Joram Kihango vs Willy Gamba

Joram Kihango, yaani nikisoma kitabu kama SALAMU KUTOKA KUZIMU, nilikuwa nasisimka mwikli mzima, nywele zikinisimama na vipele kunitoka mwili mzima.
 
Nilivutiwa zaidi na Willy Gamba, yaani nilikuwa nikisoma hadithi zake nilikuwa najisikia mzalendo halisi na nilitamani niwe kama yeye yaani niwe tayari wakati wote kuipigania Afrika, nakumbuka harakati za WG katika vitabu kama NJAMA, HOFU, KK (KIKOSI CHA KISASI), na kile cha wizi wa almasi mwadui. Huwa najiuliza kama mzee Aristablus Elvis Musiba angeendelea kuandika vitabu hivi, sijui angeandika nini juu ya Willy Gamba na mapambano yake na wahujumu kama wa EPA na RICHMOND! yaani Willy Gamba alinifanya nivutiwe sana kusoma riwaya za upelelezi kama zile za mtunzi James Hadley Chase!
 
Ulikuwa unavutiwa zaidi na yupi kati ya wakali hao?

Ninavyofahamu mimi willy Gamba hakuwa mwandishi wa vitabu vya hadithi isipokuwa ni jina lililotumiwa na mwandishi wa vitabu maarufu wakati huo ambaye sasa ni mfanyabiashara maarufu vilevile anayeitwa A.MUSIBA. Nakumbuka KITABU CHAKE CHENYE HADITHI YA KUSISIMUA YA KIPELELEZI KATIKA JIJILA KINSHASA ( KUFA NA KUPONA )cha A.MUSIBA aliyetumia jina la Wily Gamba Kama Muhusika mkuu.
 
Kwa kweli umenikumbusha mbali enzi hizo kusoma vitabu vya hadithi ilikuwa ni mojawapo ya starehe kama si kwenda cinema.Nimesoma karibu vitabu vyote vya willy gamba,kuanzia kikomo,kikosi cha kisasi,hofu,njama,tutarudi na roho zetu,na vile vile vya joram kiango kama najisikia kuua tena,pesa zako zinanuka,dar es salaam usiku na vingine.Naweza kusema kila mmoja alikuwa na uzuri wake ila pointi nyingi atachukua willy gamba ambaye alikuwa anacheza kama mtu wa usalama wa taifa tofauti na joram kiango ambaye alikuwa anacheza kama mpelelezi wa kujitegemea.
 
Joram Kiango malaika wa Shetani..lakini wote kwa ujumla Riwaya zao zilikuwa nzuri sana .
Hivi mbona sasa hazipatikani?anayejua zunzuzwa waoi tafadhari tuwasiliane

Zawadi ya ushindi mtunzi alikuwa nani nimesahau?
 
du nilivutiwa sana na willy gamba hasa vitabu vya njama na kikosi cha kisasi. na mwandishi wa hivi vitabu yupo hapa mikocheni naona kajikita zaidi kwenye biashara zake. naona aliamua kuajipumzisha na fasihi andishi kwa heshima. yaani ameacha kuandika huku jamii ikiwa bado inapenda kazi zake. anaitwa mzee elivis musiba kwa sasa ni mwenyekiti wa CTI but sina hakika kama bado anaendelea au muda wake umeisha
 
Joram Kiango malaika wa Shetani..lakini wote kwa ujumla Riwaya zao zilikuwa nzuri sana .
Hivi mbona sasa hazipatikani?anayejua zunzuzwa waoi tafadhari tuwasiliane

Zawadi ya ushindi mtunzi alikuwa nani nimesahau?

FL1 umekumbusha mbali kidogo na Mambo ya Sikamona! Mtunzi wa kitabu hiki ni Ben R. Mtobwa ambaye ndiye aliyekuwa anaandika Riwaya za Kusisimua za Joram Kiango. Nilipokuwa nasoma hizi riwaya nilikuwa nafanya imagination kumhusu Joram Kiango! Nilikuwa napata picha eti ni kweli Joram Kiango ni mtu kweli, Mwembamba, Mrefu amenyoa panki Ha ha ha
 
Ninavyofahamu mimi willy Gamba hakuwa mwandishi wa vitabu vya hadithi isipokuwa ni jina lililotumiwa na mwandishi wa vitabu maarufu wakati huo ambaye sasa ni mfanyabiashara maarufu vilevile anayeitwa A.MUSIBA. Nakumbuka KITABU CHAKE CHENYE HADITHI YA KUSISIMUA YA KIPELELEZI KATIKA JIJILA KINSHASA ( KUFA NA KUPONA )cha A.MUSIBA aliyetumia jina la Wily Gamba Kama Muhusika mkuu.
Tena Musiba aliandika vitabu vyote hivyo kipindi alichokuwa anatumikia kifungo kirefu jela. Baada ya kifungo, alirudi uraiani, biashara imemchanganyia uandishi ndio basi tena.
 
Kwa kweli umenikumbusha mbali enzi hizo kusoma vitabu vya hadithi ilikuwa ni mojawapo ya starehe kama si kwenda cinema.Nimesoma karibu vitabu vyote vya willy gamba,kuanzia kikomo,kikosi cha kisasi,hofu,njama,tutarudi na roho zetu,na vile vile vya joram kiango kama najisikia kuua tena,pesa zako zinanuka,dar es salaam usiku na vingine.Naweza kusema kila mmoja alikuwa na uzuri wake ila pointi nyingi atachukua willy gamba ambaye alikuwa anacheza kama mtu wa usalama wa taifa tofauti na joram kiango ambaye alikuwa anacheza kama mpelelezi wa kujitegemea.

Mkuu hapo kwenye red muhusika mkuu hakuwa Willy Gamba alikuwa Joram Kiango
 
Ulikuwa unavutiwa zaidi na yupi kati ya wakali hao?

Sidhani kama anaitwa Joram KIHANGO......................... Mimi mkali wangu ni Ben R. Mtobwa na baadhi ya vitabu vyake ni Dar es salaam usiku, tutarudi na roho zetu, hiba ya wivu, najisikia kuua tena,zawadi ya ushindi, kipofu mwenye miwani mweusi,malaika wa shetani, roho ya paka, salamu kutoka kuzimu, mwalimu mwenye mkono wa bandia, nyuma ya pazia na bila kusahau, Kikwete:http://www.bookfinder.com/dir/i/Kipofu_Mwenye_Miwani_Myeusi/9976963572/Safari ya Ikulu.....

RIP Ben
 
Joram Kiango malaika wa Shetani..lakini wote kwa ujumla Riwaya zao zilikuwa nzuri sana .
Hivi mbona sasa hazipatikani?anayejua zunzuzwa waoi tafadhari tuwasiliane

Zawadi ya ushindi mtunzi alikuwa nani nimesahau?[/QUOTE]



Ni Ben Mtobwa,amefariki mwaka huu mwanzoni,Mungu amrehemu.
 
Mtunzi wa Vitabu hivyo (vinavyomhusu Willy Gamba) anaitwa, ARISTABLUS ELVIS MUSIBA

Huyo Elvis Musiba nadhani ni baba yake mzazi na Aristablus, mwenye kuwafahamu vizuri watu hawa naomba atujuze tafzali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom