Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 26,184
- 68,521
Nilipoteza namba yangu ya voda kabla haujaingia mfumo huu wa sasa wa kusajili kwa NIDA na kuthibitisha. Baada ya huu utaratibu kuanza ikawa imepewa mteja mwingine.
Natamani niirejeshe iwe yangu kwa sababu nilijiunga nayo vitu vingi vya muhimu ikiwamo email na kwa sasa siwezi kutumia email yangu inahitaji verification na itatumwa huko kwenye hiyo namba ambayo kwa sasa ipo kwa mtu mwingine. Nna uhitaji sana na email yangu kwasasa kuna mambo yatakwama kabisa nikishindwa kuingia.
Nimejaribu kupiga hiyo namba ili angalau niongee na anaeitumia nimuombe anitumie ujumbe wa kuverify lakini hapatikani ni wiki sasa tangu nianze kufanya hivyo.
Nawaza akipatikana na akagoma kufanya navyoomba kutokana na uelewa na hofu ya kutapeliwa nitafanyaje maana nimeshajaribu kila recovery options zimegonga mwamba wanahitaji niverify kwa phone number.
Je, nitaweza kuirejesha hii namba? Nifanyeje
Natamani niirejeshe iwe yangu kwa sababu nilijiunga nayo vitu vingi vya muhimu ikiwamo email na kwa sasa siwezi kutumia email yangu inahitaji verification na itatumwa huko kwenye hiyo namba ambayo kwa sasa ipo kwa mtu mwingine. Nna uhitaji sana na email yangu kwasasa kuna mambo yatakwama kabisa nikishindwa kuingia.
Nimejaribu kupiga hiyo namba ili angalau niongee na anaeitumia nimuombe anitumie ujumbe wa kuverify lakini hapatikani ni wiki sasa tangu nianze kufanya hivyo.
Nawaza akipatikana na akagoma kufanya navyoomba kutokana na uelewa na hofu ya kutapeliwa nitafanyaje maana nimeshajaribu kila recovery options zimegonga mwamba wanahitaji niverify kwa phone number.
Je, nitaweza kuirejesha hii namba? Nifanyeje