"JF M & F Politician Of The Year 2011" Competition

Uko sahihi......

Sidhani kama ni BUSARA kulinganisha kifungo cha mtu kama Nelson Mandela na BAN wanazopewa watu wanaoishiwa HOJA ndani ya JF na kutoa VIROJA na hatimaye kupigwa BAN kwa sababu ya matusi/lugha za kejeli kwa kuwaita wenzao 'Masaburi', 'Magamba',Magwanda','Unafikiri kwa kutumia Masaburi', Bi Kiroboto' N.k......Itakuwa ni dhihaka kwa wapigania Uhuru wa aina ya Mandela kufananishwa na wana JF wanapigwa BAN kwa kutukana na kuharibu mijadala/kuvunja sheria za JF ....

Nijuacho mimi BAN inatolewa kwa mtu anayevunja sheria za JF na si kwa kuonewa kama ilivyokuwa kwa akina Mandela na wenzake......

Itakuwa ni kichekesho kumpa Tuzo mtu ambaye kutwa anashinda JF kuharibu hoja/mijadala kwa matusi na lugha zisizo za kistarabu na baadae kupigwa BAN....

Tafakari........Chukua Hatua
Mkuu sina haja ya kuendelea na huu mjadala lakini jambo moja nataka kuliweka sawa kwamba Mandela, Sisulu, Mbeki na wenzao walifungwa kwa KUVUNJA SHERIA. Ndio maana nikasema kwa mujibu wa makaburu na sheria zao, Mandela na wenzake walifungwa kwa uhaini. Victorie Ingabire wa Rwanda anashitakiwa kwa uhani (kwa mujibu wa sheria) lakini ukiangalia kwa makini ni suala la kisiasa. Akifungwa atakuwa amehukumiwa kwa uhaini na wala si kwa kuanzisha chama cha siasa. Hayo tu.

Niseme tu kwamba kufungwa/ban inategemea unaingalia kwa macho gani. Mimi binafsi si muumini wa matusi na sipendi jukwaa hili liwe jukwaa la matusi. Kama kweli mtu alifungiwa kwa matusi ni halali laikini kama ni kwa tofauti tu ya maoni; hapana.
 
Lazima nilishupalie kwakuwa naona bila kufanya hivyo hii tuzo itakosa maana kwa kuruhusu waporomosha matusi, wazushi na wapika majungu nao kujiita wanasiasa!

Mkuu Bala nimekusoma tuko pamoja, naona watu wanataka kumtumia vibaya mzee Madiba kuficha madhaifu yao.[/QUOTE]


Mkuu ya Madiba nimeitoa mimi kwa minajiri ya kuonyesha tu hawa wafungwa wa kisiasa. Sikuwa na haja ya kuficha udhaifu wowote ule. Mimi binafsi sijawahi kupigwa ban hapa jukwaani na wala sijatukana.
 
Kimbunga,
Majibu niliyompa rejeo ndio hoja yangu. Kwa msisitizo ni kwamba Mandera hakuwa mzushi wala muongo, alikuwa anawaambia ukweli watu wake-weusi lakini pia alikuwa anawapasha ukweli makaburu. Sasa makaburu kwa kuhofia kupoteza madaraka yao ya kuiongoza nchi ilibidi wamfunge.
Tofauti na Mandera wanasiasa wengi wanaokula ban hapa jf ni kwa sababu za kutukana, uongo, uzushi na mambo mengine ya kitoto.
Tukiruhusu wapate tuzo basi tutakuwa tunawapongeza kwa ''kazi nzuri'' ya kulidhalilisha jukwaa la siasa hapa JF!
Muraaaaa Mwita, tata Amang'ana gasarekire!
 
Wakuu

Wakati mnaendelea na mjadala, msisahau kufanya nominations la sivyo mtakuta candidate mnaowategemea hawapo.

Ni angalizo tu.
 
Wakuu mie naombeni maelezo kifupi, wapi faiza fox siku hizi? Nn kimempata. Pia nampendekeza Josphine Mshumbuzi.
 
SlidingRoof (hiki kichwa hatari tupu!),Mchambuzi na Mwanakijiji (hawa ni kwa Male politician) and Faiza Foxy hana mpinzani kwa kina dada!!
 
Ila napendekeza MM Mwanakijiji atolewe ili washindani wengine washindanishwe kwa haki! Tukubali MM Mwanakijiji akiwemo hakuna wa hata kumfuata!!
 
Mzee Mwanakijiji (Male)
Faiza Foxy (female)
Kumbukeni, tunaongea kuhusu 2011, sio 2012...
 
Napendekeza Paka Jimmy kwa wanaume - ananifurahisha anavyojenga na kutetea hoja zake hapa jamii forum
Kwa wanawake nampa Big Up Faiza Foxy japo siku hizi ameadimika lakini huwa ukifuatilia hoja zake unaenjoy, ni mbishi kwa kutetea hoja zake hakubali kushindwa hata kidogo hata pale anapotakiwa kushindwa.
 
Ha ha haaaa. Kimbunga umeanza viroja sasa.
Hivi kwa hali kama hii ukikosa tuzo utalalamika?

Superman tuvumiliane kidogo ili tukamilishe ule mchakato wetu wa kawaida kwa wanasiasa wa kufanya feasibility study!!


Mkuu nilikuwa nakukumbusha tu siyo viroja, lakini ahsante. Siwezi kukosa tuzo kwa hilo!

Superman mimi kwenye male politician nampendekeza Mchambuzi. Huyu Mkuu huwa anatoa uchambuzi wa kisiasa ulioenda shule na si shule ya kata bali zile za middle school. Japokuwa nadhani ni muumini wa CCM lakini hutoa uchambuzi wake ambao hauko biased na huwa havutwi na mahaba kwa chama chake.
 
kwenye uchambuzi wa kisiasa napendekeza, NGURUVI 3, MUSHI, MWITA MANYARA, MKANDALA

NB. napendekeza kushindanisha na mtu anayetoa vya jikoni na vyakutoka UWT, mfano JB, MTOA HABARI, HUTAKI UNAACHA, WA 16 ...........
 
Ila napendekeza MM Mwanakijiji atolewe ili washindani wengine washindanishwe kwa haki! Tukubali MM Mwanakijiji akiwemo hakuna wa hata kumfuata!!

Vigezo gani hivi mkuu?
Toa sababu ya maana kwa nini tusimchague Mzee Mwanakijiji?
 
Nampendekeza, ''Hutaki Unaacha'' kwa upande wa politician man. Huwa namkubali sana kwenye mada zake hasa ile yenye tittle isemayo ''JK huu Mtandao ni hatari , Usipoangalia waweza kuwa History Party I.'' Na pia Histort party II. Bravo sana Hutaki Unaacha!! Kwa upande wa politician lady nampendekeza Josephine Mshumbuzi. Huyu mama huwa akirusha thready yake inapata mshiko sana hapa JF. Akirusha tu utashangaa wanabody waliokuwa likozo wote wanajitoza pasipojulikana wanakotokea. Bravo sana sister J. Mshumbuzi!!
 
Back
Top Bottom