Jibu la prof Sheriff kwa prof Tibaijuka

Kwenye huu muungano wa kulazimisha, mengi tu yatashuhudiwa. Kisicho halali hakiliki, nyie mwalazimisha, mtatapika tu.
 
Tibaijuka uko sawa profesa wangu, ungekuwa hauko sawa basi ungeenda UN kuomba msumbiji na kenya ziongezewe eneo. Muungano haufai, watanganyika hatuutaki, na wazanzibari ndo kabisa hawautaki. Muungano umebaki kwa wana ccm na wacuf tu
 
Barubaru,
Mjadala unaendelea, Nilishafafanua kama waafrika haswa kuanzia mashariki ya kati mpaka kusini wote ni wamoja. Kabla ya
wazungu kuweka mipaka na kuchora ramani ya kwanza ya Afrika na kujigawia makoloni. waafrika wa sehemu hizo
tajwa walikuwa wanaishi popote pale wanapotaka na wanapoona panawafaa. Sasa basi mpango huo wa kuanza kuzitenga
jamii barani Afrika , uliitwa "Berlin Conference" na ulifanyika kuanzia November, 1884 mpaka February 1885. katika mji wa
Berlin, Ujerumani. Nyuma ya hapo kulikuwa hamna mipaka. Ukiangalia Tanganyika baada ya michoro ya kuigawa Afrika
tayari ilishawafungia watu kwa kutokuweza kwenda wanapotaka kuhamia au kurudi kule walipotoka.
Makabila mengi ya Tanganyika yamekuja kutoka Kaskazini, Kusini na magharibi. Tuchulie mfano Wapare, Wamasai wametokea
" ABYSSINIA "yaani ETHIOPIA. Wangoni wametokea AFRIKA YA KUSINI . Wabembe, Wamanyema hao wametokea KONGO.
huo ni mfano mchache tu, na hayo makabila yote yalikuwa na sababu za kuhamia sehemu nyingine, aidha malisho ya mifugo,
aidha ardhi ya kulima, aidha kuvua samaki, aidha kushindwa vita na kukimbia na kuhamia sehemu nyingine.
Aina hiyo ya maisha ilikwama na kuwa mwanzo wa civilization kwa waafrika Waarabu wahindi waliokutwa katika sehemu husika.
Na ukazidi kuwa mgumu kwa watu kwenda na kuhamia sehemu nyingine,baadaya kuchorwa ramani ingine ya kiugawanya Afrika, ramani iliitwa " Political colonial africa, " 1916.
Turudi katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar. yaani " THE ARTICLES OF UNION BETWEEN TANGANYIKA AND ZANZIBAR "
ndio wenye matatizo madudu mengi ndani yake. kutokana na wakati wanatakiwa wakae mezani tena na ufanyiwe marekebisho.
kwa mapungufu na yote yanayohitajika muhimu yaingie humo, kwa sababu ulaghai upo. Baada ya hapo Articles mpya ya
muungano, yaani Union agreement inatakiwa ifanyiwe registrering katika secretariat ya UN, Legal Councel.
Na hapo Muungano ndio utakuwa umekamilika, Basi ikiwa kutakuwa na mwelekeo kutokuelewana kati ya nchi hizo mbili
mmoja wapo akipeleka mashtaka umoja wa mataifa, registered treaties to invoked. Kazi sasa imebakia kwa Watanganyika
na Wazanzibar kuuweka sawa Muungano, ilo ndio Darsa.

Nakubaliana kabisa na wewe. Siku zote ndoa haramu uzaa mtoto wa haramu.

Je unajuwa makubaliano haya ya muungano ambayo yaliridhiwa na Bunge la muungano hapo 1964 mpaka leo hayajaridhiwa na BLW na hivyo kuwa haramu na si halali kwa Znz kwa mujibu wa sharia za Muungano na zile za Znz.

Wakati umefika Baraza la Wawakilishi Zanzibar lipewe nafasi ya kuridhia mkataba wa Muungano uliofikiwa Aprili 26, 1964 baina ya hayati Mwalimu Nyerere na hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Baada ya kufikiwa kwa Muungano mwaka 1964, Baraza la Kutunga Sheria la Zanzibar ambalo lilikuwa ni Baraza la Mapinduzi halikupewa nafasi ya kuridhia Muungano huo.
"Lazima Baraza la kutunga sheria la Zanzibar kwa sasa ambalo ni Baraza la Wawakilishi lipewe nafasi ya kuridhia mkataba huo ili kuupa uhalali wa kisheria kwa upande wa Zanzibar," na vile mkataba wa Muungano upitiwe upya na kurekebishwa maeneo ambayo yalikuwa na utatanishi baina ya pande mbili za Muungano.
 
Tibaijuka uko sawa profesa wangu, ungekuwa hauko sawa basi ungeenda UN kuomba msumbiji na kenya ziongezewe eneo. Muungano haufai, watanganyika hatuutaki, na wazanzibari ndo kabisa hawautaki. Muungano umebaki kwa wana ccm na wacuf tu

The article of the Union between Tanganyika and Zanzibar inasema
(v) The existing laws of Tanganyika and of Zanzibar shall remain in force in their respective territories subject-

The initial “Union Matters” included the following elevenareas as Union matters:
· The constitution and government of the UnitedRepublic;
· External affairs;· Defense;· Police;· Emergency powers;· Citizenship;· Immigration;· External trade and borrowing;· The Public service of the United Republic;· Income tax, corporation tax, customs and excise duties,and· Harbours, civil aviation, posts and telegraph.

Haya yameingizwa kinyemela na kufikia 22.

22 were: · All matters concern coinage, currency for thepurposes of legal tender (including notes), banks(including savings banks) and all banking business;foreign exchange and exchange control · Industrial licensing and statistics · Higher education · Mineral oil resources, including crude oil and naturalgas · The National Examinations Council of Tanzania andall matters connected with the functions of thatCouncil · Civil Aviation · Research · Meteorology · Statistics · The Court of Appeal of the United Republic · Registration of political parties and other mattersrelated to political parties

Zanzibar retains jurisdiction over issues which include:
· Information, Agriculture, Natural Resources,Environment and Cooperatives, Trade, Industry,Marketing, Tourism, Education, Culture and Sports,Health and Social Welfare, Water, Construction,Energy and Land, Communication and Transport andfinally, youth, employment, women and childrendevelopment, etc ZANZIBAR: A “SOVEREIGN STATE’’

 
Nitarudie tena kwa mara ya mwisho kama hutanielewa nitakufuata huko "nikuzabe vibao" maana kuna wanafunzi hawaezi kuelewa ila kwa viboko!

Sio kila jambo inaloamua SMT au SMZ lazima lipitie kwenye bunge la JMT au BLW. Vivyo hivyo wakati hili jambo EEZ linajadiliwa na kufikishwa UN halikupelekwa kwenye bunge la JMT au BLW (ni makosa ya katiba yetu mbovu).

Lakini hilo haliondoi ukweli kwamba Zanzibar haikushirikishwa. Hili jambo liliamulia kwenye baraza la mawaziri la SMT ambalo kuna wajumbe kutoka ZNZ nao VP Dr. Bilal, Dr. Shein (waziri asiye na wizara maalumu), Shamsi Vuai Nahodha (mambo ya ndani), Hussein Mwinyi (Ulinzi), Samia Hassan Suluhu (Muungano), Omari Nundu (Mawasiliano/Uchukuzi) etc.

Balozi Seif Idd kutojua kama kiongozi wa BLW, haina maana kwamba SMZ ilikuwa haifahamu. Ndiyo maana kwenye ule ujumbe ulio kwende UN kupeleka ombi walikuwepo wajumbe kutoka BLW, SMZ. Je, hawa wote walitoroka makazini kuapata ruhusa?! TAFAKARI

Tatizo kubwa la viongozi wa ZNZ wanapokuwa na wa wenzao wa muungano wanaongea lugha tofauti, wanapokwenda huko ZNZ wanaongea lugha nyingine, hii haikuanza leo tangia wakati wa Abood Jumbe Mwinyi na kitabu chake THE PARTNERSHIP. Matokeo yake Nyerere akamuweka kizuizuni Kigamboni.

This is the root causes ya maatizo yenu Wazanzibari, bila kuwa take into task viongozi wenu mtabaki kuwalalamikia Watangayika milele. Mfano mwingine ni sheria ya mabadiliko ya katiba mpya wabunge wenu (CCM na CUF) walivyoshadadia hiyo sheria inayominya uhuru wa kutoa maoni kwenye mambo yanahohusu muungano.

Mtajibaraguza huko kwenye masikani ya kahawa na kashata lakini we know finally mtafyata mkia na eno litaongezwa. Mark my words.

Hah ha ha...utanizaba kibao sio...Sisi tumeacha kuzaba vibao. Sasa ni tindikali tu. Sisi tunaelewa kama kuna vibaraka ndani ya SMZ mnawatumia. Lakini muda wao unafikia ukingoni, Zanzibar ya sasa ni ya vijana na hatutaki tena mchezo kwenye rasilimali zetu. Kazi itaanza hapo Mambo ya katiba mpya yakianza. Just stay tuned.
 
Tukiendelea kung'ang'ania huu muungano wa serikali mbili, matatizo hayatakwisha hata siku moja. Imefika wakati tuangalie moja kati ya options zifuatazo:-
1. Tuwe na serikali 3, ya Zanzibar, ya Tanganyika na ya Muungano.
2. Tuwe na serikali moja tu ya Muungano ili Wazanzibar nao wakubali kuipoteza serikali yao kama ilivyofanya Tanganyika
3. Tuuvunje Muungano ili kila nchi iangalie mambo yake yenyewe, Tanganyika ipate uhuru wake kwa mara nyingine na zanzibar pia iachane na "mkoloni" Tanzania.
Vinginevyo tuking'ang'ania sera za ccm za muundo wa serikali mbili, tujiandae kwa matatizo makubwa zaidi siku za mbeleni.

Natoa maoni kwa watanganyika wenzangu tuanze kampeni za kupinga muungano huu wa TZ ili tuweze kulirudisha taifa letu la Tanganyika...........tujaribuni kufanya maandamano kuanzia Posta feri mpaka magogoni ikulu tukatoe kilio chetu kwa JK Kama tumeshachoka na muungano huu!!!
wazanzibari wanajaribu sana kufanya hivyo lakini kwa vile wao ni kidogo imekuwa vigumu kwa JK kuwasikiliza haraka lakini vile sisi huku bara tupo mamilioni ya watu tukifanya hivyo JK anaweza kuogopa sana:A S 465:
 
Back
Top Bottom