Uvamizi wa Maandamano ya Wananchi Mbeya, Kosa ni la Polisi au Biteko?

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,056
Mkitaka kufanya maandamano ya aina yoyote ile yawe ya shughuli za kisiasa, kidini, michezo au yawayo yoyote, sheria inawataka kulitaarifu jeshi la Polisi. Japo polisi hawana mamlaka ya kuzuia maandamano lakini wanaweza kutoa ushauri hata wa kuahirisha au kubadilisha njia kutokana na mazingira ya siku hiyo au shughuli nyinginezo za siku hiyo hiyo. Kwa hiyo, kimantiki, Polisi ndio wanaojua maandamano yanapita wapi, yataishia wapi, na pia wanajua matukio mengine kama vile misafara ya viongozi kwa siku hiyo hiyo.

Kama hakuna dharula kama vile maafa, inatarajiwa kuwa aliyetangulia kupewa au kukubaliwa njia atakayoitumia, ndiye atapewa haki ya kuitumia njia hiyo, na shughuli nyingine ambazo taarifa zake zilifuata baadaye, watalazimika kupewa njia nyingine, maana watakapotaka kuitumia njia ambayo tayari inatumika na aliyetangulia kutoa taarifa, Jeshi la polisi litamwambia huyo mtoa taarifa wa baadaye kuwa tayari barabara hiyo ina tukio jingine.

Sasa kama ilikuwa inajulikana kuwa maandamano ya CHADEMA yalikuwa yanatumia barabara tajwa, ilikuwaje tena Jeshi hilo hilo la polisi kupitisha msafara wa Biteko kwenye barabara hiyo hiyo? Ikumbukwe kuwa Biteko ndiye waziri wa Wizara ya nishati, wizara inayohusika moja kwa moja na ukosefu wa umeme nchini, na moja ya malalamiko yaliyosababisha maandamano hayo ni pamoja na ukosefu wa umeme. Je, kwa tendo lile la msafari wa waziri anayehusika na umeme kuvamia msafara wa waandamanaji wanaolalamikia ukosefu wa umeme haikuwa tendo la kuwatia hasira zaidi wananchi ambao tayari walikuwa wamekwishakuwa na hasira? Je, tendo lile halikuwa linahatarisha usalama wa Biteko na msafara wake, na kwa upande mwingine kuhatarisha usalama wa waandamanaji kama kungetokea vurugu, na polisi kutaka kumwokoa waziri?

RPC wa Mbeya, kwa tukio lile anastahili kuwajibishwa. Labda aseme kuwa walimwelekezo Biteko an alternative road, lakini Waziri , kwa kiburi chake, alilazimisha kuwa angepita katikati ya waandamanaji ili awatie hasira zaidi. Na hilo likidhihirika, basi Biteko anastahili kuadhibiwa.

Wananchi wanaheshimu misafara ya viongozi kiasi cha kuwa tayari kuacha shughuli zao zote kuwapisha viongozi wapite bila usumbufu kwa sababu kuna sheria inayoelekeza hivyo. Sasa inakuwaje viongozi hao hao hawataki kuheshimu msafara wa maandamano ya wananchi, tena ambayo yanalindwa kwa sheria na kanuni?

Mwisho wa yote, Polisi au Biteko au wote kwa pamoja, wanatakiwa kuwaomba msamaha wananchi wa Mbeya kwa kufanya tukio lililokuwa limekusudia kuvuruga maandamano ya wananchi.
 
Sio uvamizi Chadema wapagani hata Dini hawana Biblia inasema astahiliye heshima mpe heshima

Wangempisha Kuna shida Gani after all barabara Ina njia mbili wangeendelea kuandamana upande mmoja akipita wanajaa barabara nzima.Kupita huo msafara hauzidi dalika tatu ni kukosa tu hekima Kwa viongozi wa Chadema
 
Sio uvamizi Chadema wapagani hata Dini hawana Biblia inasema astahiliye heshima mpe heshima

Wangempisha Kuna shida Gani after all barabara Ina njia mbili wangeendelea kuandamana upande mmoja akipita wanajaa barabara nzima.Kupita huo msafara hauzidi dalika tatu ni kukosa tu hekima Kwa viongozi wa Chadema
Msafara wa kiongozi ukipita na hata barabara iwe pana namna gani wananchi wanalazimishwa kusimamisha magari na kuegesha pembeni? Uliwahi kusikia wananchi wanaambiwa wapite upande mmoja na msafara wa kiongozi upite upande mwingine?

Wananchi katika umoja wao ni wakuu kuliko kiongozi yeyote mmoja. Wananchi wanastahili kuheshimiwa. Kama viongozi hawataki kuwaheshimu wananchi, basi wananchi nao hawana sababu ya kuwaheshimu viongozi.

Kwani Biteko toka mwanzo angepita huko alikopita, angepungukiwa nini?

Wananchi walitangulia kupewa hiyo njia kwaajili ya shughuli ya maandamano, alistahili kuheshimu hilo. Lakini yawezekana siyo tatizo la Biteko, bali Polisi.
 
Sio uvamizi Chadema wapagani hata Dini hawana Biblia inasema astahiliye heshima mpe heshima

Wangempisha Kuna shida Gani after all barabara Ina njia mbili wangeendelea kuandamana upande mmoja akipita wanajaa barabara nzima.Kupita huo msafara hauzidi dalika tatu ni kukosa tu hekima Kwa viongozi wa Chadema

Suala siyo muda bali ujumbe unaoupeleka kwa watu kwa kitendo hicho. Ni sawa uwe unaishi mtaani. Una gari lako. Halafu dereva wako kwa bahati mbaya akamgonga jirani yako mmoja, akafariki. Siku ya maziko, kundi la watu wamebeba jeneza wanaenda kuzika wapo barabarani, nawe ukawapigia honi ya kutaka kupita katikati yao. Ni kweli hutachukua hata dakika 1 kuwapita kama wakikupisha, lakini unapeleka ujumbe gani kwa hao majirani zako?

Watu wanaandamana, moja ya sababu ni ukosefu wa umeme. Anayelalamikiwa kusababisha ni TANESCO ambayo kwa sasa ipo chini ya Biteko. Watu wanaandamana kutokana na janga la kukoseshwa umeme, anayesababisha anawapigia honi waandamanaji, anataka apite katikati yao!! Hii inaweza kutafsiriwa ni kiburi, kejeli na dharau dhidi ya waandamanaji.
 
Sio uvamizi Chadema wapagani hata Dini hawana Biblia inasema astahiliye heshima mpe heshima

Wangempisha Kuna shida Gani after all barabara Ina njia mbili wangeendelea kuandamana upande mmoja akipita wanajaa barabara nzima.Kupita huo msafara hauzidi dalika tatu ni kukosa tu hekima Kwa viongozi wa Chadema
Umeme uwe wa shida kisha anayewajibika na umeme ajipitushe mbele ya wenye hasira ya kukosa umeme utegemee watamchekea?
 
Kilichotokea hapo kimeonesha nini kipo kwenye vichwa vya polisi wetu, siku zote wanawachukulia viongozi wa serikali na CCM kama mabosi wao na mabosi wetu raia, wanawaona wao wapo juu ya sheria.

Nafahamu walijua hiyo njia wanayompitisha Dr. Biteko inatumiwa na Chadema kwa maandamano, lakini kwasababu waliamini wanampitisha mkuu wao, basi wakajua hata waandamanaji wangempisha wakasahau maandamano yapo kisheria, na wa kwanza kuitumia barabara ndio mwenye haki hiyo.

Kwanini Dr. Biteko asingepitishwa kwenye barabara nyingine tofauti? siamini kama haipo hiyo barabara, hiki ndicho kinathibitisha ubosi walionao viongozi wa serikali na CCM kwa jeshi letu la polisi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Umeme uwe wa shida kisha anayewajibika na umeme ajipitushe mbele ya wenye hasira ya kukosa umeme utegemee watamchekea?
Na tena wangemchinja wangetuma ujumbe safi sana. Labda huko serikalini wangejua zaidi maana ya neno, “ ameuwa na watu wenye hasira kali”…na Kwa siku zijazo dhihaka Kama hizi za Biteko zingekoma kabisa…
 
Back
Top Bottom