Humphrey Polepole aelezea sababu za Kibeberu ya nchi moja kufunga ubalozi

Ni maslahi gani ambayo Denmark (walioisaidia Tanzania tangu uhuru) wamebanwa kuyapata hadi waamue kufunga ubalozi? Kwamba nchi nyingine zote ambako hawajafunga balozi zao hawajabaniwa kupata maslahi kama walivyobanwa Tanzania? Huyu jamaa na stori zake za kijinga anakera sana!
Ni Mwathirika wa mawazo ya kikomunist
 
Mama akija kushituka, itakuwa imekula kwake.

Mama anaaminishwa Mbowe na CHADEMA ndio maaduii wake, kumbe maadui wake wamo humo humo katika chama chake na serikali yake.
Kwanini wanachama wenzie wageuke maadui zake?
Her failure to observe the laws of power asitafutie excuse nje.
Observe law # 43 from 48 laws of power by Robert Green
 
Eti baada ya kubanwaaa, hao wapo mjini kitambo tangu mwalimu.udikteta ndio umewakimbiza
Udikteta upi Tena? Si tulikubaliana dikteta ameshakufa kwa corona na Sasa anaoza huko Chato?
Mama mbona anabrand nchi na anaupiga mwingi sana kwanini wanamfanyia hivi?
 
Tatizo ananunulika. Alikuwa na msimamo mzuri wakati wa Katiba Mpya hasa ile Rasimu ya Warioba alikuwa anaichambua vyema sana, kukosa kwake msimamo kukamfanya auze utu wake.
 
Ungemjuwa wakati hana chama, enzi za katiba ya Warioba, angekuowa kabisa, nilimzimia sana sana, yaani nikisikia sauti ya Pole naacha shughuli zangu namsikiliza, alipotamka rasmi yeye CCM, dah, kwenye ile ya katiba mpya alobakia nnayemwamini ni Warioba tu aisee!
Pole Mkuu, usiolewe ase..
 
Pole pole ameelezea jinsi mabeberu wanavyojaribu kutudhoofisha lakini ameweka wazi sababu za nchi moja kufunga ubalozi na kusema ni Mambo ya KIUCHUMI kwani baada ya serikali hiyo kubanwa kupata maslai wameamua kuondoka, msikilize hapa akiongelea uzalendo wa Hali ya juu


Nimesikiliza mpaka mwisho,sijaona alipoelezea sababu za nchi moja kufunga ubalozi wake,nafikiri hiyo ni majumuisho ya mleta Uzi,zaidi ameelezea kuhusu mifumo ya uporaji wa rasilimali za afrika,na umuhimu wa TZ na DRC katika uchumi na jamii duniani.
Geopolitical and strategic importance of TZ na DRC,
 
Pole pole ameelezea jinsi mabeberu wanavyojaribu kutudhoofisha lakini ameweka wazi sababu za nchi moja kufunga ubalozi na kusema ni Mambo ya KIUCHUMI kwani baada ya serikali hiyo kubanwa kupata maslai wameamua kuondoka, msikilize hapa akiongelea uzalendo wa Hali ya juu


Siwezi kumsikiliza mtu huyu hata kidogo!
 
Mama akija kushituka, itakuwa imekula kwake.

Mama anaaminishwa Mbowe na CHADEMA ndio maaduii wake, kumbe maadui wake wamo humo humo katika chama chake na serikali yake.
Mkuu 'Salary', acha kuwastua. Ingependeza zaidi ungechochea kuni ili moto uzidi kukorea!
 
Nimeamini Mama ni dhaifu haya hayajawahi kutokea katika history ya CCM, wanakosoana lakini sio hadharani wakitoka nje wamoja lakini leo watu hawaogopi tena hapa Mama ajitafakari sana wanamchokonoa na kuhoji maamuzi yake na yeye kakaa kimya tu. Sasa huko 2025 ndio atawaweza hawa ikiwa leo hawamuogopi na kumuheshimu. kweli JPM alikuwa kiboko ya hawa hakuna aliyempinga waliuvyata wote. Mama amka kama bado umelala... dalili ya mvua mawingu
 
Ni maslahi gani ambayo Denmark (walioisaidia Tanzania tangu uhuru) wamebanwa kuyapata hadi waamue kufunga ubalozi? Kwamba nchi nyingine zote ambako hawajafunga balozi zao hawajabaniwa kupata maslahi kama walivyobanwa Tanzania? Huyu jamaa na stori zake za kijinga anakera sana!
 
Sijui kama ni memwelewa maana kuna maisha aliyokulia yalisaidiwa na hao anao waita mabeberu sasa sijui hapo anapambanuaje kwakweli
Kuna siku za nyuma sana, kabla Bwana Pole pole hajafahamika, niliwahi kukutana nae mara kadhaa kwenye ofisi za Ubalozi wa Denmark. Nilijiuliza maswali mengi, sikupata majibu. Sasa ndio nimepata mwanga.
 
Sijui kama ni memwelewa maana kuna maisha aliyokulia yalisaidiwa na hao anao waita mabeberu sasa sijui hapo anapambanuaje kwakweli
Kama naanza kukuelewa, kuna siku za nyuma sana, wakati Bwana Polepole hakuwa akifahamika niliwahi kugongana nad mara kadhaa kwenye ofisi za ubalozi wa Denmark
 
Ni maslahi gani ambayo Denmark (walioisaidia Tanzania tangu uhuru) wamebanwa kuyapata hadi waamue kufunga ubalozi? Kwamba nchi nyingine zote ambako hawajafunga balozi zao hawajabaniwa kupata maslahi kama walivyobanwa Tanzania? Huyu jamaa na stori zake za kijinga anakera sana!
Wapumbavu hawa ndio walikuwa 'inner cycle' ya Magufuli. Ndiyo maana misamiati ya kipuuzi hii ya "mabeberu" ilishamiri sana wakati huo.

Kwanza ningependa kujua 'background' ya huyu Polepole ipoje, kwa sababu simjui vizuri mtu huyu. Kisomo chake kipoje, amesomea vitu gani?

Nimeanza kumsikia akiota kama uyoga wakati wa mchakato wa katiba iliyoshindikana, na tokea hapo naona amekuwa mtu mwenye 'influence' kuzidi kiasi halisi cha ujuzi alionao.

Mwenye kujuwa 'background' yake vizuri, tafadhari naomba aiweke hapa; maanake huwezi kumjadili mtu usiyefahamu habari zake vizuri.
 
Nimekumbuka miradi ya DANIDA na mingine mingi.
Nawapongeza Denmark kwa kutuunga mkono kwa kipindi kirefu.
Pamoja na hayo hatuwezi kuishi kwa kutegemea misaada hata wao raia wao wanahitaji unafuu, pia tujenge utamaduni wa kujitegemea ikibidi nchi zooote ziache kutoa misaada TUFE tusio na akili ili kije kizazi kitakachoweza kupambana na KUTOBOA.

Sijutii WAONDOKE kwa Amani. Tuwapungukie Mkono wakawasalimie wananchi wao waliokuwa wanalipishwa KODI kutusaidia.

Kila leo Afrika inataka MISAADA kwa kisingizio cha UKOLONI au MABEBERU huku hatuwezi kuzalisha kukidhi mahitaji yetu, tukiwa na SERA MBOVU za kutaifa, WIZI wa mali za Umma.

Kukosa Elimu ya kufanya biashara na mataifa mengine.
Tunataka kila kitu tuhurumiwe
Are we cursed?
NGOs za Kijasusi nazo ziondoke na misaada yao ya kipuuzi, eti wanagawia wanakijiji mbuzi mmoja wa maziwa kwa kikundi cha watu 50, hadi lini hawa watu watakuwa na mbuzi 100?
NGOs zinazogawa miche 50 ya mparachichi kwa wakulima.

Afrika UJINGA MWINGI
 
Back
Top Bottom