Kama haki itatendeka ndani ya CC ya CCM, Dkt Salim A Salim ndie Rais bora ajaye

Salim Ana fit hata Mimi nitampigia kura atasaidia sana kujenga muundo wa muungano na katiba
 
MAHANJU

Sorry, He would have been in 2005. He would have done a better job. He is not what he was in 2005 and furthermore, I doubt his resolve to root out mega corruption and deal with the whales and sharks. Tunahitaji mfumo mzima uwe overhauled ili kujenga institutions. Sioni kwenye CCM atakayeanza kwa kuifuta katiba pendekezwa ambayo ndiyo chanzo cha matatizo.

Umenena yote mkuu.

Fursa ya Salim kuongoza taifa ilishapotea tayari. WaTanzania wa leo wanahitaji kiongozi mkakamavu ambaye atakuwa tayari kuwa muhanga wa vita ya ufisadi na hilo silioni kwa SAS.

SAS amekuwa muoga mno hata kukemea mambo ambayo sivyo ndivyo kwenye chama na serikali yake. Sasa mtu asiyeweza kutetea mambo madogo atawezaje kukemea au kubadilisha mfumo wa kulindana na hatarishi kwa mustakabali wa maisha ya mTanzania wa leo?
 
Kwa mazingira ya siasa za sasa ambapo waislam wamekuwa wakiandamwa na maadui wa taifs hili hasa wale wanaoona kuwa wenye dini yao tu ndo wanastahili kuongoza, sioni nafasi ya Salim kwenye mfumo huu dhalimu. Pia kuna kautamaduni ka kubalilishana baina ya Waislam na Wakristo katika nafasi ya Urais. Ni utamaduni mzuri japo una kasoro zake

Ndugu yangu Lizaboni, hako ka mfumo sio rasmi na hakana maana, kinachotakiwa sio Shehe au Mchungaji/padri anatafutwa RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kiongozi aliyebora ni zaidi ya mwislam na mkristu.
 
Dr. Salim simpingi ila muda umeisha. Nchi hii ya wezi, mafisadi tena papa wehu kibao. Anatakiwa rais anaefanana na Edward Sokoine au Augustin Mrema wa 1990 na 1995. Nchi hii haiitaji tena uswahili na uswahiba.
 
Wasalaam wanajukwaa!

Nadhani kila mtu anamjua huyu mwanamapinduzi,mwanadiplomasia aliyebobea wa siasa za kitaifa na kimataifa,Waziri mkuu mstaafu, katibu mkuu mstaafu wa Umoja wa Africa(AU),Mtumishi wa umma wa miaka mingi asiyekua na doa katika uongozi wake!

Huyu ni kiongozi aliyewahi kutia nia kugombea urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka ya nyuma ndani ya CCM lakini rafu za kimakundi zikamchezea!

Ni mtu mwenye maono na anayekubalika kila kona ya dunia, Hakika hii ndio dhahabu ambayo CCM hakitakiwi kucheza nayo, Kama kweli inavyosemekana kua atachukua form ya kuwania urais naye wiki ijayo basi ndiye atakayemaliza kazi maana mpaka hapa kwa waliotia nia wote hakuna wa kufanana naye!

Ni mtu ambaye kwakweli kama atapitishwa ndiye atakayewapa wakati mgumu sana upinzani nchini.

Huyu mzee ni Turufu ya Taifa.

Sidhani kama atagombea ila kama umemsikia akisema hivyo sawa.

Kupita CCM ni vigumu sana kwa sababu kwa sasa kamati ya walioba iliyopita na kukusanya maoni haiko vizuri na CCM, kulikuwa na ile misuguano ya katiba mpya. pili Huyu mzee alidhalilishwa sana mara ya mwisho kugombea na waliomdhalilisha bado wapo.
 
labda achukue form kugombea zanzibar. wabara wazuri hawakosekani. rais wa muungano ndio pia rais wa tanganyika. muda wa salim ulishapita akijitokeza sasa atapata dissapointment.
 
Wasalaam wanajukwaa!

Nadhani kila mtu anamjua huyu mwanamapinduzi,mwanadiplomasia aliyebobea wa siasa za kitaifa na kimataifa,Waziri mkuu mstaafu, katibu mkuu mstaafu wa Umoja wa Africa(AU),Mtumishi wa umma wa miaka mingi asiyekua na doa katika uongozi wake!

Huyu ni kiongozi aliyewahi kutia nia kugombea urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka ya nyuma ndani ya CCM lakini rafu za kimakundi zikamchezea!

Ni mtu mwenye maono na anayekubalika kila kona ya dunia, Hakika hii ndio dhahabu ambayo CCM hakitakiwi kucheza nayo, Kama kweli inavyosemekana kua atachukua form ya kuwania urais naye wiki ijayo basi ndiye atakayemaliza kazi maana mpaka hapa kwa waliotia nia wote hakuna wa kufanana naye!

Ni mtu ambaye kwakweli kama atapitishwa ndiye atakayewapa wakati mgumu sana upinzani nchini.

Huyu mzee ni Turufu ya Taifa.

Kama unampenda kanywe naye chai, au kalambe miguu yake. Sasa hivi ni zamu yetu wa...... Nafikiri umenipata
 
labda achukue form kugombea zanzibar. wabara wazuri hawakosekani. rais wa muungano ndio pia rais wa tanganyika. muda wa salim ulishapita akijitokeza sasa atapata dissapointment.
Ukweli ambao sijui kwanini watu wanakwepa kuusema. Watanganyika hatuhitaji expatriate president. Muda wa wazanzibar ulikwisha na mwinyi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom