figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Salaam Wakuu,
Tusaidiane kuangazia hii kesi, tupo huru kuongea sababu Hukumu imeshatoka.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Simiyu ilimhukumu kifungo cha miaka saba na faini ya Tsh 15 milioni, Levinus Kidanabi maarufu kama 'Chief Son's kwa makosa matatu ikiwamo kumkashifu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Hukumu iliyotolewa Oktoba 19, 2022 na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Matha Mahumbuga SIMIYU: Levinus Kidanabi Jela miaka saba na faini mil 15 kwa kumkashifu Rais Samia
Baada ya kuona Makosa yake, nikagundua hakuna hata sehemu moja alipomkashifu Rais Samia. Tujikite kwenye Makosa Mawili ya kumashifu Rais Samia.
Wakili wa Serikali Daniel Masambu na Mwendesha mashitaka wa Polisi Johndon Buhure Walidai Makosa hayo alitenda kwenye Group la WhatsApp la "Simiyu Breaking News".
Walidai Kosa la kwanza alilitenda 3/12/2021 kwamba aliandika:
"Mzazi mwenzao anawatetea Wazazi Wenzake, Mkiongozwa na Mwanamke Lazima mtafanywa kama wote mnanyonyesha; taifa limekuwa kama lina wanawake wote. Kila siku tunaongelea mambo ya kike kike"
Kosa la pili wanadai alilitenda 4/12/2021. Kwamba alitoa taarifa za Uongo:
"Mama yenu anakaribia kuugua ukichaa kitaalam tunaita anachokifanya hallucinations. Aka kamuungano tufungeni tumuombe Mungu kavunjwe ipo siku Hawa watu was kuvuka maji watatuingia kwenye Madeni madeni Makubwa maana Wanapenda starehe kuliko kazi"
Wakili wa Serikali Daniel Masambu alidai kuwa alikuwa akimkashifu Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
MASWALI YANGU:
1. Ni wapi Levinus Kidanabi kamtaja Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan?
2. Mtu kusema Mama yenu inakuwa inamanisha Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan?
3. Ni watu gani Wanavuka maji?
4. Je, Kumuomba Mungu aingilie kati kuvunja kitu ni kosa?
Hii kesi ikibidi Kibata au Jebra Kambole, achangiwe aende kumtetea huyu Mwana CCM. Natamani kuona Tanganyika Law Society TLS, Watetezi mko wapi?
Kafungwa miaka 7 na atalipa Mil 15
Tusaidiane kuangazia hii kesi, tupo huru kuongea sababu Hukumu imeshatoka.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Simiyu ilimhukumu kifungo cha miaka saba na faini ya Tsh 15 milioni, Levinus Kidanabi maarufu kama 'Chief Son's kwa makosa matatu ikiwamo kumkashifu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Hukumu iliyotolewa Oktoba 19, 2022 na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Matha Mahumbuga SIMIYU: Levinus Kidanabi Jela miaka saba na faini mil 15 kwa kumkashifu Rais Samia
Baada ya kuona Makosa yake, nikagundua hakuna hata sehemu moja alipomkashifu Rais Samia. Tujikite kwenye Makosa Mawili ya kumashifu Rais Samia.
Wakili wa Serikali Daniel Masambu na Mwendesha mashitaka wa Polisi Johndon Buhure Walidai Makosa hayo alitenda kwenye Group la WhatsApp la "Simiyu Breaking News".
Walidai Kosa la kwanza alilitenda 3/12/2021 kwamba aliandika:
"Mzazi mwenzao anawatetea Wazazi Wenzake, Mkiongozwa na Mwanamke Lazima mtafanywa kama wote mnanyonyesha; taifa limekuwa kama lina wanawake wote. Kila siku tunaongelea mambo ya kike kike"
Kosa la pili wanadai alilitenda 4/12/2021. Kwamba alitoa taarifa za Uongo:
"Mama yenu anakaribia kuugua ukichaa kitaalam tunaita anachokifanya hallucinations. Aka kamuungano tufungeni tumuombe Mungu kavunjwe ipo siku Hawa watu was kuvuka maji watatuingia kwenye Madeni madeni Makubwa maana Wanapenda starehe kuliko kazi"
Wakili wa Serikali Daniel Masambu alidai kuwa alikuwa akimkashifu Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
MASWALI YANGU:
1. Ni wapi Levinus Kidanabi kamtaja Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan?
2. Mtu kusema Mama yenu inakuwa inamanisha Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan?
3. Ni watu gani Wanavuka maji?
4. Je, Kumuomba Mungu aingilie kati kuvunja kitu ni kosa?
Hii kesi ikibidi Kibata au Jebra Kambole, achangiwe aende kumtetea huyu Mwana CCM. Natamani kuona Tanganyika Law Society TLS, Watetezi mko wapi?
Kafungwa miaka 7 na atalipa Mil 15