Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,305
- 12,969
ITV ni kituo kikongwe na kikubwa hapa nchini ambacho hutegemewa na watazamaji wengi kwa habari na burudani. Mimi ni mmoja wa watu wanaokiamini sana kituo hicho hasa kwa taarifa za habari kwakuwa huwa wanajitahidi kuwa neautral na kufanya coverage kubwa. Ushauri wangu kwao ni kuwa wafanye kila jitihada kuhakikisha kuwa wanaingiza channel yao katika king'amuzi cha Dstv ili kujitanua zaidi kwani king'amuzi hicho ni cha kimataifa. Sidhani kama ITV wanaweza kushindwa na TBC, Channel 10 na Star tv ambavyo vinapatikana katika Dstv. Uongozi harakisheni hilo.