Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Mwishoni mwa juma linalokuja, natarajia kusafiri kwenda Mbekenyela huko Lindi, kuhudhuria na kuwa msimamizi wa ndoa ya shoga yangu wa siku nyingi sana. Kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusafiri maeneo hayo huko Bara, ningependa kama yupo Mwana JF mwenyeji wa huko anielezee mazingira yakoje? Je kuna baridi, au joto, umeme upo, mitandao inapatikana, kwa maana ya simu na internet. Vipi maji ya kunywa ni salama, je kuna mbu na hali ya barabara na usafiri ikoje?
Nimesita kumuuliza mwenyeji wangu, naogopa asije akadhani namdharau na ninapaona kwao ni Bush.
Nimesita kumuuliza mwenyeji wangu, naogopa asije akadhani namdharau na ninapaona kwao ni Bush.