Inawezekana vipi mtu kuweka roho yake kwenye mti?

Kwani unataka tuanze kukuelezea namna wazungu walivyoua mila desturi na tamaduni zetu, na kisha kuweka mifumo ambayo itatulemaza milele?!
Mzee wako kaweka roho msituni hafi ila mwili unaoza. Mzungu anakuzuiaje kutoa hiyo taarifa? Mbona ukirikodi tu video na kuelezea kinachoendelea waandishi wa habari watajazana hapo. Ikitokea mara nyingi hiyo elimu itakuwa wazi.

Kuna shida mahali.
 
Haya ni mazindiko ya kiafrika, roho haikai kwenye mti ila anafanya zindiko anaungana na ule mti ukitaka kumuua ni mpaka ule mti ufe kwanza. Hizi zilitumika kama kinga enzi zile watu wanatekwa maporini safari za miguu hamna magari. Zipo nyingi ambazo nimewahi kuziona in action ni kama;
1. Dawa ya mbio- hii kulikuwa na jambazi sugu wanamtafuta kila wakija akitoka mbio hata mbwa hawafati hiyo speed ya jamaa.

2. Kukosekana kwenye hatari- hii mtu akija akudhuru anakuwa hakuoni, walihangaika na huyo mtu mpaka wakaamua kuua mwanae kwa hasira baada ya kumkosa muhusika kila wakati.

3. Dawa ya kurusha ngumi- hii ukimpiga mtu ngumi anazikwa, inafanya kazi pale tu unapokuwa unaonewa lakini ukianzisha ukorofi utapigwa kama ngoma.

4. Dawa ya kurusha jiwe au fimbo - hii kama mtu kakukimbia na huwezi mpata basi ukichukua kitu chochote ukarushia uelekeo wake humkosi, hata awe mbali wa viwanja 3 vya mpira.

Na zingine kibao kwa nyie watoto wa miaka ya 90 na 2000 hamuwezi elewa.
Sahihi kabisa, kumbe humu wazee wezangu mpo wengi sana. Kujitafuta kuna mengi sana, enzi zetu lazima uage nyumbani na hayo ndo mazindiko yenyewe tuliofanyiwa kabla hatujaondoka.
 
Ni kweli, kijijini kwetu kuna bibi mmoja yeye mtoto mchanga hata augue vipi ukimpelekea anamwangalia anakwambia njoo kesho na kiasi flani cha pesa uchukue dawa yako, na asilimia 90 ya watoto wanaponea kwake na dawa za mitishamba za majani na mizizi
Bibi kwanini msimfate akaweka wazi hiyo elimu ya matibabu? Au wazungu wamewazuia?
 
Mimi naamini kwa 100%
Kwetu Mpimbwe huko Katavi wilaya ya Tanganyika mila hii ipo.
Sio mti tu, kuna maji, mnyama, mmea, shallow graves n.k.
So sishangai huyo ndugu yako kusema hayo.
Mie mwenyewe siku nikiamua kuzindika mwili wangu, naenda tu home kwa bibi, mambo yanakuwa safi.
Sema masharti yake ndio yananishinda
Ni wilaya ya Mlele barna Madame B nakujua kwenu kule! Nishawahi kusikia sana story kama hizi
 
Mzee wako kaweka roho msituni hafi ila mwili unaoza.

Kuna shida mahali.
Kutokufa na kuoza kwenye scenario kama hii ni exception case, na hakuna kitu kina advantage kikose disadvantage hiyo ni nature, ndio maana pia dawa za mzungu tunameza ila zinaharibu figo, hapa tunaangalia advantage mtu aliyopata kuanzia kuwekewa imemkinga na hatari ngapi mpaka kufikia huo umri wa tamati
 
Hiyo elimu ipo na watu wanaitumia, ni wewe hapo huijui kutokana na mifumo iliyowekwa inayopanga wewe ulishwe nini na ufichwe nini,
Wajanja wachache ndo wanajua
Ipo wapi? Kwanini haipo kwa uwazi? Mbona elimu nyingine za asili zipo kwa uwazi? Dawa za asili zipo kibao kwa uwazi, ukihitaji mafunzo yapo tena mjini kabisa wazee wanakufundisha aina za miti na namna ya kuitumia. Kwanini hiyo ifichwe fichwe? Ina ubaya gani?
 
Kutokufa na kuoza kwenye scenario kama hii ni exception case, na hakuna kitu kina advantage kikose disadvantage hiyo ni nature, ndio maana pia dawa za mzungu tunameza ila zinaharibu figo, hapa tunaangalia advantage mtu aliyopata kuanzia kuwekewa imemkinga na hatari ngapi mpaka kufikia huo umri wa tamati
Shida ninayosema ni elimu kubwa kama hiyo iwe ya kufichwa fichwa, ipo kwenye hadithi na hakuna hata mmoja anayeweza toka hadharani akasema huyu mzee hafi huyu hapa. Hafi sababu roho ipo kwenye miti.
 
Shida ninayosema ni elimu kubwa kama hiyo iwe ya kufichwa fichwa, ipo kwenye hadithi na hakuna hata mmoja anayeweza toka hadharani akasema huyu mzee hafi huyu hapa. Hafi sababu roho ipo kwenye miti.
Mkuu kuna mambo yapo ila hayasemwi, binafsi hii kesi ya mdau nimeshuhudia sana ila kwa kule kwetu sijawahi shuhudia mtu akioza huwa wazee wanamuwahi wakiona hapa hamna kitu, Na wapo wazee mpaka dakika hii wana umri mrefu hawaumwi ila familia zao zinasema huyu naye ana kizizi. Na dawa za kuwaondoa zinatofautiana pia
 
Mkuu kuna mambo yapo ila hayasemwi, binafsi hii kesi ya mdau nimeshuhudia sana ila kwa kule kwetu sijawahi shuhudia mtu akioza huwa wazee wanamuwahi wakiona hapa hamna kitu, Na wapo wazee mpaka dakika hii wana umri mrefu hawaumwi ila familia zao zinasema huyu naye ana kizizi. Na dawa za kuwaondoa zinatofautiana pia
Ndo maana nakwambia kuna shida mahali. Either hiyo elimu ina gharama kubwa sana ambayo jamii haiwezi kuikubali au ni elimu ya mdomoni ukiingia kujifunza unakuta si kweli. Otherwise, jambo kama hilo lingeshakuwa rasmi.
 
Tuna Mzee wetu hapa tunamuuguza kwa muda mrefu miaka mitatu sasa tunampambania nae alipata tatizo kuparalalaizi mpaka sana yupo ICU hali yake sio nzuri miguu yake imeanza kuoza

Imenibidi kuandika thread hii humu sababu siku mbili hizi tumepigiwa simu huko kijijini kwamba Mzee wetu twende huko kijijini wanafamilia wote tukafanye mambo ya Mila twende na kondoo wawili inasemekana Mzee wetu Kuna miti miwili ndio aliweka roho yake

Kwahiyo tutaendelea kupoteza muda kumuuguza atakufa mpaka aoze mwili wote inatubidi tuende tukafanye mambo ya Mila maana tukimuacha aoze mwili mzima ndio afe hali hiyo itakuja kumkuta mwanafamilia
Mzee hana presha wala kisukari?
 
Hiyo ipo hasa kwa watu wenye umri mkubwa ni mambo ya dawa za asili mara nyingi anachukuliwa mgonjwa husika anawekwa ndani alafu sehem ya paa inatobolewa kidogo anapigwa na ule mwaga wa jua akiwa ndani hapo ndio anakata roho vingnevyo ataoza na harufu juu
Sasa kwa ujenzi wa kisasa wa mapaa ya gipsum utatoboaje?
 
Tuna Mzee wetu hapa tunamuuguza kwa muda mrefu miaka mitatu sasa tunampambania nae alipata tatizo kuparalalaizi mpaka sana yupo ICU hali yake sio nzuri miguu yake imeanza kuoza

Imenibidi kuandika thread hii humu sababu siku mbili hizi tumepigiwa simu huko kijijini kwamba Mzee wetu twende huko kijijini wanafamilia wote tukafanye mambo ya Mila twende na kondoo wawili inasemekana Mzee wetu Kuna miti miwili ndio aliweka roho yake

Kwahiyo tutaendelea kupoteza muda kumuuguza atakufa mpaka aoze mwili wote inatubidi tuende tukafanye mambo ya Mila maana tukimuacha aoze mwili mzima ndio afe hali hiyo itakuja kumkuta mwanafamilia
Wai aisee usidharua tamaduni za Africa na ndio msingi wetu sss
 
Hayo ni mambo ya kale, maarifa wazee wetu walikuwa nayo miaka hiyo. Sasa hivi vijana hawajui hayo mambo na wanaona ni kama uchawi.

Hata vita vya maji maji, wajerumani walishindwa sema kuficha aibu wakasema wao ndiyo walishinda, ila kiundani sisi tulishinda na ile dawa ya kugeuza risasi kuwa maji ilifanya kazi kweli.
Na mm nakubaliana na wewe mnk wazee wwetu ndio ilikuwa tamaduni zao na zilifanya Kaz vzr tu leo tuvijna wanaona utamaduni Kama uchawi wakt mungu yupo na tamaduni zipo palepale
 
Ni wilaya ya Mlele barna Madame B nakujua kwenu kule! Nishawahi kusikia sana story kama hizi
Ndio hukohuko.
Origin yangu ni Tanganyika, sema si unajua tunapokuwa wakubwa huwa tunapakwepa kwetu kwa sifa za uchawi..😕
Ila kwetu wamezidi asiee.
Huwa kunakuwaga na mashindano ya uchawi mchana kweupe.
Na unaitoa roho yako sadaka, ukifa mchezoni hakuna wa kulaumiwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom