SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,449
- 23,774
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.
Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.
Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.
Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.
Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.
Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.
Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.
Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.
Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.
Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.
"Habari?" Tukionana.
"Asante." Tukiagana.
Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.
Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.
Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.
Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.
Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.
Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.
Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.
Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"
Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.
Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.
Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.
Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?
Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.
Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.
Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.
Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.
Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.
Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.
Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.
Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.
Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.
Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.
Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.
Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.
Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.
Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.
Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.
Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.
Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!
Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?
Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.
***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
====
SEHEMU YA 2
SEHEMU YA 3
SEHEMU YA 4
SEHEMU YA 5
SEHEMU YA 6
SEHEMU YA 7
SEHEMU YA 8
SEHEMU YA 9
SEHEMU YA 10
BONUS-A
BONUS-B
BONUS C
SEHEMU YA 11
SEHEMU YA 12
SEHEMU YA 13
Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.
Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.
Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.
Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.
Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.
Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.
Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.
Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.
Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.
"Habari?" Tukionana.
"Asante." Tukiagana.
Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.
Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.
Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.
Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.
Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.
Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.
Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.
Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"
Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.
Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.
Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.
Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?
Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.
Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.
Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.
Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.
Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.
Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.
Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.
Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.
Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.
Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.
Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.
Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.
Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.
Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.
Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.
Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.
Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!
Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?
Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.
***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
====
SEHEMU YA 2
SEHEMU YA 3
SEHEMU YA 4
SEHEMU YA 5
SEHEMU YA 6
SEHEMU YA 7
SEHEMU YA 8
SEHEMU YA 9
SEHEMU YA 10
BONUS-A
BONUS-B
BONUS C
SEHEMU YA 11
SEHEMU YA 12
SEHEMU YA 13