Jee Bunge La Dharura Kuitishwa?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,599
Wanabodi,

JK ameteua wabunge watatu wapya na kuna uwezekano wawili kati yao atawateua mawaziri!.

Ili mtu kuteuliwa waziri lazima kwanza uwe mbunge. Mtu akiteuliwa Mbunge, hawi mbunge bali huwa mbunge mteule mpaka baada ya kuapishwa!.

Mbunge mteule hawezi kuteuliwa kuwa waziri mpaka kwanza awe mbunge!.

Hivyo jee kutaitishwa kikao cha bunge la dharura ili hao wateuliwa wapya waukwae uwaziri, au JK atatuvunjia tena katiba kwa kututeuliwa mawaziri ambao sio wabunge bali ni wabunge wateule?!.

Ila kama atambadili PM basi ni lazima kwanza bunge la dharura likutane kupitisha jina la PM, then PM na Rais ndio wakae chini kupendekeza baraza la mawaziri!.

Subirieni taarifa ya kikao cha bunge la dharura!.

Pasco.
 
Wanabodi,

JK ameteua wabunge watatu wapya na kuna uwezekano wawili kati yao atawateua mawaziri!.

Ili mtu kuteuliwa waziri lazima kwanza uwe mbunge. Mtu akiteuliwa Mbunge, hawi mbunge bali huwa mbunge mteule mpaka baada ya kuapishwa!.

Mbunge mteule hawezi kuteuliwa kuwa waziri mpaka kwanza awe mbunge!.

Hivyo jee kutaitishwa kikao cha bunge la dharura ili hao wateuliwa wapya waukwae uwaziri, au JK atatuvunjia tena katiba kwa kututeuliwa mawaziri ambao sio wabunge bali ni wabunge wateule?!.

Ila kama atambadili PM basi ni lazima kwanza bunge la dharura likutane kupitisha jina la PM, then PM na Rais ndio wakae chini kupendekeza baraza la mawaziri!.

Subirieni taarifa ya kokao cha bunge la dharura!.

Pasco.

Mkuu Pasco tangia juzi tumekuwa tukiongelea suala hili na tulikuwa tukiongelea kama Rais angetaka kumtumia Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa UN kwenye baraza lake la mawaziri. Ingebidi amteue kuwa mbunge kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1) (e). Na mbunge anatakiwa aaape. Lakini nimepata hii ibara 68 inasema hivi, "Kila mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za bunge ..." Labda watatumia haka kakifungu kwamba anaweza akashika madaraka ya uwaziri lakini kabla hajashiriki shughuli za bunge akaapishwa. Jinsi nionavyo huenda hakuna Bunge la dharura. Angeliitisha kabla hata hajatangaza wateule. Kwa kuwa huwezi kuitisha bunge la dharura ndani ya siku mbili; nadhani kwa uchache inabidi wapate taarifa hata wiki moja kabla.
 
Kuendelea na Pinda ni kurudi kulekule Misri!
Pinda atasababisha hata mawaziri waliokuwa wazuri waanze kuiba hela zetu, maana watajihakikishia kutoguswa na mtu!
Whatever new faces that the president could employ into his cabinet, with Pinda being the PM, everything will go into shambles...ni kama mmasai kuingia disco na sime!
 
...labda mabadiliko ni juni.
Au wataapa baadae kama sio ofisi ndogo za bunge.
 
Kuendelea na Pinda ni kurudi kulekule Misri!
Pinda atasababisha hata mawaziri waliokuwa wazuri waanze kuiba hela zetu, maana watajihakikishia kutoguswa na mtu!
Whatever new faces that the president could employ into his cabinet, with Pinda being the PM, everything will go into shambles...ni kama mmasai kuingia disco na sime!


....Mkuu nakubaliana nawe lakini si Pinda pekee hata kuendelea kuwepo msanii pale Ikulu ni janga kubwa la Taifa. Sioni kipya chochote ha kuwatia moyo Watanzania kuhusu mabadiliko katika utendaji Serikalini kati ya sasa na 2015.
 
Mkuu Pasco tangia juzi tumekuwa tukiongelea suala hili na tulikuwa tukiongelea kama Rais angetaka kumtumia Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa UN kwenye baraza lake la mawaziri. Ingebidi amteue kuwa mbunge kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1) (e). Na mbunge anatakiwa aaape. Lakini nimepata hii ibara 68 inasema hivi, "Kila mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za bunge ..." Labda watatumia haka kakifungu kwamba anaweza akashika madaraka ya uwaziri lakini kabla hajashiriki shughuli za bunge akaapishwa. Jinsi nionavyo huenda hakuna Bunge la dharura. Angeliitisha kabla hata hajatangaza wateule. Kwa kuwa huwezi kuitisha bunge la dharura ndani ya siku mbili; nadhani kwa uchache inabidi wapate taarifa hata wiki moja kabla.


Mkuu Kimbunga,
Hata mimi nilikuwa na mashaka sana juu ya jambo hilo, kwamba mbunge mteule anawezaje kuteuliwa kuwa waziri kabla hajaapishwa?
Kama ulivyofafanua, ndivyo niliisikia BBC jana jioni wakim-quote katibu wa bunge kwamba wanaweza kuteuliwa kuwa mawaziri na wakaendelea na majukumu yao isipokuwa yale tu ya kibunge. Kwa mfano kujibu maswali bungeni.

Kwahiyo Kikwete atakuwa ameshapata ushauri mapema kabla ya kufanya uteuzi wa wabunge ili akamilishe kazi yake ya kulisuka upya baraza la mawaziri. Sitegemei kabisa kuwepo kwa bunge la dharura kwa ajili ya hoja ya kumjadili waziri mkuu. Hata hivyo matarajio yangu ni kwamba Pinda ataendelea kuwa waziri mkuu hadi akamilishe ngwe yake sioni dalili za kikwete kumtosa.
 
Last edited by a moderator:
Ndani ya katiba hakuna mnachoita "Bunge la Dharura". Hata hivyo, uwezekano wa kuitwa hilo mnaloliita "Bunge la Dharura" kwa hali ya sasa kinaweza kutokea kwa sababu mbili:

1:
JK asipoteua leo Cabinet, basi Jumatatu Zitto na wale wenzake 70 wataanza kumbana Spika kuwa anasubiri nini kuhusu hoja yao ambayo kikatiba inataka kuanzia Jumatatu uanze mchakato wa kuwaita wabunge Dodoma wapige kura ya kutokuwa na Imani na PM. Hoja hii inajitegemea na haina uhusiano na siasa au porojo zinazoendelea nje ya Bunge, bila kujali ni Ikulu, magzetini au mitandaoni. Kuna mada tuliijadili hapa last week imeliweka vizuri sana hili. Link yake hii hapa:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...zi-cha-zitto-kinavyomtesa-spika-serikali.html


2:
JK akiteua Mawaziri na aakaondokana na Pinda, basi hilo BUnge lazima liitwe.

NB:

Haya ni mambo mawili ambayo lazima moja litokee ili bunge liitwe ndani ya hizi wiki mbili. Na kutokana na mazingira inaelekea mojawapo linaweza kutokea.
 
Mkuu Kimbunga,
Hata mimi nilikuwa na mashaka sana juu ya jambo hilo, kwamba mbunge mteule anawezaje kuteuliwa kuwa waziri kabla hajaapishwa?
Kama ulivyofafanua, ndivyo niliisikia BBC jana jioni wakim-quote katibu wa bunge kwamba wanaweza kuteuliwa kuwa mawaziri na wakaendelea na majukumu yao isipokuwa yale tu ya kibunge. Kwa mfano kujibu maswali bungeni.

Kwahiyo Kikwete atakuwa ameshapata ushauri mapema kabla ya kufanya uteuzi wa wabunge ili akamilishe kazi yake ya kulisuka upya baraza la mawaziri. Sitegemei kabisa kuwepo kwa bunge la dharura kwa ajili ya hoja ya kumjadili waziri mkuu. Hata hivyo matarajio yangu ni kwamba Pinda ataendelea kuwa waziri mkuu hadi akamilishe ngwe yake sioni dalili za kikwete kumtosa.

Naaam Mwita Maranya nimekuwa nikipitia Katiba ndio nikaona hilo. Ila kama angemtoa Waziri Mkuu ingebidi kwanza atangaze kulivunja baraza la mawaziri (au PM ajiuzulu - automatically baraza linavunjika) , aitishe bunge kumpitisha jina la PM kisha wakae na PM kushauriana kuunda baraza jipya.

Kwa hali ilivyo sasa kinachofanyika ni mabadiliko ya baraza la mawaziri na Pinda ndiye Waziri Mkuu pasipo na shaka yoyote.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kimbunga,
Hata mimi nilikuwa na mashaka sana juu ya jambo hilo, kwamba mbunge mteule anawezaje kuteuliwa kuwa waziri kabla hajaapishwa?
Kama ulivyofafanua, ndivyo niliisikia BBC jana jioni wakim-quote katibu wa bunge kwamba wanaweza kuteuliwa kuwa mawaziri na wakaendelea na majukumu yao isipokuwa yale tu ya kibunge. Kwa mfano kujibu maswali bungeni.

Kwahiyo Kikwete atakuwa ameshapata ushauri mapema kabla ya kufanya uteuzi wa wabunge ili akamilishe kazi yake ya kulisuka upya baraza la mawaziri. Sitegemei kabisa kuwepo kwa bunge la dharura kwa ajili ya hoja ya kumjadili waziri mkuu. Hata hivyo matarajio yangu ni kwamba Pinda ataendelea kuwa waziri mkuu hadi akamilishe ngwe yake sioni dalili za kikwete kumtosa.

Hivi kwa nini tunakimbilia kudhani lazima apate ushauri kwa masuala mengine ambayo ni rahisi sana. Hebu tusome ibara zifuatazo za Katiba, ili tuone ilivyo wazi hata mtoto wa primary akisoma ataelewa:


{KATIBA: 55(4)}:
Mawaziri na Naibu Mawaziri wote watateuliwa kutoka miongoni mwa Wabunge

{KATIBA: Ib. 56}:
Waziri au Naibu Waziri hatashika madaraka yake ila mpaka awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

{KATIBA: Ib. 51(1)}:
Muda wa kushika madaraka ya Waziri na Naibu Waziri utaanza tarehe atakapoteuliwa kushika madaraka hayo.
 
Mamlaka ya rais ni kuteua Mbunge kuwa waziri ila Hana mamlaka ya kumteua Mbunge mteule ie Mbunge ambaye hajala kiapo kuwa waziri. Maelezo ya katibu wa bunge yanaishia kwenye bunge tuu, hatuwezi kustretch kwa mawaziri. Ndio maana hata marehemu sumari alipofariki pamoja na kuwa hakuwa ameapa na hakufanya kazi yoyote ya kibunge lakini lakini bunge lilimtambua Kama hivyo.

Waziri asiye Mbunge akila kiapo cha uwaziri basi kiapo litakuwa batili.

Hayo hapo juu hayaharamishi rais kuteua Mtu asiyenasifa kuwa waziri, lakini hatafanya kazi ya uwaziri aliyoteuliwa mpaka atakapoapa.
 
Hivi kwa nini tunakimbilia kudhani lazima apate ushauri kwa masuala mengine ambayo ni rahisi sana. Hebu tusome ibara zifuatazo za Katiba, ili tuone ilivyo wazi hata mtoto wa primary akisoma ataelewa:

Vuta pumzi kidogo Nikupateje ili uelewe kinachozungumzwa hapa.
Ndio maana kuna ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, kikwete ama raisi yeyote hawezi kufanya/kujua kila kitu, vinginevyo asingehitaji kuwa na Jaji Werema.

{KATIBA: Ib. 56}:
Waziri au Naibu Waziri hatashika madaraka yake ila mpaka awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Ibara hii, hasa huo mstari nilio-highliht ndio ulisababisha madukuduku yote hadi tukaanza kuhoji na kutafuta ushauri kwa wajuzi wa sheria, na bila shaka hata raisi kikwete alim-consult werema ili kuona kwamba kama atawateua wabunge wateule kuwa mawaziri asikiuke katiba.
 
Last edited by a moderator:
Nikupateje, bunge la dharura lipo, niko mobile nikitulia nitakuletea vifungu
 
Mamlaka ya rais ni kuteua Mbunge kuwa waziri ila Hana mamlaka ya kumteua Mbunge mteule ie Mbunge ambaye hajala kiapo kuwa waziri. Maelezo ya katibu wa bunge yanaishia kwenye bunge tuu, hatuwezi kustretch kwa mawaziri. Ndio maana hata marehemu sumari alipofariki pamoja na kuwa hakuwa ameapa na hakufanya kazi yoyote ya kibunge lakini lakini bunge lilimtambua Kama hivyo.

Waziri asiye Mbunge akila kiapo cha uwaziri basi kiapo litakuwa batili.

Hayo hapo juu hayaharamishi rais kuteua Mtu asiyenasifa kuwa waziri, lakini hatafanya kazi ya uwaziri aliyoteuliwa mpaka atakapoapa.

Mkuu Ngambo Ngali, kama sijakuelewa vizuri ama unajichanganya maelezo yako.

Unasema raisi hawezi kumteua mbunge mteule kuwa waziri kwakuwa bado hajala kiapo.
Lakini hapo hapo unamtaja marehemu sumari ambaye hakuwa ameapishwa kuwa mbunge lakini alipofariki alipewa heshima zote za mbunge, sasa hapo tofauti ni nini kati ya mbunge mteule na mbunge aliyekula kiapo?


Kama unakubali na kutambua kwamba maelezo ya katibu wa bunge yanaishia kwenye bunge tu, na katibu huyo wa bunge amaefafanua kwamba waziri atakayeteuliwa huku akiwa mbunge mteule atafanya kazi zote za uwaziri isipokuwa tu zile zinazohusiana na bunge mathalani kuingia bungeni kujibu maswali n.k, kwa maana hiyo basi raisi anaweza kumteua mbunge mteule kuwa waziri na hatokuwa amevunja katiba.
 
Last edited by a moderator:
{KATIBA: 55(4)}:
Mawaziri na Naibu Mawaziri wote watateuliwa kutoka miongoni mwa Wabunge
Kifungu hicho kimemaliza kila kitu!. Kiukweli hakuna uhakika wabunge walioteuliwa ndio sura mpya kwenye BM yote ni speculations tuu!.

Ila lazima nikiri baadhi ya teuzi za JK leave much to be desired!. Sikuona mantiki ya kumteua Mama Meghji mpaka sasa sina kumbukumbu kama amewahi kuchangia chochote!.

Bunge lililopita aliwateua Mama Mbene na Jussa kuwa wabunge at 11th hour!. Kwa kumbukumbu yangu Mama Mbene alichangia mara 1 tuu mpaka bunge lilipovunjwa!. Sasa kama kamteua tena asipompa uwaziri au unaibu then sisi tunaomfahamu vizuri JK tutajua huo ni uteuzi wa asante kwa mambo yetu yale!.
 
Back
Top Bottom