Je nimpe talaka au nifanyaje

Ndoa Ndoano baba, yawezekana mengi uliyafumbia macho wakati wa uchumba wenu, sasa yanakuumiza, sasa mbona hii inaoneka kama ni story ya upande mmoja tu? wewe umemfanyia nini mwenza wako labda kuna kitu na yeye hakipendi, au ulimfanyia kitu kibaya, kuwa wazi mkuu
 
Nimesoma nikahema. Yote ni kweli au umetia chumvi kidogo?? kwenye suala la haki ya ndoa hujasema, ni shwari au?

Kwa kifupi kama uliyoyasema ni kweli na kama unapenda ndoa yako isivunjike, basi tafuta ndugu wa karibu wa mkeo (mara nyingi shangazi yake wanayeelewana) halafu mweleze yote bila kuficha na umpe kazi ya kumfunda mkeo??


Umesema pia kuwa huwa anakuwa nyumbani?? Kwa hiyo ni mama wa nyumbani??? Amesoma hadi darasa la ngapi?? Maana hata House girl aliyemaliza darasa la saba anaimudu nyumba!!!

Bottom line unapoamua kuoa au kuolewa fanya kazi ya ziada kumpekua mchumba wako hadi uridhike naye angalao 75% na 25% iwe ni yale mazoea ambayo hayana madhara makubwa kwa familia mtakayoijenga. Tofauti na hapo ukisema atabadilika akiwa ndani ya nyumba unajidanganya.

Makosa ni yako, pengine hukufanya upekuzi wa kutosha wakati wa urafiki, uchumba na hatimaye kuoana. Tusaidie lipi na kuacha lipi katika hili gazeti la matatizo ulilotundika hapa. Kweli utajuta na ndiyo maana ukaona ni vema ujiite majuto hapa. Utajutaaa kuzaliwa!!!
 
kweli hii kali,Lakini fanya hivi,

1. Huyo kuna tatizo zaidi ya usafi,labda hujui au hujawa muwazi.Ni psychological problem/matatizo ya akili. ambayo inakimbilia kwenye uzembe,uchafu na uvivu.Mchunguzeujue ana tatizo gani,kisha tafuta wataalamu wa ushauri,wamshauri
2.Tafuta mama mmoja mwaminifu kanisani,kama akiwa mama mchungaji itakuwa nzuri zaidi,awe anakuja hapo nyumbani na kumpa semina ikiwezekana kwa vitendo.Na wakati mwingine atoke kwenda kuona nyumba za wenzie.
3.Mtafutie hausigeli au hausiboi
4.Jina lako la majuto linakufatilia,badilisha.
5.Vumilia huku ukiendelea kumuelekeza.

Na hayo yote yasipoleta matunda, basi aoe mke wa pili mwenye kuonesha mfano na kuleta ushindani, huenda anafanya hivyo kwa kujiachia eti hana upinzani. Au mwanamke huyo hajampenda na hivyo anatafuta sababu za kufunga virago, then hakuna sababu ya kumnyima anachotaka. Kila upandacho ndicho utakachovuna. Hivyo, muonjeshe hiyo joto ya jiwe anayoitafuta. Lakini kwa hali hii, housegirl anaweza kuchukua nafasi yake bila kujua.
 
Kaka Majuto

Kama ni kweli hiyo ni kali ila kila mtu ana mapungufu yake.. Je kuanzia mnaoana yupo hivi mpaka leo? Mawasiliano yenu mazuri yaani kumwelezea hivi vitu vinavyokukera abadilike au umsaidie kubadilika?
Isijekuwa unaelezea yote hapa wakati hujafanya bidii zozote za kumrekebisha hapo kwenye mji wenu..
Niliona ishara mapema ila nilijua mambo yatabadilika punde akisha zoea ugenini, lakini naona muda wapita. Nimeisha ongea sana na nafanya kwa vitendo lakini ukimaliza kufanya anarudia makosa yale yale sasa nimetulia kabisa kwani naongea sana kama kasuku kwenye nyumba. Nitajaribu hii ya kanisani, kwani hata mimi nimeisi kitu kama matatizo ya akili ya kusahau. Kila siku anatafuta vitu vyake ajui alipo ziweka. Hata mtoto mdogo anajua Mama hamsikii baba si hatari hiyo!
 
Ndoa Ndoano baba, yawezekana mengi uliyafumbia macho wakati wa uchumba wenu, sasa yanakuumiza, sasa mbona hii inaoneka kama ni story ya upande mmoja tu? wewe umemfanyia nini mwenza wako labda kuna kitu na yeye hakipendi, au ulimfanyia kitu kibaya, kuwa wazi mkuu
Ubaya wa kungu ni mgumu kubadilisha kwani mwenzangu hapendi ndugu, nawapenda ndugu; hawapendi marafiki especially wa kike ansema hao ni wapenzi wangu akisha pata namba ya rafiki yeyote anampgia simu na kidogo kidogo naona urafiki unakufa hawaji tena nyumbani. Kwa marafiki wanaume anawafukuza kwa kuwa anapo ongea hatumii busara matokeo yake mtu akisha ongea naye kwa muda wanamwacha kama alivyo. Anapenda kufanya shopping sana, nime mwambia lazima tuangalie mbele na kuwa na akiba, anapenda kwenda out sana, nime stop hiyo kwani - pesa jamani. Anataka nikae nyumbani muda wote, nani ataleta mkate ? Kwa ufupi kwake muda ni mwingi sana kwangu sioni muda
 
...uliminya jicho moja ulipomchumbia na kumuoa, yakubidi sasa uyafunge yote mawili upate kuishi naye.

BTW, mapungufu yake yapo ndani ya uwezo wako, ...angekuwa mwasherati tungekuwa tushakuzika.
Akiwa kwao utajuaje huko mwenzangu, akija kwako we si unaona nje poa! nafikiri kucha ilifichwa sana ningelijua nisingeandika haya -
 
Majuto.... Kama walivyoshauri wadau..Mimi naona hapo mwanzo palipokuwepo neno ulikosea... ulikuwa unamfanyia kila kitu ili akukubali... akabweteka na wewe ukaona umeshinda mchezo.... Hiyo fungate baada ya kumuoa imeendelea hadi kufikia hali hii...sasa ameshindwa kurudi kwenye ukweli uu ya maisha.. UNA KAZI KUBWA MNO YA KUMREKEBISHA..TUMIA BUSARA YAKO NA FUATA MOYO WAKO KAMA KWELI UNAMPENDA..MLINDE ABAKI NDAN A NDOA NA MFUNDISHE UHALISIA WA MAISHA YA NDOA NA NYUMBA...
 
MAjuto
Aya yako ni ndefu mno ila umeongea kwa uchungu sana.
Chukua jukumu la kumfulia nguo zake na uwe unahakikisha unaporejea home anakoga na unapotoka naye hata kwenda dukani anakoga, na umnunulie wese na unyunyu wa kufaa.
Kuhusu bajeti, nunua daftari la matumizi halafu kila mnachotumia mwezi huu kiandikwe humo na gharama zake halisi utajua tu ni how much mnatumia na mtajibana vipi. Kingine kikubwa naomba umpeleke shemeji kozi yoyote ile apate ujuzi ambao utasaidia kuongeza japo tonge moja au mbili mezani.

Ukiona umemmchoka just PM me na namba yake nitampa ushauri ambao atafaidika sana
 
Duu inasikitisha sana yaani...yaani ukipata mwanamke kama huyo kwa kweli ni mipango ya mungu tu yaani na mpaka aje kubadilika ita take time kidogo.....ila kama walivyokushauri wadau hapo juu wewe usimuonee aibu mwambie hali halisi kila kitu!!
 
MAjuto
Aya yako ni ndefu mno ila umeongea kwa uchungu sana.
Chukua jukumu la kumfulia nguo zake na uwe unahakikisha unaporejea home anakoga na unapotoka naye hata kwenda dukani anakoga, na umnunulie wese na unyunyu wa kufaa.
Kuhusu bajeti, nunua daftari la matumizi halafu kila mnachotumia mwezi huu kiandikwe humo na gharama zake halisi utajua tu ni how much mnatumia na mtajibana vipi. Kingine kikubwa naomba umpeleke shemeji kozi yoyote ile apate ujuzi ambao utasaidia kuongeza japo tonge moja au mbili mezani.

Ukiona umemmchoka just PM me na namba yake nitampa ushauri ambao atafaidika sana
Nilishatengeneza Excel sheet kwenye computer na kuingiza kila column yeye ni kujaza tu risiti na jina, hilo nalo hafanyi; Nilianza na madafatari lakini madaftari yanapotea kila siku huwezi kujua yanakwenda wapi, ukija kufanya usafi unayakuta yametupwa kwenye stoo. Siwezi nikaweka kitu chochote nje nikaja nikaikuta sehemu yake. Vyombo kila mwaka lazima ninunue upya zote zinavunjwa period! Mfano sasa hivi nimegundua hatuna glasi vikombe inabisi nikanunue upya!!!
 
Pole sana, kuna jamaa alikuwa na tatizo kama lako, alipoona mke hafundishiki aliamua kumrudisha kwao kwa muda - kwa shangazi yake. Aliwaambia amempeleka mke wake afundishwe jinsi ya kutunza nyumba na familia, vinginevyo yeye atashindwa kuendelea kuishi nae - yule dada alijifunza kwa bidii maana ndoa ilikuwa hatarini!
 
Pole sana, kuna jamaa alikuwa na tatizo kama lako, alipoona mke hafundishiki aliamua kumrudisha kwao kwa muda - kwa shangazi yake. Aliwaambia amempeleka mke wake afundishwe jinsi ya kutunza nyumba na familia, vinginevyo yeye atashindwa kuendelea kuishi nae - yule dada alijifunza kwa bidii maana ndoa ilikuwa hatarini!
Nitajaribu ushauri huu nione kama kuna mabdailiko hapo baadaye
 
Mwenzangu anisikii kabisa, amekuwa mbishi umwambii kitu akifanye; anajibizana nami kama watoto,mwana mke wangu ni mchafu sana ina bidi wakati nikichoka nikubali kuwa mchafu kidogo, asafishi nyumba, jiko ni chafu, bafu chafu, ukiweka glass chini sebuleni inaweza kukaa wiki anaipita anaipiga teke na haikoti, si glasi tu kitu chochote, ukinunua vyakula na groceries ukaleta nyumbani anachofanya ni kuyachukua vitu na kutupa ndani ya makabati ukimuhuliza alipoweka kitu ajui. Na akisha weka kitu hakumbuki nini kaweka wapi hata mwaka unapita kitu hakijaguswa mpaka nifanye campeni ya kukagua kila kitu na kuweka nje ili nijue vilipo.
Fridge ni chafu, haipangwi vitu vinatupwa tu ndani yake bila hata kuoshwa vikitoka kwenye store. Chakula akipika nimemwambia siku nyingi inabidi kuya toa kwenye sufuria na kuweka kwenye makopo madogo ndo yawekwe kwenye fridge. Yeye akisha kula ana acha sufuria hapo hapo juu ya jiko bila hata kufunika na vijiko alivyotumia kuchotea chakula anaweka juu ya jiko hapo alafu anakwenda kulala, uki msema anachukua sufuria anaingiza ndani ya fridge na afuniki ingawa zipo wraping-makaratasi ya kufunika vyakula. Vyombo vina lala hapo kwenye sink mpaka kesho yake asubuhi.

Afui shuka mpaka ichafuke kweli au umwambie na akifua nguo au mashuka apigi pasi analundika hapo chini au popote pale alafu ana chambua mmoja baada ya nyingine na kupiga pasi akitaka kwenda sehemu alafu baada muda anarudi kuyafua tena unakuta ngua nyingine wala hazija valiwa zinafuliwa tena; Nimejaribu kuongea na kufundisha lakini asikii, aelewi au hajifunzi
Akilala nimeisha mwambia afunike nywele kwani anaweka dawa lakini afanyi hivyo mashuka na mito yote ina utomvu wa curls, watoto wanashindwa kupumua kwa sababu ya hewa nzito. Nimemnunulia cover ya nywele ya kulala lakini hajui alipo ziweka na ata kama ipo mpaka nimwambie kwa force ndo aweke.

Nnguo zake zina toa harufu mbaya nimemwambia kwa muda mrefu lakini asikii wala hafanyi jitihada kubadilika. Kupika ndo hajui kabisa anajua kupika chakula cha aina mmoja chakula cha mchuzi. Kupika Kuku wa mchuzi na nyama ya mchuzi hajui kupika hata andazi akipika vhapati utavunja meno ngumu kama jiwe. Nimeangalia kwenye internet siku mmoja nikiamka asubuhi nikapika kama mandazi 60 na yakawa mazuri kama ya mama nitilie na watoto wakayapenda lakini ukimwambia apike tena ingwa nimeandika kila kitu hawezi.Anayo internet 24 hours nyumbani
Nikitoka nje wala anipokei wala ani tengei chakula mezani labda kama wote tuko nyumbani ndo anapika alafu anaweka chakula mezani.
Wakati watu wakila yeye akai na watu mezani anakula peke yake, asubuhi namwacha analala wakati nakwenda kazini wala anipikii chai, napika mwenywe. Nawa ogesh watoto kabla ya kuwapeleka shule na kuwa tengea chai. Yeye akiamka anakwenda kwenye nywele za motto ndo anacho jua. Hamsaidii motto na assignment mpaka motto analia nikiingia kuwa mama hanisaidii. Hata kuwasomea watotoneno nalo ni shida nawakuta watoto wana nisubiri niwaombee ili walale yeye wakati huo analala.

Nimemwambia mke wangu awe incharge wa nyumba ajue matumizi yetu ya kila siku lakini hadi leo hajafanya na hajui tunatumia kiasi ghani au tunalipa bill kiasi gain kwa mwezi hajui
Nina ka imani kidogo kabla ya kwenda kulala nataka tisome biblia na kuomba lakini yeye kila siku akisha kula yuko kwenye TV mkitaka kuomba yeye anakwenda kulala.
Sijawahi kumwona mke wangu ameshika kitabu anasoma kitu ambacho ni kibaya sana
Siku nimetoka kazini ghafla nilisahau kitu nyumbani nikarudi nikakuta amekaa chumbani n a chai niliyo mwandalia Baba yangu anaye tutembelea hajamtolea sukari na kikombe anywe hivyo ikabidi nimpe Baba yangu chai. Kusudi baba asione tunashirikiana kumfanyia ubaya nikamuuliza kwa sauti kabisa kwanini hujampa baba chai?

Najua Biblia imeandika uache mke kwa Uasherati tu je hii si zaidi ya uasherati?

Mke wangu afanyi kazi ni mimi ndo naleta kila kitu sasa ni miaka mitano ila naelekea ukingoni. Nilikuwa msafi lakini naelekea kuwa mchafu. Mtoto akitoka shule amwambii akaoghe anamwambia utaoga kesho, dawa akipewa au ya watoto anakunywa mara mmoja tu alafu anatupa hapa mezani – Nifanyaje –Kukwepauchafu nemetoa nguo zangu zote kwenye makabati na kuyafungia kwenye sanduku na nimebadilisha namba ili niwe na nguo hata mmoja ya kutokea, kwani yeye hana nguo ya kutoka zote ni za sokoni na za kutokea

Du pole sana mkuu japo mie sijafikia stage ya kuoa but kwa uliyoyasema hapo yamenistua na kunifanya nitafakari mara mbili mbili juu ya huyo mkeo....but i gues atakua na tatizo hususani la kisaikologia....jaribu kutafuta wataamu wa hilo tatizo.......maana kwa mtu mzima hawezi kua mchafu na careless kiasi hiyo....
....i hope she will change....dont give up kaka she is ua wifey......
 
Nimesoma nikahema. Yote ni kweli au umetia chumvi kidogo?? kwenye suala la haki ya ndoa hujasema, ni shwari au?

Kwa kifupi kama uliyoyasema ni kweli na kama unapenda ndoa yako isivunjike, basi tafuta ndugu wa karibu wa mkeo (mara nyingi shangazi yake wanayeelewana) halafu mweleze yote bila kuficha na umpe kazi ya kumfunda mkeo??


Umesema pia kuwa huwa anakuwa nyumbani?? Kwa hiyo ni mama wa nyumbani??? Amesoma hadi darasa la ngapi?? Maana hata House girl aliyemaliza darasa la saba anaimudu nyumba!!!

Bottom line unapoamua kuoa au kuolewa fanya kazi ya ziada kumpekua mchumba wako hadi uridhike naye angalao 75% na 25% iwe ni yale mazoea ambayo hayana madhara makubwa kwa familia mtakayoijenga. Tofauti na hapo ukisema atabadilika akiwa ndani ya nyumba unajidanganya.

Makosa ni yako, pengine hukufanya upekuzi wa kutosha wakati wa urafiki, uchumba na hatimaye kuoana. Tusaidie lipi na kuacha lipi katika hili gazeti la matatizo ulilotundika hapa. Kweli utajuta na ndiyo maana ukaona ni vema ujiite majuto hapa. Utajutaaa kuzaliwa!!!
Hakuna chumvi hiyo ndo summary kidogo tu ... mengine sisemi!
 
Majuto.... Kama walivyoshauri wadau..Mimi naona hapo mwanzo palipokuwepo neno ulikosea... ulikuwa unamfanyia kila kitu ili akukubali... akabweteka na wewe ukaona umeshinda mchezo.... Hiyo fungate baada ya kumuoa imeendelea hadi kufikia hali hii...sasa ameshindwa kurudi kwenye ukweli uu ya maisha.. UNA KAZI KUBWA MNO YA KUMREKEBISHA..TUMIA BUSARA YAKO NA FUATA MOYO WAKO KAMA KWELI UNAMPENDA..MLINDE ABAKI NDAN A NDOA NA MFUNDISHE UHALISIA WA MAISHA YA NDOA NA NYUMBA...
Hii kweli nilijaribu kumpa kila alichotaka naziada wakati fulani nikiwa na maana nzuri ya ubinadamu
 
........This is terrible wife!! Huyu mdada anahitaji kufundwa kwa mara ya pili.

Vile vile mtu wa kulaumiwa hapa ni mama yake kama alilelewa na mama yake mzazi. Uchafu aliokuwa nao ni kwamba kapitiliza. I'm so sorry for u, I know u love your wife ndio maana hadi leo mpo pamoja. Muhimu hapo tafuta wamama watu wazima wakae naye chini na kumueleza A to Z kuhusu mwanamke na usafi. Vp usafi wa mwili wake upoje?
 
Back
Top Bottom