Kama hivi ndivyo ilivyo muda wowote dr. Ulimboka atatutoka duniani, baba yake aangua kilio.

Siku moja baada ya Serikali kutangaza kutumia hospitali za Jeshi na madaktari wastaafu kunusuru afya za wagonjwa kufuatia mgomo wa madaktari nchini, juhudi zaidi zimechukuliwa na sasa itatumia pia hospitali binafsi.

Hospitali zilizotajwa kukubali kushirikiana na Serikali kutoa huduma za afya kwa watakaohitaji tiba ya haraka na walio katika tiba isiyoweza kusitishwa ni pamoja na TMJ, Regency, Aga Khan, Hindu Mandal, CCBRT na Hospitali ya Jeshi Lugalo.

Aidha, nguvu zimeongezwa katika hospitali za Mwananyamala, Amana na Temeke za Dar es Salaam kunakodaiwa hakuna mgomo, ili kutotoa rufaa nyingi kwa wagonjwa kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kunakodaiwa kuwa na mgomo.
Na sisi wa huku Tandahimba tutaenda hospitali gani?

Huko nako kuna mgomo (Tandahimba)
 
Na endapo akifa viongozi wa taifa wasikanyage kwenye msiba wake kabisa. Huu ni ujinga unaofanywa na serikali badala ya kushughulikia mgomo wanashughulikia watu!!!!

Madai yao ni ya msingi sana na yanapaswa kutekelezwa. Walimu mko wapi na nyie?????
 
Sisi tumefiwa na vichanga vyetu baada hospitali hapa nchini kukosa vacuum pump ya kuvuta maji machafu ambayo vichanga humeza wakati wa zoezi la mama kujifungua na kuziba njia za hewa. Pampu hiyo huuzwa Shs 5,000/= tu. Posho za kukaa ambazo maafisa waandamizi wa Serikali ya CCM hulipana ya Shs 200,000/= kwa kila kikao, hata kama ni kuhudhuria kikao mlango wa pili toka ofisi zao ingetosha kununua pampu 40 kama hizo na kukoa maisha ya vichanga hizi. Je ni akina mama wangapi wamepoteza vichanga vyao baada ya kubeba mimba miezi 9 kwa kukosekana kifaa hiki?

Sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa kukosekana sindano ya kuingiza maji ya dripu mwilini inayouzwa shs 250/= tu.

Jana katika tarifa ya habari ya ITV akina wawili waliopata ajali ya pikipiki na kukanyagwa na gari kubwa wametelekezwa katika vitanda vya hospitali ya Bombo Tanga wakingoja kupoteza maisha kwa sababu hospitai hiyo haina kifaa cha kupiga picha za X-ray, madakatari walikuwepo lakini hawakuweza kuwapatia huduma kwa wagonjwa wanalazimka kuwa na fedha za kuhamishiwa katika hospitali binafsi kupiga picha hizo. Gharama ya shangingi moja wanalopanda maafisa waandamizi wa CCM na Serikali yake zingetosha kuzipatia hospitali 3 vifaa vya aina hiyo. Je ni watanzania wangapi hupoteza maisha kila siku kwa kukosekana vifaa vya X-ray, Ultra sound, CT scan n.k katika hospitalia ilihali mashangingi yanannunuliwa kila mwaka na fedha Serikali ya CCM hutenge mabilioni kwa ajili ya kulipana posho za kukaa na safari zisizo na tija?

Katika madai yao madakatari wamesema wamechoka kuwaona watanzania wenzao wakipoteza maisha kimya kimya kwa kukosekana vifaa muhimu vya matibabu ilihali nchi ikisamehe Dola Bilioni kama kosi. Kuanzia sasa ni vyema idadi ya watanzania wanaopoteza maisha ikaanza kuwekwa wazi na sababu zake,

ukweli 100%
 
BABA wa Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Madaktari, mzee Steven
Mwaitenda amejikuta akiangua
kilio kwa uchungu mbele ya
wanaharakati ambao
walimtembelea mwanae, Dk.
Steven Ulimboka kumpa pole
kufuatia tukio la kutekwa na
kujeruhiwa vibaya na watu
wasiojulikana.
Hali hiyo ilitokea jana jioni katika
Taasisi ya Tiba ya Mifupa
Muhimbili (MOI), ambapo
wanaharakati kutoka taasisi na
asasi mbalimbali za utetezi wa
haki za binadamu walifika kwa
lengo la kumpa pole Dk. Ulimboka
kufuatia kitendo kilichomfika.
Mzee Mwaitenda alijikuta
akibubujikwa na machozi na
kushindwa kuendelea
kuzungumza alipokuwa akitoa
shukrani kwa wanaharakati hao,
kwa niaba ya mwanaye ambaye
wanaharakati hao walishindwa
kumuona wote kutokana na hali
yake ilivyo sasa.
“Niseme wazi nimefarijika sana
kwa ujio wenu kumwona
mwanangu dhidi ya mambo ya
kikatili aliyofanyiwa akitetea haki
za wengine…,” alisema mzee
Mwaitenda kabla ya kushindwa
kuendelea na kuangua kilio mbele
ya wanaharakati.
Baada ya tukio hilo baadhi ya
wanaharakati walimshika
wakishirikiana na wanafamilia ya
mzee Mwaitenda na kumbebeleza
kisha kumtoa mbele ya
mkusanyiko huo wa
wanaharakati na kumrudisha
wodini huku wakimfariji.
Wakizungumza mara baada ya
tukio hilo wanaharakati
wameelezea kusikitishwa na
vitendo vinavyoendelea MOI eneo
ambalo amelazwa kiongozi huyo
wa madaktari ambavyo
vimeendelea kutishia usalama wa
Dk. Ulimboka.
Akifafanua zaidi mwakilishi wa
wanaharakati hao, Markos Albania
alisema taarifa walizozipata usiku
wa juzi kuna wagonjwa ‘feki’
ambao walijitokeza MOI huku
wakitaka kulazwa wodi ya
Wagonjwa Mahututi (ICU)
alipolazwa Dk. Ulimboka lakini
baadaye waligoma kuingizwa
wodini.
“Wapo wagonjwa ambao
waliletwa na kutaka kupelekwa
ICU moja kwa moja…kuna watu
wanakuja usiku wa manane
wakitaka kumtembelea Dk.
Ulimboka…matendo
yanayoendelea kutokea
ukilinganisha na kauli za Serikali
zilizotolewa bungeni yanatishia
usalama na uhai wa mgonjwa,”
alisema Albania.
Aidha amesema kitendo cha
vyombo vya usalama kuendelea
kumuhoji Dk. Ulimboka akiwa hoi
hospitalini si vya kiungwana
kwani tayari muhusika amewataja
hadi kwa majina watu ambao
anawashuku lakini hadi sasa
hakuna aliyechukuliwa hatua
yoyote.
Pamoja na hayo wanaharakati
hao wameitaka Serikali kuunda
tume huru mchanganyiko na raia
ambayo itachunguza kiundani
suala hilo, kwani hawana imani
na Jeshi la Polisi ambalo limedai
kuunda timu ambayo
inachunguza kwa kina suala hilo.
Dk. Ulimboka ambaye ni kiongozi
wa madaktari ambao
wanaendelea na mgomo wan chi
nzima kuishinikiza Serikali
kutekeleza madai yao alitekwa
juzi na watu wasiojulikana na
kupigwa na kuteswa kikatili kabla
ya kutelekezwa katika msitu wa
Mabwepande.
*Habari hii imeandaliwa na
kuletwa hapa na Mtandao wa
Thehabari.com


Kichwa cha hii thread ni kama kina ushetani ndani yake, sioni kama kwenye hii habari kuwa madaktari wanasema Dr Ulimboka ana hali mbaya karibia ya kufa. Nadhani tuache kuwa nusu ibilisi kwenye hoja zinazogusa uhai wa watu wengine. Ni wakati wa kuendelea kumuombea na kumtakia wepesi kamanda Ulimboka kwa mwenyezi Mungu, na Mungu atamponya na kumrudisha tuendelee na mapambano ya kuwang'oa wakoloni weusi. Get well soon Kamanda Dr Ulimboka.
 
we punguwani nini?sasa ndugu zako wanatuhusu nini sisi?

Wewe kigogo ndio punguani kuliko wote waliowahi kujulikana.Sasa kama ndugu ,jamaa na watanzania wengine wanaopoteza maisha kwa sababu ya mgomo HAWAWAHUSU,unadhani huyo Dr Ulimboka anamhusu nini Do Santoz?Kwangu mimi Dr Ulimboka ni mwanataaluma mwenzangu,achilia mbali kusoma nae pale palipokuwa MUCHS,jibu lako kwa Do Santoz ni la kihuni.Kwa hiyo na wewe unaunga mkono watanzania kufa kwa kukosa huduma kwa vile madaktari wamegoma?Nasikia uchungu watanzania wenzetu kufa wakati madaktari wamegoma lkn NAPINGA NA KUKEMEA UTEKAJI UNYANYASAJI NA UTELEKEZAJI WA DR ULIMBOKA.Na kwangu mimi mazungumzo na serikali tuyape nafasi.
 
MUNGU atamtetea,kwani sauti ya watu ni sauti ya MUNGU!!!!!
Dr alikuwa akitetea maslahgi ya wote;kwani madaktari watakapotimiziwa haja zao,basi huduma mahospitalini zitaboreka na wananchi wote tutanufaika kwa hili!!!!
 
Mlaumuni Kikwete kwa kushindwa kutatua kero za madaktari.
Hivi ni akili kweli kutumia Bilioni 200 kwa ajili ya kukodi madaktari ughaibuni? Kwanini hiyo hela isingetumika kutatua kero za madaktari wa hapa nchini?
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

watu wenye mawazo km yako,siku ukifa tukisha kuzika,juu ya kaburi tunachapa kiboko kuashiria level ya upumbavu na mawazo mfu km yako.
 
Nakupa 100%
Hawa wagonjwa wanafia nyumbani kwa madaktar? Kama wanafia nyumbani kwao basi wao ndio wauaji then hizi hospitali ni za madaktari au za serekali?ukipata jibu hapa nadhani utajua muuaji ni nani?
 
natamani watanzania wenzangu mngekijua kile ambacho Dr Ulimboka anachokipigania katika hospitali zetu, naamini wengi wetu hapa tumeshawahi kupata huduma katika hospitali mbalimbali za Tanzania esp zile za serikai MNH ikiwepo pia, how many times unaenda unaambiwa x-ray haifanyi kazi ama dawa fulani hakuna kanunue sehemu fulani? kiukweli mazingira ya kufanyia kazi hospitali ni magumu sana watoa huduma wanatoa huduma katika mazingira magumu, mama zetu wangapi wanaenda kujifungua anaambiwa kanunue gloves? naumia sana tena tena sana na nina machungu sana kwa hiki kinachotokea hapa kwetu
 
Kauli zako hazitofautiani sana na mabosi zako
1. Wasichana wanaopata mimba wakiwa mashuleni ni viherehere vyao
2. Wanaoua albino nao wauwawe
3. Liwalo na liwe
4. Kama upinzani wanasikia uchungu na hii nchi waende leba wakazae
5. Kudadadeki

Kumbe wao ccm hawana uchungu na hii nchi ndo maana wanayafanya yote haya!
 
Mungu awahurumie wale wote ambao hawajaelewa kuwa mgomo wa madaktari, ni utetezi wa watanganyika. Mungu awahurumie wale wote wanaodhani kilio chao ni kwa ajili ya manufaa yao. Mungu awahurumie wanao ona kuwa madaktari hawakustahiri kuishinikiza serikali kuboresha mazingira ya kazi. Eeeeh Mwenyezi Mungu, wahurumie.
 
Asante Doctor. Ufafanuzi kama huu utasaidia watanzania wasiowaelewa kufahamu kuwa ni serikali inayogoma kutuhudumia.
 
Sisi tumefiwa na vichanga vyetu baada hospitali hapa nchini kukosa vacuum pump ya kuvuta maji machafu ambayo vichanga humeza wakati wa zoezi la mama kujifungua na kuziba njia za hewa. Pampu hiyo huuzwa Shs 5,000/= tu. Posho za kukaa ambazo maafisa waandamizi wa Serikali ya CCM hulipana ya Shs 200,000/= kwa kila kikao, hata kama ni kuhudhuria kikao mlango wa pili toka ofisi zao ingetosha kununua pampu 40 kama hizo na kukoa maisha ya vichanga hizi. Je ni akina mama wangapi wamepoteza vichanga vyao baada ya kubeba mimba miezi 9 kwa kukosekana kifaa hiki?Sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa kukosekana sindano ya kuingiza maji ya dripu mwilini inayouzwa shs 250/= tu.Jana katika tarifa ya habari ya ITV akina wawili waliopata ajali ya pikipiki na kukanyagwa na gari kubwa wametelekezwa katika vitanda vya hospitali ya Bombo Tanga wakingoja kupoteza maisha kwa sababu hospitai hiyo haina kifaa cha kupiga picha za X-ray, madakatari walikuwepo lakini hawakuweza kuwapatia huduma kwa wagonjwa wanalazimka kuwa na fedha za kuhamishiwa katika hospitali binafsi kupiga picha hizo. Gharama ya shangingi moja wanalopanda maafisa waandamizi wa CCM na Serikali yake zingetosha kuzipatia hospitali 3 vifaa vya aina hiyo. Je ni watanzania wangapi hupoteza maisha kila siku kwa kukosekana vifaa vya X-ray, Ultra sound, CT scan n.k katika hospitalia ilihali mashangingi yanannunuliwa kila mwaka na fedha Serikali ya CCM hutenge mabilioni kwa ajili ya kulipana posho za kukaa na safari zisizo na tija?Katika madai yao madakatari wamesema wamechoka kuwaona watanzania wenzao wakipoteza maisha kimya kimya kwa kukosekana vifaa muhimu vya matibabu ilihali nchi ikisamehe Dola Bilioni kama kosi. Kuanzia sasa ni vyema idadi ya watanzania wanaopoteza maisha ikaanza kuwekwa wazi na sababu zake,
asante doctor (bila shaka) kwa ufafanuzi mzuri. Watanzania wakielezwa namna hiyo wataelewa kuwa anaegoma kutoa huduma zote (si afya tu) ni serikali yetu iliyofikia ukomo ktk upeo wake.
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

Yaani una maana mtu akikataa kufanya kazi yake adhabu ni kifo?
 
Back
Top Bottom