Ilitokea Kigamboni kama sinema!

Tram Almasi

JF-Expert Member
Feb 26, 2009
749
226
kama miezi miwili hivi nilishuhudia hili tukio la gari kuzama(Angalia picha). Ilikuwa kama tunaangalia movie vile. Kilichonisikitisha ni kuona kwamba hata wale amabao tunategemea kwamba wangesaidia kutoa taarifa katika vyombo vya usalama na uokozi, hawakuonekana kuguswa kabisa na tukio lile mpaka wavuvi na baadhi ya wananchi walipoamua kujitosa na kusiadia kuiopoa gari iliyozama kutoka majini.Bahati nzuri ni kwamba, mwenye gari alipoona inazama aliamua kufungua mlango na kuruka baada ya kuona pantoni inafunga lango lake akiwa nusu ndani na nusu nje.
MY TAKE:
Ni jana tu nikiwa ktk pantoni nimejaribu kuchunguza na nikaona kwamba hakuna jitihada zozote za kuhakikisha kuna huduma za uokozi iwapo ajali kama hiyo itatokea tena.inasikitisha na kutisha kwa kweli. au tunasubiri kuunda tume ajali ikitokea?
DSC_2216.JPG DSC_2209.JPG DSC_2230.JPG DSC_2238.JPG DSC_2254.JPG DSC_2271.JPG
 
Pale Kigamboni wahudumu wanaangalia pesa tuu wanazoiba.
Isue za safety hawazingatii kabisa.
Kuna maboya yamechakaa na hayaonekani kama hufanyiwa safety inspection.
 
Kwa hapa tulipofika nchi hii , kunahitajika mabadiliko makubwa sana ya kimfumo kuanzia ngazi za chini hadi juu. Mabadiliko haya yataletwa na watu walio nje ya mfumo uliopo sasa. Vinginevyo tutaendelea kupiga kelele kila siku. Watanzania tuhakikishe hatufanyi makosa uchaguzi wa mwaka 2015.
 
mambo mengine yanaudhi hadi unashindwa usemeje, halafu ndio tunasema tunaserikali inayotujali watu wanapata tabu taasisi zake na wahusika hata hawana mpango. na hakuna anayechukuliwa hatua kwa lolote.
 
Hayo ni manyunyu tu ya mvua, subirini daraja liishe kama hamjaona watu kwa makusudi tu wanajitoa muhanga kwa kujirusha na magali yao ili waandikwe magazetini. Salaaaale, Bongo hii?
 
nilikuwepo siku ile nilisikitika sana baada ya wavuvi kulitoa polic ndio wanajitokeza kuwafukuza eti ni wezi du!!!!!!!nilikasirika kweli na kama ningekuwa na bomu ningewarushia sidhani kama ile gari itapona maana walivyolichelewesha pale badala wamruhusu yule jamaa fasta akalifanyie service maana maji ya cumvi noma wanaendelea kuvuta jinsi watakavyopata kula .
 
He inakuwaje gari linazama wakati inatakiwa wafanyakazi wa pantoni wahahakikishe magari yote yameingia ndipo waruhusu iondoke?? Hii hatari sana!
kama miezi miwili hivi nilishuhudia hili tukio la gari kuzama(Angalia picha). Ilikuwa kama tunaangalia movie vile. Kilichonisikitisha ni kuona kwamba hata wale amabao tunategemea kwamba wangesaidia kutoa taarifa katika vyombo vya usalama na uokozi, hawakuonekana kuguswa kabisa na tukio lile mpaka wavuvi na baadhi ya wananchi walipoamua kujitosa na kusiadia kuiopoa gari iliyozama kutoka majini.Bahati nzuri ni kwamba, mwenye gari alipoona inazama aliamua kufungua mlango na kuruka baada ya kuona pantoni inafunga lango lake akiwa nusu ndani na nusu nje.
MY TAKE:
Ni jana tu nikiwa ktk pantoni nimejaribu kuchunguza na nikaona kwamba hakuna jitihada zozote za kuhakikisha kuna huduma za uokozi iwapo ajali kama hiyo itatokea tena.inasikitisha na kutisha kwa kweli. au tunasubiri kuunda tume ajali ikitokea?
View attachment 67551 View attachment 67552 View attachment 67553 View attachment 67554 View attachment 67555 View attachment 67556
 
Kweli Mkuu, baada ya wavuvi kumaliza kazi ndio hawa askari na wanajeshi wakajitokeza. Katika picha moja unamuona askari wa maji(Marine) na yeye amekaa hana tofauti na wananchi wa kawaida vivyo hivyo askari wengine na wanajeshi. Duh hatari hii.
View attachment 67662 DSC_2212.JPG DSC_2267.JPG
 
Kwa hapa tulipofika nchi hii , kunahitajika mabadiliko makubwa sana ya kimfumo kuanzia ngazi za chini hadi juu. Mabadiliko haya yataletwa na watu walio nje ya mfumo uliopo sasa. Vinginevyo tutaendelea kupiga kelele kila siku. Watanzania tuhakikishe hatufanyi makosa uchaguzi wa mwaka 2015.

Mkuu haya maneno i hope Watanzania wengi wanayasoma, nashukuru kwa post hii muhimu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom