Kama MWAKYEMBE na MAGUFULI wanafanya uhuni huu basi CCM imedhamiria kuwazika Watanzania!!!

Bwana Paulo,kuwa makini katika kuyachanganua mambo,kama kuna sehemu zenye idadi kubwa ya watu na hasa wenye hali ya kawaida sana ni maeneo ya mbagala(Wilaya ya Temeke) na Gongo la mboto(wilaya ya Ilala) kisha kinondoni, Treni hizi za TRL na TAZARA hata kama unasema hazifiki kila sehemu kitu ambacho kwanza unadhihilisha ubazazi wako, kwani magari yanafika kila sehemu? hujashuhudia utitiri wa pikipiki kila sehemu na hasa sehemu ambako magari hayafiki?

Ikiwa treni ya TAZARA ina ruti 24 kwa siku na kwa sehemu kubwa itawahudumia watu wa Temeke walio wengi huoni mchango wake? Treni ya TRL itakuwa na ruti kama hizo na kwa sehemu kubwa watu Ilala itawahudumia huoni mchango wake?

Hapo kwenye nyekundu kwani tatizo la teknolojia ndo limeonekana kuwa tatizo zaidi kwa kuanzishwa hizi ruti? au vp ulitaka kufumba na kufumbua ziwepo treni za umeme zinazokwenda kasi ama zisizokuwa na muongozaji binadamu? Pls.. jifunze kutambua juhudi za wenzako, mi ninavyoona hapo walipoanzia sio pabaya huo ushauri wako utafuata baadaye lakini kwanza tambua jitihada za mwanzo, ndo ugomvi wangu mimi na wewe Bwana Paulo!!

Unachangia ukiwa biased na waheshimiwa tayari!!! Nadhani la msingi ukirudi kwa heading na posit nzima sijaongelea Reli tu? Hivi BRT hukuiona? Sasa imagine Mwakyembe anahamishwa Wizara na jinsi ujuavyo mawaziri wetu hujiamlia ata kwa kushahuriwa na wake zao...... na wakati mwingine maamuzi huwa ya kukurupuka na kuvunja sheria mf. Kufunga vizibiti mwendo amabao ulikuwa mpango wa kifisadi au kuamua masomo ya biashara kufutwa....,. Lowasa kuja na njia tatu.... nk.
 
Nilipokusoma kwenye hizo quotes hao juu........NIKAJUA umevamia FANI za watu......na hata kama wewe upo kwenye fani hiyo basi........experience yako ni ndogo.......halafu usijidanganye ukifikir maamuzi wanayofanya Mwakyembe na Magufuli ni ya kwao binafsi.........kwa taarifa yako.....wameshauriwa na wataalamu waliopo kwenye Wizara zao............

Nevertheless.....Nakupongeza kwa kuwa Umejaribu!!.............BTW....hizi fani zina wenyewe aisee........wapi Morani75 .....wapi Fundi Mchundo ....

Mkuu, never trust wataalum wetu hawa ambao wametufikisha tulipo. Nadha madkt si mbumbu kiasi kwamba wasijue kuwa hela wanayoiwekeza hapo ingefungua barabara zote kwa kiwango cha lami hasa kuondoa utitiri wa magar
i Moro road hasa na maeneo mengine ya jiji.... !!!! Hivi kwa mtu mwenye akili timamu anahitaji shu kujua kwamf. kuwa ukifungua njia za Kimara, Mbezi nk to Tegeta au Uwanja wa Ndege utaondoa magari mengi ya kuelekea Ubungo asubuhi na jioni?
 
kwa hili la reli tupongeze kwa dhati kabisa kelele zisizochoka za chadema kuisukuma serikali hii Vivu ya ccm na kikwete hadi kimeelewka.
Kamanda, hujue utalazimika kunitafuta na kuniomba radhi kwa kutokubali kudanganyika...! UKISHANGAA ya UDA utayaona ya RELI na BRT.
 
Mkuu naona umechanganya. Reli ipo chini ya Wizara ya Uchukuzi na Barabara zipo chini ya Wizara ya Ujenzi na kila moja ina bajeti yake serikalini. Huwezi kuhamisha pesa za kukarabati reli toka wizara ya Uchukuzi kuzipeleka Wizara ya Ujenzi eti wakajengee Flyovers au Feeder roads. Kila mmoja anajaribu kuangalia kwa upande wake ni jinsi gani anapambana na tatizo hili la Usafiri/ foleni jijini.
Pakusifu, Sifu.

Hahahahahahaha.....! Watz bwn! Kuna sababu ya msingi ya kutenganisha hizi Wizara???? Najua kuwa ni Wizara tofauti ila nakushangaa kujaribu kuwaona mawaziri hawa kama watu ambao wanaishi mabara tofaut tofauti.
 
Duh! Kichwa cha habari na mada mbona haviendani. Hakuna uhuni hapo. Ulizotaja wewe ni changamoto. Mtoto akizaliwa si anaanza kwanza kukaa, kutambaa, kutembea mwisho anakimbia. Hizo route mbili ni mwanzo tu. Haiwezekani kuanza route zote kwani kuna gharama za kufufua mabehewa, route zenyewe, kulipa mafundi n.k. Hizo treni zitasaidia sana sisi wanyonge tunaopoteza masaa mawili kutoka nyumbani hadi mjini hata kama foleni hazitapungua tautawahi kazini. Ubaya wake uko wapi? Binafsi naona hii inastahili pongezi. Ila wana JF acheni kutukana katoa mawazo yake tumkosoe tu bila matusi.

Tanzania imezaliwa leo mkuu? Kuishi kwa matumaini kwa wasanii bila kujifunza ni jambo la hatari sana. Mimi nawaamini hawa jamaa 2 kuwa ni wachapa kazi ila kwa issue hizi mbili wameingia kwenye mtindo ule ule wa KUZUGA kama tulivyozoea!!!
 
we unatokea kundi gani mkuu?
maana hao uliowataja sidhani kama ni threat kwa kundi lolote la Urais.

Kwahiyo anayejenga hoja Tanzania anakundi!!!!!! Mbona unawaza kitoto sana??? Mimi Rais wangu ni yule Rais wa Watz, Dr. W. P. Slaa.
 
Watu kama wewe JF mmebaki wachache sana. Kamanda Paul kaandika vizuri. Ila hakua sahihi kuwabeza akina Mwakyembe. Magufuli na Mwakyembe wamethubutu hawajaweza. Ila well done Mwakyembe na Magufuli.

Kuhusu parking mjini, hivi hakuna wakala au taasisi au chombo kinachoratibu ubora wa majengo? Kwanini majengo yajengwayo town, kariakoo nk hayana Parking?. Kweli tunahitaji mzungu aje atwambie hili?.

Hoja za Paul ni nzuri. Fly overs zinakuja ndugu Paul. Hoja zako zote zipo kwenye pipeline!. Hoja ya majengo yenye parking city center hamna kaka maana wala rushwa washakula rushwa!

FairPlayer,Nashukuru kwa kunitendea haki ila aliyethubutu akashindwa kwa kukataa njia mbadala hatakiwi kusifiwa.....!!!
 
Ni jambo la kusikitisha na kushangaza kuona Watanzania wanashabikia matukio haya mawili la Basi ziendazo Kasi BRT
(BRT) na uzinduzi wa
Reli kwa Jiji la Dar es Salaam. Mipango hii yote inaongozwa na watu wanaojitambulisha kuwa kuwa wachapa kazi kina Magufuli na Mwakyembe.
Ukweli kwamba ni danganya toto kwa sababu zifuatazo:

1. Tatizo la msongamano wa magari halisababishwi na kuwepo kwa gari za abiria ( public transport) bali ni private cars na maroli.
2. Msongamano huu unaletwa na kwenye junctions( nodes) mf. Ubungo mataa, Shekilango, Njia panda ya Tabata, Buguruni, Magomeni Mapipa,......
na suluhisho ni fly overs.
3. Reli hizi zinaishia pafupi sana na haziondoi au kuzuia watu binafsi kwenda na magari yao.
4. Hakuna parking Dar na watu wengi hubakia barabarani wakizunguka wkt wengine walionao wanafanya issue zilizowaletra mjini.
5. Upanuaji Barabara haupunguzi foleni bali hupunguza urefu wake na kutengeneza foleni fupi yenye mistari mingi ya magari mf. barabara ya Mwenge to Ubungo kupita Mcity.
kwa msisitizo zaidi ni sawa na kuweka maji kwnye mrija wa kunywea soda ukajaa alafu na mengine ukajaza beseni na mtoto akaulizwa maji mengi yako wapi naye akachagua mrija kisa umezidi beseni kwaurefu.

Sasa hela kubwa inayotumika kutengeneza barabara za BRT na Reli ingefanya yafuatayo kama si ufisadi:
  1. kutengeneza barabara zote mbovu za kupunguza msongamano kwemye Barabara ya Moro kwa kiwango cha lami ili kupunguza kufurika kwa magari Morogoro road mf. Barabara ya Kimara na Mbezi to Uwanja wa Ndege, Kimara na Mbezi to Tegeta........
  2. kuwekeza kwenye Fly Overs kwenye mataa yote.
  3. kuboresha na kupanua barabara hasa vituo amabvyo viko barabarani hasa mf. njia ya Tandare.


MUHIMU: wATANZANIA tunapenda kushabikia mambo bila kuyachunguza na sasa tusubiri tuone jinsi hii mipango 2 isivyo na tija bali danganya toto.

ubongo uliooza
 
Wewe roho mbaya zitakuua. Mahali pa kusifiwa sifu, na mahali penye utata sema. Ukiwa kila siku negative utakuwa unaboa

huyu jamaa mpuuzi sana wenzio wamethubutu kuahidi na kutekeleza..atleast ss tunazipanda hizo train..kinachofuata ni kuziboresha na kuzifikisha maeneo yote ya pembezoni mwa mji.au unaona biashara yako ya daladala imedoda..pole tulichoka nanyi na vidaladala vyenu kukatiza route.galafu kichwa cha habari wala hakina uhusiano ba hayo uliyoyaeleza..roho mbaya tu inakusumbua na wivu wa kipuuzi
 
Mkuu Kijoka pole sana kwa kushambuliwa na watu ambao are extreme fans wa watu. Kuna msemo wa Kiingereza kuwa "never judge a book by its cover". Hawa 2 personalities Magufuri na Mwakeyembe waliwahi kuwalaghai Watanzania kwa nyakati tofauti. Magufuri became a one eyed man among the blind wakati wa serkali ya awamu ya tatu. He wasn't very briliant or hardworking but as long as his compatriots were struggling with no clear strategy yeye akawa mtu pekee kwa kusimamia ujenzi wa barabara. Na ujenzi wa barabara hauitaji akili sana maana fedha zinatolewa na wafadhili, contractor anakuwepo na consultant as well. Tena pengine wanachaguliwa kwa shinikizo la aliyekupa mkopo na wao wanafanya close monitoring. Designs wanatoa wao. Sasa wewe waziri kwanini ushindwe kusimamia even if remotely. Na pili watu wanasahau kuwa huyu aliyeonekana a king among the blind alifikiri umma wote uko katika usingizi wa pono. Aliuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa. Na leo hubaki anapiga kelele akifikiri tumesahau au anataka atusahaurishe. Bado tunakumbuka and all Mafuri does is primary objective to raise public awareness, brainwash the public, lie and manipulate the public ili tusihoji madudu. Naomba tufanye analysis in East Africa ni nchi gani ambayo costruction costs ziko juu kwa vipimo vilevile na wakati mwingine mkandarasi yuleyule. Kwa kutumia neno uhuni umetumia soft terms sana. ingekuwa mimi ningetumia neno baya mno.

Mwakyembe naye a bird of the same feather. Akitumiwa na walio na personal vendetta alihakikisha anamg'oa Lowasa kwenye wadhifa wa waziri mkuu basi. Yale anayosema walificha kuilinda serikali yanatutesa mpaka hii leo. Hiwezekani mchakato wa manunuzi ya umma unaeleweka na unalindwa kwa sheria, halafu ati waziri mkuu aende kinyume na wanaosimamia sheria wapo, wanaoilinda wapo, aliyemeteua yupo na nchi inaingizwa katika uhuni mbaya kuwahi kushuhudiwa na leo watu wanamwona Mwakyembe shujaa. To me he such a tragic hero. When we analyse interms of value for money, what did we get as a country? Kumlipa DOWANS labda. Halafu kuna kitu ambacho akamati ay Mwakyembe hawakuwahi kukisema, wamiliki wa Richmond walikuwa hawajulikani lakini on daily basis walikuwa wanalipwa. Hizo pesa ziliingia account gani? Kama haikuwa banking transactions ziliwekwa chini ya mkuyu halafu mzimu ukaja ukazitafuna? Leo nakuja na style ya fukuzafukuza wafanyakazi mara bandari, ATC na kwingineko halafu anatutangazia. Wakati wanaajiliwa na kupewa kazi mlitutanganzia? Kama mnawajibishana fanyeni kimyakimya huko. It's non of our business kujua nani kafukuzwa. Leo tunaletewa train, katika karne hii tunadanganywa na scraps na kumabiwa ndio mkombozi wa wanyonge. Wanyonge wapo Dar peke na pale ziendako trains hizo. Hivi ni viini macho

Thanks mkuu, unajua humu kumejaa vilaza sana au watu wanaofanya kazi fulani maalumu au Wadanganyika!!! Ni jambo la kushangaza kuona zinatolewa hoja za msingi alafu watu hawasomi bali wanaishia kwa kichwa na kuropoka tu!!!! Binafsi I never and I WILL NEVER trust any leader from CCM! Think of the way JK started TRL na mbwembwe kibao alafu hawa hawa wanaojiita wanaharakati wa JF wakampigia makofi na leo yako wapi mkuu???? Unakumbuka issue ya umeme wa Dharura ya Richmond? Unakumbuka ahadi ya kutengeneza mvua toka Pakstan?......
 
kumbe unatambua kwamba foleni zinasababishwa na malori,sasa unampongeza vipi mtu ambaye hajatimiza wajibu wake? Siku akianza kufufua reli zetu,ziweze kubeba mizigo mikubwa na kusafirisha abiria kwa gharama nafuu nitampongeza.

Nikusaidie masikini maana wewe umefun gwa kwnye chupa. kwanza nikuambie maneno ya busara, ni vyema kuishi kidogo ukiwa na akili kuliko kuishi miaka mingi ukiwa mbuzi! Treni za TZ haziwezi kuendelea wakati vigogo, watoto wao wanamiliki malory ya kupeleka mzigo mkoani.
 
Sikubaliani kwa asilimia 100 na hoja ya bwana Paul ingawa mambo aliyoongea mengine ni ya msingi...kuna watu nawafahamu wanaokaa njia hzo reli zinapopita na wanafanya kazi City Centre kutokea Ubungo siku hizi hawaji na magari wanapanda Treni kwa hiyo naona inasaidia kwa kiwango fulani...halafu huu mradi wa mabasi yaendayo kasi BRT nadhani ndio utasaidia zaidi maana watu wanaenda na magari mjini kwa kuwa hakuna usafiri wa uhakika na uliopo hizi daladala sio za uhakika na zinajaza sana kiasi kwamba kama uanapandia. Kituo cha katikati ni shida sana maana basi linakuwa limejaa kupita kiasi...lakini mabasi ya BRT utakuwa na uhakika wa kuondoka kituo chako kwa muda uliopangwa na kufika safari katika muda uliopangwa...watu wengi wanakuja na magari mjini kwa kuwa usafiri sio wa uhakika na kwa hali hii ya uchumi sidhani kama kuna mtu kweli anapenda kutumia elfu 10,000 ya mafuta kila siku...
Tutafika huko lakini tuanze hapa
 
Watu kama wewe JF mmebaki wachache sana. Kamanda Paul kaandika vizuri. Ila hakua sahihi kuwabeza akina Mwakyembe. Magufuli na Mwakyembe wamethubutu hawajaweza. Ila well done Mwakyembe na Magufuli.

Kuhusu parking mjini, hivi hakuna wakala au taasisi au chombo kinachoratibu ubora wa majengo? Kwanini majengo yajengwayo town, kariakoo nk hayana Parking?. Kweli tunahitaji mzungu aje atwambie hili?.

Hoja za Paul ni nzuri. Fly overs zinakuja ndugu Paul. Hoja zako zote zipo kwenye pipeline!. Hoja ya majengo yenye parking city center hamna kaka maana wala rushwa washakula rushwa!

Mkuu FP.....heshima mbele,

hilo suala la fly overs.....Mkuu paul kazungumza jambo ambalo mara kadha wa kadha limejadiliwa sana hapa JF......na wal sio geni...........lakini kitendo chake cha kubeza juhudi za Mwakyembe na Magufuli.......leaves alot to be desired na UELEWA wake..........

najua wewe ni Mchumi.......kumbukeni any investments should have a meaningful returns........hatuwezi kuendelea kujenga/kupanua mabarabara kila kukicha.......na watu waendelee kununua magari kila kukicha............wherever possible other means should be explored..........

kwenye Metropolitan kibao.....a reliable and efficient Public Transport is the way to go.....nina hakika unalifahamu vizuri suala hilo............unaweza kuwa na ma-fly over hata mia moja......na bado ukawa na congestion...........
 
Ni jambo la kusikitisha na kushangaza kuona Watanzania wanashabikia matukio haya mawili la Basi ziendazo Kasi BRT
(BRT) na uzinduzi wa
Reli kwa Jiji la Dar es Salaam. Mipango hii yote inaongozwa na watu wanaojitambulisha kuwa kuwa wachapa kazi kina Magufuli na Mwakyembe.
Ukweli kwamba ni danganya toto kwa sababu zifuatazo:

1. Tatizo la msongamano wa magari halisababishwi na kuwepo kwa gari za abiria ( public transport) bali ni private cars na maroli.
2. Msongamano huu unaletwa na kwenye junctions( nodes) mf. Ubungo mataa, Shekilango, Njia panda ya Tabata, Buguruni, Magomeni Mapipa,......
na suluhisho ni fly overs.
3. Reli hizi zinaishia pafupi sana na haziondoi au kuzuia watu binafsi kwenda na magari yao.
4. Hakuna parking Dar na watu wengi hubakia barabarani wakizunguka wkt wengine walionao wanafanya issue zilizowaletra mjini.
5. Upanuaji Barabara haupunguzi foleni bali hupunguza urefu wake na kutengeneza foleni fupi yenye mistari mingi ya magari mf. barabara ya Mwenge to Ubungo kupita Mcity.
kwa msisitizo zaidi ni sawa na kuweka maji kwnye mrija wa kunywea soda ukajaa alafu na mengine ukajaza beseni na mtoto akaulizwa maji mengi yako wapi naye akachagua mrija kisa umezidi beseni kwaurefu.

Sasa hela kubwa inayotumika kutengeneza barabara za BRT na Reli ingefanya yafuatayo kama si ufisadi:
  1. kutengeneza barabara zote mbovu za kupunguza msongamano kwemye Barabara ya Moro kwa kiwango cha lami ili kupunguza kufurika kwa magari Morogoro road mf. Barabara ya Kimara na Mbezi to Uwanja wa Ndege, Kimara na Mbezi to Tegeta........
  2. kuwekeza kwenye Fly Overs kwenye mataa yote.
  3. kuboresha na kupanua barabara hasa vituo amabvyo viko barabarani hasa mf. njia ya Tandare.


MUHIMU: wATANZANIA tunapenda kushabikia mambo bila kuyachunguza na sasa tusubiri tuone jinsi hii mipango 2 isivyo na tija bali danganya toto.

Tatizo la wabongo kila mtu anajifanya anajua, kama umeridhika na hali ya daladala na kuona mradi wa mabasi ni upotevu wa hela, sina la kuchangia, time will tell..

Ninachojua mimi serikali inatambua kuhusu kutengeneza barabara za pembezoni na imeshaanza na inaendelea kutengeneza. Haiwezekani kutengeneza zote kwa wakati mmoja
 
Simple! Ndugu Paul Kijoka amka mapema uende pale ubungo maziwa ukawaeleweshe waTZ wenzio ndani ya treni au wanaosubiri treni kwamba hicho "WANACHOSHABIKIA" ni "UHUNI". Then uje utupe majibu!

hawezi kwenda hata kwa kutania na akithubutu atapata kipigo cha paka mwizi haya maneno yake yaishie hapahapa jf
 
Watz tunafuata mkumbo na kushobokea mambo ya kijinga sana bila kutafakari ndio maana kwa kuongozwa na serikali nzima ya Dhaifu baba Riz1 (na mama Riz1 of course) tulikimbilia Loliondo kwa gharama kuuuuubwa kunywa kikombe cha kipuuzi cha babu.
Hiyo miradi miwili kama sio ya kuondoa msongamano wa magari ni ya nini? kwa sababu haiwezi kuondoa misongamano
Huyu ndugu yetu katufungua macho, wanachofanya ni usanii mtupu, ni miradi isiyo na maana au ina maana kidogo saaaana hivyo siyo ya kupongeza kihivyo
 
Mwakyembe na Magufuli ni watu wa kupongezwa na kupigiwa mfano, wao wameweka mile stone na wewe na mimi tuvute kuelekea mbele tutakapofika ndio kipimo chenyewe. Manake hakukuwa na bench mark, kiukweli kutoka moyoni kabisa nimefarijika sana baada ya kupanda train leo kutoka matumbi mpaka kamata na nimekumbuka mbali saaana, yaani enzi hizo tunaenda Tabora tukifunga school kwa wale wa Tambaza in 1994 watakumbuka zaidi.

Na nikiona vituo vya mabasi yanendayo kasi inanikumbusha mwaka jana nilikuwa J'burg nilipanda mabasi hayo na soon itakuwa bongo. We all know that mengi yanatakiwa kufanyika sasa na hayo ni machache tuwape moyo ili wafanye mengi zaidi tuendembele. Mkianza tena kupiga politike tutakwama watata, Just do it! do it! kusema imetosha na tuwape na nafasi hata ya kukosea ndio kujifunza kwenyewe.
 
Next time uje na title inayoendana na maelezo yako.
Mimi siyo CCM ila umenishangaza sana na utoaji wako wa hoja.
Nadhani una maslahi binafsi katika hoja zako.
Treni la Mwakyembe ni moja ya suluhisho ya kero za daladala na foleni za mjini. Usafiri wa daladala haujitoshelezi na mahitaji yetu.
 
Ni jambo la kusikitisha na kushangaza kuona Watanzania wanashabikia matukio haya mawili la Basi ziendazo Kasi BRT
(BRT) na uzinduzi wa
Reli kwa Jiji la Dar es Salaam. Mipango hii yote inaongozwa na watu wanaojitambulisha kuwa kuwa wachapa kazi kina Magufuli na Mwakyembe.
Ukweli kwamba ni danganya toto kwa sababu zifuatazo:

1. Tatizo la msongamano wa magari halisababishwi na kuwepo kwa gari za abiria ( public transport) bali ni private cars na maroli.
2. Msongamano huu unaletwa na kwenye junctions( nodes) mf. Ubungo mataa, Shekilango, Njia panda ya Tabata, Buguruni, Magomeni Mapipa,......
na suluhisho ni fly overs.
3. Reli hizi zinaishia pafupi sana na haziondoi au kuzuia watu binafsi kwenda na magari yao.
4. Hakuna parking Dar na watu wengi hubakia barabarani wakizunguka wkt wengine walionao wanafanya issue zilizowaletra mjini.
5. Upanuaji Barabara haupunguzi foleni bali hupunguza urefu wake na kutengeneza foleni fupi yenye mistari mingi ya magari mf. barabara ya Mwenge to Ubungo kupita Mcity.
kwa msisitizo zaidi ni sawa na kuweka maji kwnye mrija wa kunywea soda ukajaa alafu na mengine ukajaza beseni na mtoto akaulizwa maji mengi yako wapi naye akachagua mrija kisa umezidi beseni kwaurefu.

Sasa hela kubwa inayotumika kutengeneza barabara za BRT na Reli ingefanya yafuatayo kama si ufisadi:
  1. kutengeneza barabara zote mbovu za kupunguza msongamano kwemye Barabara ya Moro kwa kiwango cha lami ili kupunguza kufurika kwa magari Morogoro road mf. Barabara ya Kimara na Mbezi to Uwanja wa Ndege, Kimara na Mbezi to Tegeta........
  2. kuwekeza kwenye Fly Overs kwenye mataa yote.
  3. kuboresha na kupanua barabara hasa vituo amabvyo viko barabarani hasa mf. njia ya Tandare.


MUHIMU: wATANZANIA tunapenda kushabikia mambo bila kuyachunguza na sasa tusubiri tuone jinsi hii mipango 2 isivyo na tija bali danganya toto.

Watu kama nyie huwa hamkosekani! Tupishe tupite
 
Back
Top Bottom