Huu ni mwezi mtukufu, natabiri Rais Samia atachukua point zote tatu atakapoulizwa kuhusu ndoa za jinsia moja

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
914
4,261
Huu ni mwezi WA toba Kwa Wakristo na Waislam; Ni mwezi ambao Tanzania inategemea kupata ugeni wa Makam wa Rais wa USA na moja ya Jambo linalosumbua katika safari yake ni hoja ya mahusiano ya jinsia moja.

Hatuna shaka kwamba Mhe. Rais wetu atakutana na swali linalohusu msimamo wa Tanzania kama ambavyo Rais wa Ghana ameulizwa.

Rais wa Ghana ameshindwa kueleza kwa kauli moja kama nchi yake inapinga au inakubali. Sitegemea Rais Samia awe na kigugumizi kwenye hii hoja, nategemea majibu makavu yasiyo na chembe ya ukakasi.

Majibu yake yatatuma salam kwa taasisi zote zinazoratibu usodoma hapa nchini. Tuwe makini pia na wale watakaobeba mabango kudai Haki Yao ya jinsia moja. Tuwe makini na misaada tunayopewa
 
Aseme nini wakati sheria imeshasema kuwa ndoa ya jinsia moja jela miaka 7 na kufanya mapenzi kinyume na maumbile jela miaka 25-30
 
Acheni ujinga!

Wizi MKUBWA unasukwa nyie hamna habari! Mnatengenezewa propaganda za jinsi na umri mnahangaika nazo mnasahau yale ya msingi!

Amkeni!!
 
kwanza ni tegmeo langu kuwa protokali itampeleka huyo mgeni kw counterpart wake na pia kwamba waandishi wa habari watakuwa na heshima waulize vitu vya maana. ati unamuuliza Rais mambo ya hivo! adabu gani hiyo. waonywe, waambiwe kuwa "it is a taboo to ask the President those kinds of questions" kabla hata ya kuingia kwnye kuonana na viongozi. hayo yaishie kwa wahusika wa mambo ya kisheria tu
 
Huu ni mwezi WA toba Kwa Wakristo na Waislam; Ni mwezi ambao Tanzania inategemea kupata ugeni wa Makam wa Rais wa USA na moja ya Jambo linalosumbua katika safari yake ni hoja ya mahusiano ya jinsia moja.

Hatuna shaka kwamba Mhe. Rais wetu atakutana na swali linalohusu msimamo wa Tanzania kama ambavyo Rais wa Ghana ameulizwa.

Rais wa Ghana ameshindwa kueleza kwa kauli moja kama nchi yake inapinga au inakubali. Sitegemea Rais Samia awe na kigugumizi kwenye hii hoja, nategemea majibu makavu yasiyo na chembe ya ukakasi.

Majibu yake yatatuma salam kwa taasisi zote zinazoratibu usodoma hapa nchini. Tuwe makini pia na wale watakaobeba mabango kudai Haki Yao ya jinsia moja. Tuwe makini na misaada tunayopewa
Wajinga nyie,hakuna kitu kama hicho mezani,Ghana umekisikia?

Kamala akiwa Ghana amesema amekuja Afrika kuendeleza ushirikiano wa siku nyingi wa Marekani na Africa hasa kwenye business innovation na on other way ku counter off growing influence from other powers,hakutaja other powers Kwa majina ila.inajukikana ni China na Russia.

Hayo ya ushoga yanatoka wapi?
 
Back
Top Bottom