Hukumu ya kesi kupinga ubunge Sumbawanga mjini

Ptz

JF-Expert Member
Aug 23, 2011
541
384
Kesi ya uchaguzi ya kupinga kutangazwa kwa ndg Aeshi Hiraly CCM kuwa mbunge wa Sumbawanga mjini leo mashahidi wa pande zote mbili wamehitimisha kutoa ushahidi wao mbele ya jaji wa mahakama kuu mh Jaji`Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla “J.4”(Judge incharge mahakama kuu Mbeya). Kesi hiyo inasikilizwa katika mahakama kuu mjini Sumbawanga, ambapo hoja za msingi zilizokuwa zikisikilizwa ni, moja, mchakato mzima wa uchaguzi kugubikwa na rushwa iliokuwa ukitolewa na mgombea wa CCM na pili ni uchakachuzi wa matokeo uliopelekea kutangazwa kwa bw Aeshi. Katika kesi hiyo iliyofunguliwa na bw Noberth Yamsebo aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA (mlalamikaji) anayetetewa na wakili mmoja toka mbeya na upande wa washitakiwa unatetewa na mawakili wanne. Kesi hiyo ilianza kusikilizwa rasmi tangu tarehe 27/03/2012 na leo tarehe 14/03/2012 ndio mashahidi wote wamemaliza kutoa ushahidi wao, upande wa mlalamikaji ulikuwa na mashahidi 25 na upande washitakiwa ulikuwa na mashahidi wanne tu ambao wawili kati yao “ bw Vitusi Silago mchambuzi wa mifumo manispaa ya Sumbawanga na bi Silvia Siriwa aliyekuwa mkurugenzi wa manispaa na msimamizi mkuu wa uchaguzi wa jimbo la sumbawanga mjini” (kwa sasa yuko halmashauri ya wilaya ya Ileje kama mkurugenzi) ndo wamefunga pazia la mashahidi. Vielelezo mbalimbali vilitolewa upande wa mlalamikaji na mashahidi kama ushahidi kuihakikishia mahakama kutilia manani hoja za msingi za kesi hii, moja kati ya vielelezo hivyo ni fomu mbalimbali zilizotumika kujaza, kujumlishia na kutangazia matokeo ya ubunge ambazo zilitumiwa kuchakachulia matokeo, mashahidi upande wa mlalamikaji walitoa ushahidi wao dhidi ya mgombea wa CCM ukiwepo wa kununuliwa pombe, kununuliwa baiskeli, kupewa fedha cash, ununuzi wa shahada za kupigia kura, ununuzi wa vinanda “keyboard” kwa ajili ya kwaya za makanisa mbalimbali na kuwa vyote hivyo vilitolewa kwa mashariti ya kumpigia kura mgombea wa CCM bw Aeshi. Leo mara baada ya wakili mojawapo toka wa upande washitakiwa kuiambia mahakama kuwa mashahidi toka upande wake wameisha, alisimama wakili upande wa mlalamikaji na kuomba kuwa kwakuwa kesi inaelekea mwisho basi itolewe fursa kuandaliwa majumuisho ya kesi, hoja iliyoungwa mkono na upande wa mshitakiwa, hatimaye katika kuitekeleza hoja hii, upande wa walalamikaji waliihakikishia mahakama kuu kuwasilisha majumuisho yao tarehe 26/03/2012 na washitakiwa wakaahidi kupeleka tarehe 10/04/2012, na mwisho kabisa mh jaji Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla akahitimisha mjadala kwa kusema kuwa hukumu ya kesi hii itakuwa tarehe 30/04/2012, na ndo ukawa mwisho wa shughuli za leo kuhusiana na kesi hiyo ya uchaguzi wa Sumbawanga mjini. Katika hatua nyingine, waandishi wa habari walioko Sumbawanga na mkoa wa Rukwa kwa ujumla wamekuwa wakilalamikiwa kwa kutekwa na bw Aesh kwa kutoripoti matukio mbalimbali yanayotokea katika mwendelezo wa kesi hii tangu ianze kwani kwa kiasi kikubwa kumekuwa kukitolewa ushahidi ambao kwa kiasi kikubwa ni udhalilishaji wa bw Aeshi, moja kati ya viongozi waandamizi wa klub ya waandishi wa habari mkoa wa Rukwa alipoulizwa kuhusu hili alijibu kwa madaha kuwa “waandishi tunaangalia matukio yenye maslahi” na kusema kuwa hawajaahidiwa chochote na yeyote na kuwa wao wansubiria hukumu. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI SUMBAWANGA ILI HAKI ITENDEKE. AMINA. Nikiripoti moja kwa moja toka mahakama kuu kanda ya Sumbawanga ni mimi PTZ wa JF.
 
Mkuu Ptz, ahsante kwa taarifa, ila unaweza edit tarehe (mwaka) nadhani kuna makosa ya typing
 
..mbona nimeota vibaya kuhusu kesi itakavokwisha? nimeota; majumuisho yatakayotolewa na walalamikaji (26.3.2012; mapema kabla ya walalamikiwa) watapewa washitakiwa iliyatumike kuandaa majumuisho yao; ikiwa walalamikaji wakijua yapo salama katika mikono salama. baada ya walalamikiwa kuwasilisha majumuisho ndipo jaji atatumia majumuisho hayo kuisaidia CCM kushinda kesi. Ni ndoto tuu Lakini.; kwani si ndivy taratibu zinavyosema kisheria?
 
Bravo cdm bravo Yamsebo lakini mtangazaji Joshua joel ndio gamba kwelikweli hivyo hawezi kulipoti
 
Bravo PTZ. tuhabarishe zaidi brother, Je, Majumuisho yameshafanyika? na je upande wa Mlalamikaji ndugu YAMSEBO wameshawasilisha? Tutegemee nini brother? Hao waandishi wa Sumbawanga - Choka mbaya, na wate wamewekwa mfukoni.
 
Bravo PTZ. tuhabarishe zaidi brother, Je, Majumuisho yameshafanyika? na je upande wa Mlalamikaji ndugu YAMSEBO wameshawasilisha? Tutegemee nini brother? Hao waandishi wa Sumbawanga - Choka mbaya, na wate wamewekwa mfukoni.

Yaah! Chadema tayari walisha peleka majunuisho yao kama ilivyoamuliwa na mahakama kwa tar 26 Machi. Imani yangu ni ileile kuwa iwapo judgement itakuwa fair kwa kesi hii Chadema wataibuka kidedea! kinachonishangaza ni kuwa hukumu imepelekwa mbali sana kwani ushahidi ulifungwa tar 13/Machi na hukumu ikatangazwa tar 30/ April. Hafu kuhusu waandishi wa habari, ni kweli wote wamewekwa mfukono, na baadhi yao ni makada wakubwa wa ccm, mfano, Yupo Ndg KISIKA yeye ni reporter wa RFA na afsa uhusiano wa Manispaa ya Sumbawanga na hivyo ile Sumbawanga Tv yeye ndo msimamizi mkuu lakini la kushangaza huwaweka ccm tu kwani ni mjimbe wa UVCCM mkoa wa Rukwa
 
Kwanini iwe hivyo? Iweje hao wa CCM waruhusiwe kukaa mda mrefu namna hiyo baada ya majumuisho ya Chadema? Kama Chadema ikishindwa rufani na iwe suluhishwa kwani ni dhahiri kwamba Mahakama kuu upo mchezo mchafu! Viva Chadema.
 
Tjiandae tena kwa uchaguzi mwingine mdogo hapa, Lusinde andaa matusi mapya kamanda wa chipukizi wa ccm
 
Ngome nyingine ya CDM ni Swanga mjini naomba viongozi wa chama muwe makini na ngome hii tuichukue rasmi. Enditaaaaa
 
Kesi ya uchaguzi ya kupinga kutangazwa kwa ndg Aeshi Hiraly CCM kuwa mbunge wa Sumbawanga mjini leo mashahidi wa pande zote mbili wamehitimisha kutoa ushahidi wao mbele ya jaji wa mahakama kuu mh Jaji`Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla “J.4”(Judge incharge mahakama kuu Mbeya). Kesi hiyo inasikilizwa katika mahakama kuu mjini Sumbawanga, ambapo hoja za msingi zilizokuwa zikisikilizwa ni, moja, mchakato mzima wa uchaguzi kugubikwa na rushwa iliokuwa ukitolewa na mgombea wa CCM na pili ni uchakachuzi wa matokeo uliopelekea kutangazwa kwa bw Aeshi. Katika kesi hiyo iliyofunguliwa na bw Noberth Yamsebo aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA (mlalamikaji) anayetetewa na wakili mmoja toka mbeya na upande wa washitakiwa unatetewa na mawakili wanne. Kesi hiyo ilianza kusikilizwa rasmi tangu tarehe 27/03/2012 na leo tarehe 14/03/2012 ndio mashahidi wote wamemaliza kutoa ushahidi wao, upande wa mlalamikaji ulikuwa na mashahidi 25 na upande washitakiwa ulikuwa na mashahidi wanne tu ambao wawili kati yao “ bw Vitusi Silago mchambuzi wa mifumo manispaa ya Sumbawanga na bi Silvia Siriwa aliyekuwa mkurugenzi wa manispaa na msimamizi mkuu wa uchaguzi wa jimbo la sumbawanga mjini” (kwa sasa yuko halmashauri ya wilaya ya Ileje kama mkurugenzi) ndo wamefunga pazia la mashahidi. Vielelezo mbalimbali vilitolewa upande wa mlalamikaji na mashahidi kama ushahidi kuihakikishia mahakama kutilia manani hoja za msingi za kesi hii, moja kati ya vielelezo hivyo ni fomu mbalimbali zilizotumika kujaza, kujumlishia na kutangazia matokeo ya ubunge ambazo zilitumiwa kuchakachulia matokeo, mashahidi upande wa mlalamikaji walitoa ushahidi wao dhidi ya mgombea wa CCM ukiwepo wa kununuliwa pombe, kununuliwa baiskeli, kupewa fedha cash, ununuzi wa shahada za kupigia kura, ununuzi wa vinanda “keyboard” kwa ajili ya kwaya za makanisa mbalimbali na kuwa vyote hivyo vilitolewa kwa mashariti ya kumpigia kura mgombea wa CCM bw Aeshi. Leo mara baada ya wakili mojawapo toka wa upande washitakiwa kuiambia mahakama kuwa mashahidi toka upande wake wameisha, alisimama wakili upande wa mlalamikaji na kuomba kuwa kwakuwa kesi inaelekea mwisho basi itolewe fursa kuandaliwa majumuisho ya kesi, hoja iliyoungwa mkono na upande wa mshitakiwa, hatimaye katika kuitekeleza hoja hii, upande wa walalamikaji waliihakikishia mahakama kuu kuwasilisha majumuisho yao tarehe 26/03/2012 na washitakiwa wakaahidi kupeleka tarehe 10/04/2012, na mwisho kabisa mh jaji Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla akahitimisha mjadala kwa kusema kuwa hukumu ya kesi hii itakuwa tarehe 30/04/2012, na ndo ukawa mwisho wa shughuli za leo kuhusiana na kesi hiyo ya uchaguzi wa Sumbawanga mjini. Katika hatua nyingine, waandishi wa habari walioko Sumbawanga na mkoa wa Rukwa kwa ujumla wamekuwa wakilalamikiwa kwa kutekwa na bw Aesh kwa kutoripoti matukio mbalimbali yanayotokea katika mwendelezo wa kesi hii tangu ianze kwani kwa kiasi kikubwa kumekuwa kukitolewa ushahidi ambao kwa kiasi kikubwa ni udhalilishaji wa bw Aeshi, moja kati ya viongozi waandamizi wa klub ya waandishi wa habari mkoa wa Rukwa alipoulizwa kuhusu hili alijibu kwa madaha kuwa “waandishi tunaangalia matukio yenye maslahi” na kusema kuwa hawajaahidiwa chochote na yeyote na kuwa wao wansubiria hukumu. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI SUMBAWANGA ILI HAKI ITENDEKE. AMINA. Nikiripoti moja kwa moja toka mahakama kuu kanda ya Sumbawanga ni mimi PTZ wa JF.

summarize bana!
 
Kesi ya uchaguzi ya kupinga kutangazwa kwa ndg Aeshi Hiraly CCM kuwa mbunge wa Sumbawanga mjini leo mashahidi wa pande zote mbili wamehitimisha kutoa ushahidi wao mbele ya jaji wa mahakama kuu mh Jaji`Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla "J.4"(Judge incharge mahakama kuu Mbeya).

Kesi hiyo inasikilizwa katika mahakama kuu mjini Sumbawanga, ambapo hoja za msingi zilizokuwa zikisikilizwa ni, moja, mchakato mzima wa uchaguzi kugubikwa na rushwa iliokuwa ukitolewa na mgombea wa CCM na pili ni uchakachuzi wa matokeo uliopelekea kutangazwa kwa bw Aeshi.


Katika kesi hiyo iliyofunguliwa na bw Noberth Yamsebo aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA (mlalamikaji) anayetetewa na wakili mmoja toka mbeya na upande wa washitakiwa unatetewa na mawakili wanne. Kesi hiyo ilianza kusikilizwa rasmi tangu tarehe 27/03/2012 na leo tarehe 14/03/2012 ndio mashahidi wote wamemaliza kutoa ushahidi wao, upande wa mlalamikaji ulikuwa na mashahidi 25 na upande washitakiwa ulikuwa na mashahidi wanne tu ambao wawili kati yao " bw Vitusi Silago mchambuzi wa mifumo manispaa ya Sumbawanga na bi Silvia Siriwa aliyekuwa mkurugenzi wa manispaa na msimamizi mkuu wa uchaguzi wa jimbo la sumbawanga mjini" (kwa sasa yuko halmashauri ya wilaya ya Ileje kama mkurugenzi) ndo wamefunga pazia la mashahidi.

Vielelezo mbalimbali vilitolewa upande wa mlalamikaji na mashahidi kama ushahidi kuihakikishia mahakama kutilia manani hoja za msingi za kesi hii, moja kati ya vielelezo hivyo ni fomu mbalimbali zilizotumika kujaza, kujumlishia na kutangazia matokeo ya ubunge ambazo zilitumiwa kuchakachulia matokeo, mashahidi upande wa mlalamikaji walitoa ushahidi wao dhidi ya mgombea wa CCM ukiwepo wa kununuliwa pombe, kununuliwa baiskeli, kupewa fedha cash, ununuzi wa shahada za kupigia kura, ununuzi wa vinanda "keyboard" kwa ajili ya kwaya za makanisa mbalimbali na kuwa vyote hivyo vilitolewa kwa mashariti ya kumpigia kura mgombea wa CCM bw Aeshi.

Leo mara baada ya wakili mojawapo toka wa upande washitakiwa kuiambia mahakama kuwa mashahidi toka upande wake wameisha, alisimama wakili upande wa mlalamikaji na kuomba kuwa kwakuwa kesi inaelekea mwisho basi itolewe fursa kuandaliwa majumuisho ya kesi, hoja iliyoungwa mkono na upande wa mshitakiwa, hatimaye katika kuitekeleza hoja hii, upande wa walalamikaji waliihakikishia mahakama kuu kuwasilisha majumuisho yao tarehe 26/03/2012 na washitakiwa wakaahidi kupeleka tarehe 10/04/2012, na mwisho kabisa mh jaji Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla akahitimisha mjadala kwa kusema kuwa hukumu ya kesi hii itakuwa tarehe 30/04/2012, na ndo ukawa mwisho wa shughuli za leo kuhusiana na kesi hiyo ya uchaguzi wa Sumbawanga mjini.

Katika hatua nyingine, waandishi wa habari walioko Sumbawanga na mkoa wa Rukwa kwa ujumla wamekuwa wakilalamikiwa kwa kutekwa na bw Aesh kwa kutoripoti matukio mbalimbali yanayotokea katika mwendelezo wa kesi hii tangu ianze kwani kwa kiasi kikubwa kumekuwa kukitolewa ushahidi ambao kwa kiasi kikubwa ni udhalilishaji wa bw Aeshi, moja kati ya viongozi waandamizi wa klub ya waandishi wa habari mkoa wa Rukwa alipoulizwa kuhusu hili alijibu kwa madaha kuwa "waandishi tunaangalia matukio yenye maslahi" na kusema kuwa hawajaahidiwa chochote na yeyote na kuwa wao wansubiria hukumu.


MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI SUMBAWANGA ILI HAKI ITENDEKE. AMINA. Nikiripoti moja kwa moja toka mahakama kuu kanda ya Sumbawanga ni mimi PTZ wa JF.​


 
Hapa sumbawanga mjini hakuna waandishi wa habari kabisa na kama wapo basi wanaandika habari za kujitugia nazile wanazopewa na viongozi wa ssm kwa kutpewa posho na kubebwa kwenye magari ya chama. Hawana utamaduni wa kutafuta habari.Yapo matukio mengi ya vipongozi kukandamiza wananchi na kutowajibika vema lakini sijawahi kusikia wanafuatwa na kuhojiwa ili taarifa zifike kwa wananchi na watanzani wenzao wajue wenzao wa Rukwa wanashida zipi. Zaidi sasa hivi kuna sumbawanga tv ambayo Kisika anawachukua ccm na kuweka vipindi vya ovyo badala ya kukusanya wanancihi kueleza kero zao na kuwafikishia viongozi na nafikiri sababu ni u uvccm wa Juma Kisika.Kesi AESHY anaweza kutupwa nje hakimu akiwa fair!
 
Back
Top Bottom