Jussa: Hakuna "kupatana" na Watanganyika

Hata huyo kamshna m'bara wa tume ya katiba anajua moyoni mwake fika kuwa wazanzibari hawautaki muungano, ila kwa sababu yeye yuko kwenye tume hiyo ndio maana anajibu kidiplomasia ili asijeonekana anaunga mkono hoja yao.
 
My take
Naanza kuona kwamba Tanganyika inafaidika na huu muungano kuliko zanzibar.Kama isingekuwa inafaidika,basi wangejitokeza hadharani wanaharakati (kutoka Tanganyika wanaotambuliwa na serikali) kufanya harakati kama hizo za akina Jussa na Maalim Seif kuhusu Tanganyika huru.

Wanaharakati wapo JF lakini wananishangaza kweli.

Wao wanakuja na makala na maoni kutushawishi tudai serikali moja, nchi moja, taifa moja.

Hawa wanaharakati wengi wa JF wanamawazo tofauti na yako. Wana hoja ya kuwa Zanzibar inapata umeme bure, biloni 32 kapewa Bilali nk.Mimi nakubaliana na wewe kidogo. Tanganyika kama nchi au sehemu ya Muungano inafaidika na pia Zanzibar au wananchi wazanzibari wanapata faida binafsi ya biashara na ardhi.
Lakini anaefaidika hasa na hii set up ya sasa ya Muungano ni CCM na viongozi wa CCM.

Sisi kama wadanganyika bado hatuoni faida ya kuidai Tanganyika huru lakini ujio wa Tanganyika utasawazisha dosari ya mchanganyo wa mambo mengi ambayo yanaleta utata katika muungano huu.

Faida kubwa itakuwa ni kuupata utaifa wetu wa Tanganyika na wengi wetu ambao tumeambulia kujiita wabara au watanzania bara tutajitanafasi kama wanavyojivunia wazanzibari kujiita wazanzibari.Tutasema kwa vinywa vipana kuwa sisi ni watanganyika. Wenzetu wa UK wanajivunia kujiita British nawakati huo huo kujiita English ,Welsh au Scottish. Hakuna mkinzano kujiita Mtanzania na pia mtanganyika.

Faida ya pili itakayopatikana ni kumaliza ukiritimba wa CCM juu ya karata ya muungano na mfumo wake.

Tatu na muhimu zaidi kila Taifa/upande wa muungano utakuwa na uhuru wa kujiamulia mambo ya ndani kivyake bila ya siasa za sasa za" wasiokubaliana na sera ya chama ya serikali mbili waondoke au warudishe kadi". Muungano hautakuwa kiini macho tena ya kudumaza maendeleo ya pande mbili za muungano.

Ya pamoja yatajulikana haya ni ya pamoja baina ya Tanganyika na Zanzibar na ya kila upande kivyake yatajulikana bila ulalamishi au visingizio vya "upuuzi".

Wanasiasa wanaonekana hawana ujasiri wa kumaliza fitina na vijineno neno visivyoisha juu ya muungano.Wananchi tudai mabadiliko ya Muungano. Akina warioba watakapokuja sehemu tunazoishi, tutoe maoni bila ya kutafuna maneno.Tuseme tunaitaka Tanganyika yetu na utanganyika wetu.

Muungano wa Tanzania ndio ukiini macho/mazingaombwe pekee yaliyolipoteza jina la nchi moja mwanachama wa Muungano katika dunia hii. Kama unaweza kupata mfano wa muungano mwengine ambapo jina la nchi mwanachama limepotea, nijulishe na mimi.

Tuamke tudai Tanganyika huru.
 
zanzibar sio nchi

Unaweza kukumbuka kauli ya mkulu
"Zanzibar ni nchi ndani lakini si nchi nje."
Au unaweza kulianzisha tifu tena kama Pinda alivyolianzisha aliposema" Zanzibar si nchi". Nini kilifuatia baada ya kauli ya Pinda.

Tanzania imeundwa na nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar.
Kwa hiyo Tanzania ni Muungano wa nchi mbili, zipi? Bara/Tz bara au (Tanganyika?) na Zanzibar.

UK ni nchi(muungano) na pia kuna nchi nne ndani yake. Tusijifanye vipofu, tumebarikiwa akili. Jipige msasa hapa link http://en.wikipedia.org/wiki/Countries_of_the_United_Kingdom
 
WataNzania Munaogopa Sana Changes,

Hata KAma sio wala Kesho...Zanzibar itapata Kile inachodai..Sauti yao JMT hamwezi Kwepa...

Wapeni Kisiwa Chao pelekeni Pesa kwenye. Utalii,Kilimanjaro,Ngorongoro,Ruaha,NK

Hakika hawa. Wanaontoka Povu kwa uwazi leo..Kesho watakuwa Maarufu kwa kusimamia kweli ya WanaNchi wa Zanzibar

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Yani natamani huyo jussa, cuf na hao uamsho siku uwekwe mdahalo ambapo tundu lissu, nguruvi3 na mzee mwanakijiji wamchachafye hadi aisome namba
 
Unamzungumzia nguruvi3 na mwanakijiji
Wanaharakati wapo JF lakini wananishangaza kweli.

Wao wanakuja na makala na maoni kutushawishi tudai serikali moja, nchi moja, taifa moja.

Hawa wanaharakati wengi wa JF wanamawazo tofauti na yako. Wan hoja ya kuwa Zaznibar inapata umeme bure, biloni 32 kapewa Bilali nk.Mimi nakubaliana na wewe kidogo. Tanganyika kama nchi au sehemu ya Muungano inafaidika na pia Zanzibar au wananchi wazanzibari wanapata faida binafsi ya biashara na ardhi.
Lakini anaefaidika hasa na hii set up ya sasa ya Muungano ni CCM na viongozi wa CCM.

Sisi kama wadanganyika bado hatuoni faida ya kuidai Tanganyika huru lakini ujio wa Tanganyika utasawazisha dosari ya mchanganyo wa mambo mengi ambayo yanleta utata katika muungano huu.

Faida kubwa itakuwa ni kuupata utaifa wetu wa Tanganyika na wengi wetu ambao tumeambulia kujiita wabara au watanzania bara tutajitanafasi kama wanavyojivunia wazanzibari kujiita wazanzibari.Tutasema kwa vinywa vipana kuwa sisi ni watanganyika. Wenzetu wa UK wanajivunia kujiita British nawakati huo huo kujiita English ,Welsh au Scottish. Hakuna mkinzano kujiita Mtanzania na pia mtanganyika.

Faida ya pili itakayopatikana ni kumaliza ukiritimba wa CCM juu ya karata ya muungano na mfumo wake.

Tatu na muhimu zaidi kila Taifa/upande wa muungano utakuwa na uhuru wa kujiamulia mambo ya ndani kivyake bila ya siasa za sasa za" wasiokubaliana na sera ya chama ya serikali mbili waondoke au warudishe kadi". Muungano hautakuwa kiini macho tena ya kudumaza maendeleo ya pande mbili za muungano.

Ya pamoja yatajulikana haya ni ya pamoja baina ya Tanganyika na Zaznibar na ya kila upande kivyake yatajulikana bila ulalamishi au visingizio vya "upuuzi".

Tuamke tudai Tanganyika huru.
 
Facts, umenena
kuongezea ikiwezekana kuwepo na utaratibu wa pass kuingia tanganyika au zanzibar.

Hapo kwenye swala la umeme ndiko kutawafanya wautamani muungano na washindwe kuuvunja.



Na sisi Watanganyika tuna kero zetu za Muungano;-


  • Rais wa Zanzibar ajaye naye atokee bara, maana mwinyi alishatoka zanzibar - kama urais ni kwa zamu
  • Watanganyika turusiwe kununua ardhi zanzibar, ikishindikana ardhi zinazo milikiwa na wazanzibar zilizopo bara tuzitaifishe
  • Sehemu ya wabunge au wabunge wote wa bara waruhusiwe kuingia katika bunge la zanzibar, ikishindikana basi wabunge kutoka zanzibar wasiingie bunge la bara.
  • Bei za umeme, tutozwe wote bei sawa ikishindikana iwe zamu ya zanzibar kutuuzia umeme bara kwa bei ya chini kuliko inavyotoza raia wake.
  • Pasiwapo upendeleo wowote katika usahihishaji wa mitihani....!

Jusa ni m'baguzi, na hata wakoloni walioitawala zanzibar wenye asili yake walitubagua sana weusi.....hapa hana lolote, shida yake anataka apewe cheo au nafasi fulani katika muungao ili anyamaze. Good move JUHa

Kibanga Msese
 
Huyu jussa alipaswa kumjibu huyo kamishna maneno hayo aliyoandika fesibuku.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Jussa na Wazanzibari wote VIZABAZABINA. Tutaendelea kuwaoa hadi mtakapotia akili vichwani mwenu.

Hayo anayoyadai Jussa ndiyo Tundu Lissu aliyesema mbele ya BUNGE TUKUFU la JMT.

Surprising enough WAZANZIBARI WOTE (read CCM na CUF) wakasimama na kumpinga Lissu tena kwa kejeli na matusi. Leo anaandika uharo ktk face book, hakuna atakaye kutawaza. Go to hell Jussa you are opportunistic politician.

The last nail to the coffin of ZNZ huru was CUF kukubali KUWEKWA KIMADA NA CCM.

The writting is already on the wall.
 
Kwenye facebook wall yake ametupia kitu hiki:
"Wakati tunaelekea India wiki iliyopita tukiwa Uwanja wa Ndege wa Dubai wakati tunabadilisha ndege, tulikutana na mmoja wa Makamishna wa Tume ya Katiba kutoka upande wa Tanganyika ambaye ni msomi wa hali ya juu.

Katika majibu ya kustaajabisha wakati nilipomuuliza vipi hali ya utoaji maoni inaendelea, alitujibu kuwa inaendelea vizuri na pamoja na kwamba upande mmoja (nna hakika alikusudia Zanzibar) unatoa madai makubwa, yeye haimpi tabu kwa sababu anajua wanaofanya hivyo wanajipa nafasi kubwa ya kuja kupatana (alitumia neno la Kiingereza 'bargaining') ili kupata muafaka wa kati na kati.

Bahati mbaya mawazo kama haya ya Kamishna huyu ndiyo mawazo mgando ya watunga sera na sheria wengi wa Tanganyika wanaojiona kama ni watawala au wamiliki wa Zanzibar na hivyo kujipa matumaini kuwa Zanzibar tunaposema tunataka kurejesha mamlaka yetu kamili kitaifa na kimataifa tukiwa na kitu chetu Umoja wa Mataifa huwa tunatafuta 'kupatana' au kwamba hatuna uwezo huo mpaka Tanganyika waridhie.

Wanapaswa wajue sasa kabla hawajachelewa kwamba mamlaka kamili ya Zanzibar (Sovereign Zanzibar) siyo ombi ni matakwa ya Wazanzibari na tutayasimamia kwa nguvu na uwezo wetu wote. Na katika kulifikia lengo hilo hakuna wa kutuzuia isipokuwa Mwenyezi Mungu. Pamoja Daima!"


My take
Naanza kuona kwamba Tanganyika inafaidika na huu muungano kuliko zanzibar.Kama isingekuwa inafaidika,basi wangejitokeza hadharani wanaharakati (kutoka Tanganyika wanaotambuliwa na serikali) kufanya harakati kama hizo za akina Jussa na Maalim Seif kuhusu Tanganyika huru.

Hivi akina Lipumba na Mtatiro huwa wanasemaje kuhusu hili au ni MABUBU mbele ya akina Jussa na Maalim?

Cuf ni mali ya maalim seif. Cuf ni seif na seif ni cuf. Ajaribu prof. lipumbavu kumbishia kama hajafrumshwa kama ilivyotokea kwa mnyamwezi mwenzie mapalala. Na huyu Mtatilo si ndiye ana brush viatu vya maali, kwani hamjui hilo!
 
Facts, umenena
kuongezea ikiwezekana kuwepo na utaratibu wa pass kuingia tanganyika au zanzibar.

Hapo kwenye swala la umeme ndiko kutawafanya wautamani muungano na washindwe kuuvunja.

Zanzibar imekuwa ikitumia umeme kabla ya Tanganyika, vili vile imekua na umeme kabla ya Muungano...Hatuwezi kuuza nchi yetu kwa sababu ya umeme kutoka Tanganyika.
 
Katika hili la Muungano mimi namsikiliza Rais Mstaafu wa Zanzibar Abeid Karume. Wawazo yake yana uzito zaidi kuliko wakina Jussa mia moja. Kama tulivyoona kwenye Serikali ya Kitaifa. Kina Jussa are inconsequential. Ni kelele tupu!
 
BINAFSI sijawah kuona umuhmu wa muungano. Sijafaidika kwa namna yoyote ile, nikiagza gar toka zanzibar natozwa ushuru. Labda wanaofaidka ni viongoz wakubwa
 
Muungano huu ni wa ccm, cuf kupitia vibaraka wao kama Uamsho na wengineo hawaupendi. Wazanzibar waondoke salama ili alkaida wawekeze vizur pale ili washirikiane na UAMSHO!
 
Jussa yuko sahihi hasa kuhusu hawa wanaojiita wasomi wa kitanganyika ambao ni mabingwa wa kujipendekeza kwa wanasiasa kama alivyo Dr. Bana.

Jussa ametoa mtazamo wake juu ya muungano anaoutaka yeye na washabiki wa chama anachokiongoza hivyo hakuna haja ya kumtukana wala kumkashifu. Kama watanganyika tuna hoja kuhusu huu muungano na Zanzibar na sisi tuziweke wazi ili ijulikane nini hasa kinaendelea.
 
Watanganyika wanafiki, hawako wazi juu ya Muungano. Mimi binafsi faida za muungano huu ni chache kuliko kero/mabaya ya muungano wenyewe. Hautufai, tuwe na serekali tatu, Tanganyika, Jamhuri ya watu wa Zanzibar na Serekali ya shirikisho la Tanganyika na Jamhuri ya watu Wa Zanzibar. Full stop.
Heri ya waTg waliojikalia kimya kuliko unafiki wa wazenj! Huku wataka na huku wataka! Manake dawa ya kuuvunja Muungano haiko mwezini ili utafute chombo cha kufika mwezini! TL aliwapa dawa hawakuitaka kwa sababu wanautaka mfumo uliopo wa muungano! Hivyo basi waTg hatutaki kero zenu wazenj na chokochoko na mashairi yenu!
 
Back
Top Bottom