Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,504
- 113,617
Wanabodi,
Hili ni bandiko la pongezi kwa jeshi letu la polisi. Wewe kama ni mmoja wa wale wenye allergy na pongezi zozote kwa awamu hii ya tano, naomba nikushauri, uishie hapa ili tusiharibiane siku.
Nasisitiza, jeshi letu la polisi likifanya vyema, lipongezwe!, hongera FFU kusambaratisha maandamano ya jana pale ubalozi wa Afrika Kusini bila virungu, bila mabomu ya machozi, bila maji ya washa washa, na bila risasi za moto, hivyo maandamano hayo kusambaratishwa bila kutokea kwa maafa yoyote!.
Niliwahi kuzungumzia humu kuwa taasisi yeyote ikifanya jambo zuri la kustahili pongezi, ipongezwe as encouragement izidi kutenda mazuri hayo!.
Kufuatia kusambaratishwa huko kwa yale maandamano ya jana, jeshi letu la polisi, limeonyesha uwezo, linastahili pongezi.
Pongezi hizi ni kufuatia a simple comparative analysis ya kusambaratishwa maandamano haya ambapo mimi niliuliza swali hili humu jf, Je, Polisi washitakiwe kusababisha vifo kizembe vya random shootout? RIP Aqulina Akwilini, Baftaha, She is an Angel!
Kuhusiana na polisi wetu na maandamano yasiyo na vibali, wakati wapinzani walipounda UKUTA na kupanga kuandamana, niliwahi kutoa ombi hili kwa jeshi letu la polisi Ombi Muhimu Kwa Jeshi Letu La Polisi."Nyinyi ni Wenzetu, September Mosi, Please Msigeuke Makaburu!".
Hivyo kama kumetokea maandamano ya amani yasiyo na kibali, yamesambaratishwa kwa amani, bila kuleta maafa yoyote, hili ni jambo jema kwa jeshi letu la polisi kustahili pongezi, ili hii sasa ndio iwe standard format ya usambaratishaji wa maandano yasiyo na vibali.
Kumbe polisi wetu wanaweza kusambaratisha maandamano bila kuleta maafa, na utaratibu huu ungeanza tangu zamani, ungekuta saa hizi Daudi Mwagosi yupo akiendelea na kazi na kuihudumia familia yake, ambayo hata sijui saa hizi inahudumiwa na nani na ina hali gani!. Ungekuta saa hizi Aquiline Akwilin, angekuwa anamaliza kozi yake na kugraduate, aje apate kazi nzuri, apate mchumba, aolewe ajenge familia yake na kujenga taifa la Tanzania.
RIP Daudi Mwangosi, RIP Aquiline Akwilin, Hongera Jeshi letu la Polisi, Hongera FFU wetu, kumbe mkiaamua kwa dhati kulinda amani na kulinda raia na mali zao, mnaweza.
Hongera sana IGP Sirro na vijana wako,
bila kusahau kutoa hongera kwa CinC maana...
Paskali.
Rejea zangu kwa Jeshi la Polisi na Maandamano
Je, Polisi washitakiwe kusababisha vifo kizembe vya random ...
Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? - JamiiForums
Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...
Hili ni bandiko la pongezi kwa jeshi letu la polisi. Wewe kama ni mmoja wa wale wenye allergy na pongezi zozote kwa awamu hii ya tano, naomba nikushauri, uishie hapa ili tusiharibiane siku.
Nasisitiza, jeshi letu la polisi likifanya vyema, lipongezwe!, hongera FFU kusambaratisha maandamano ya jana pale ubalozi wa Afrika Kusini bila virungu, bila mabomu ya machozi, bila maji ya washa washa, na bila risasi za moto, hivyo maandamano hayo kusambaratishwa bila kutokea kwa maafa yoyote!.
Niliwahi kuzungumzia humu kuwa taasisi yeyote ikifanya jambo zuri la kustahili pongezi, ipongezwe as encouragement izidi kutenda mazuri hayo!.
Kufuatia kusambaratishwa huko kwa yale maandamano ya jana, jeshi letu la polisi, limeonyesha uwezo, linastahili pongezi.
Pongezi hizi ni kufuatia a simple comparative analysis ya kusambaratishwa maandamano haya ambapo mimi niliuliza swali hili humu jf, Je, Polisi washitakiwe kusababisha vifo kizembe vya random shootout? RIP Aqulina Akwilini, Baftaha, She is an Angel!
Kuhusiana na polisi wetu na maandamano yasiyo na vibali, wakati wapinzani walipounda UKUTA na kupanga kuandamana, niliwahi kutoa ombi hili kwa jeshi letu la polisi Ombi Muhimu Kwa Jeshi Letu La Polisi."Nyinyi ni Wenzetu, September Mosi, Please Msigeuke Makaburu!".
Hivyo kama kumetokea maandamano ya amani yasiyo na kibali, yamesambaratishwa kwa amani, bila kuleta maafa yoyote, hili ni jambo jema kwa jeshi letu la polisi kustahili pongezi, ili hii sasa ndio iwe standard format ya usambaratishaji wa maandano yasiyo na vibali.
Kumbe polisi wetu wanaweza kusambaratisha maandamano bila kuleta maafa, na utaratibu huu ungeanza tangu zamani, ungekuta saa hizi Daudi Mwagosi yupo akiendelea na kazi na kuihudumia familia yake, ambayo hata sijui saa hizi inahudumiwa na nani na ina hali gani!. Ungekuta saa hizi Aquiline Akwilin, angekuwa anamaliza kozi yake na kugraduate, aje apate kazi nzuri, apate mchumba, aolewe ajenge familia yake na kujenga taifa la Tanzania.
RIP Daudi Mwangosi, RIP Aquiline Akwilin, Hongera Jeshi letu la Polisi, Hongera FFU wetu, kumbe mkiaamua kwa dhati kulinda amani na kulinda raia na mali zao, mnaweza.
Hongera sana IGP Sirro na vijana wako,
bila kusahau kutoa hongera kwa CinC maana...
Paskali.
Rejea zangu kwa Jeshi la Polisi na Maandamano
Je, Polisi washitakiwe kusababisha vifo kizembe vya random ...
Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? - JamiiForums
Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...