Kama hivi ndivyo ilivyo muda wowote dr. Ulimboka atatutoka duniani, baba yake aangua kilio.

Nashauri watu wanapoanzisha mada yoyote waweke 'titles' zinazobeba ujumbe uliopo na siyo kujaribu kuvuta hisia. Tusimwumbie daktari hisia na hofu zetu. Tuache madaktari wanaomtibu ndiyo waeleze maendeleo ya mgonjwa na siyo kila mtu kurusha hewani kitu anachohisi au kuwaza. Iwapo tunaamini ukuu na uweza wa Mungu aliyekuwa naye tangu mwanzo, basi tuache kutangaza hofu zetu.
 
Siku moja baada ya Serikali kutangaza kutumia hospitali za Jeshi na madaktari wastaafu kunusuru afya za wagonjwa kufuatia mgomo wa madaktari nchini, juhudi zaidi zimechukuliwa na sasa itatumia pia hospitali binafsi.

Hospitali zilizotajwa kukubali kushirikiana na Serikali kutoa huduma za afya kwa watakaohitaji tiba ya haraka na walio katika tiba isiyoweza kusitishwa ni pamoja na TMJ, Regency, Aga Khan, Hindu Mandal, CCBRT na Hospitali ya Jeshi Lugalo.

Aidha, nguvu zimeongezwa katika hospitali za Mwananyamala, Amana na Temeke za Dar es Salaam kunakodaiwa hakuna mgomo, ili kutotoa rufaa nyingi kwa wagonjwa kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kunakodaiwa kuwa na mgomo.
Na sisi wa huku Tandahimba tutaenda hospitali gani?
 
Siku moja baada ya Serikali kutangaza kutumia hospitali za Jeshi na madaktari wastaafu kunusuru afya za wagonjwa kufuatia mgomo wa madaktari nchini, juhudi zaidi zimechukuliwa na sasa itatumia pia hospitali binafsi.

Hospitali zilizotajwa kukubali kushirikiana na Serikali kutoa huduma za afya kwa watakaohitaji tiba ya haraka na walio katika tiba isiyoweza kusitishwa ni pamoja na TMJ, Regency, Aga Khan, Hindu Mandal, CCBRT na Hospitali ya Jeshi Lugalo.

Aidha, nguvu zimeongezwa katika hospitali za Mwananyamala, Amana na Temeke za Dar es Salaam kunakodaiwa hakuna mgomo, ili kutotoa rufaa nyingi kwa wagonjwa kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kunakodaiwa kuwa na mgomo.
Na sisi wa huku Tandahimba tutaenda hospitali zipi?
 
Mwenyezi Mungu alikuwa pamoja nawe Dr Ulimboka ucku ule wa tukio, ataendelea kuwa pamoja kupambana ktk kupona kwako, na yupo pamoja na wale wote wapambanaji dhidi ya hao wapinga Haki kwa Watanzania.

Tupo pamoja Dr Ulimboka, Wanaharakati wote, Madaktari wote, Family ya Dr Ulimboka na Watanzania wote ktk hizi harakati tufanikiwe ktk Tiba ya Dr, na pia kupambana ktk kuleta Ukombozi wa kweli kwa Taifa la Tanzania dhidi ya Udhalimu wa aina yeyote.

vita hii twapaswa kumsaidia wote.
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

lazima una fistula ya ubongo
 
Kwa hali hii lazima wahuni wa taifa wanaojiita usalama watamuua Dr. Ulimboka ili wafute ushahidi.
Pinda una sababu zipi za wewe kushindwa kujiuzulu coz wewe ndiyo umewatuma hawa watu na bado unawatuma waende ICU wakammtoe Uhai Dr. Ulimboka.
J. Kikwete nchi imekushinda jiuzulu, kama madaktari tu wamekutoa kamasi ni kipi utaweza? ? Au kutuma wahuni kupiga Dr. Ulimboka ndiyo umeona umetatua tatizo?
Muda si mrefu itakuwa vice versa.
Vita mnavikaribisha wenyewe
 
Sisi tumefiwa na vichanga vyetu baada hospitali hapa nchini kukosa vacuum pump ya kuvuta maji machafu ambayo vichanga humeza wakati wa zoezi la mama kujifungua na kuziba njia za hewa. Pampu hiyo huuzwa Shs 5,000/= tu.

Watanabe,

Wewe umeona kifaa cha hospitali ni hiyo vacuum tu peke yake?
 
Sisi tumefiwa na vichanga vyetu baada hospitali hapa nchini kukosa vacuum pump ya kuvuta maji machafu ambayo vichanga humeza wakati wa zoezi la mama kujifungua na kuziba njia za hewa. Pampu hiyo huuzwa Shs 5,000/= tu. Posho za kukaa ambazo maafisa waandamizi wa Serikali ya CCM hulipana ya Shs 200,000/= kwa kila kikao, hata kama ni kuhudhuria kikao mlango wa pili toka ofisi zao ingetosha kununua pampu 40 kama hizo na kukoa maisha ya vichanga hizi. Je ni akina mama wangapi wamepoteza vichanga vyao baada ya kubeba mimba miezi 9 kwa kukosekana kifaa hiki?

Sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa kukosekana sindano ya kuingiza maji ya dripu mwilini inayouzwa shs 250/= tu.

Jana katika tarifa ya habari ya ITV akina wawili waliopata ajali ya pikipiki na kukanyagwa na gari kubwa wametelekezwa katika vitanda vya hospitali ya Bombo Tanga wakingoja kupoteza maisha kwa sababu hospitai hiyo haina kifaa cha kupiga picha za X-ray, madakatari walikuwepo lakini hawakuweza kuwapatia huduma kwa wagonjwa wanalazimka kuwa na fedha za kuhamishiwa katika hospitali binafsi kupiga picha hizo. Gharama ya shangingi moja wanalopanda maafisa waandamizi wa CCM na Serikali yake zingetosha kuzipatia hospitali 3 vifaa vya aina hiyo. Je ni watanzania wangapi hupoteza maisha kila siku kwa kukosekana vifaa vya X-ray, Ultra sound, CT scan n.k katika hospitalia ilihali mashangingi yanannunuliwa kila mwaka na fedha Serikali ya CCM hutenge mabilioni kwa ajili ya kulipana posho za kukaa na safari zisizo na tija?

Katika madai yao madakatari wamesema wamechoka kuwaona watanzania wenzao wakipoteza maisha kimya kimya kwa kukosekana vifaa muhimu vya matibabu ilihali nchi ikisamehe Dola Bilioni kama kosi. Kuanzia sasa ni vyema idadi ya watanzania wanaopoteza maisha ikaanza kuwekwa wazi na sababu zake,

well said!
 
Sisi tumefiwa na vichanga vyetu baada hospitali hapa nchini kukosa vacuum pump ya kuvuta maji machafu ambayo vichanga humeza wakati wa zoezi la mama kujifungua na kuziba njia za hewa. Pampu hiyo huuzwa Shs 5,000/= tu. Posho za kukaa ambazo maafisa waandamizi wa Serikali ya CCM hulipana ya Shs 200,000/= kwa kila kikao, hata kama ni kuhudhuria kikao mlango wa pili toka ofisi zao ingetosha kununua pampu 40 kama hizo na kukoa maisha ya vichanga hizi. Je ni akina mama wangapi wamepoteza vichanga vyao baada ya kubeba mimba miezi 9 kwa kukosekana kifaa hiki?

Sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa kukosekana sindano ya kuingiza maji ya dripu mwilini inayouzwa shs 250/= tu.

Jana katika tarifa ya habari ya ITV akina wawili waliopata ajali ya pikipiki na kukanyagwa na gari kubwa wametelekezwa katika vitanda vya hospitali ya Bombo Tanga wakingoja kupoteza maisha kwa sababu hospitai hiyo haina kifaa cha kupiga picha za X-ray, madakatari walikuwepo lakini hawakuweza kuwapatia huduma kwa wagonjwa wanalazimka kuwa na fedha za kuhamishiwa katika hospitali binafsi kupiga picha hizo. Gharama ya shangingi moja wanalopanda maafisa waandamizi wa CCM na Serikali yake zingetosha kuzipatia hospitali 3 vifaa vya aina hiyo. Je ni watanzania wangapi hupoteza maisha kila siku kwa kukosekana vifaa vya X-ray, Ultra sound, CT scan n.k katika hospitalia ilihali mashangingi yanannunuliwa kila mwaka na fedha Serikali ya CCM hutenge mabilioni kwa ajili ya kulipana posho za kukaa na safari zisizo na tija?

Katika madai yao madakatari wamesema wamechoka kuwaona watanzania wenzao wakipoteza maisha kimya kimya kwa kukosekana vifaa muhimu vya matibabu ilihali nchi ikisamehe Dola Bilioni kama kosi. Kuanzia sasa ni vyema idadi ya watanzania wanaopoteza maisha ikaanza kuwekwa wazi na sababu zake,

Nakupa 100% mkuu! Huyo zuzu hapo juu hajui anachokiongea!
 
acheni kulalama na kutafuta huruma za watz,huyo hajafa sisi tumefiwa na ndugu zetu kwa mgomo wao hamkuona kugoma kwao ni kitendo kisicho cha kiungwana? hali ya kuwa wapo wagonjwa mahututi? na tena wanataabika.mbona hamkuwahimiza kuwatibu wagonjwa wanaoteseka.Acheni ahojiwe hata kama anaumwa,ili ajue uchungu wanaopata wale wagonjwa wakati wao wamegoma kuwatibia.Pumbav

Waliokufa kwa mgomo wa daktari ni wachache kuliko wanaokufa miaka nenda rudi kwa vifaa vitendea kazi duni ktk mahospitali nchini. Mifaano ni mingi ikiwapo ya kutokuwa na vyanzo vya umeme vya kuaminika mfaani wagonjwa wanaopumua kupitia vifaa maalum wamekuwa wakipoteza maisha mara umeme unapokatika. Kuna watoto wanazaliwa wanaopata matatizo wakati wa kuzaliwa mfaano kunywa majimaji hakuna vifaa vya kuwasaidia na hii madaktari kwao inasumbua kuona mtu anakufa wakati kulikuwa na uwezekano wa kuokoa uhai.
 
huyo dokta ulimboka akipoteza uhai serekali na ccm mtapitia kwenye wakati mgumu ambao hamjawahi pitia tangu kuumbwa kwa tanganyika


Huu sasa ndio tunao semaga ni umajinuni, kwani yeye ndio wa kwanza kufa? unajua idadi ya wanao kufa kwa sasa kwa upuuzi wake wa mgomo?
 
Inatia huzuni sana, Dr. Ulimboka amewasili airport na ambulance ili kuelekea nje ya nchi kwa ajili ya matibabu zaidi
 
huu sasa ndio tunao semaga ni umajinuni, kwani yeye ndio wa kwanza kufa? Unajua idadi ya wanao kufa kwa sasa kwa upuuzi wake wa mgomo?
wameanza kumpopoa rais wa nec...kikwete.....tu
namsubiri rais wetu dr slaa arudi..rais wa watanzania wote
 
Huyo Mzee ajiulize, kuna wagonjwa wangapi ambao wazee wao, mama zao, ndugu zao, watoto zao, rafiki zao, wanabubujikwa na machozi kwa kukosa huduma kwa kuwa mwanawe ni kibaraka wa vikundi visivyoitakia mema Tanzania.

Damu na mateso ya binaadam, kwa huyo kijana kujitakia mafanikio kidogo ya kidunia huwa haipotei bure (huyo kafanya dhulma kubwa sana kwa binaadam wengi sana). Simuonei huruma hata kidogo.

Mzee, fikiri! kama uonavyo wewe uchungu kuna wengi kama wewe wanaona huohuo uchungu kwa kukosa matibabu na au kwa wawapendao kukosa matibabu.
 
Watanabe,

Wewe umeona kifaa cha hospitali ni hiyo vacuum tu peke yake?

Mimi sio mtaalamu wa tiba ila ninanukuu kauli za madakatari, ikiwa Serikali hii dhaifu inashandwa kuzipatia hospitali kifa cha Shs 5,000/= itaweza vipi kuzipatia hospiatali kama ya Bombo tanga x-ray Machine?
 
Back
Top Bottom