Dodoma, sasa kama unajinasibu una mamlaka kamili, lakini bado kiongozi wenu mkuu anateuliwa kwa vikao nje ya nchi yenu, ninyi ni watumwa tu.

Hata hizi fursa wanazopata sasa hivi, kama kufutiwa deni na Tanesco, bado naziona kama pipi tu wanazopewa ili kudanganywa kwa utamu wake, lakini kimsingi, siku akiondoka Mmakunduchi kwenye utawala, hao wazanzibari wataendelea kuishi kwa matumaini tu, migao mingi wanayoipata sasa, licha ya kwamba ipo kiutaratibu, lakini ukweli asipokuwepo ndugu yao kuongoza Tanganyika, hawaipati kwa uzito kama waipatavyo sasa.

Baada ya kuandika hayo, binafsi sioni kama tuna haja ya kubabaishwa na uwepo wa bunge, mahakama, serikali, majeshi, na katiba kule Zanzibar, kwani hivyo vyote walivyonavyo ni kama pipi tu za kuwazubaisha watoto wazuri ili wasililie kujitoa kwenye muungano.
Zanzibar wakiamuwa serious wanavunja muungano na wanawakodi Wagner kuwalinda, hakuna Jeshi la Tanganyika litathubutu kutia puwa yake Zanzibar.
 
Mwaka 1964, Rais Nyerere na Karume Walipoamua kuunganisha Taifa la Zanzibar na Tanganyika, kila nchi ilipoteza katiba yake, bendera yake na Wimbo wa Taifa lake.

Wakati wa utawala wa Jakaya Mrisho Kikwete, baada ya kupita zaidi ya miaka 40 tangu kuasisiwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Zanzibar wakaandaa katiba mpya, wakaitisha kura ya maoni, wazanzibari wakapiga kura kuipitisha katiba yao. Katiba hiyo mpya, iliitambua Zanzibar kama nchi yenye katiba yake, bendera yake na wimbo wake wa Taifa. Katiba hiyo ikaainisha mipaka ya nchi ya Zanzibar. Katiba hiyo ikayaondoa baadhi ya mambo yaliyokuwa ya Muungano kama bandari, gas na mafuta.

Kwa hiyo, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo, leo Zanzibar ina katiba yake ya nchi iliyoidhinisha bendera ya nchi ya Zanzibar, iliyoidhinisha vikosi vyake vya ulinzi vinavyofanana na polisi, iliyoidhinisha matumizi ya wimbo wake wa Taifa.

Kwa unafiki wa viongozi wetu wa wakati ule, wote walikaa kimya, kama vile hakuna kilichotokea.

Leo hii, sijui ni kwa ujinga au unafiki, mtu akitamka tu Tanganyika, eti ni mbaguzi na mtu mwenye dhamira ya kudhoofisha Muungano.

Tuwaulize hawa viongozi wanafiki na waongo, Zanzibar ilipokuwa inaandika katiba yake na kuitambua Zanzibar kama nchi, yenye alama zote za Taifa linalojitegemea, walikuwa wapi? Hawakuona? Au waliona, lakini waliona ni haki na ni sahihi?

Kama ni sahihi kwa Zanzibar, basi na sisi Tanganyika, tuandike katiba yetu, itakayoitambua Tanganyika kama nchi, katiba itakayorudisha nembo za nchi ya Tanganyika, na kuainisha mipaka yake. Na katiba ya Tanganyika ianishe wazi kuwa masuala yasiyo ya Muungano, na rasilimali za Taifa kama bandari na madini, iwe ni marufuku kwa asiye Mtanganyika kuyafanyia maamuzi.

Viongozi waache unafiki, wafumbe vinywa vyao kama walivyokuwa wamefumba wakati Zanzibar ikiandika katiba yake, na wakae kimya, wasinene lolote.
Hapa ni kama mwanamke alie achika kwenye ndoa. Jamaa kaoa mke mwingine na familia yake imeendelea vizuri tu. Ila yule mwanamke wa kwanza bado anajitambulisha ni mke wa jamaa
 
Hivi huwa hamuoni aibu? Watu millioni 1 wa Zanzibar kila siku mlalamike wanawanyonya watu million 60 hapo nani hana akili sasa?
Punguza mihemko daktari, tafakari kwa kina, vipi kuhusu mchango wa hao watu milioni moja kwenye pato la taifa, linaendana na gawio/favor wanazopata. Kiuhalisia bajeti ya Znz ilipaswa kuwa sawa na bajeti ya mkoa wa Singida kama tukiangalia idadi ya watu.
 
Mwaka 1964, Rais Nyerere na Karume Walipoamua kuunganisha Taifa la Zanzibar na Tanganyika, kila nchi ilipoteza katiba yake, bendera yake na Wimbo wa Taifa lake.

Wakati wa utawala wa Jakaya Mrisho Kikwete, baada ya kupita zaidi ya miaka 40 tangu kuasisiwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Zanzibar wakaandaa katiba mpya, wakaitisha kura ya maoni, wazanzibari wakapiga kura kuipitisha katiba yao. Katiba hiyo mpya, iliitambua Zanzibar kama nchi yenye katiba yake, bendera yake na wimbo wake wa Taifa. Katiba hiyo ikaainisha mipaka ya nchi ya Zanzibar. Katiba hiyo ikayaondoa baadhi ya mambo yaliyokuwa ya Muungano kama bandari, gas na mafuta.

Kwa hiyo, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo, leo Zanzibar ina katiba yake ya nchi iliyoidhinisha bendera ya nchi ya Zanzibar, iliyoidhinisha vikosi vyake vya ulinzi vinavyofanana na polisi, iliyoidhinisha matumizi ya wimbo wake wa Taifa.

Kwa unafiki wa viongozi wetu wa wakati ule, wote walikaa kimya, kama vile hakuna kilichotokea.

Leo hii, sijui ni kwa ujinga au unafiki, mtu akitamka tu Tanganyika, eti ni mbaguzi na mtu mwenye dhamira ya kudhoofisha Muungano.

Tuwaulize hawa viongozi wanafiki na waongo, Zanzibar ilipokuwa inaandika katiba yake na kuitambua Zanzibar kama nchi, yenye alama zote za Taifa linalojitegemea, walikuwa wapi? Hawakuona? Au waliona, lakini waliona ni haki na ni sahihi?

Kama ni sahihi kwa Zanzibar, basi na sisi Tanganyika, tuandike katiba yetu, itakayoitambua Tanganyika kama nchi, katiba itakayorudisha nembo za nchi ya Tanganyika, na kuainisha mipaka yake. Na katiba ya Tanganyika ianishe wazi kuwa masuala yasiyo ya Muungano, na rasilimali za Taifa kama bandari na madini, iwe ni marufuku kwa asiye Mtanganyika kuyafanyia maamuzi.

Viongozi waache unafiki, wafumbe vinywa vyao kama walivyokuwa wamefumba wakati Zanzibar ikiandika katiba yake, na wakae kimya, wasinene lolote.
Kwani tumekosa nini hasa au tutapata nini hasa ambacho sasa hatukipati kwa kufanya hivyo na manufaa gani zaidi au ndio hila tu za kitoto na mimi nataka pipi kama zile mbona anazo zake za blue kwa nini zangu nyeupe bila tafakari kuu.
 
Mwaka 1964, Rais Nyerere na Karume Walipoamua kuunganisha Taifa la Zanzibar na Tanganyika, kila nchi ilipoteza katiba yake, bendera yake na Wimbo wa Taifa lake.

Wakati wa utawala wa Jakaya Mrisho Kikwete, baada ya kupita zaidi ya miaka 40 tangu kuasisiwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Zanzibar wakaandaa katiba mpya, wakaitisha kura ya maoni, wazanzibari wakapiga kura kuipitisha katiba yao. Katiba hiyo mpya, iliitambua Zanzibar kama nchi yenye katiba yake, bendera yake na wimbo wake wa Taifa. Katiba hiyo ikaainisha mipaka ya nchi ya Zanzibar. Katiba hiyo ikayaondoa baadhi ya mambo yaliyokuwa ya Muungano kama bandari, gas na mafuta.

Kwa hiyo, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo, leo Zanzibar ina katiba yake ya nchi iliyoidhinisha bendera ya nchi ya Zanzibar, iliyoidhinisha vikosi vyake vya ulinzi vinavyofanana na polisi, iliyoidhinisha matumizi ya wimbo wake wa Taifa.

Kwa unafiki wa viongozi wetu wa wakati ule, wote walikaa kimya, kama vile hakuna kilichotokea.

Leo hii, sijui ni kwa ujinga au unafiki, mtu akitamka tu Tanganyika, eti ni mbaguzi na mtu mwenye dhamira ya kudhoofisha Muungano.

Tuwaulize hawa viongozi wanafiki na waongo, Zanzibar ilipokuwa inaandika katiba yake na kuitambua Zanzibar kama nchi, yenye alama zote za Taifa linalojitegemea, walikuwa wapi? Hawakuona? Au waliona, lakini waliona ni haki na ni sahihi?

Kama ni sahihi kwa Zanzibar, basi na sisi Tanganyika, tuandike katiba yetu, itakayoitambua Tanganyika kama nchi, katiba itakayorudisha nembo za nchi ya Tanganyika, na kuainisha mipaka yake. Na katiba ya Tanganyika ianishe wazi kuwa masuala yasiyo ya Muungano, na rasilimali za Taifa kama bandari na madini, iwe ni marufuku kwa asiye Mtanganyika kuyafanyia maamuzi.

Viongozi waache unafiki, wafumbe vinywa vyao kama walivyokuwa wamefumba wakati Zanzibar ikiandika katiba yake, na wakae kimya, wasinene lolote.

Tanganyika ni watumwa wa Zanzibar.
Utajiri mwingi wa Tanganyika unawanufaisha wazanzibar.
 
Punguza mihemko daktari, tafakari kwa kina, vipi kuhusu mchango wa hao watu milioni moja kwenye pato la taifa, linaendana na gawio/favor wanazopata. Kiuhalisia bajeti ya Znz ilipaswa kuwa sawa na bajeti ya mkoa wa Singida kama tukiangalia idadi ya watu.
Muungano wa Tanzania ni wa nchi mbili Tanganyika na Zanzibar, siyo nchi na mkoa.

Na Karume alishasema muungano ni kama koti tu likikubana unalivuwa.

Tumechoka na hizi kelele zenu hazina maana yoyote.

Wanaolazimisha muungano ni Watanganyika na siyo Wazanzibar, Wazanzibar hawataki huu muungano.
 
Mwaka 1964, Rais Nyerere na Karume Walipoamua kuunganisha Taifa la Zanzibar na Tanganyika, kila nchi ilipoteza katiba yake, bendera yake na Wimbo wa Taifa lake.

Wakati wa utawala wa Jakaya Mrisho Kikwete, baada ya kupita zaidi ya miaka 40 tangu kuasisiwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Zanzibar wakaandaa katiba mpya, wakaitisha kura ya maoni, wazanzibari wakapiga kura kuipitisha katiba yao. Katiba hiyo mpya, iliitambua Zanzibar kama nchi yenye katiba yake, bendera yake na wimbo wake wa Taifa. Katiba hiyo ikaainisha mipaka ya nchi ya Zanzibar. Katiba hiyo ikayaondoa baadhi ya mambo yaliyokuwa ya Muungano kama bandari, gas na mafuta.

Kwa hiyo, tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo, leo Zanzibar ina katiba yake ya nchi iliyoidhinisha bendera ya nchi ya Zanzibar, iliyoidhinisha vikosi vyake vya ulinzi vinavyofanana na polisi, iliyoidhinisha matumizi ya wimbo wake wa Taifa.

Kwa unafiki wa viongozi wetu wa wakati ule, wote walikaa kimya, kama vile hakuna kilichotokea.

Leo hii, sijui ni kwa ujinga au unafiki, mtu akitamka tu Tanganyika, eti ni mbaguzi na mtu mwenye dhamira ya kudhoofisha Muungano.

Tuwaulize hawa viongozi wanafiki na waongo, Zanzibar ilipokuwa inaandika katiba yake na kuitambua Zanzibar kama nchi, yenye alama zote za Taifa linalojitegemea, walikuwa wapi? Hawakuona? Au waliona, lakini waliona ni haki na ni sahihi?

Kama ni sahihi kwa Zanzibar, basi na sisi Tanganyika, tuandike katiba yetu, itakayoitambua Tanganyika kama nchi, katiba itakayorudisha nembo za nchi ya Tanganyika, na kuainisha mipaka yake. Na katiba ya Tanganyika ianishe wazi kuwa masuala yasiyo ya Muungano, na rasilimali za Taifa kama bandari na madini, iwe ni marufuku kwa asiye Mtanganyika kuyafanyia maamuzi.

Viongozi waache unafiki, wafumbe vinywa vyao kama walivyokuwa wamefumba wakati Zanzibar ikiandika katiba yake, na wakae kimya, wasinene lolote.
Kaka yangu tambua kwanza Zanzibar ilikuwa nchi kabla ya muungano...hata muungano ulipokuja kuna mambo yamefanywa kuwa ni ya muungano na yasiyo ya muungano ..jiulize mambo yaliyoyamuungano yanaendeshwa na serikali ya muungano kwa katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania wewe unafikiri mambo yasiyo ya muungano ya Zanzibar yangeendeshwa kwa katiba gani ikiwa zanzibar hatutaki iwe na katiba? Its true aina ya muungano tulio nao una changamoto zake lakini ndio ilikuwa most feasible form ya kuungana kwa wakati ule na hata sasa kwa uono wangu...ukitaka kuelewa vizuri mambo haya ya muungano wetu rudi ukasome upya kwanza kwanini tuliungana, nani alipendekeza muungano na aina ya muungano(kuna aina zaidi ya moja ambapo nchi zinawezackuungana), kwanini wazee wetu mwisho wa siku wakubaliane kwa namna ile ya muungano?
 
Zanzibar ni nchi kabla ata ya muungano, so what's your point?
Unayasema hayo kwa hisia au kwa mujibu wa katiba ya JMT? Hakuna mahali popote kwenye katiba ya JMT inapotamkwa kuwa Zanzibar ni nchi. Katiba inasema nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuunda nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kama una kumbukumbu nzuri, baadhi ya wabunge baada ya kuiona katiba ya Zanzibar, walimwuliza Waziri Mkuu Mizengo Pinda, je, Zanzibar ni nchi? Pinda akajibu kuwa Zanzibar siyo nchi. Baada ya jibu hilo, Wazanzibari walikuja juu sana dhidi ya Waziri Mkuu. Ili kupooza mambo Kikwete akaamua kupooza mambo kisanii. Rais Kikwete akasema kuwa wote wapo sahihi. Wanaosema Zanzibar siyo nchi wapo sahihi, na wanaosema Zanzibar ni nchi wapo sahihi. Akaongeza kuwa Zanzibar ni nchi tukiwa ndani ya mipaka ya Tanzania, lakini siyo nchi ukiwa nje ya Tanzania.

Katiba ya JMT inatamka kuwa Zanzibar ni sehemu ya JMT, haitamki popote kuwa ni nchi. Katiba ya Zanzibar waliyoitengeneza miaka ya karibuni, wakati wa utawala wa Jakaya Kikwete, ndiyo pekee inayotamka kuwa Zanzibar ni nchi.
 
Kwani tumekosa nini hasa au tutapata nini hasa ambacho sasa hatukipati kwa kufanya hivyo na manufaa gani zaidi au ndio hila tu za kitoto na mimi nataka pipi kama zile mbona anazo zake za blue kwa nini zangu nyeupe bila tafakari kuu.
Manufaa tutakayoyapata ni kusimamia rasilimali zetu, na kuzuia kutapanywa bure l kwa rasilimali zetu kwa wageni kama vile hazina mwenyewe, kama inavyofanyika sasa. Wasio Watanganyika, ambao hawana uchungu wowote wa rasilimali za Tanganyika wanazigawa bure kwa yeyote wanayemtaka bila ya kufuata hata taratibu na katiba, kama walivyofanya kwa bandari na mbuga zetu za wanyama.

Unadhani ni kwa nini rasilimali za Tanganyika zinagawiwa kwa wageni pale tu ambapo uongozi wa juu unapokuwa umeshikiliwa na watu wasio Watanganyika?
 
Back
Top Bottom