Joram Kihango vs Willy Gamba

Joram Kiango v Nunda Mla Watu patamu hapo lakini Willie Gamba alikuwa mwisho wa matatizo!
 
Sunday, November 16, 2008
Buriani Ben Mtobwa



Nimepokea kwa mshtuko mkubwataarifa ya kifo cha mwandishi maarufu, Ben Mtobwa ama 'Joram Kiango'. Taifa limepoteza kinara mwingine wa kutumia fasihi andishi kufichua masuala mazito yaliyoigubika jamii yetu. Hivi karibuni nilimwona gwiji Ben pale kwenye Mkahawa wa Vitabu wa Soma akipanga mikakati ya uandishi na uchapishaji.

Nilidhani huo ni mwendelezo wa kumwona mpiganaji huyu akiwa katika harakati za kutumia 'mtutu wa kalamu' kufichua uzandiki na ufisadi katika jamii. Lakini upeo wa mwanadamu una kikomo. Hivyo, sikujua kuwa hiyo ilikuwa mara ya pili na ya mwisho kumwona mwanaharakati huyo ambaye pia alijitosa katika fani ya uhariri wa gazeti la Heko na uchapishaji kupitia kampuni yake ya Heko Publishers.

Nawasihi tumpe mtunzi huyu'Zawadi ya Ushindi' kwa kusoma kwa undani vitabu vyake ili tutambue ni nini hasa amejaribu kutufunulia 'Nyuma ya Mapazia' ya jamii yetu iliyozingirwa na 'Malaika wa Shetani' na mafisadi wenye'Roho ya Paka' wanaomsulubisha 'Mhariri Msalabani' na kudiriki kusema 'Najisikia Kuua Tena' kupitia mikataba mibovu wanayoisaini 'Dar-es-Salaam Usiku' pasipo kumwambia mwekezaji uchwara 'Peza Zako Zinanuka' na tena bila kuogopa 'Salamu Kutoka Kuzimu' au kilio chetu cha 'Tutarudi na Roho Zetu?' Buriani Ben Mtobwa!

UDADISI: Rethinking in Action: Buriani Ben Mtobwa
 
Vitabu vya Ben R Mtobwa vinapatikana kwenye maduka ya vitabu yaliyopo DSM na vimetolewa tena na Mkuki na Nyota
<br />
<br />
Vp vya willy Gamba vinapatikana wapi ili nasi ambao hatukuvisoma tuvifaidi manake tittle tu inaonyesha vimekamilika.
 
Nataka nicheze movie nikitumia script ya vitabu hivi. Je nani ana haki ya hakimiliki kwa mujibu wa sheria?
 
Willy Gamba kama mhusika mkuu katika vitabu bora kabisa vya hadithi kutoka kwa mtunzi Elvis Musiba ambaye alitoa vitabu kama Njama,Hofu,kufa na kupona,Kikosi cha Kisasi na Almasi mwadui. mtunzi Ben R. Mtobwa akimtumia Joramu Kiango katika riwaya zake kama salamu kutoka kuzimu,roho ya paka ,malaika wa shetani na vingine ni watunzi mahiri wa enzi hizo wote wakali lakin willy gamba alikuwa zaidi.
 
nakumbuka vitabu vya hawa jamaa vilinifanya nitamani kujitolea hata kufa kwa ajili ya taifa langu,natamani tubuni njia ya kuwaenzi hata kuwajengea mnara wa kumbukumbu.Kwaheri willy Gamba,kwaheri Joram kirango!
 
Wandishi wote wawili walikua wabunifu...Marehemu Aristablus Elvis musiba and Ben R Mtobwa na wahusika wote wawili waliowatumia Joram Kiango na Willy Gamba waliweza kuuvaa uhusika ipasavyo.....lakini kuna utofauti kidogo...wakati Joram visa vyake vingi vilitokea accidentally wakati Willy Gamba
ilikua ni ajira yake......by the way Mimi nilikua nampenda zaidi Joram Kiango...alikua hatari...makini na pia asietabirika.....Willy Gamba alinifurahisha na upendaji wake wanawake...alikua mtu wa madem kweli...But all in All R.I.P Musiba and Mtobwa...
 
Riwaya hizi, angepatikana mtu wa kutengenezea muvi yenye uhalisia , ingeuza sana muvi hiyo
 
Ninavyofahamu mimi willy Gamba hakuwa mwandishi wa vitabu vya hadithi isipokuwa ni jina lililotumiwa na mwandishi wa vitabu maarufu wakati huo ambaye sasa ni mfanyabiashara maarufu vilevile anayeitwa A.MUSIBA. Nakumbuka KITABU CHAKE CHENYE HADITHI YA KUSISIMUA YA KIPELELEZI KATIKA JIJILA KINSHASA ( KUFA NA KUPONA )cha A.MUSIBA aliyetumia jina la Wily Gamba Kama Muhusika mkuu.

Willy Gamba na Joram Kihango yalikua majina ya wahusika wakuu waliochaguliwa na wahandishi mashuhuri wa vitabu Elvis Musiba na Ben R. Mtobwa. Kwa hakika nilibahatika kusoma vitabu vyote vya waandishi hawa na nilivutiwa zaidi na vitabu vya Musiba (Willy Gamba) kwani alijua kuwatengeneza wahusika walioweza kumtoa msomaji machozi hasa walipouwawa!
 
mmenikumbusha mbali,hivi nani alikuwa mtunzi wa kitabu cha Juma na Roza?enzi zile za ndizi ni chakula huleta pesa pia.
 
Je wanakumbwa waandishi hawa.?
Lakini nashukulu baadhi ya vitabu vinatumika kwenye mitaara ya sekondari.
Mungu warehemu huko waliko.
Hoja hii ni mojawapo wa kuwakumbuka kwa mchango wao.
 
Ulikuwa unajisikiaje unapomuona mwenzako ameshika KUFA NA KUPONA, NJAMA, KIKOSI CHA KISASI, KIKOMO ama SALAMU TOKA KUZIMU, TUTARUDI NA ROHO ZETU?, LAZIMA UFE JORAM, MIKONONI MWA NUNDA, NAJISIKIA KUUA TENA!!!HEBU KUMBUKA ULIPOKUWA UNASUBURI ZAMU YAKO NA WEWE UAZIME!!!
Nimeshangazwa kujua kwamba karibia kila mwandishi bora wa nyakati hizi amefariki. Nataka tuwakumbuke na kuwaombea. Lakini ni lazima nimpongeze mwandishi bora wa nyakati hizi HUSSEIN TUWA. kwa kweli ni mkali sana hebu kwa wale wapenzi wa riwaya tutafute riwaya zake MKIMBIZI, UTATA WA 9/12 NA MDUNGUAJU
 
Kwa kweli umenikumbusha mbali! Nakumbuka kitabu cha NJAMA, mwanafunzi mmoja alikiiba nyumbani kwao na kuja nacho shuleni. Ilikuwa kukipata kwa kuazima lazima ufanye booking ya moja week mbili. Baadae ikawepo booking ya mchana na ya usiku. Ukiamua kusoma mchana maana yake ukose vipindi, ukibahatika kupewa uende nacho nyumbani basi kama hujamaliza kesho yake unajifanya kuugua ili usije shule. Ila jamaa walivyokuwa na usongo unashutukia wamekufuata huko huko.
 
Cjui nin kilicho kusukuma maana umenkumbusha mbali sana, yaan nw dayz namtazama wily kama jack wa 24. Nahc vijana nw dayz wankosa uhonda, nakumbuka nliwahi kuchukua kitab cha njama bila idhin ya baba aseee, w mkuu umenkumbusha long ago big up, halafu mmoja anisaidie kujua kitabu cha MUNUKO WA DAMUi no mbili. Maana nlisoma nakala moja tu plz.
 
Kwa kweli umenikumbusha mbali! Nakumbuka kitabu cha NJAMA, mwanafunzi mmoja alikiiba nyumbani kwao na kuja nacho shuleni. Ilikuwa kukipata kwa kuazima lazima ufanye booking ya moja week mbili. Baadae ikawepo booking ya mchana na ya usiku. Ukiamua kusoma mchana maana yake ukose vipindi, ukibahatika kupewa uende nacho nyumbani basi kama hujamaliza kesho yake unajifanya kuugua ili usije shule. Ila jamaa walivyokuwa na usongo unashutukia wamekufuata huko huko.

umeona ee? ulijisikiaje pale VERONICA amechomwa kisu! au pale jamaa wamekoswa na bomu!!!hahaha!!! jamaa alikuwa anatufanya tusisimke na usiku usilale kwa msisimko!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom