Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,833
Baada ya kusimamishwa kazi mambo mengi yalikwama kiasi cha kutimuliwa kwenye nyumba nliyokuwa naishi anga za Sinza.
Mama mkwe alinibembeleza sana nikakae nyumbani kwake Tegeta ambako ana nyumba kubwa na anaishi peke yake.
Nilienda ili nikae kwa wiki moja then niondoke ili nirudi kijijini kwetu Nassa Jeneri ili nikauze ng'ombe na nije kuanza maisha upya.
Siku ya tatu ya ukaaji wangu ukweni nikiwa busy na JF mara sms ikaingia. Ile msg inaingia tu waif akaidaka simu na kukimbia nayo.
Akampelekea mama yake, ambaye akaja akiwa amekasirika sana. Mke wangu akaanza kunitukana kuwa mimi ni malaya na mama mkwe akaanza kuchana chana nguo zangu huku akinisimanga kuwa sina mbele wala nyuma na matusi mengine mengi mazito yasiyoelezeka.
Nguo zangu zikachanwa kiasi cha kuniacha mtupu kabisa, nikamwagiwa maji na kutolewa nje ya geti mchana kweupe.
Simu yangu, vyeti, laptop na vitu vyangu vyote vikabaki kwa mama mkwe wangu.Niliondoka hadi mitaa ya jirani ambako kuna rafiki zangu walionisitiri.
Baada ya siku chache nikaenda Mwanza kuuza ng'ombe wangu, sikuwa na simu wala namna yoyote ya mawasiliano.
Nikiwa Mwanza niliuza ng'ombe nikanunua simu na kumpigia mama watoto.
Akaniambia kuwa yale yote yalitokana na hasira, ndipo nikamuuliza kwani ile msg iliyoleta songombingo ilikuwa inasemaje?
Akaniambia ilitumwa na sekretari wangu na aliiandika Dear boss, hali ya ofisini ni mbaya sana amna amani, i m praying for you. Dah.. Nlivyo ambiwa hivyo nkatamani kucheka na kulia kwa wakati mmoja.
Nikauliza vyeti vyangu, nikaambiwa mama mkwe kachoma moto vyeti vyangu vyote vya sekondari hadi chuo.
Nliposikia hivyo niliumia sana.
Sasa nina mtaji wa milioni saba, wana jamvi anaombeni ushauri wenu je nifanye biashara gani kwa mtaji nilionao? Maana sina tena vyeti, biashara ndio maisha yangu yajayo.
Mama mkwe alinibembeleza sana nikakae nyumbani kwake Tegeta ambako ana nyumba kubwa na anaishi peke yake.
Nilienda ili nikae kwa wiki moja then niondoke ili nirudi kijijini kwetu Nassa Jeneri ili nikauze ng'ombe na nije kuanza maisha upya.
Siku ya tatu ya ukaaji wangu ukweni nikiwa busy na JF mara sms ikaingia. Ile msg inaingia tu waif akaidaka simu na kukimbia nayo.
Akampelekea mama yake, ambaye akaja akiwa amekasirika sana. Mke wangu akaanza kunitukana kuwa mimi ni malaya na mama mkwe akaanza kuchana chana nguo zangu huku akinisimanga kuwa sina mbele wala nyuma na matusi mengine mengi mazito yasiyoelezeka.
Nguo zangu zikachanwa kiasi cha kuniacha mtupu kabisa, nikamwagiwa maji na kutolewa nje ya geti mchana kweupe.
Simu yangu, vyeti, laptop na vitu vyangu vyote vikabaki kwa mama mkwe wangu.Niliondoka hadi mitaa ya jirani ambako kuna rafiki zangu walionisitiri.
Baada ya siku chache nikaenda Mwanza kuuza ng'ombe wangu, sikuwa na simu wala namna yoyote ya mawasiliano.
Nikiwa Mwanza niliuza ng'ombe nikanunua simu na kumpigia mama watoto.
Akaniambia kuwa yale yote yalitokana na hasira, ndipo nikamuuliza kwani ile msg iliyoleta songombingo ilikuwa inasemaje?
Akaniambia ilitumwa na sekretari wangu na aliiandika Dear boss, hali ya ofisini ni mbaya sana amna amani, i m praying for you. Dah.. Nlivyo ambiwa hivyo nkatamani kucheka na kulia kwa wakati mmoja.
Nikauliza vyeti vyangu, nikaambiwa mama mkwe kachoma moto vyeti vyangu vyote vya sekondari hadi chuo.
Nliposikia hivyo niliumia sana.
Sasa nina mtaji wa milioni saba, wana jamvi anaombeni ushauri wenu je nifanye biashara gani kwa mtaji nilionao? Maana sina tena vyeti, biashara ndio maisha yangu yajayo.